Iran yashambulia kambi za Marekani kwa Ballistic Missiles 12 wanazosema zinatumiwa na Mossad nchini Iraq

Mambo yalianzia hapa iran walisema israel na marekani watalipa na watajibu na wamejibu kweli

Mambo yalianzia hapa



IRGC: Israel italipa gharama ya kuua shahidi Wairani wawili huko Syria
Mar 09, 2022 10:24 UTC
IRGC: Israel italipa gharama ya kuua shahidi Wairani wawili huko Syria
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limesema hakuna shaka utawala wa Kizayuni wa Israel utalipa gharama kubwa kwa jinai yake ya kutekeleza shambulizi lililopelekea kuuawa shahidi askari wawili wa SEPAH nchini Syria.

Taarifa ya Ofisi ya Uhusiano Mwema ya IRGC imeeleza kuwa, shambulizi la kombora la utawala haramu wa Israel viungani mwa mji mkuu wa Syria, Damascus juzi Jumatatu liliua shahidi mashujaa wawili wa jeshi hilo, ambao ni Kanali Ehsan Karbalaeepour na Kanali Morteza Saeednejad.

Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu limesisitiza kuwa, hakuna chembe ya shaka kuwa litalipiza kisasi kwa jinai hiyo iliyofanywa na Wazayuni maghasibu.

Hii si mara ya kwanza kwa utawala huo khabithi kufanya hujuma dhidi ya washauri wa kijeshi wa Kiirani, ambao wako nchini Syria kwa mwaliko rasmi wa Rais halali wa nchi hiyo, Bashar al-Assad.
Hawa sasaivi watapigwa kuanzia Asia mpaka Europe
 
Na ukristo wangu sijawahi furahia hilo taifa la Israel juu ya udhalimu wake kwa palestina, USA kwasasa hana nguvu ya kujifanya super power kwani anapata changamoto nyingi kwa mataifa makubwa kama China, Russia huku Waingereza wenyewe hawana ubavu kuichumi, Japan athari za Hiroshima na Nagasaki bado ni kovu tisha, Germany hana mpango wa vita.
Akijichanganya wanaume wataenda kumpiga kwake
Israel hajawahi mpiga mtu asiyemchokoza
 
Ha ha ha!! Kwa namna umewasilisha ingetendeka hivyo Iran leo kungekua kunanyesha makombora....punguza mahaba bana.
Hamna kambi ya Marekani imepigwa, ha ha ha!! Eti kambi imeteketezwa...duh!
Kombora limepiga karibu na ubalozi wa Marekani.

"Ballistic Missiles Strike Near U.S. Consulate"

https://www.washingtonpost.com/world/2022/03/12/irbil-attack-iraq/
Huu atakuwa bwana mdogo mjinga mjinga tu.

Hakuna nchi ina ujasiri kuishambulia US kirahisi rahisi namna hii
 
tokea lini hao watu wakaimbea mema Africa(mtu mweus)?.kama una spiritual power iombee aman congo,ethiopia,na bara zima la Africa.hao acha wachinjane no matter the impacts to us economically hao ni majibwa ambayo hayatupendi black races tuache kujipendekeza
Tuache kabisa huo ungese, mkristo anamuona mzungu ndio mtu na muislam anamuona mwarabu ndio mtu mtakatifu yaan nifull shobo. Vita ina advantages na disadvantage zake.

Ilitakiwa tuangalie nivip tutafaidika navita zao hata wakifa wote nifresh tuu

Sent from my Infinix X680 using JamiiForums mobile app
 
Marekani nae atoke kwenye minchi ya watu yani linakuwa kama limwanamke lisilotulia kwake linadanga tu!
Wewe lione hivyo kama dangaji lakini hata kwa maisha yako haya ya kila siku kwa nchi zetu hizi, kuna watu maisha yao kuendelea kuishi yanawategemea wao.hasa kwenye sekta ya Afya
 
Back
Top Bottom