Ipyana Malecela (10 years on) - RIP

Status
Not open for further replies.
Aise mmenikumbusha mbali sana kweli ni muda sasa. nakumbuka nilikuwa natoka Dodoma naelekea dar siku ambayo msela alikuwa anazikwa Ndugu shabiby enzi hizo ndio alikuwa anaongoza kwa gari nzuri za kwenda Dar to Dom, mabasi yote alipeleka msibani na lile bovu ndilo tulilopanda kwenda Dar, huwezi amini tuliondoka dodoma saa 2 asubuhi tukafika dar saa 11 jioni, RIP kaka
 
Duh!

Ipy daima tutakukumbuka yaani nakumbuka tulionana muda mfupi kabla ya mauti kukufika, nakumbuka ulitokea kwenye mkutano uliokuchagua kuwa Mwenyekiti wa UVCCM siku ya jumamosi ukaja Mgulani JKT hall kwenye harusi ya rafiki yetu sote tukakushangilia na ukahaidi kuwafuata maharusi hotelini asubui ukawape supu kwani ulitaka kuchinja mbuzi asubui yake ilikuwa mida ya saa 6:30 usiku sitokaa ni sahau asubui yake tukapigiwa simu kuwa umetutoka, wengi wetu kwenye ile group yetu hatukuaamini tulidhani ni uongo lakini tulipofika upanga tukakuta ni kweli umetangulia mbele ya haki, ni vigumu sana kuamini kuwa ulitutoka ingawa yalisemwa mengi sana juu ya kifo cha Ipy ila Mwenyezi Mungu pekee ndie ajuae.

:rip: Ipy.... RIP Brother daima tunakukumbuka miaka 10 imepita ila ni kama juzi umetutoka,

Mwenyezi Mungu ailaze roho yako mahala pepma peponi Amen.


Pole zangu nyingi sikufie we Kamanda pamoja na Ndg,jamaa na hata marafiki.
MUNGU mwenye huruma nyingi awajaze nguvu zake mwenye!



Rest In Peace Ipyana Malecela!
 
RIP Pal... sitaki kabisa kukumbuka kifo hiki ! Uliaga unakwenda home ku-change chap chap baada ya pilika pilika za then ungekuja maskan pale kontena kupata moja mbili na kuendeleza libeneke la mjadala wa kuimarisha chama letu la msimbazi na within few minutes tukaambiwa umedondoka nyumbani na unakimbizwa hospitali, na kwa vile ilikuwahapo karibu tayari next minute wanasema umetutoka !!

Will always be missed "jenerali" !!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom