Ipi nafasi ya Tanzania katika mgogoro wa Mashariki mwa Congo (DRC)?

Ipi nafasi ya Tanzania katika mgogoro wa Mashariki mwa Congo (DRC)?

covid 19

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2014
Posts
8,036
Reaction score
20,031
Kinachoendelea Mashariki mwa Congo DRC si mgogoro wa mbali kama wengi tunavyodhani. Huu ni mgogoro ambao hakuna nchi ya Afrika Mashariki itakayobaki salama. Kuna chaguo mbili tu: ama uwe sehemu ya mchezo na uchague upande, au ubaki mpweke kisha upokonywe hata kile kidogo ulichonacho.

Tukirudi nyuma kidogo, Tanzania haijawahi kuwa mgeni kwenye siasa na migogoro ya ukanda huu. Kwa muda mrefu jina la nchi yetu limetajwa kuhusishwa na kusaidia kuwapandisha madarakani baadhi ya viongozi wakuu wa eneo hili—kina Kagame, Museveni na wengineo. Hii peke yake inatosha kuthibitisha kuwa Tanzania ni mdau halisi wa kinachoendelea DRC, iwe tunapenda au hatupendi.

Kwa sasa hali inaonekana kama Tanzania imepunguza waziwazi ushiriki wake, au tuseme imechagua siasa ya ukimya. Hatueleweki tunavuta upande gani hasa:

- Upande wa (M23 + Rwanda + Uganda)

- au upande wa (Congo DRC + Burundi)

Kinachoonekana ni kwamba Tanzania inasaidia Congo na Burundi kwa tahadhari kubwa, huku ikimwogopa au kumuangalia Rwanda kwa jicho la kibiashara hasa kwa sababu Rwanda ni mdau mkubwa wa Bandari ya Dar es Salaam.

Kenya wao hawajifungi na upande wowote. Wapo pale kwa maslahi yao binafsi, biashara na ushawishi nothing else.

HATARI ILIYO MBELE YETU

Kama hali itaendelea hivi, kuna uwezekano mkubwa sana Tanzania ikajikuta iko chini ya ushawishi wa Rwanda huko mbeleni. Sio kwa vita ya moja kwa moja, bali kwa nguvu ya uchumi na masharti.

Mkakati wa Kagame uko wazi kwa anayefuatilia:

- Kupitia M23, Rwanda inameza mikoa ya Mashariki mwa Congo mkoa baada ya mkoa

- Ana silaha za kisasa, jeshi lililoandaliwa vizuri, na fedha nyingi

- Generali wa Congo wanahongwa waziwazi

- Maeneo yanayotekwa yanachimbwa rasilimali bila huruma

Mfano: kipindi Goma ilipotekwa, zaidi ya tani 300 za dhahabu ziliporwa hapo goma. Hii inaonyesha pesa zipo, na mpango ni mkubwa.

TARGET HALISI SI GOMA – NI HII:
Katanga – moyo wa migodi Africa mashariki

Lubumbashi – moyo wa biashara mashariki ya congo

Rwanda ikifanikiwa kufika Lubumbashi, hapo ndipo Tanzania itakapopoteza pakubwa sana. Kwa nini? Karibu nusu ya shehena ya Bandari ya Dar es Salaam inaelekea Congo kupitia Lubumbashi. Lubumbashi ikidhibitiwa na Rwanda/M23:

- Watadhibiti njia za biashara

- Wataweka masharti yao

- Tutahitaji pesa → tutalazimika kutii masharti yao

Hapo ndipo utawala wa kiuchumi unaanza, bila hata risasi moja kupigwa Dar es Salaam.

Kagame tayari:
Amejenga bandari kavu kubwa Kigali

Ameanzisha kiwanda cha kusafisha dhahabu

Kigali inajengwa kisasa isivyo kawaida Haya yote si bahati mbaya ni maandalizi ya jambo kubwa linalokuja.

Katika mazingira haya yote, Unafikiri Tanzania ifanye nini sasa?

Karibuni mchangie. Huu mjadala hauhitaji jazba, unahitaji akili, historia na ujasiri wa kusema ukweli.
 
