Iran just outplayed the United States again

Iran just outplayed the United States again

I'm certain that, if Trump was among the warmongers, then today, the news media would have the better titles bolded on their front pages.

Trump is good at damage controlling, whoever against America should atleast be thankful to Trump.
Unafikiri Iran akishambulia allies na military za kijeshi za u.s, kwamba Kwa sababu sio warmonger hata retaliate acha ushabiki kijana
 
Mkuu habari za masiku. Turudi madani:
Mwaka 1961 Raisi wa Marekani Jenerali Dwight Eisenhower anavyoaga alitoa hotuba na akawaonya wamarekani kwa kusema "Be ware of the Military Industrial Complex" . Ukweli ulikuja kujulikana miaka ya 80's kwamba nani ndiye anaendesha sera ya mambo ya nje ya Marekani na hawa maraisi huwa wanapelekeshwa sana na makundi yenye nguvu.

Hivi unafahamu Urusi ilivyoanguka Raisi George Bush alipata msongo wa mawazo kwasababu alijua Wamarekani wangesema bajeti ya jeshi ipunguzwe hivyi kupelekea makampuni makubwa ya silaha, ulinzi na mafuta (The Military Industrial Complex) kupata hasara na uchumi kushuka.

Ndiyo wakaja na mkakati mpya (The Wolfowitz Doctrine) wa mwaka 1992 ambao ilikuja kuandikwa vizuri na Colin Powell na Dick Cheney. Paul Wolfowitz alitoa mkakati utao hakikisha uhai wa The Military Industrial Complex pamoja na uchumi wa Marekani kwa miaka mingi ijayo. Huu mkakati ndo umeiingiza Marekani kwenye mitafaruku isiyoisha duniani kote: It's all about the money.

Sasa ndiyo maana nawauliza wadau wangu hapa kwamba wanadhani Donald J Trump anaweza kushindana na hili dubwasha la The Military Industrial Complex ambalo ni kitovu cha uchumi wa Marekani ???
Bajeti kubwa ya kijeshi inachangiwa kuwa na zaid ya military 200+ za kijeshi duniani

Na ukiachia hio Obama alipunguza bajeti ya ulinzi lakin trump alipoingia akaongeza maradufu bajeti ya jeshi jiulize kwanini alifanya hivyo

Na akarudisha project za nuclear kumbuka mpaka sahivi maraken inatumia billion of dollar ku-manage radioactive waste zinazotokana na military equipment zote hizo zinaongeza ukubwa wa bajeti

Ili marekani apunguze bajeti ya ulinzi ni sharti apunguze kambi za kijeshi zilizo dunia nzima kitu ambacho hakiwezekan. Na apunguze nuclear arsenal kitu ambacho hakiwezekani
 
TUJITEGEMEE mbona unawezo mkubwa sana wa kufikiri kuamini katika hizi conspiracies za deep state, Trump did all he did cause he has to fight impeachment na uchaguzi mkuu. Power ya kuamua tofauti anayo kumbuka alipojisifia kuwa aliahirisha shambulizi zidi ya Iran dakika kumi kabla ya kufanyika baada ya kuuliza watu wangapi watakufa alipoambuwa ni hamsini aka call off the mission iweje leo amefanya
Mkuu, mwanzo nilipozipata habari za Marekani kuongozwa na 'deep state' yaani elite fulani hivi tena walionje ya White House sikuziamini. Tena nikapata wana JF nguli hapa jukwaani wakasisitiza US inaendeshwa kwa mujibu wa katiba na demokrasia iliyotukuka. Lakini kadri nilivyozidi kufuatilia masuala haya kwa taarifa zilizowazi mitandaoni nikagundua kweli, kuna nguvu ya ziada tena kubwa ya uendeshaji wa Marekani kuliko nguvu ya WH na Pentagon tunazofikiria.

