IPTL haponi mtu

IPTL haponi mtu

BAK

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2007
Posts
124,769
Reaction score
288,283
IPTL haponi mtu


  • Makundi ya urais yatia mguu, watuhumiwa hofu tupu
  • Profesa Muhongo ajipanga kulipua bomu la mwaka



KASHFA kuchota fedha kwenye Akaunti Maalum ya Escrow zaidi ya sh bilioni 200, zilizohifadhiwa kwenye Benki Kuu ya Tanzania (BoT), itang'oa idadi kubwa ya watendaji wakuu Serikalini na wanasiasa, Tanzania Daima Jumapili limedokezwa.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili kwa wiki moja iliyopita tangu kuanza kwa mkutano wa 16 na 17 wa Bunge mjini hapa, umebaini kuwa joto la kashfa hiyo linazidi kupanda huku baadhi ya wabunge bila kujali vyama vyao, wakiungana kuhakikisha wahusika wanawajibishwa, ikiwemo kung'olewa madaraka yao.

Mjadala wa wabunge wengi, ndani ya viunga vya Bunge na nje ya eneo hilo ni kuhusu kashfa hiyo iliyotokana na mradi wa kuzalisha umeme wa Kampuni ya Independent Power Tanzania LTD (IPTL).

Watuhumiwa katika kashfa hiyo ni Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, Katibu Mkuu Eliachiam Maswi ambao imeelezwa kuwa wanafanya kila aina ya ushawishi kuhakikisha wanaepuka kikombe hicho.

Wengine ni Gavana wa Benki Kuu (BoT), Benno Ndullu, Waziri wa Fedha na Uchumi, Saada Mkuya, Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema Mkurugenzi wa Shirika la Umeme nchini (Tanesco), Felches Mramba.


Pinda anahusishwa kwenye kashfa hiyo kwa madai alishindwa kuchukua hatua za haraka kuzuia uchotwaji fedha hizo.

Baadhi ya wabunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM), wameungana na Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR-Mageuzi) na kambi nzima ya wabunge wa upinzani, kuishikia bango kashfa hiyo.

Mmoja wa wabunge maarufu wa CCM ambaye aliomba jina lake lihifadhiwe, alisema hoja hiyo ni ya wabunge wote, wakiwemo wa CCM ambao wakati mwingine huwapa hoja mpya wenzao wa upinzani kuhusu kashfa hiyo.

Zaidi ya yote, hoja hiyo imekolezwa na baadhi ya makundi ya wataka urais ambao duru za siasa zinaelezea kuwa wanataka hoja hiyo ifike mwisho na hakuna namna inaweza kumwacha Waziri Mkuu Mizengo Pinda salama.

Pinda ambaye ameshaweka bayana kwamba ameanza mbio za kuwania urais kimya kimya katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwakani anaonekana ndiye mlengwa.

Pinda tayari ameshaonekana tishio kwa baadhi ya makundi ya urais hasa yale ya vijana ambao wanadhani kuchafuka kwake na kashfa hiyo, kutapunguza kasi yake ya kutaka kuwania urais.

Hata hivyo wabunge wanaotajwa kuwa kwenye kambi ya Pinda wamejipanga na kuweka mkakati wa kumnusuru kiongozi huyo.

Kambi ya Pinda inahofia kashfa hiyo inaweza kukifanya CCM kuzalisha makundi hasimu na hivyo kukosa mwelekeo kwenye uchaguzi mkuu kama ilivyotokea mwaka 2010 baada ya kashfa Richmond iliyomng'oa mtangulizi wake Edward Lowassa mwaka 2008.

Hofu hiyo ndiyo inayodaiwa kukikumba CCM kilichokuwa kikitaka mjadala huo usipelekwe bungeni lakini jitihada hizo zimegonga mwamba baada ya Bunge kutangaza kujadili wiki hii.

