Interview with President Joseph Kabila Kabange in Namibia

Interview with President Joseph Kabila Kabange in Namibia

Bagamoyo

Platinum Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
29,877
Reaction score
34,037
March 2025
Windhoek, Namibia

EXCLUSIVE MAHOJIANO : NA JOSEPH KABILA RAIS MSTAAFU WA CONGO DR

View: https://m.youtube.com/watch?v=kX6AYffI1Hc

Kama Mwandishi nataka kufahamu Baada ya miaka 18 ya kutumika kama rais wa DR Congo na baadaye kustaafu, mh. Joseph Kabila umepotea sana je nini kinaendelea?

Ndugu mwandishi - Nipo mzima napumua kama unavyoniona na ninaendelea na masomo ..

Mheshimiwa umesema umekuwa una harakati za kichuo ktk chuo kikuu cha University of Johannesburg ....

Bwana Mwandishi, Ni kweli nilikuwa katika harakati za kisomi, lakini nimekatisha masomo miezi mitatu iliyopita... kwa kuwa Congo siyo mazuri na katika hili siwezi kuwa mtu mshika yote (multitasking) kama mambo mazito nyeti kama masomo... na pia kufuatilia mambo ya nyumbani Congo ...

Hivyo (Joseph Kabila) nimechukua likizo ya kusitisha masomo ili nguvu zote ziende katika suala la Congo na chama cha siasa ambacho nakiongoza ..

Lakini mheshimiwa mwaka 2008 wewe ulikuwa mtu muhimu ulioanzisha makubaliano maridhiano ili usalama upatikane ..

Ni kweli nilishiriki moja kwa moja michakato ya Zambia mwaka 2001, mazungumzo ya Sun City South Africa 2006 na pia 2008 kuhusu ushirikishwaji, haki za wakongomani wote ... lakini kwa jinsi tunavyoongea leo 2025 kuna mikono ya wadau wengi inayoingilia tatizo la Congo ...

Kuondolewa kwa majeshi ya kigeni kama SADC SAMIDR nchini Congo mheshimiwa rais una neno la kusema mwaka 2025...

Ndigu mwandishi ni kweli kuondolewa kwa majeshi ni muhimu, maana hata mwaka 2001 nikiwa vijana na wenzangu tulijitosa kichwa kichwa pengine kwa ujana wetu tukafanikiwa kufanya maamuzi magumu ..

Ndugu mwandishi Lakini leo 2025 tumerudi katika changamoto ile ile ya 2001 ya kuondoa majeshi ya kigeni 7 yaliyopo Congo... mamluki wa kutoka ulaya pia makundi ya mgambo wa kicongomani yanayozidi 100 hivyo unaona hali ilivyo mbaya ...

Na ndugu mwandishi majeshi ya kigeni yakiondolewa ndiyo tutajua nia njema ya makundi ya wakongomani kama kweli wanataka amani... hali ilivyo ni mbaya na inaelekea katika hatari kubwa ... hivyo inaelekea itabidi tutoe mchango wetu kuzuia tusikfikie hatari iliyopo mbele..

Ndugu mwandishi hakuna mtu kutoka nje anayejua muarubaini wa matatizo ya Congo kama wakongomani wote, hivyo ni jukumu letu wakongomani kutunza sovereignty (mipaka)ya nchi yetu ..


Mheshimiwa rais baada ya miaka 35 kuwepo katika siasa na mambo ya kiinchi, unaweza kutuambia nini kuhusu wewe siku za mbeleni zinazokuja ?

Ndugu mwandishi kuhusu siku zijazo ni mwenyezi Mungu ndiyo anajua, kweli nimepata uelewa, ujuzi na hekima na bado nina nguvu zimebaki kidogo hivyo sijui nitatumika vipi ... Ni hayo tu.

Source : Patient Sayiba Tambwe
 
March 2025

Rais wa DRC Felix Tshisekedi amshutumu Rais Joseph Kabila kwa kufadhili waasi wa M23


View: https://m.youtube.com/watch?v=3DuuAcAO4AI
imeripotiwa kuwa maafisa wa chama cha Rais wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Joseph Kabila, wameitwa kufika mbele ya mwendesha mashtaka wa kijeshi Jumatatu.