Nikijikita kwenye mjadala huu!
Ukweli siwezi kuendelea kudhani kuwa Trump ana ubavu wa kimaamuzi ya kukataa vita visianzishwe na nchi yake huko ugenini. Maana imejidhihirisha sasa kuwa makampuni ya silaha yameweka lobbyists wa kutosha huko Pentagon na WH kuhakikisha biashara inafanyika kwa namna yoyote ile na wapigadebe hawa wanafanya kazi yao barabara. Kazi inafanyika barabara, maana kubadili maamuzi ya kichwa ngumu na mwenye majivuno kama Trump, si kazi ya kitoto.

Inasemwa pia kuwa si hisa za makampuni ya silaha tu zilizopanda thamani bali hata makampuni ya mafuta pia hisa zao zimepanda thamani. Tukumbuke siku si nyingi Trump alitamba kuwa sasa US ndiye mzalishaji wa mafuta mkubwa ulimwenguni. Unganisha nukta hapo.

Inasemwa pia kuwa nguvu ya US hasa imejikita kwenye nguvu ya ela yake(dollar) kutumika kibiashara ulimwenguni hasa mafuta, teknolojia, sekta silaha, mifumo ya fedha. Mambo haya nadhani ndiyo aliiwezesha hasa kuwa super power na kuanza kutumia unipolar system brutally kwa nchi nyingine. Sasa ni kwa kuchoshwa na unipolar system hii ya US, nafikiria washindani/wapinzani wa US kama China na Russia wakaanza kutafuta mbinu ya kudhoofisha nguvu za US.

Washidani hawa wameanza kukataa kutumia dollar kwenye biashara zao(tuna petroyuan); teknolojia sasa China anamkimbiza US na 5G/6G, kwenye space nchi washiriki zimeongezeka, mifumo ya kuunga internet ushindani wa kutosha n.k; mifumo ya fedha nchi nyingi zimetafuta mbadala wa Swift ambayo inanatumiwa vibaya na US, BRICS ameanza kuwa na mifumo yake ya kibenki kukwepa IMF na WB; na kwenye silaha ndipo sasa Russia kaamua kukaza msuli asymmetrical kwa kufanya silaha ghali za US kuwa useless kwa silaha bora na za kisasa lakini za bei ndogo za Russia. Hili limewachanganya sana. Wamarekani.

Nadhani anachotaka kufanya US kwa sasa nikuhakiksha anaendelea kudhibiti visima vyake hapo Mashariki ya kati kwa kuiyumbisha nchi Tata Iran ambayo inatishiia kufunga strait of Hormuz inayopitisha mabilioni ya galoni za mafuta. Ikishindikana kumdhibiti Iran, nasikia US na plan B, atapitisha mafuta yake na gesi kutoka hapo Middle East kwenda Ulaya kupitia kwa mshirika wake Israel kupitia Cyprus, Greece na hatimaye Italy. Mpango hupo tayari maana juzi Netanyahu aliwasainisha Cyprus na Greece mkataba wakupitisha bomba la mafuta/gesi nchini mwao. Hii ni baada ya mpago wake wakupitisha bomba lake kutoka Kuwait, Iraq ,Syria, Turkey kushindikana.

Kwa majumuisho, nikuwa taasis ya urais ya Marekani ni picha haina mamlaka ya juu kabisa kama inavyooneka hasa kwenye masuala mengi ya kimaamuzi bali nguvu iliyojificha ya industrial complex. Na wapinzania wa Marekani wameanza kuishughulikia nguvu halisi ya Marekan badala ya kuangaika na WH. Kuna uwezekano washindani hawa wa US wakafanikiwa.

