Iran shoots down US drone

Nakuunga mkono Mkuu. Hili ni la kweli kabisa. Vita inaidhoofisha sana US kiuchumi sijui kwanini hawalioni hili.

Wanaliona sana hili, mkuu BAK. Kwa sasa Wanajaribu silaha zao kabla ya kumkabili China na Urusi ana kwa ana, kosa wanalolifanya wanasahau kuwa China na Urusi wanawafuatilia kwa karibu kabisa "nyendo zao".
 
Hivi vita tunavyopigana left and right vina gharama na gharama yake ndio hiyo ya kufilisika kwa mataifa makubwa sababu ya overspending. Sioni kwanini tunaeneza vita kila mahali.
 
Tukubali tu hili Taifa la Marekani ni tatizo kuwepo Duniani hapa, ni genge kuu la kishetani ambalo wanadamu wanatakiwa kuliondoa ila sasa tutawaondoaje?!! ni shida sana kwa kweli,,,nadhani sasa Dunia ifanye mpango wa kulifuta hili Taifa la kishetani ili tuwe na amani..
 
Iran announced three years a go it built an unmaned aircraft with a range of more than 600 miles(1000Kms)Far enough to reach Israel.Aircraft reportedly use to keep watch on OSAMA BIN LADEN's compaund in Pakistan as the raid that killed him was taking place earlier this year.
 
Iran yatungua ndege ya kijasusi isiyokuwa na rubani ya Marekani

Afisa mwandamizi wa Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema jeshi la anga la nchi hii limetungua ndege ya kijasusi isiyokuwa na rubani ya Marekani , mashariki mwa nchi hii. Kamanda huyo wa Jeshi la Iran ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema kuwa, ndege hiyo aina ya RQ-170 na yenye kuongozwa kwa mbali imetunguliwa baada ya kuingia katika anga ya Iran karibu na mpaka wa nchi hii na Afghanistan.

Jeshi la Iran limesisitiza kuwa, litaendelea kuimarisha usalama katika mipaka yake na kuwa liko tayari kukabiliana na hujuma yoyote ya maadui.
 

Ndugu, usipende sana kuamini kila kitu wanachokiandika "alphabet agents", hawa jamaa huwa wana cook data pia. Hata hao huwa wananunuliwa na big corporations ili ku-justufy matakwa yao. Usibishe ndugu vita inaharibu uchumi, hata kama kuna makampuni machache yanayo faidika (greedy) kiujumla uchumi wa nchi nzima hudidimia.

Sababu ya Marekani kuendelea kwa kasi baada ya vita ya pili ya dunia ni kwasababu british pound amabayo ilikuwa ni pesa ya dunia kwa miaka takriban 150 ili poteza umaarufu (confidence) kwasababu ya uingereza kudorora kiuchumi. Na kwasababu nchi za ulaya ziliitaji fedha ili zijijenge upya Marekani ikawa ndiyo nchi pekee ya kukopa. Ndiyo chanzo cha economoc boom ya 50s, 60s na 70s. Dola ndipo ilianza kutumika kununulia mafuta na kuwa pesa ya dunia na wala siyo eti vita ndiyo vilileta maendeleo miaka hiyo.

..naona mnawaelewa hawa US kinyume kabisa,FYI war is a very good business kwa Economy ya US na ndio maana miaka yote wako busy kutafuta hizo war,hizi war zinaongeza sana nguvu za uchumi wao lakini hakuna hata

Siyo kweli, vita ni nzuri kwa matajiri wachache wanaomiliki viwanda vya silaha.Na kwataarifa yako viwanda vya silaha siyo waajiri wakubwa Marekani. Waajiri wakubwa ni small businesses, wale wanaoajiri watu chini ya 100, mfano carpet cleaning campanies, small software companies, nk



Kwani mkuu unafikiri kuongezeka kwa bei ya vyakula inatokana na nini? Ni kutokana na machafuko yanayoletwa na vita. Mambo kama gharama za uzalishaji, uhaba wa mafuta n.k Kama utakumbuka wakati vita ya Iraki ilipopamba moto (2004) bei ya mafuta ilifika $4/gallon wamiliki wengi (wadogo wadogo) wa malori waliyaegesha kwasababu hawakuwa wanatengeneza faida kusafirisha mzigo. Na hii ilileta mfumuko wa bei ya vyakula Marekani.
 
....Mkuu Mushi reconstruction ambayo kwa sasa imegomba, huwezi kufanya reconstruction kama hakuna pesa na wakati huo huo unajaribu kupunguza budget deficit...... na kama ujuavyo wale GOP kwa sasa wamekataa kabisa kupandisha kodi.
Mkuu wangu, kwa kifupi,vita kwa wenzetu ni "investment" fwatilia...
 
Mkuu wangu,wenye ku invest kwenye vita ndo walioshika mpini kwa sasa mkuu wangu, siyo kwamba naamini kama ulivyosema, ila ndo reality, na dhumuni halisi ni kuwa na mjadala kama huu...

Kuwaondoa hao walioshika mpini ni kazi kubwa, unajuwa kuwa defense ndiyo wanaspend zaidi kuliko hata domestic?