Hatua hiyo inajiri huku waasi wa M23 wakisonga mbele kupitia maeneo muhimu ya maeneo ya mashariki mwa DRC.

Mwandishi wa VOA Esther Githui-Ewart alizungumza na Hubert Kabasu Babu Katulondi, Gavana wa zamani wa jimbo la Kasai katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kuhusu matukio ya hivi majuzi ya kisiasa na machafuko ambayo yanasababishwa na mzozo wa Kasai..
Source : VOA Africa
 
MWANDISHI AZUNGUMZIA UHUSIKA WA UBEBERU WA NCHI ZA KIAFRIKA KATIKA CONGO

View: https://m.youtube.com/watch?v=72Nw5RWXAwU

Mwandishi anasema Afrika ina nchi zinazo sifa za kibeberu kama nchi zingine za bara ulaya na Marekani ya Kaskazini

Mwandishi anataja mataifa beberu ya kiAfrika ni South Africa, Uganda, Tanzania, Rwanda na Kenya ni mataifa yanayojiingiza katika mambo ya ndani ya Congo kwa kuingiza majeshi yao ya kigeni.

Mataifa hayo tajwa ya kiafrika yakiwa na vimelea vya kibeberu kunufaika na madini kama dhahabu na madini adimu ya thamani ya kimkakati kwa manufaa ya mataifa yao.

Ndiyo maana mgogoro Congo hauishi anakazia mwandishi. Akikingia kifua hoja yake kuwa Congo ina askari 150,000 huku mataifa ya kibeberu vamizi ya kutoka Kenya, Tanzania, Uganda, Rwanda, South Africa mengine kwa kivuli cha EAC / SAMIDRC / SADC na MUNOSCO yanashindwaje kwa kuwepo kwao wote Congo kumaliza vikundi vya waasi nchini Congo anahoji mwandishi ?


Mwandishi Hubert Kasabu Nabu Katulondi aliyepata kuwa gavana wa jimbo la Kasai nchini Congo DR msomi wa chuo kikuu cha Lubumbashi University na degree ya pili MA ya Sayansi ya siasa
 
Kanisa, Dola na ukoloni Kusini Mashariki mwa Congo (1890 - 1962)


View: https://m.youtube.com/watch?v=w-NAQ85YuTM

Mgogoro mkubwa kati ya Sultani wa Zanzibar na mfalme Leopold wa Ubelgiji.
1742174754762.png


Ambapo dola ya Zanzibar Kubwa ilikuwa tayari imeota mizizi yake huko Kongolo kabla ya mfalme wa Belgium kugawiwa pande kubwa la bara la Afrika ambapo Kongolo ilikuwamo mwaka 1884 kufuatia mkutano wa mabeberu wa Berlin Ujerumani kugaewiana makoloni.

Himaya ya mji wa Kongolo katika jimbo la Tannganyika magharibi ya mto Luabala nchini Congo

Hivyo yanayoonekana leo ni muendelezo wa mgongano wa maslahi ulioanza miaka 130 iliyopita mwanahistoria anasimulia ...
 
18 March 2025
Johannesburg
Houghton, Gauteng
South Africa

DRC Kabila | Marais wa zamani Mbeki na Kabila wafanya mazungumzo mjini Johannesburg



View: https://m.youtube.com/watch?v=7h58P9RuD1E

Rais wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia Congo - DRC Joseph Kabila alikutana na Rais wa zamani wa Afrika Kusini Thabo Mbeki mjini Johannesburg Jumanne mchana.

Haya yanajiri huku hali katika eneo la mashariki mwa DRC ikiwa si shwari baada ya vuguvugu la M23 kutangaza kuwa hawatashiriki mazungumzo hayo yanayolenga kutafuta suluhu la kudumu la mzozo uliopo.

Wengi wametoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kusukuma pande zinazozozana kushiriki katika meza ya mazungumzo ya kutafuta amani na maridhiano yatakayopelekea kusitishwa kwa mapigano.

Kwa zaidi kuhusu mazungumzo hebu tuende kwa Mhariri wa Kimataifa wa Habari wa SABC, Sophie Mokoena akichambua mazungumzo ...
Source : SABC News
 
21 March 2025

How DRC was Captured for Power & Mineral Wealth | Dr Kibiswa..