Shinikizo la kambi nzima ya upinzani, wabunge wa CCM na makundi ya urais, ndiyo yaliyofanikisha kuzima mkakati wa Serikali uliotaka kuizima hoja hiyo isije kwenye mkutano wa Bunge hili kwa madai kuwa ripoti ya uchunguzi wake kutoka kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), haijakamilika.

Tayari Kamati ya Uongozi baada ya mjadala mzito, imelijulisha Bunge kuwa hoja hiyo sasa itapelekwa bungeni Novemba 27 na 28.
Naibu Waziri kutolewa kafara?

Wakati ripoti ya CAG ikisubiriwa kwa hamu Bungeni, baadhi ya wabunge wamedokeza kuwa ripoti hiyo iko hadharani na imewataja baadhi ya vigogo wa wizara ya nishati na madini kuhusika.

Kutokana na hali hiyo, duru hizo za siasa zinadai kuwa Naibu Waziri mmoja wa wizara hiyo ameandaliwa kisaikolojia kutolewa kafara ili kuwalinda vigogo hao wasiaibike.

Wizara hiyo ina Manaibu Waziri wawili ambo ni Steven Masele (Madini), Charles Kitwanga (Mawe matatu ambaye anashughulika na Nishati.

Taarifa za kuwapo mpango wa kutoa kafara Waziri huyo mdogo, wili iliyopita ziliibuliwa Bungeni na Mbunge wa Nyamagana, Ezekie Wenje.

Bila kutaja jina, Wenje alidai kuwa mpango huo upo na tayari Waziri huyo aliitwa jijini Dar es Salaam ghafla kwenda kujengwa kisaikolojia.

Muhongo ajipanga kulipua bomu
Wiki iliyopita (JUMATANO) baada ya kiindi cha maswali na majibu kumalizika, Waziri Muhongo alikuwa akizungumza na baadhi ya wabunge kwenye eneo la viwanja vya Bunge, kwamba anataka kuomba nafasi ya kuzungumza bungeni kabla ya ripoti hiyo kuwasilishwa.

Alisema katika mazungumzo hayo, amepanga kufichua siri kubwa iliyojificha nyuma ya sakata hilo na kutaja majina ya wabunge na watendaji wengine aliodai wamepata mlungula kusukuma ajenda hiyo bungeni.

Mgogoro uliosababisha fedha kuwekwa katika akaunti hiyo ya Tegeta ya BoT ulitokana na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kugoma kulipa gharama za uwekaji mitambo (Capacity Charge) kwa IPTL mwaka 2006 kwa vile ilibainika IPTL ilikuwa ikitoza gharama kubwa kuliko iliyopaswa.

Akaunti hiyo ya Tegeta ilianzishwa kwa sababu ya kuhifadhi fedha zote zilizopaswa kulipwa na Tanesco hadi hapo mgogoro baina ya pande hizo mbili umalizike.

Hata hivyo, Septemba mwaka jana, serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini, iliagiza BoT kulipa fedha hizo kwa kampuni ya PAP mara baada ya kuridhishwa na uamuzi wa Mahakama Kuu uliosema kwamba mgogoro baina ya wamiliki wa IPTL na Tanesco umemalizika na hivyo Benki Kuu haina sababu ya kuhifadhi fedha hizo.

Uamuzi huo wa kulipwa ulizua upinzani mkali bungeni ambapo wabunge wawili wa kambi ya upinzani; Mbunge wa Kigoma Kusini (NCCR-Mageuzi), David Kafulila na Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA), Zitto Kabwe.

Wabunge hao walidai kuwa zoezi hilo limejaa ufisadi na Bunge liliazimia kwamba suala la kutolewa fedha katika akaunti ya Tegeta lifanyiwe uchunguzi wa kina na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) pamoja na ile ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).

Chanzo: Tanzania Daima
 
PROF MUHONGO WALA ASIPEWE HIYO CHANSI YA KUONGEA MANAKE ANACHOTAKA KUTUHAMISHA TU KWENYE LENGO KUU. Hapa anajaribu kutafuta watu wa kufa nae kwakuwa ndio kawaida ilivyo mfa maji haishi kutapata.

