Iran inawezaje kufanya haya

Iran inawezaje kufanya haya

Keyboard_Warrior

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2015
Posts
6,288
Reaction score
10,965
Nimekuwa nikiona kila mahala huko mtandaoni, watu wanauliza kwa kebehi, eti kwanini Iran anashambulia nchi karibia zote hapo Mashariki ya kati, lakini hashambulii Israel!?

Hili ndio swali linalotrend huko mitandaoni kwasasa, lakini wote wanaouliza hili swali ni watu wanaofanana kwenye jambo fulani hivi.

Anyways, tuachane na hii.
Mpaka saa hii nimetoka huko mtandaoni, nimekutana na habari za Iran kushambulia Bahrain na Kuwait na kuua askari kadhaa wa Marekani, hii habari inazunguka sana huko mtandaoni saa hii.

Lakini pia, jana nilisoma mahali nilikutana na habari kuwa Pakistan ametishia kuwa endapo Iran itaishambulia Saudi Arabia, basi itakuwa ni sawa wameishambulia Pakistan.

Ajabu usiku wa kuamkia leo Iran imepiga kituo cha kijeshi cha Marekani kilichopo Saudi Arabia, sijui itakuaje sasa?

Kuwait nao visima vyao vya maji safi vimepigwa na kituo cha kuzalisha umeme kimepigwa pia.

Nakuja kwenye swali langu sasa.
Hawa Iran, wanawezaje kupambana na USA na wakati huo huo kupiga kambi za kijeshi za marekani zilizopo katika nchi za Kiarabu? Hawa jamaa wameishi katika vikwazo kwa takribani miaka zaidi ya 40, wanawezaje kupambana na USA!?

Hapohapo mashabiki wanataka akiwa anapambana na USA aingie ulingoni kupambana na Israel pia, jamani hii Iran mbona kama mnaikuza sana?

Yaani mnaona kupigana na Marekani haitoshi, inatakiwa apigane na Israel kwa wakati huohuo, anawezaje sasa!?

Bila kusahau, Strait of Hormuz haipitiki.

Trump anasema ipo wazi, lakini meli zikikatisha zinapigwa kiberiti na Waajemi.

Trump amepereka meli zake za kijeshi kulinda meli zinazokatisha hapo, lakini bado Iran wanaweza kuzishambulia meli zinazokatisha hapo bila ruhusa ya Jeshi la Iran.

Inashangaza sana.

Hawa Iran wanawezaje kufanya haya yote!?
Mbona kama kuna kiini macho hivi!


HNggRdbXsAADn2Q.jpeg
 
Kwanza ifahamike Iran hana shida na hizo nchi ambazo zinamzunguka,ila shida ipo kwa hao ambao wanaruhusu nchi zap kuwa base za kijeshi za Marekani,ugomvi upo hapo tu

Kuhusu Israel ni kwamba,mara nyingi Iran haianzishi vita ila inamaliza vita,kwa maana anza wewe kisha yeye anaingia,kama umesikia Israel katishia kutumia Nuclear,Iran kasema we tumia Lakini jua Iran ni kubwa haitaathirika sana,ila mimi nitaangamiza vituo vyako vya kuzalisha nuclear na nchi yenu itapotea
 
View attachment 3631672

Trump ameripua daraja, majamaa yanakatisha pembeni kama hakuna kilichotokea.
Hii Iran ni nchi ina kiburi cha ajabu sana, hiki kiburi sijui wanakitoa wapi!?

Ndio ujinga wa kibabu cha kilokole kinaongozwa na pepo la chuki badala ya Akili 🫎🫎🫎🤠

Sasa ukisikia matumizi mabaya ya Kombora ndio ayoo !!!

Daraja lenyewe maji hakuna kabisaa sasa umevunja nini kwa lango lipi!!!
.

Tena Daraja yenyewe rakawaida sana!!

Sasa Iranian imeenda piga Daraja uko Saudia sio la mchezo

Iranian wapo mbele ya muda!!
 
Ume andika kishabiki sana., kutetea Magaidi ya Iran.

Ila ukweli ni tofauti
Ugaidi wao ni upi? Kama ni kufadhili Hebzollah na Hamas hata Israel/US ilifadhili Al qaeda wa Syria (HTS) hadi kumsaidia kuwa Rais wa Syria au huo sio ugaidi?

Vikisaidiwa na Israel vinaitwa vyama vya ukombozi ila wakisaidiwa na Iran inageuka magaidi!!!
 