Mchango wangu ndio huo na unaweza kuwa na mapungufu kadhaa!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
TUJITEGEMEE mbona unawezo mkubwa sana wa kufikiri kuamini katika hizi conspiracies za deep state, Trump did all he did cause he has to fight impeachment na uchaguzi mkuu. Power ya kuamua tofauti anayo kumbuka alipojisifia kuwa aliahirisha shambulizi zidi ya Iran dakika kumi kabla ya kufanyika baada ya kuuliza watu wangapi watakufa alipoambuwa ni hamsini aka call off the mission iweje leo amefanya

Sent using Jamii Forums mobile app
Asante sana Mkuu, kwa kusoma post yangu na kisha kutoa maoni yako juu yangu ya kwanini siku hizi naamini Taasisi ya uraisi ya US haina maamuzi ya mwisho kwa baadhi ya mambo hasa ya nje yanayohusisha 'interest za industrial complex'. Na umejenga hoja yako kwa kusisitiza kuwa Trump ana maamuzi ndiyo maana alisitisha revenge ya kudunguliwa drone yake ya bei kubwa kabisa iliyotunguliwa na Iran; kisa eti Trump alihofia zaidi ya watu 50 watauawa.

Kwa kutumia hoja yako hiyo ya idadi ya watu; nikuulize, kwa nini mara hii Trump hakuwaza kabisa idadi ya watu wataodhurika kwa shambulio hili!? Inaelezwa watu wengi wameuawa kwenye shambulio hili lilowaua makamanda wa Iran na wale wa jeshi la Iraq. Ushahidi huu hapa:

On January 3, Major General Qassem Soleimani, the commander of the Qods Force of Iran’s Islamic Revolution Guards Corps, and Abu Mahdi al-Muhandis, the second-in-command of Iraq’s Popular Mobilization Units (PMU) were killed by US strikes on the Iraqi capital of Bahdad. The US strike that also killed several others Iraqi and Iranian commanders caused a regional crisis and put the entire Middle East on the edge of a new open military conflict.
source: southfront.org


Na Je. Trump anapotangaza kuwa atashambulia maeneo 52 Iran yakiwemo yale ya utamaduni, tena kwa kutumia silaha mpya na ya kisasa tena kwa muda mfupi bado ana simamia kuto ua wairan 50 ama la!? Zipo taarifa kuwa US ameboresha silaha zake nyuklia na kuwa katika vipimo vidogo. Na mpango huu ameusimamia Trump akiwa chini ya kivuli cha lobbyist nguli Bolton. Ushadi huu hapa:

Katika mazingira haya bado unaamini Trump ndiye mwamuzi juu ya nini kifanyike ukizingatia ni Trump aliyeingia Madarakani akijipiga kifuani atakomesha "useless and endless war' zinazopiganwa na US, ni Trump huyu aliyesema hakuna haja ya kuwa na NATO hata baada ya kuingia Madarakani....! Kwa nini amebadili mawazo yake!?

Nimeona nianze kukupa haya; kisha unaweza kupitia hoja zilizowasilishwa na Wakuu wengine hapo juu akiwemo Malcom Lumumba na hapo utazidi kupima kama 'deep state' ni myth ama real thing!!!

Karibu.
 
Sidhani kama unajua kinachojadiliwa hapa au hata kama unajua basi uelewa wako nauweka kwenye mabano.
Unavyosema outplay unamaanisha nin sababu uchumi wake uko mahututi hata mim elewa wako nauweka kwenye mabano unaongelea sana conspiracy theory na sio uhalisia
 
Kwahiyo unatakaje
Imetangazwa kwamba baada ya shambulio la Janerali Sulemani hisa za makampuni makubwa ya silaha nchini Marekani zimepaa ghafla: Raytheon, Lockheed Martin na Northrop Grumman wanasherehekea sasa.

Bado unadhani haya maamuzi ya Donald Trump ya kutotaka vita yana uzito wowote kwenye mazingira ya nchi kama ya Marekani ??? Hebu tujadili.....

NB: Pia tukumbuke kwamba hisa za makampuni mengine muhimu zimedondoka huku hiza makampuni ya silaha zikipanda.

