"Kabla sijaokoka na kuwa Nabii nilikuwa Muislam, nilitoka kwenye Uislamu nikaja kwenye Ukristo kwa neema ya wokovu Mungu aliyonipa ndio maana naweza kuzungumza vizuri Lugha zote mbili kwa ufasaha (Uislamu na Ukristo) lakini kwa nia nzuri na siwezi kukashifu sehemu niliyotoka"
"Nimezaliwa kwenye Uislamu, wazazi wangu ni Waislamu, ndugu zangu ni Waislamu na nafahamika hivyo kwamba mimi nilikuwa kijana wa Kiislamu nimesoma dini na vyuo vya kiislamu wakati huo ambapo bado nilikuwa Muislam"
"Nakumbuka ilikuwa siku ya Ijumaa ambapo nilikuwa niko msikitini, wakati tunaswali swala ya Ijumaa wakati nimesema (Allah Akbar) nimeweka mikono kifuani, kuna kitu ambacho kilitokea nikiwa pale (Kbra) ambapo ulitokea mwanga mkubwa sana ulikuwa ni mwanga mkali kiasi kwamba nilishindwa kuuangalia hata kwa sekunde moja"
"Kwangu kilikuwa ni kitu cha ajabu kuwahi kutokea maishani mwangu, ghafla sauti ilianza kutoka kwenye ule mwanga ikawa inazungumza na mimi kwamba (Mimi nalikuwako kabla ya chochote kuwako, nalizaliwa, nalikuwako kama fundi staili wa kazi wa Mungu lakini Mungu alinituma nikaja nikaikamilisha kazi yangu hapa duniani na sasa niko mkono wa Kuume wa Mungu aliye hai naomba unitumikie, akataja jina langu".
"kwa mara ya kwanza nilianguka nikazimia kwasababu niliogopa sana, kanzu niliyokuwa nimevaa siku hiyo ililowa yote mpaka nguo za ndani nilizokuwa nimevaa zililowa, ndani ya mda mchache wakati naongea na huyo mtu wa ajabu, baadae nikajikuta niko pembeni nikawa naulizwa na watu ni nini kimenitokea, kwakweli sikuwaeleza kilichokuwa kimenitokea"
"Haikuishia hapo, akanitokea tena mara ya pili, hadi mara ya tano, na mara ya tano alinitokea nikiwa nyumbani chumbani akawa ananiambia maneno yaleyale aliyoniambia mwanzo kisha anapotea, nilikuwa napiga kelele sana mama alikuwa akiniuliza naogopa kumwambia, alivyonitokea mara ya sita nikapata wasiwasi zaidi nikaenda kuwashirikisha Masheikh wakiokuwa wananifundisha, hawakuamini wakasema atakuwa tu ni shetani maana Yesu alishakufa muda mrefu"
"Nilisomewa dua nyingi sana, walinisomea dua zote ambazo Masheikh wamejaliwa na Mungu, na mimi niliamini kuwa kutokana na zile dua yule jini anayenitokea na kujifanya ni Yesu asingenitokea tena, lakini niliporudi nyumbani ule mwaka ulinitokea tena ukawa unazungumza maneno yaleyale ya awali kwamba nimtumikie, niliwaza kwamba nikirudi kwa Masheikh kuwaeleza tena huu mkasa wakati waliniombea wangeniona mnafiki, niliona bora nijiue kuliko kuuacha Uislamu dini ya haki na kwenda kwenye Ukristo"
"Niliwaza kwamba nikijiua nitaenda kwa Allah kupumnzika kuliko kuwa Mkristo, sikuwahi kufikiria kama ningekuja kuwa Mkristo katika maisha yangu, kabla sijajiua nilimpigia simu rafiki yangu nikamwambia licha ya dua zote nilizoombewa lakini yule mtu amenitokea tena, rafiki yangu akaniambia kwamba ni bora nijiue kuliko kuwa Mkristo, maana adhabu ya kufa ukiwa Mkristo ni kukatwa kichwa siku ya kiama"
"Nikaenda kununua dawa za kujiua nikaziweka chumbani kwenye meza, nikaenda kuoga ili nijiandae kujiua, nilipotoka kuoaga ile naingia chumbani kunywa ile sumu ya vidonge nikakuta chumba chote kimebadilika rangi, alikuwa ni yule mtu akarudia maneno yaleyale kwamba nikamtumikie kwenye Ukristo, akaniambia sitakuacha wala sitakupungukia, kuanzia hapo nikaanza kumpenda nikasema nimekupokea moyoni mwangu kuwa bwana na mwokozi wangu"- amesema mtumishi wa Mungu, Isaac Paul ambaye ni Nabii IPM kwa sasa.