Anataka kuwavika ubaya kina Kafulila na Zitto sifa mbaya kama hivi vijituhuma wanavyookoteza okoteza wakidhani ndio watanusurika katika unyama wao huu wanaowafanyia Watanzania maskini.

Hapa hili sakata lazima lidondoshe mbuyu na sisi WATANZANIA TWASEMA HATUKO TAYARI KUDANGANYWA TWATAKA KUONA PESA ZINARUDI NA WAHUSIKA WANAWAJIBISHWA. Fullstop.
 
Ningewaona wa maana kama wangesema wanakwenda mahakamani kukata rufaa make suala hili limeamuliwa na mahakama kuu.
 
CHAMVIGA
Bavicha ndiyo shida yenu hujui kitu juu ya hili unarukia tu.
 
Last edited by a moderator:
Hivi watu kulipwa hela zao tatizo? IPTL wamezalisha umeme Tanesco wamenunuwa umemo huo na kuutumia na wameuza kwetu sisi. Kulikua na malalamishi kuwa charges wanazotozwa ni kubwa hivyo wakagoma kulipa. Tanesco walifungua kesi kuangalia upya mkataba na kesi imeeisha na Tanesco wameshindwa .

Makosa ya wao Tanesco kukubali mkataba wenye charges za juu hivyo walishindwa. Pia kulikua na mgogoro wa wana hisa kuhusu IPTL ilofanya fedha hizo zizuiwe kulipwa wenyewe hadi watapo maliza mgogoro wao. IPTL wamemaliza tofauti zao na BOT ikaamrishwa iwalipe sasa kashfa iko wapi.

Labda kama Tanzania tumezoea kutoheshimu mikataba na wawekezaji hasa kama sio kutoka nchi za magharibi. Ilokua sakata la Richmond yalikua kama haya na kilicho fata ni yule mwarabu wa Oman alijua kasumba za wabongo alipotaka kuwauzia ile mitambo Tanesco kina Mwakyembe wakasema labda on my dead body .

Alipotaka kuisafirisha nje TRA wakatiwa maneno ...Mwarabu akajua hawa adabu yao Wamarekani . Basi ile mitambo ikauzwa kwa kampuni ya Marekani na ipo na sasa tunanunua umeme bukheeeri kabisa na mwarabu akachukua hela yake na huku Tanesco wakishindwa kesi ya kimataifa na ndani na kulazimishwa kulipa malipo wanayo daiwa na Dowans.

Na hili la IPTL lipo kama hilo isipikua ccm hawana msimamo na huwa hawana uwexo wa kukabiliana na malumbano na wenyewe wapo weak huingia mtegoni.
 
....tulimwoma ni mtu safi tena msomi mzuri atakayetumia taaluma yake vyema kwa taifa letu kumbe nae ni....?
 
Huyu Profesa mwizi Muhongo kwa sasa amezoea rushwa na ufisadi, je baada ya hiki kimbunga kumzoa atarudi kupiga chaki aka kufundisha?

Mtoto wa mkulima aliyegeuka fisadi ataenda kusubiri hadi nyuki watoe asali auze ndio apate hela wakati alizoea kuchota za bure kama alivyochota za IPTL?