View: https://m.youtube.com/watch?v=S4pSWVyW3uk
Dr. Naupess K . Kibiswa is a 2014 PhD graduate in Conflict Analysis and Resolution from Nova Southeastern University, Davie, FL, 2004 Master in Peace and Justice Studies at the University of San Diego (USD), CA, and Professeur Associé in the Facultés des Sciences Politiques and Droit at the Université Catholique du Congo (UCC),Université Catholique de Bukavu (UCB), the Institut Supérieur de Techniques Médicales de Kinshasa (ISTM-Kin), and the School of Electoral Training of Central Africa (EFEAC) in the DRCongo (DRC).
 
February 2025

Congo Conflict Explained | Paul Kagame's Role in destabilizing the DRC


View: https://m.youtube.com/watch?v=f4M0pz3biaY
Yahunde Batakane a filmmaker, Graphic Designer, Researcher and Author was born in Goma, a tourist town in the Eastern DR Congo, where he completed primary and secondary education, he then moved to Kenya when he was a teenager.
 
Ndugu mwandishi kuhusu siku zijazo ni mwenyezi Mungu ndiyo anajua, kweli nimepata uelewa, ujuzi na hekima na bado nina nguvu zimebaki kidogo hivyo sijui nitatumika vipi ... Ni hayo tu.

15 Aprili 2025
Goma, Nord Kivu
DR Congo

DR Congo : Joseph Kabila athibitisha atarejea Congo hivi karibuni


View: https://m.youtube.com/watch?v=FcH5R5Dyn08

Na ataelekea mjini Goma jimbo la Kivu ya Kaskazini lililopo Mashariki ya Congo walipo M23 na siyo mji mkuu wa Kinshasa taarifa za ndani zimedokeza kufuatia rais huyo wa zamani Joseph Kabila kutangaza kurejea kwake.

Jimbo hilo la Kivu ya Kaskazini linapakana na Rwanda nchini mojawapo inayoshutumiwa kuwa kuisaidia M23

Hali hiyo mpya imekuwa gumzo, katika media za ndani ya Congo na diaspora ya waKongomani pande zote za ulimwengu.

Haijajulikana kama rais huyo wa zamani Joseph Kabila atajiunga na kina Corneille Nangaa kuelekea hadi Kinshasa kurudia historia ya vuguvugu la Mzee Laurent Kabila aliyetia msukumo wa kutoka Mashariki ya Congo hadi Kinshasa na kumtoa madarakani rais Mobutu Sese Seko au Joseph Kabila ataamua safari hii awe chachu ya kuwezesha mazungumzo badala ya vuguvugu la Mapinduzi kupeleka Kinshasa kijeshi.
 
16 April 2025
wafuasi wa UDPS kuhusu hatua ya kurudi nyumbani kwa Rais wa zamani Joseph Kabila .


View: https://m.youtube.com/watch?v=9gzILmy9O6Y

UDPS ni chama cha siasa cha Umoja wa Demokrasia na Maendeleo ya Jamii.

Muungano wa Demokrasia na Maendeleo ya Kijamii UDPS ni chama kikuu cha kisiasa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo UDPS (Union pour la Démocratie et le Progrès Social) muasisi wake ni mkongwe Étienne Tshisekedi baba wa rais Felix Tshisekedi.

Chama kilichoanzishwa mwaka 1982, huku kukiwa na utawala wa chama kimoja cha Mobutu Sese Seko na chama chake maarufu cha Vuguvugu la Mapinduzi MPR , ndicho chama kikongwe zaidi nchini Congo.
 
21 April 2025
Goma Nord Kivu
DR Congo

Kurudi kwa Joseph Kabila kunazua hisia tofauti kwa maoni ya umma
Goma: Kurudi kwa Joseph Kabila kunazua hisia tofauti kwa maoni ya umma
Photo : Rais wa zamani Joseph K. Kabila

Aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Joseph Kabila Kabange, alirejea kwa njia ya kushangaza Ijumaa hii, Aprili 18, 2025 huko Goma, mashariki mwa nchi. Njia yake, kupitia Kigali (Rwanda), haikukosa kufufua uvumi na mivutano ya kisiasa huko Kinshasa, mji mkuu wa Kongo, na pia ndani ya nchi.

