Mkuu
britanicca asante Kwa data hii maana wengi wetu tunashabikia Kwa mrengo wa Imani Fulani ya dini bila kujua uwezo na historia ya US hasa Kwenye mambo ya vita.
Tukumbuke kuwa hawa US hawafanyi vitu vyao Kwa kukurupuka hata siku moja ndiyo maana Kwa muda mrefu wamemfanyia Iran trade sanctions ili adhoofike kiuchumi,miezi 3 iliyopita wananchi wa Iran walikuwa wanaandamana kushinikiza raisi wao ang'atuke madarakani Kwa sbb ya Hali mbaya ya uchumi wao.
Hata Saudi Arabia nao Wana mgogoro na Irani juu ya mapigano ya nchini Yemen na wanatamani Iran ipigwe na kusambaratika Kutokana na Imani zao za kidini,ukiona mpaka huyo kamanda wa Iran anauwawa tujue kabisa kuwa nchi ilishajipanga Kwa matokeo yoyote yale