Stay tuned
 
Hivi watu kulipwa hela zao tatizo?
IPTL wamezalisha umeme Tanesco wamenunuwa umemo huo na kuutumia na wameuza kwetu sisi.
Kulikua na malalamishi kuwa charges wanazotozwa ni kubwa hivyo wakagoma kulipa.
Tanesco walifungua kesi kuangalia upya mkataba na kesi imeeisha na Tanesco wameshindwa .
Makosa ya wao Tanesco kukubali mkataba wenye charges za juu hivyo walishindwa.
Pia kulikua na mgogoro wa wana hisa kuhusu IPTL ilofanya fedha hizo zizuiwe kulipwa wenyewe hadi watapo maliza mgogoro wao.
IPTL wamemaliza tofauti zao na BOT ikaamrishwa iwalipe sasa kashfa iko wapi.
Labda kama Tanzania tumezoea kutoheshimu mikataba na wawekezaji hasa kama sio kutoka nchi za magharibi.
Ilokua sakata la Richmond yalikua kama haya na kilicho fata ni yule mwarabu wa Oman alijua kasumba za wabongo alipotaka kuwauzia ile mitambo Tanesco kina Mwakyembe wakasema labda on my dead body .Alipotaka kuisafirisha nje TRA wakatiwa maneno ...Mwarabu akajua hawa adabu yao Wamarekani .
Basi ile mitambo ikauzwa kwa kampuni ya Marekani na ipo na sasa tunanunua umeme bukheeeri kabisa na mwarabu akachukua hela yake na huku Tanesco wakishindwa kesi ya kimataifa na ndani na kulazimishwa kulipa malipo wanayo daiwa na Dowans.
Na hili la IPTL lipo kama hilo isipikua ccm hawana msimamo na huwa hawana uwexo wa kukabiliana na malumbano na wenyewe wapo weak huingia mtegoni.

nimeipenda hii.
 
hakuna kitu hapo...wananchi msidanyike wala kugeuzwa mazuzu na hawa wasaka tonge
 
Hivi watu kulipwa hela zao tatizo?
IPTL wamezalisha umeme Tanesco wamenunuwa umemo huo na kuutumia na wameuza kwetu sisi.
Kulikua na malalamishi kuwa charges wanazotozwa ni kubwa hivyo wakagoma kulipa.
Tanesco walifungua kesi kuangalia upya mkataba na kesi imeeisha na Tanesco wameshindwa .
Makosa ya wao Tanesco kukubali mkataba wenye charges za juu hivyo walishindwa.
Pia kulikua na mgogoro wa wana hisa kuhusu IPTL ilofanya fedha hizo zizuiwe kulipwa wenyewe hadi watapo maliza mgogoro wao.
IPTL wamemaliza tofauti zao na BOT ikaamrishwa iwalipe sasa kashfa iko wapi.
Labda kama Tanzania tumezoea kutoheshimu mikataba na wawekezaji hasa kama sio kutoka nchi za magharibi.
Ilokua sakata la Richmond yalikua kama haya na kilicho fata ni yule mwarabu wa Oman alijua kasumba za wabongo alipotaka kuwauzia ile mitambo Tanesco kina Mwakyembe wakasema labda on my dead body .Alipotaka kuisafirisha nje TRA wakatiwa maneno ...Mwarabu akajua hawa adabu yao Wamarekani .
Basi ile mitambo ikauzwa kwa kampuni ya Marekani na ipo na sasa tunanunua umeme bukheeeri kabisa na mwarabu akachukua hela yake na huku Tanesco wakishindwa kesi ya kimataifa na ndani na kulazimishwa kulipa malipo wanayo daiwa na Dowans.
Na hili la IPTL lipo kama hilo isipikua ccm hawana msimamo na huwa hawana uwexo wa kukabiliana na malumbano na wenyewe wapo weak huingia mtegoni.

Before nlikuwa najua kama scenario ndio hii but after all the issue yakina Tibaijuka kusema wamewekewa pesa with no reason from BOT na ilikuwa inahusu mshiko wa IPTL that imeleta a lot of questions
 
Before nlikuwa najua kama scenario ndio hii but after all the issue yakina Tibaijuka kusema wamewekewa pesa with no reason from BOT na ilikuwa inahusu mshiko wa IPTL that imeleta a lot of questions
huyo mama kapewa hela na rugemalila ama iptl.
nasema hapa hamna kitu.hizi ni siasa mtaniambia
 
Ningewaona wa maana kama wangesema wanakwenda mahakamani kukata rufaa make suala hili limeamuliwa na mahakama kuu.

Hivi kwanini unatetea wezi? Hata kama kwa kiasi flani unanufaika na hii stystem ya mavampire lkn umezidi aisee.
 
Back
Top Bottom