Ipi tafsiri sahihi ya madawa ya kulevya?

Ipi tafsiri sahihi ya madawa ya kulevya?

Bangi ni dawa ya kulevya. Na mara kadhaa watu wamekamatwa kwa kukutwa na bangi nchini. Ila ni dhahiri serikali haijatilia maanani kutekeleza sheria dhidi ya bangi na ndiyo maana imefika mahali bangi imeonekana kama siyo dawa ya kulevya kama dawa za kulevya zingine. Hatahivyo, kitabibu madhara ya bangi ni kidogo ukilinganisha na dawa nyingine za kulevya kama heroine na cocaine.

Dawa nyingine za kulevya ni opioids ambazo zinatumika mahospitalini kupunguza maumivu makali kama maumivu ya mwanamke kujifungua, au maumivu ya kung'oa jino, au kama sehemu ya matibabu ya cancer. Hapa nchini haifahamiki sana kwamba opioids zinatumika kwa mtu aliyeng'oa gego, lakini nchi zilizoendelea kama USA ni kawaida sana kwa mama anayejifungua au mtu anayeng'oa jino kupewa hizi dawa. Kwenye maduka ya madawa zinatambulika kama Oxycontin, Oxycodone, Percocet etc.

Kwa kifupi, hizi dawa za kulevya nyingi zina matumizi halali mahospitalini, tatizo ni pale zinapotumika nje ya ushauri wa daktari, kwa dozi kubwa zaidi, na kwa muda mrefu kwa malengo ya kujiburudisha kama mtu anavyovuta sigara au kunywa pombe kama sehemu ya burudani ya mwili. Hapo ndipo effect ya madawa ya kulevya inapoanzia.
 
Kwa hiyo maana yako, ina maana kuwa as long as gongo na pombe nyingine ambazo hazijathibitishwa na TFDA na TBS,basi hizo ni dawa za kulevya.
Sijasema pombe za kienyeji ni dawa za kulevya na zinakatazwa but kwa mujibu wa sheria ya Tanzania gongo ni haramu.Pombe za kienyeji sio dawa za kulevya
 
Mkuu wa mkoa ndie mgunduzi pekee duniani aliyegundua shisha ni dawa ya kulevya.labda lengo loote arukie na ugoro ili wamasai waandamane.
 
Hili swala linaipa taabu serikali ya Zambia,juzijuzi wamemkamata dada mmoja muuza ubani,amekula miaka thalathini.
 
Tutofautishe kulevya na haramu.
Ila nasikitika sana serikali kuruhusu viroba ila miaka nenda rudi wameitangaza Congo kama Haramu.
Gongo inahitaji Tu usimamizi na maelekezo jinsi ya kutengeneza kitaalum kuondoa uwezekano wa kutengeneza methanol. Idadi ya watu wanaotengeneza na kutumia gongo ni kubwa kuitwa haramu.... Meaning imekuwa social accepted.na madhara yake sio tofauti sana na pombe nyingine zilizoruhusiwa kisheria.
Unaingia kijijini, kila MTU kuanzia mwenyekiti wa kijiji, mtendaji na diwani km ni wa kijiji hicho wanajua linapouzwa gongo... Nao wanalitumia.... Ukifika kwa mama muuza unamkuta mganga/muuguzi wa zahanati ya kijiji, mwalimu...hakimu wa mahakama ya mwanzo... Wote wako wanaburudika.
Nawashangaa sana wabunge kutolisemea hili. Vinginevyo unafiki Tu.
 
Hivi madawa ya kulevya kwa mujibu wa sheria za nchi yetu ni nini hasa. Na ni wakati gani mtu anaweza ama hawezi kuwa na umiliki wa madawa hayo? Maana kwa mfano kama mtu anatumia majani ya Bangi kama Mboga ama mbegu zake kama kiungo cha mboga, je akikamatwa itakuwa amekamatwa na madawa ya kulevya ama mboga?

Hao watu wanaokamatwa na "madawa ya kulevya" huwa wanakamatwa na aina moja ya madawa. Ama wanaotajwa kuhusika na biashara hiyo wanauza aina moja ya madawa na wakikamatwa kosa huwa sawa kwa wote? Yaani kwa mfano anayekamatwa na Heroine na anayekamatwa na Bangi wote kosa lao huwekwa kwenye daraja moja kisheria?
Dawa za kulevya ni ambazo tuazi import kutoka Malaya huko kwa ajili ya kuwapigia waginjwa nusu kaputi, kwa hiyo ni dawa kama dawa nyingine zikitumika kwa wagonjwa unakuwa msaada ila zikitumika kwa vijana wazima zinaleta madhara

Hizo bangi mirungi, n.k za ki Africa hivyo ni viburudisho tu kama Pombe konyagi, burudani, banana n.k
 
Back
Top Bottom