Joseph Kabila, ambaye yuko Afrika ya kusini tangu 2024, alitangaza nia yake ya kurejea Aprili 8, 2025 akitaja katika taarifa “kuzorota kwa usalama” na “hali ya wasiwasi ya taasisi.” Kisha akataja kwamba alitaka kuanza ziara yake mashariki mwa nchi, “kwa sababu kuna hatari huko.”

Kurejea kwake kunakuja huku jeshi la Kongo (FARDC) likiendelea kupambana na waasi wa M23, ambao sasa wamejumuishwa ndani ya Muungano wa Mto Congo (AFC). Katika muktadha huu, athari ni kali na imegawanyika.

Wasiwasi katika asasi za kiraia
Kwa Marion Ngavho, kiongozi wa mashirika ya kiraia katika Kivu Kaskazini, uwepo wa Kabila huko Goma ni muhimu:
“Joseph Kabila ni mwanasiasa mwenye heshima na msomi wa Kongo. Ninaamini kuwa hawezi tu kuwa mhusika mkuu katika vita dhidi ya M23, lakini pia mpinzani mkuu wa utawala mbovu wa utawala wa sasa.”
Sauti zingine ni za tahadhari zaidi, hata za kukosoa, zikilaani kurejea kwa malengo yasiyo wazi katika muktadha wa kulipuka. Mashirika ya kiraia yanahofia makabiliano ya wazi kati ya marais wa zamani na wa sasa.

PPRD ilitia aibu
Chama cha Raia ili Kujenga na Demokarasia (PPRD), chama cha kisiasa cha Joseph Kabila, kinaonekana kushangazwa.
“Hatujui kama yuko Goma au la. Na kama ni hivyo, inamhusu yeye binafsi tu, si PPRD,” alijibu Marc Musafiri, katibu mtendaji wa chama huko Kivu Kaskazini.
Kauli inayoakisi kutokuwa na uhakika fulani ndani ya chama cha siasa kilichoanzishwa na Kabila, ambacho kilisherehekea miaka 23 hivi karibuni.


Shutuma nzito kutoka Kinshasa
Mwezi Februari 2025 mjini Munich, Rais wa Kongo Félix Tshisekedi alimshutumu Joseph Kabila kwa kuwa “mfadhili” wa upinzani wenye silaha unaoungwa mkono na Rwanda. Nadharia iliyowasilishwa na Jean-Pierre Bemba, Waziri wa zamani wa Ulinzi, ambaye anaahidi kufichua ushahidi.

Jina la Eric Nkuba Shebandu, karibu na Corneille Nangaa na mshauri wa kimkakati wa AFC, pia linakuja. Corneille Nangaa ni mkuu wa Muungano wa Mto Kongo AFC , vuguvugu la kisiasa na kijeshi ambalo kundi lenye silaha la M23 linashirikiana nalo, ambalo sasa linadhibiti miji mikuu ya majimbo ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini, mashariki mwa Kongo, eneo lenye utajiri mkubwa wa madini.
Alipokamatwa na FARDC mnamo Aprili 2024, inasemekana alimtaja Kabila miongoni mwa mawasiliano ya kijeshi ya vuguvugu la waasi.

Mkakati hatari wa kurudi?
Kwa waangalizi wengi, uchaguzi wa kupitia Kigali, Rwanda mji mkuu wa nchi inayotuhumiwa kuingilia kijeshi nchini DRC, unazua maswali. Je, kiongozi wa zamani wa nchi anawezaje kuchukua njia kama hiyo, wakati ambapo maoni ya Wakongo yangali yanaangaziwa na ukatili unaofanywa mashariki mwa nchi hiyo?

Kuelekea kurudi kisiasa?
Huku nyuma, kurejea kwa Joseph Kabila kunaweza kuashiria mwanzo wa dhamira mpya ya kisiasa, wakati chama chake kikijaribu kurejesha nafasi katika uwanja wa kitaifa. Lakini mandhari ya Kongo imebadilika, na ardhi sasa ni ngumu zaidi, imegawanyika zaidi, na chini ya mvutano.

