Ipo Siku Atakufa Mtu Mkubwa!

Wa Busiya

JF-Expert Member
Dec 21, 2012
326
67
Kwa muda wa miaka mitatu sasa tangu tukio la kuuawa watu watatu kule Arusha imekuwa kawaida kusikia matukio ya mauaji huku watuhumiwa wakiwa ETI ni chadema. Nakumbuka wakati huo tbc1 waliandaa kipindi maalum wakituonyesha watanzania jinsi chadema walivyofanya uhalifu huo. MUNGU AEPUSHE MBALI!
Yakaja matukio ya Zanzibar, padre akapigwa risasi, sheikh akamwagiwa tindikali, makanisa yakachomwa moto kabla ya padri Mushi kuuawa kwa kupigwa risasi. Kisha mambo yakarudi bara na ikawa mchuano kati ya wakristo na waislam. halafu yakaingia kwenye siasa za ccm na chadema. Watu wakafa kwa kupigwa vitu vizito kichwani huku wengine wakipigwa mabomu yaliyosemekana kurushwa na wafuasi wa chadema na kufumua utumbo wa wahanga.

Mungu atusaidie! Matukio yote hayo yanabaki bila mtu hata mmoja aliyekamatwa na kufikishwa mbele ya sheria ukiacha DHAMBI mbaya ya kutaka kuwaaminisha watanzania kuwa matukio yote hayo yanafanya Rwakatare na CHADEMA. Hivi tutaangalia matukio mabaya yakitukia bila wahusika hadi lini? Dr ulimboka, mwangosi, katibu wa bakwata; nani mhusika?

Haya yakiachwa yaendelee kutokea huku wahusika wakifumbiwa macho kwa lengo la kupata ummarufu na kuwachafua wengine kisiasa tusishangae kusikia siku moja wale wanaodhani wanapanda mbegu njema kwao wakajikuta wanakumbana na mavuno ya kile walichokipanda.
 
Hapa ndipo utakuwa mwanzo wa machafuko.Hatuangalii mtu binafsi ila tunaangalia watu wanaomfuata(wafuasi).
 
Hapo arusha kaoswa koswa mwenyekiti wa chama..kiongozi wa upinzani...hii ni hatari kuliko mtu anavyoweza kufikiria..
 
Ccm hawataondoka madarakani kwa amani, mpaka tuuane kwanza ndo watatuona tuko serious na kutuheshimu. Vinginevyo tutarajie hayo mauaji yao yataendelea.
 
Mauaji yote yanayofanywa hayawagusi ccm moja kwa moja.
Subiri siku mwandamizi wao mmoja apatikane, huenda hatua serious zitaanza kuchukuliwa.
 
Kwa muda wa miaka mitatu sasa tangu tukio la kuuawa watu watatu kule Arusha imekuwa kawaida kusikia matukio ya mauaji huku watuhumiwa wakiwa ETI ni chadema. Nakumbuka wakati huo tbc1 waliandaa kipindi maalum wakituonyesha watanzania jinsi chadema walivyofanya uhalifu huo. MUNGU AEPUSHE MBALI!
Yakaja matukio ya Zanzibar, padre akapigwa risasi, sheikh akamwagiwa tindikali, makanisa yakachomwa moto kabla ya padri Mushi kuuawa kwa kupigwa risasi. Kisha mambo yakarudi bara na ikawa mchuano kati ya wakristo na waislam. halafu yakaingia kwenye siasa za ccm na chadema. Watu wakafa kwa kupigwa vitu vizito kichwani huku wengine wakipigwa mabomu yaliyosemekana kurushwa na wafuasi wa chadema na kufumua utumbo wa wahanga.

Mungu atusaidie! Matukio yote hayo yanabaki bila mtu hata mmoja aliyekamatwa na kufikishwa mbele ya sheria ukiacha DHAMBI mbaya ya kutaka kuwaaminisha watanzania kuwa matukio yote hayo yanafanya Rwakatare na CHADEMA. Hivi tutaangalia matukio mabaya yakitukia bila wahusika hadi lini? Dr ulimboka, mwangosi, katibu wa bakwata; nani mhusika?

Haya yakiachwa yaendelee kutokea huku wahusika wakifumbiwa macho kwa lengo la kupata ummarufu na kuwachafua wengine kisiasa tusishangae kusikia siku moja wale wanaodhani wanapanda mbegu njema kwao wakajikuta wanakumbana na mavuno ya kile walichokipanda.


Tunaambiwa kuwa kila mtu ataonja mauti na hao wakubwa ni watu, wacha ifike zamu yao!
 
Back
Top Bottom