Utawala haramu hauwezi kuona uchingu wa kupoteza nchi
Kikao cha magenerali wa Tanzania kimefunguliwa leo na Rais natamani sana jambo la Congo na nafasi yetu kwenye mgogoro huo lijadiliwe na litolewe maamuzi haraka.. bado tuna nafasi kubwa sana ya kuwa salama kama tutacheza kete zetu vyema.
 
Tanzania inawakati mgumu kwakua Kabila ambaye Bado anaushawishi Mkubwa kwenye Jeshi la Congo, Ameungana na Kagame ili ku mnyoosha Tsheshekedi.

Ni Mgogoro mkubwa wa siasa za ndani ya Nchi unaoleta majanga kwa Raia wa Kawaida.
Kwasasa Wazungu wanajiokotea tu
 
Tanzania inawakati mgumu kwakua Kabila ambaye Bado anaushawishi Mkubwa kwenye Jeshi la Congo, Ameungana na Kagame ili ku mnyoosha Tsheshekedi.

Ni Mgogoro mkubwa wa siasa za ndani ya Nchi unaoleta majanga kwa Raia wa Kawaida.
Kwasasa Wazungu wanajiokotea tu
Tena wanakusanya haswa.
 
Umewahi kumsikia kanali Nangaa akizungumza? Kiswahili chake ni ishara tosha alipata mafunzo huko kwenye kambi za kitanzania.

Silaha nyingi za hao m23 wanafadhiliwa na serikali ya Tz na hata maficho yao wengi hukumbilia Tz.

Msumbuji wakati ISIS wameingia jeshi la kwanza kutia maguu kusaidia ni la Tz baada ya kama wiki wakatelekeza vifaa vyote na magari kwa madai wamezidiwa.

Tz ilipeleka wanajeshi wake huko biafra miaka ya 60 huko ili kuigawanya Nigeria. Baada ya kushindwa kwa biafra ikaona iunde boko haram na viongozi wakubwa wa boko haram wapo Tz wanajificha.

Tz ndio ilituma magaidi kummaliza Abeid ili waimiliki znz miaka ya 70 huko.

Tz ndio ilifanya mipango ya west gate kule nairobi.

Tz ina historia ya kufadhili vikundi vya kigaidi barani africa kupitia serikali ya ccm.
 
Wakifika kibondo au kakonko wadau mliopo huko mnishtue plz

Nahitaji chuma kwa gharama yoyote!
 
Umewahi kumsikia kanali Nangaa akizungumza? Kiswahili chake ni ishara tosha alipata mafunzo huko kwenye kambi za kitanzania.

Silaha nyingi za hao m23 wanafadhiliwa na serikali ya Tz na hata maficho yao wengi hukumbilia Tz.

Msumbuji wakati ISIS wameingia jeshi la kwanza kutia maguu kusaidia ni la Tz baada ya kama wiki wakatelekeza vifaa vyote na magari kwa madai wamezidiwa.

Tz ilipeleka wanajeshi wake huko biafra miaka ya 60 huko ili kuigawanya Nigeria. Baada ya kushindwa kwa biafra ikaona iunde boko haram na viongozi wakubwa wa boko haram wapo Tz wanajificha.

Tz ndio ilituma magaidi kummaliza Abeid ili waimiliki znz miaka ya 70 huko.

Tz ndio ilifanya mipango ya west gate kule nairobi.

Tz ina historia ya kufadhili vikundi vya kigaidi barani africa kupitia serikali ya ccm.
acha utani mjuba
 
Kinachoendelea Mashariki mwa Congo DRC si mgogoro wa mbali kama wengi tunavyodhani. Huu ni mgogoro ambao hakuna nchi ya Afrika Mashariki itakayobaki salama. Kuna chaguo mbili tu: ama uwe sehemu ya mchezo na uchague upande, au ubaki mpweke kisha upokonywe hata kile kidogo ulichonacho.