Katika hafla ya hadhara mjini Johannesburg mwezi Machi mwaka jana 2024, rais huyo wa zamani alikanusha uhusiano wowote na M23, akiziita tuhuma dhidi yake “hazina msingi” na akitaka “suluhisho la Kongo kwa matatizo ya Kongo.”
Mwitikio wa serikali

Jumamosi hii, Aprili 19,2025 msemaji wa serikali ya Kongo, Patrick Muyaya, alijibu kutoka Kinshasa:
“Kurejea kwa Bw. Joseph Kabila, katika muktadha huu, ni ukweli mkubwa wa kisiasa. Lakini tunakukumbusha kwamba hakuna mtu aliye juu ya sheria. Ikiwa kuna ushahidi wa kuanzisha uhusiano na makundi yenye silaha, mfumo wa haki utafanya kazi yake.”
Tangazo ambalo linaonyesha kuwa mamlaka inafuatilia kwa karibu kila hatua ya rais huyo wa zamani.
Inabakia kuonekana ikiwa kurejea kwake kutachangia kutuliza hali au kuchochea zaidi mvutano katika nchi ambayo bado imegubikwa na mizozo ya kivita na sintofahamu ya kisiasa.

View: https://m.youtube.com/watch?v=E7ecCRaPFjc
 
Wakati huo huo, serikali ya Kinshasa imetoa tangazo la kupiga marufuku chama cha Joseph K. Kabila, na kutoa tangazo kwa umma kupiga marufuku shughuli za kisiasa za chama cha PPRD :

Ushirikiano wa Kabila na washirika wake dhidi ya DRC: Shughuli za chama chake cha PPRD zimesitishwa katika eneo lote la taifa (Uamuzi wa Wizara ya Mambo ya Ndani​

-
Aprili 20, 2025


IMG-20250420-WA0004.jpg
 
Matangazo mazito ya serikali ya Kinshasa kufuatia kurejea kwa Joseph Kabila huko Goma baada ya kuishi uhamishoni Afrika ya Kusini :

Waziri wa mambo ya ndani wa DR Congo mheshimiwa Constant Mutamba atoa tangazo (communique) kwa umma


Washirika wa Rwanda na vibaraka wake wa M23: Constant Mutamba aamuru kesi za kisheria zichukuliwe dhidi ya Joseph Kabila na washirika wake wote wa karibu (taarifa kwa vyombo vya habari)​

Na
Aprili 20, 2025


IMG-20250420-WA0000.jpg
 
23 May 2025

HOTUBA YA RAIS WA ZAMANI WA DR CONGO JOSEPH KABILA KWA TAIFA


View: https://m.youtube.com/watch?v=rEa5V7W8XCs

Wapendwa raia wa nchi, miaka sita iliyopita nilichukua hatua ya kungatuka, kitendo cha kihistoria ktk taifa letu lililoweza kufanya na mkuu wa nchi toka taifa letu kupata uhuru

Tangu hapo nimekuwa katika hali ya ustaarabu kukaa kimya licha ya matukio ya kujikashifu, kunishambulia kwa uchokozi lakini nilistahimili.

Lakini leo nachuchukua hatua kujibu matukio yote ya kunishambulia kwa kila hali... nimeamua kuvunja ukimya ili kuokoa raia zaidi ya 100 milioni wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ..

Wapendwa wananchi nchi yetu ya DR Congo ipo eneo la kimkakati la kikanda ...
.
Kwa ufupi Katika hotuba:
iliyotangazwa moja kwa moja kwenye YouTube, Joseph Kabila anatoa uchambuzi wa kina wa hali ya sasa nchini DRC na anapendekeza ramani ya njia (Road map) ya kuiondoa nchi katika mgogoro huo.

Miaka sita baada ya kuondoka madarakani, Joseph Kabila anatoa taswira ya hali mbaya ilivyo nchini DRC.

Kulingana na Joseph Kabila , kwa sasa nchi hiyo "ni kama mgonjwa aliye mahututi , na hivyo ni muhimu ushauri wake ukazingatiwa kuliokoa taifa."

Rais wa zamani Joseph Kabila analaani kwa nguvu zote kile anachokiita "utawala usio wa kawaida" chini ya utawala wa mrithi wake aliyepo Kinshasa , rais Félix Tshisekedi.