TUJITEGEMEE, Barbarosa, Root

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa kukumbusha tu hii mada/ uzi umetokana na Makala iliyoandikwa kwenye jarida/ gazeti la Washington Post la Marekani. Rejea post ya kwanza ya uzi huu.
Washington post, new York times yameandika hivyo Kwa sababu ni ant trump yana jaribu kumdiscredit trump Kwa kuaminisha conspiracy theory na sio uhalisia

Article zao nilikua nazisomaga lakin sizisomi tena,
 
Sasa mbona kule juu ulikuwa unaandika ujinga wakati kumbe una IQ kubwa namna hii
Kuna kitabu kimeandikwa na mwanahistoria David Talbot kinaitwa The Devil's Chessboard:Allen Dulles, the CIA and the Rise of America's Secret Government. Humo ndani mwandishi anaelezea kwamba CIA ni chombo cha ajabu mno ambacho kiuhalisia hakiwajibiki kwa mtu hata kwa Raisi wa nchi.

Anasema The Dulles Brothers ni moja kati ya watu waliowahi kuwa na nguvu kubwa sana nchini Marekani na walimshinda hadi Raisi John F Kennedy. Mwanzoni mwa utawala wa Kennedy, 1961 kulikuwa na uasi mkubwa wa kijeshi kwenye koloni la Ufaransa la Algeria (Algiers Putsch) ambapo yalilalizimisha serikali ya Jenerali Charles De Gaulle kutii matakwa yao ya kutoruhusu Algeria iwe nchi huru kwa kuogopa ukomunisti.

Paris wakapiga simu Washington kuuliza kwanini majasusi wenu wanataka kuivuruga Ufaransa ??? Raisi Kennedy akashituka sana na kusema kwamba yeye hana ufahamu wowote ule kuhusu huo mkakati. Kumbe Mkurugenzi Allen Dulles ndiyo kauratibu mkakati mkubwa hivyo bila idhini ya Raisi. Sasa kama walifanya hivyo miaka ya 1961 leo hii watakuwa wanafanya nini ???

JF Kennedy alimfukuza kazi Allen Dulles, na kuahidi kuivunja CIA vipande vipande lakini kumbe Dulles alikuwa bado ni mkurugenzi kivuli (The Shadow Director) ambaye alikuwa anakaa kwenye nyumba ya siri ya CIA huku akiendelea kuendesha mfumo. Talbot anasema kwamba Lee Harvey Oswald alikuwa anapokea amri kutoka kwa wakina Dulles.

Sasa nini kilitokea: JF Kennedy kauwawa aliyekuwa mwenyekiti wa The Warren Commission iliyochunguza kifo cha Raisi unajua alikuwa nani ??? Allen Dulles, mtu yuleyule ambaye Kennedy alimfukuza kazi kwa kufanya mambo ambayo ni kinyume na sheria za nchi.

Mwisho kabisa: Raisi wa Marekani Harry S Truman kwenye kumbukizi zake (Memoirs) aliandika majuto yake ya kutoridhishwa na mwenendo wa CIA na akasema hakutegemea kwamba ingegeuka kuwa vile. Anasema vyeo vya juu kabisa vya CIA vilijaa watoto wa matajiri wa WallStreet ambao walikuwa na ajenda zao wenyewe na wenye nguvu kubwa sana ya ushawishi na pesa.

Jambo hili Jenerali Dwight Eisenhower alikuja kuligundua baadae na kuna kipindi hadi yeye alikataziwa kufahamu nini kilichokuwa kinaendelea Area 51, akaamua kutishia kuvamia na nguvu ya jeshi ndiyo akaambiwa atume wawakilishi wa Ikulu ili wakakague kilichokuwa kinaendelea mle ndani. Haya siyo maneno yangu bali maneno ya aliyekuwa Waziri wa Ulinzi wa Canada Paul Theodore Hellyer. (Japo wengi wanambishia)

Mwishoni kabisa anamaliza Uraisi wake mwaka 1961 Dwight Eisenhower naye alionekana kutoridhika na mwenendo wa The State of Security na aliwaonya sana Wamarekani kwamba " Be ware of the Military Industrial Complex".