Ume andika kishabiki sana., kutetea Magaidi ya Iran.

Ila ukweli ni tofauti

Gaidi la kwanza ni upeo wa Akili yako!!!

Marekani ndio kaanzisha vita kwenye nchi ya watu!!

Lkn mizwazwa ya kilokole wanawaona Iranian ndio tatizo!!!

Kweli kondoo waliopotea kwamujibu wa Bible👈
ilikuwa mbele ya Muda😂

Akili za Zwazwa 🫎🫎 ipo ivyo nakuvamia👈

Na ww ndio mpenda fujo sio yeye mvamizi😇🫎🫎🫎 kondoo
 
Gaidi la kwanza ni upeo wa Akili yako!!!

Marekani ndio kaanzisha vita kwenye nchi ya watu!!

Lkn mizwazwa ya kilokole wanawaona Iranian ndio tatizo!!!

Kweli kondoo waliopotea kwamujibu wa Bible👈
ilikuwa mbele ya Muda😂

Akili za Zwazwa 🫎🫎 ipo ivyo nakuvamia👈

Na ww ndio mpenda fujo sio yeye mvamizi😇🫎🫎🫎 kondoo
Fungua akili yako,akili yako yako isifungwe na udini.mimi ni mkristo ilq katika mizozo yote natumia logic wala sio udini.
Kwa akili yako unadhani marekani anapigana dhidi ya dini ya islam?
hao israel wenyewe hawamtambui kristo,watu wanapigana kwa maslahi ya mataifa yao na vizazi vyao,wewe mmatumbi unaingizia dini.
Mnashabikia sana russia unajua majority ya russia ni makafiri kulingana na vitabu vyenu?
 
Sababu ni kadhaa zikiwemo,
1. Iran wanauzoefu wa muda mrefu katika vita.
2. Iran anafahamu mbinu za marekani ni kupima upepo kwahiyo ukilegeza msimamo umekwisha
3. Iran anafahamu hana uwezo wa kupambana na USA kutokana na ukwebwa wa jeshi la Marekani ila silaha pekee ni kuathiri maslahi ya kiuchumi ya USA ndani ya middle East
 
Ume andika kishabiki sana., kutetea Magaidi ya Iran.

Ila ukweli ni tofauti
Onesha ushabiki wangu ulipo!

Iran hapigani na jeshi la Marekani?
Iran hajashambulia kambi za Jeshi la Marekani hapo middle east!?
Iran haijawa na vikwazo miaka zaidi ya 40?
Iran haijafanya Strait of Hormuz kutopitika!?

Huko ulipo bei ya mafuta (diesel/petrol) ipoje!?
Unajua ni nani anasababisha ununue mafuta hiyo bei unayonunua sasa!?

Kama hauna hoja, tulia.
 
Fungua akili yako,akili yako yako isifungwe na udini.mimi ni mkristo ilq katika mizozo yote natumia logic wala sio udini.
Kwa akili yako unadhani marekani anapigana dhidi ya dini ya islam?
hao israel wenyewe hawamtambui kristo,watu wanapigana kwa maslahi ya mataifa yao na vizazi vyao,wewe mmatumbi unaingizia dini.
Mnashabikia sana russia unajua majority ya russia ni makafiri kulingana na vitabu vyenu?
Uko sahihi
Kwa kukazia tuu, wabongo wengi imani za kidini zimewafanya wamekuwa wajinga, ndo maana wengine wanatapeliwa kwa kutajiwa neno dini au Mungu
Vita ni uchumi, watu au mataifa yanaingia vitani kwa ajili ya maslahi yao ya kiuchumi, ila huku kwenye walevi wa kidini wao chapchap wanahusisha na dini
 
Sababu ni kadhaa zikiwemo,
1. Iran wanauzoefu wa muda mrefu katika vita.
2. Iran anafahamu mbinu za marekani ni kupima upepo kwahiyo ukilegeza msimamo umekwisha
3. Iran anafahamu hana uwezo wa kupambana na USA kutokana na ukwebwa wa jeshi la Marekani ila silaha pekee ni kuathiri maslahi ya kiuchumi ya USA ndani ya middle East
Kwanini Marekani na USA na hizo nchi za Kiarabu (Saudis, Kuwait, Bahrain, Jordan) wasiivamie kijeshi Iran!?
 
Tangu vita ianze February Iran anadai kushambulia na kuangamiza hizo kambi kila siku mpaka unajiuliza Marekani ana maelfu ya makambi mangapi kwenye hizo nchi.
 
Back
Top Bottom