Tukirudi nyuma kidogo, Tanzania haijawahi kuwa mgeni kwenye siasa na migogoro ya ukanda huu. Kwa muda mrefu jina la nchi yetu limetajwa kuhusishwa na kusaidia kuwapandisha madarakani baadhi ya viongozi wakuu wa eneo hili—kina Kagame, Museveni na wengineo. Hii peke yake inatosha kuthibitisha kuwa Tanzania ni mdau halisi wa kinachoendelea DRC, iwe tunapenda au hatupendi.

Kwa sasa hali inaonekana kama Tanzania imepunguza waziwazi ushiriki wake, au tuseme imechagua siasa ya ukimya. Hatueleweki tunavuta upande gani hasa:

- Upande wa (M23 + Rwanda + Uganda)

- au upande wa (Congo DRC + Burundi)

Kinachoonekana ni kwamba Tanzania inasaidia Congo na Burundi kwa tahadhari kubwa, huku ikimwogopa au kumuangalia Rwanda kwa jicho la kibiashara hasa kwa sababu Rwanda ni mdau mkubwa wa Bandari ya Dar es Salaam.

Kenya wao hawajifungi na upande wowote. Wapo pale kwa maslahi yao binafsi, biashara na ushawishi nothing else.

HATARI ILIYO MBELE YETU

Kama hali itaendelea hivi, kuna uwezekano mkubwa sana Tanzania ikajikuta iko chini ya ushawishi wa Rwanda huko mbeleni. Sio kwa vita ya moja kwa moja, bali kwa nguvu ya uchumi na masharti.

Mkakati wa Kagame uko wazi kwa anayefuatilia:

- Kupitia M23, Rwanda inameza mikoa ya Mashariki mwa Congo mkoa baada ya mkoa

- Ana silaha za kisasa, jeshi lililoandaliwa vizuri, na fedha nyingi

- Generali wa Congo wanahongwa waziwazi

- Maeneo yanayotekwa yanachimbwa rasilimali bila huruma

Mfano: kipindi Goma ilipotekwa, zaidi ya tani 300 za dhahabu ziliporwa hapo goma. Hii inaonyesha pesa zipo, na mpango ni mkubwa.

TARGET HALISI SI GOMA – NI HII:
Katanga – moyo wa migodi Africa mashariki

Lubumbashi – moyo wa biashara mashariki ya congo

Rwanda ikifanikiwa kufika Lubumbashi, hapo ndipo Tanzania itakapopoteza pakubwa sana. Kwa nini? Karibu nusu ya shehena ya Bandari ya Dar es Salaam inaelekea Congo kupitia Lubumbashi. Lubumbashi ikidhibitiwa na Rwanda/M23:

- Watadhibiti njia za biashara

- Wataweka masharti yao

- Tutahitaji pesa → tutalazimika kutii masharti yao

Hapo ndipo utawala wa kiuchumi unaanza, bila hata risasi moja kupigwa Dar es Salaam.

Kagame tayari:
Amejenga bandari kavu kubwa Kigali

Ameanzisha kiwanda cha kusafisha dhahabu

Kigali inajengwa kisasa isivyo kawaida Haya yote si bahati mbaya ni maandalizi ya jambo kubwa linalokuja.

Katika mazingira haya yote, Unafikiri Tanzania ifanye nini sasa?

Karibuni mchangie. Huu mjadala hauhitaji jazba, unahitaji akili, historia na ujasiri wa kusema ukweli.
Rais form 4 failure, TISS imejazwa uvccm, jeshini zimajaa division 0. Unafikiri tunaweza kuwa mkakati wowote kama taifa hapo?
 
We 're not safe any more, Tuache uzwazwa hakuna Mungu anaelinda Nchi. Kikubwa tujipange kimkakati vinginevyo tutashtuka ikiwa too late.
 
Huyo Rais
Kikao cha magenerali wa Tanzania kimefunguliwa leo na Rais natamani sana jambo la Congo na nafasi yetu kwenye mgogoro huo lijadiliwe na litolewe maamuzi haraka.. bado tuna nafasi kubwa sana ya kuwa salama kama tutacheza kete zetu vyema.
[/QUOTE Huyo Raisi wako ukimuuliza Ujiji, Shirati hipo Mkoa gani hawezi kukupa jibu sembuse aweze kuijua CONGO hipo Ukanda gani wa Afrika.
 