Kitafute kitabu cha Talbot ni kizuri sana, kinafikirisha na kimejaa rejea za kutosha zenya kushawishi. Soma halafu toa hukumu yako mwenyewe.

NB: Jambo nalowaza ni kwamba tunasema Donald Trump ni mtu asiyependa vita lakini je kutopenda kwake vita kunaweza kubadilisha chochote kile nchini Marekani ??? Upande mwingine tusisahau kwamba Donald Trump ni sehemu ya mfumo wa Marekani unaopingana na mfumo mwingine wa Marekani lakini wote hao lengo lao ni moja na taasisi wanazozitumia ni zilezile tu.

TUJITEGEMEE, Barbarosa , Red Giant

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwamba trump hapendi vita acha uobgo na upotoshaji marekani inaingia vitani kama maslai yake yapo hatarini hats vita vya pili vya dunia aliingia vitani baada ya kuona maslai take yako hatarini

Moja ya kosa wamarekan wanajuta ni kutumia dhana yako hawapendi vita mpaka ayatollah kufanya mapinduzi

So far trump ameshindwa mzibiti Iran Kwa sababu Obama alitumia vikwazo lakin kipind cha kampeni trump kuahidi kuwa aggressive lakin amejikuta amerudi kule kule Kwa Obama anatumia vikwazo


Sababu yangu ya kusema D.Trump hataki vita ni base yake iliyomchagua na ambayo inampa inampa sapoti mpaka sasa hivi haitaki vita na aliwaahidi kutokuiingiza USA in foreign wars, na mpaka sasa hivi karibia miaka 4 Trump hajaanzisha Vita wala kuivamia nchi yoyote ile hiyo ni record kwa standard ya Maraisi wa USA kwani wote walivamia nchi nyingine isipokuwa Trump hata hili la Irani hakuna vita hapo, kwani Trump atapoteza sana sapoti yake akiingiza USA vitani, Trump siyo war monger kama Obumer, Bush, Clintons & Co.
 
TUJITEGEMEE mbona unawezo mkubwa sana wa kufikiri kuamini katika hizi conspiracies za deep state, Trump did all he did cause he has to fight impeachment na uchaguzi mkuu. Power ya kuamua tofauti anayo kumbuka alipojisifia kuwa aliahirisha shambulizi zidi ya Iran dakika kumi kabla ya kufanyika baada ya kuuliza watu wangapi watakufa alipoambuwa ni hamsini aka call off the mission iweje leo amefanya

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwani si ameua watu kumi tu jamani, tena ni wanajeshi watupu.
Tumpe heko Trump tafadhali.
 
Sababu yangu ya kusema D.Trump hataki vita ni base yake iliyomchagua na ambayo inampa inampa sapoti mpaka sasa hivi haitaki vita na aliwaahidi kutokuiingiza USA in foreign wars, na mpaka sasa hivi karibia miaka 4 Trump hajaanzisha Vita wala kuivamia nchi yoyote ile hiyo ni record kwa standard ya Maraisi wa USA kwani wote walivamia nchi nyingine isipokuwa Trump hata hili la Irani hakuna vita hapo, kwani Trump atapoteza sana sapoti yake akiingiza USA vitani, Trump siyo war monger kama Obumer, Bush, Clintons & Co.
Hivi bill Clinton kuna nchi aliivamia
 
Ndiyo, Kosovo, Serbia, vita kubwa sana huko Ulaya chini ya Bill Clinton, hata Somalia imeharibiwa na Clinton!
Alifyatua makombora Iraq kwa siku nne mfululizo mwaka 1998 kupitia Operation Desert Fox. Mwaka 1999 akiwa na NATO akavamia Yugoslavia bila idhini ya Umoja wa Mataifa: Tena kipindi harakati za kumtoa madarakani (Impeachment Proceedings) zikiwa zinaendelea bungeni.
 
Back
Top Bottom