Wanatumia 54% on defense, 43% domestic na 3% intrernational, mimi naongelea reality, cheki hapo chini...

How does the federal government spend its money?
 
Wanaliona sana hili, mkuu BAK. Kwa sasa Wanajaribu silaha zao kabla ya kumkabili China na Urusi ana kwa ana, kosa wanalolifanya wanasahau kuwa China na Urusi wanawafuatilia kwa karibu kabisa "nyendo zao".
USA amewapita china na urusi kijeshi kwenye mambo mengi,china na urusi wanachofanya wao wanacopy na kuiba USA anachofanya,
tangu WW2 imekuwa kazi ya urusi kucopy zana za marekani,sasa hivi wanafanya wote yeye na china
 
Kama utasoma hiyo habari hapo juu, utakutana na kifungu hicho hapo juu, nenda chini utaona pie chart inayoonyesha spending ya serikali ya marekani kwa asilimia...

Hata pesa wanayotoa kama msaada kwa mataifa ya nje ina account only 3%! Lakini bado inatosha kuwanunuwa,ama kununua nchi nyingi tu!

Ila wakispend kwenye defense, basi ujuwe ni hata bases zao zilizoko kila kona ya dunia...There's nothing "cooked" on that!
 

Mimi sikatai kuwa hawatumii pesa nyingi kwenye ulinzi ila nilichosema ni kuwa hii inatokana na wamiliki wa hayo makampuni ya silaha na taasisi zinazohusika kulazimisha bajeti ya ulinzi iongezeke ili wafaidike na siyo eti kwamba nchi inafaidika kiuchumu na vita. Nafikiri kama unafuatilia vizuri mambo yao utakumbuka kuna wakati bajeti ya ulinzi wakati wa Bush na Cheny iliongezeka mara dufu kwa mwaka mmoja kuliko jumla ya bajeti yote ya NASA toka ianzishwe.
 
USA amewapita china na urusi kijeshi kwenye mambo mengi,china na urusi wanachofanya wao wanacopy na kuiba USA anachofanya,
tangu WW2 imekuwa kazi ya urusi kucopy zana za marekani,sasa hivi wanafanya wote yeye na china

Siyo kweli mkuu...
 
Mimi nilikwambia nazungumzia reality, hizo data kila mtu anaweza kuzitafsiri kivyake,ndo maana kuna different ideas and different policies on how to handle these economic issues...

Repubs watakuwa wanakumbatia vita WHERE AS sometimes Democrats but no all the times, lakini overall wote ni watu wa vita na uchumi wao umejengwa kwenye basis hizo, ama misingi hiyo, hilo ni fact!

Kwamba vita ni mbaya, hilo peke yake halitakufanya upate urais wa marekani, unaona Obama anavyofanya licha ya kwamba alipiga kelele kuhusu vita vya Irak and Afghanistan?

Hakuna radical changes zilizofanyika vs being a war mongering nation...

Ninaposhindwa kukuelewa ni what point of view are you "coming from"?

Ukiangalia wanavyodili na issues hizo ambazo wewe na baadhi yao wanaona ni tatizo, kwao siyo tatizo, wewe ukaja ukaniambia kuwa wamepika data, hiyo siyo shida yangu.

Again, i am talking ablunt reality and i have submitted some facts to back it up.

Hayo unayosema wewe nayafahamu vyema tu.

Otherwise tunaweza kuendelea na porojo...
 

We mangi, acha kudanganyika uchumi wa Marekani unadorora kwa sababu ya vita kubwa mbili zilizoandaliwa kinyemela na akina Bush and the co. vita ya Irak na ile ya Afghanistan. Wanaofaidika kiuchumi kutokana na hizo vita ni hao hao watajwa hapo juu lakini Marekani kama nchi sasa hivi imeathirika sana kiuchumi hata mwenyewe wajua hilo. Huyu Mjaluo sasa hivi anajaribu kubana matumizi hata kufikia kupunguza air craft carrier zao kutoka 11 kwenda 10, pia ule mradi wa F-35 JSF pia unakatiwa fedha kama ilivyokuwa kwenye F-22 raptors, pia kambi nyingi sana za kijeshi ndani na nje ya USA zitafungwa etc, etc. Hii yote ni kutokana na strain ya hizo vita mbili kwenye uchumi wa nchi, pia kumbuka wamekuwa wakitegemea kukopa fedha kwa ajili ya mambo yote hayo...:lol:

Chamoto said:
...Siyo kweli, vita ni nzuri kwa matajiri wachache wanaomiliki viwanda vya silaha.Na kwataarifa yako viwanda vya silaha siyo waajiri wakubwa Marekani...

Hii ni sahihi kabisa...the so called cowboy wars.😛oa
 
Mkuu, wote wanajuwa kabisa what gets the economy going is spending, lakini tatzo ndilo hilo, spending on what?

Hapo ndipo wamegawanyika...

Repubs wanasema spending ni muhimu, lakini wanataka spending on things they believe will stimulate the economy, na wanasema la muhimu ni ku cut "wasteful spending", ila defense si mojawapo kwa upande wa repubs...