Bwana kagame aishie tu kukamata maeneo ya congo, kwa tz asifikirie wala kujaribu, tuko imara, tutamfurusha mpaka kigali
 
Kinachoendelea Mashariki mwa Congo DRC si mgogoro wa mbali kama wengi tunavyodhani. Huu ni mgogoro ambao hakuna nchi ya Afrika Mashariki itakayobaki salama. Kuna chaguo mbili tu: ama uwe sehemu ya mchezo na uchague upande, au ubaki mpweke kisha upokonywe hata kile kidogo ulichonacho.

Tukirudi nyuma kidogo, Tanzania haijawahi kuwa mgeni kwenye siasa na migogoro ya ukanda huu. Kwa muda mrefu jina la nchi yetu limetajwa kuhusishwa na kusaidia kuwapandisha madarakani baadhi ya viongozi wakuu wa eneo hili—kina Kagame, Museveni na wengineo. Hii peke yake inatosha kuthibitisha kuwa Tanzania ni mdau halisi wa kinachoendelea DRC, iwe tunapenda au hatupendi.

Kwa sasa hali inaonekana kama Tanzania imepunguza waziwazi ushiriki wake, au tuseme imechagua siasa ya ukimya. Hatueleweki tunavuta upande gani hasa:

- Upande wa (M23 + Rwanda + Uganda)

- au upande wa (Congo DRC + Burundi)

Kinachoonekana ni kwamba Tanzania inasaidia Congo na Burundi kwa tahadhari kubwa, huku ikimwogopa au kumuangalia Rwanda kwa jicho la kibiashara hasa kwa sababu Rwanda ni mdau mkubwa wa Bandari ya Dar es Salaam.

Kenya wao hawajifungi na upande wowote. Wapo pale kwa maslahi yao binafsi, biashara na ushawishi nothing else.

HATARI ILIYO MBELE YETU

Kama hali itaendelea hivi, kuna uwezekano mkubwa sana Tanzania ikajikuta iko chini ya ushawishi wa Rwanda huko mbeleni. Sio kwa vita ya moja kwa moja, bali kwa nguvu ya uchumi na masharti.

Mkakati wa Kagame uko wazi kwa anayefuatilia:

- Kupitia M23, Rwanda inameza mikoa ya Mashariki mwa Congo mkoa baada ya mkoa

- Ana silaha za kisasa, jeshi lililoandaliwa vizuri, na fedha nyingi

- Generali wa Congo wanahongwa waziwazi

- Maeneo yanayotekwa yanachimbwa rasilimali bila huruma

Mfano: kipindi Goma ilipotekwa, zaidi ya tani 300 za dhahabu ziliporwa hapo goma. Hii inaonyesha pesa zipo, na mpango ni mkubwa.

TARGET HALISI SI GOMA – NI HII:
Katanga – moyo wa migodi Africa mashariki

Lubumbashi – moyo wa biashara mashariki ya congo

Rwanda ikifanikiwa kufika Lubumbashi, hapo ndipo Tanzania itakapopoteza pakubwa sana. Kwa nini? Karibu nusu ya shehena ya Bandari ya Dar es Salaam inaelekea Congo kupitia Lubumbashi. Lubumbashi ikidhibitiwa na Rwanda/M23:

- Watadhibiti njia za biashara

- Wataweka masharti yao

- Tutahitaji pesa → tutalazimika kutii masharti yao

Hapo ndipo utawala wa kiuchumi unaanza, bila hata risasi moja kupigwa Dar es Salaam.

Kagame tayari:
Amejenga bandari kavu kubwa Kigali

Ameanzisha kiwanda cha kusafisha dhahabu

Kigali inajengwa kisasa isivyo kawaida Haya yote si bahati mbaya ni maandalizi ya jambo kubwa linalokuja.

Katika mazingira haya yote, Unafikiri Tanzania ifanye nini sasa?

Karibuni mchangie. Huu mjadala hauhitaji jazba, unahitaji akili, historia na ujasiri wa kusema ukweli.
Juzi tu mlifukuzwa na M23 huko Drc au umesahau..?
 
Back
Top Bottom