Isaac Paul Hammoud au Nabii IPM ni mtumishi wa Mungu ambaye awali alikuwa muumini mwenye itikadi kali ya Dini ya kiislamu lakini sasa ni Nabii.
Follow Aston John Carter
"Nimezaliwa kwenye Uislamu, wazazi wangu ni Waislamu, ndugu zangu ni Waislamu na nafahamika hivyo kwamba mimi nilikuwa kijana wa Kiislamu nimesoma dini na vyuo vya kiislamu wakati huo ambapo bado nilikuwa Muislam"
"Nakumbuka ilikuwa siku ya Ijumaa ambapo nilikuwa niko msikitini, wakati tunaswali swala ya Ijumaa wakati nimesema (Allah Akbar) nimeweka mikono kifuani, kuna kitu ambacho kilitokea nikiwa pale (Kbra) ambapo ulitokea mwanga mkubwa sana ulikuwa ni mwanga mkali kiasi kwamba nilishindwa kuuangalia hata kwa sekunde moja"
"Kwangu kilikuwa ni kitu cha ajabu kuwahi kutokea maishani mwangu, ghafla sauti ilianza kutoka kwenye ule mwanga ikawa inazungumza na mimi kwamba (Mimi nalikuwako kabla ya chochote kuwako, nalizaliwa, nalikuwako kama fundi staili wa kazi wa Mungu lakini Mungu alinituma nikaja nikaikamilisha kazi yangu hapa duniani na sasa niko mkono wa Kuume wa Mungu aliye hai naomba unitumikie, akataja jina langu".
"kwa mara ya kwanza nilianguka nikazimia kwasababu niliogopa sana, kanzu niliyokuwa nimevaa siku hiyo ililowa yote mpaka nguo za ndani nilizokuwa nimevaa zililowa, ndani ya mda mchache wakati naongea na huyo mtu wa ajabu, baadae nikajikuta niko pembeni nikawa naulizwa na watu ni nini kimenitokea, kwakweli sikuwaeleza kilichokuwa kimenitokea"
"Haikuishia hapo, akanitokea tena mara ya pili, hadi mara ya tano, na mara ya tano alinitokea nikiwa nyumbani chumbani akawa ananiambia maneno yaleyale aliyoniambia mwanzo kisha anapotea, nilikuwa napiga kelele sana mama alikuwa akiniuliza naogopa kumwambia, alivyonitokea mara ya sita nikapata wasiwasi zaidi nikaenda kuwashirikisha Masheikh wakiokuwa wananifundisha, hawakuamini wakasema atakuwa tu ni shetani maana Yesu alishakufa muda mrefu"
"Nilisomewa dua nyingi sana, walinisomea dua zote ambazo Masheikh wamejaliwa na Mungu, na mimi niliamini kuwa kutokana na zile dua yule jini anayenitokea na kujifanya ni Yesu asingenitokea tena, lakini niliporudi nyumbani ule mwaka ulinitokea tena ukawa unazungumza maneno yaleyale ya awali kwamba nimtumikie, niliwaza kwamba nikirudi kwa Masheikh kuwaeleza tena huu mkasa wakati waliniombea wangeniona mnafiki, niliona bora nijiue kuliko kuuacha Uislamu dini ya haki na kwenda kwenye Ukristo"
"Niliwaza kwamba nikijiua nitaenda kwa Allah kupumnzika kuliko kuwa Mkristo, sikuwahi kufikiria kama ningekuja kuwa Mkristo katika maisha yangu, kabla sijajiua nilimpigia simu rafiki yangu nikamwambia licha ya dua zote nilizoombewa lakini yule mtu amenitokea tena, rafiki yangu akaniambia kwamba ni bora nijiue kuliko kuwa Mkristo, maana adhabu ya kufa ukiwa Mkristo ni kukatwa kichwa siku ya kiama"
"Nikaenda kununua dawa za kujiua nikaziweka chumbani kwenye meza, nikaenda kuoga ili nijiandae kujiua, nilipotoka kuoaga ile naingia chumbani kunywa ile sumu ya vidonge nikakuta chumba chote kimebadilika rangi, alikuwa ni yule mtu akarudia maneno yaleyale kwamba nikamtumikie kwenye Ukristo, akaniambia sitakuacha wala sitakupungukia, kuanzia hapo nikaanza kumpenda nikasema nimekupokea moyoni mwangu kuwa bwana na mwokozi wangu"- amesema mtumishi wa Mungu, Isaac Paul ambaye ni Nabii IPM kwa sasa.
Isaac Paul Hammoud au Nabii IPM ni mtumishi wa Mungu ambaye awali alikuwa muumini mwenye itikadi kali ya Dini ya kiislamu lakini sasa ni Nabii.
Follow Aston John Carter