Pia wanataka spending on private sector, walimsusia Obama, na ndiyo maana Obama ikabidi aspend kwenye federal programs, just to keep the economy going...Na pia evidently some on war ie Libya!

Kwa upande wa democrats, wao wanaamini spending pia lakini za tofauti na zile za Repubs na pia hawakubalini ku cut spending on some of the domestic programs...

Wanaamini kuwa pesa ya ziada itapatikana kwa kuwa tax matajiri their "fair tax" share, wana amini kama defense itakuwa cut, basi ni kwasababu mbinu ya vita sasa imebadilika, ambapo si lazima kuwa na majeshi sehemu flani flani, bali "predators" AKA unmanned planes, zina replace, haina maana kwamba vita ni mbaya kwao...Again wanachojali zaidi ni human cost, na ndiyo maana Bush alipiga marufuku majeneza kuonyeshwa kwenye TV yakirudi.

Wakisha pata namna ya kure shuffle spending allocations, mtaona kama defense itakuwa cut all together!

Hii issue mnavyoiangalia nyie, kwa kweli siwalaumu, lakini pia mtambuwe kuwa hayo mabomu hayawagusi wamarekani wenyewe na hivyo uchungu wa vita hawaujui kihivyo, na Gates juzi hapa alilalamika kuwa cutting defense spending will jeopordize security.

Mimi naangalia issue kama mtu huru bila kusukumwa na hisia,na ndiyo hapo tunapotifautiana.

Hadi sasa ni federal Reserves pamoja na mebenki kadhaa ie Japan, wamekuja pamoja kuisadia Euro, same stories "dejavu" like after world war 2...?! Soma hapo chini...
(http://www.cnbc.com/id/45490416)

Sasa kama hao matajiri wakikubaliana na hiyo tax policy itakayowafanya walipe ile wanayoita "fair share" Unadhani defense itakatwa?

Sijui huwa mnatizama vipi issue wakuu!?

Msiangalie issue kwa ushabiki, tizame reality, mliko huko mimi pia nilikuwepo, lakini nimejifunza kuweka reality into account!
 

Sasa hii footage imetengenezwa na wamagharibi wewe unategemea nini halafu mipango mikakati (strategy) ya Urusi na Marekani ni tofauti kabisa. Wamarekani wao ni offensive na wapo kibiashara (sio kama nchi bali watu binasi wanao tengeneza silaha) wakati warusi wao ni defensive. kwahiyo utakuta kwenye jeshi lao (warusi) hawana madege mengi kama wamarekani lakini wana ma-islander ya aina nyingi na wameendela sana katika tesla technology ambapo wanaweza kuharibu mawasiliano ya ndege, guided missiles na hata military satellites kwakutumia elecromagnetic waves.
 
Repubs watakuwa wanakumbatia vita WHERE AS sometimes Democrats but no all the times, lakini overall wote ni watu wa vita na uchumi wao umejengwa kwenye basis hizo, ama misingi hiyo, hilo ni fact!

Hapa tutatofautiana mkuu.

Waajiri wakubwa ni small businesses, federal Goverment, Wal Mart, Target, Home deport, McDonalds, IBM n.k. Uncle Sam anapata pesa kutoka kwa wafanyakazi wanaokatwa kodi kila paycheck. Sasa kama hao waajiri wakubwa si watengeneza silaha inakuwaje vita iwe msingi wa uchumi wao?

"coming from"?
Ni kwasababu ninayaona kila siku, maisha ya wamarekani wengi yamekuwa duni kipindi hichi cha vita za Iraki na Afganistani. Umasikini umeongezeka, zaidi ya watu milioni 40 wanaishi kwenye poverty line. Biashara nyingi zimekufa, watu hawana kazi na ndiyo maana kuna occupy 'everything' sikuhizi kila mahali.

Ninaposhindwa kukuelewa ni what point of view are you

Nikwamba kuna watu wana maslahi kwenye biashara ya silaha. Hawa hutumia kila njia kama kuhubiri terrolism, fear, second amendement n.k ili kuhakikisha wanachota pesa nyingi kutoka kwa walipa kodi ili ziende kwenye mambo ya vita amapo wao watafaidika.
 
Mkuu fuatilia historia ya marekani vyema,hizi unazosema hapa ni current issues,unajuwa ni kitu gani kiliuinua uchumi wa marekani?

Tuanzie hapo kwanza ili nijuwe kama ninapoteza muda wangu ama vipi.

Pia tatizo hapa ni kwamba vita haijaanza kupayback, lakini mategemeo yao ni kuwa eventually it will pay pack, and the history backs em up!

Ni wazi pia uliki ignore kipande hiki cha taarifa...Zingatia red!

Ndiyo, uchumi wa marekani umeyumba, lakini wakiondoa vita utakufa moja kwa moja, na the only way kuondoa vita ni only if watashindwa vita hivyo!

Kama kweli wewe ni mfwatiliaji mzuri wa historia ya marekani, utagunduwa pia hata nyakati zote ambapo uchumi ulikuwa mzuri, bado walikuwa kwenye vita!

Marekani hawajawahi kuwa out of war since world war II! (FACT!)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…