Miongoni mwa matatizo anayobainisha rais wa zamani Joseph Kabila katika hotuba kwa taifa ni tatizo sugu la rushwa, ubadhirifu wa fedha za umma, na mtafaruku wa kimabavu ambapo "mapenzi ya Mkuu wa Nchi wa sasa Felix Tshisekedi yanachukua nafasi ya katiba ikiyotakiwa kuheshimiwa kama sheria kuu"


Matokeo hasi ya utawala huu wa Felix Tshisekedi , kwa mujibu wa Joseph Kabila, ni makubwa: ukosefu wa ajira, malimbikizo ya mishahara ambayo hayajalipwa, kushuka kwa viwango vya maisha, kuhama vijijini, uhalifu mijini, njaa n.k.

Katika nyanja ya usalama, rais wa zamani Joseph Kabila alishutumu kuongezeka kwa ukosefu wa usalama katika majimbo ya Kivu Kaskazini, Kivu Kusini, Ituri na Mai-Ndombe, ambayo alihusisha na "utawala mbaya wa Kinshasa".

Wito wa mapatano ya raia kwa suluhisho la kimataifa
Akiwa amekabiliwa na kile anachoelezea kama mgogoro wa "kina na wa pande nyingi", Joseph Kabila anapendekeza "mkataba na raia" unaozingatia mambo kumi na mawili muhimu.

Kulingana na rais wa zamani Jospeh Kabila , mapatano haya yatalenga kurejesha utulivu, demokrasia na maendeleo nchini DRC. Hapa kuna hatua kuu za mabadikiko anazopendekeza:
  1. Kumaliza udikteta
  2. Kusitisha vita;
  3. Kurejesha mamlaka ya Serikali katika eneo lote la kitaifa;
  4. Kurejesha demokrasia kwa kurejea katika misingi ya utawala wa kweli bora wa sheria;
  5. Kurejesha uhuru wa kimsingi;
  6. Kupatanisha Wakongomani wote na kujenga upya uwiano wa kitaifa;
  7. Kuzindua upya maendeleo ya nchi kwa kuanzisha utawala bora wa uchumi, usimamizi halisi wa utawala na fedha, na mgawanyo wa haki wa rasilimali za taifa.
  8. Kuanzisha tena mazungumzo ya dhati na ya kudumu na nchi zote jirani, kwa nia ya kuweka amani na maendeleo ya kudumu katika eneo hili;
  9. Kurejesha uaminifu wa nchi na washirika, katika ngazi za kikanda, bara na kimataifa;
  10. Kuondosha vikundi vyote vya kijeshi vya kitaifa na vya kigeni na kuwarudisha katika nchi zao za asili;
  11. Kukomesha kabisa tabia ya matumizi na kukimbilia kuajiri au kualika mamluki wa kijeshi,
Anapendejezakuondolewa mara moja kwa wanajeshi wote wa kigeni kutoka eneo la kitaifa.


Joseph Kabila anahitimisha kwa kutoa wito wa uhamasishaji wa kitaifa "kuokoa nchi." Hotuba hii inakuja katika hali ya mvutano wa kisiasa na kimahakama, huku mfumo wa sheria wa kijeshi ukijiandaa kuchunguza tuhuma nzito zinazoletwa dhidi yake, hususan madai ya uhusiano wake na waasi wa M23, wanaoungwa mkono na Rwanda.

Imetolewa leo siku Vendredi 23 Mai 2025

1748109632454.jpeg
 
15 June 2025
Washington DC

MJUMBE WA RAIS WA ZAMANI JOSEPH KABILA KUELEKEA WASHINGTON KWA MAZUNGUMZO YA AMANI

View: https://m.youtube.com/watch?v=bC9oks7Jh88
Video maktaba: Prof. Kikaya Bin Karubi

According to Jeune Afrique, while delegates from Kinshasa and Kigali are traveling to Washington to negotiate a US peace plan, Joseph Kabila, former president of the DRC, is also seeking to make his voice heard. He has appointed his close collaborator Kikaya Bin Karubi to represent him.In Washington, Kikaya plans to meet with members of Congress and the National Security Council to advocate for Kabila's return and his intentions to end "Tshisekedi's tyranny."

Balozi mstaafu Prof. Kikaya Bin Karubi ametumwa kama mjumbe maalum wa Joseph Kabage Kabila kuelekea Washington kwa mazungumzo ya kuleta Amani nchini Congo.

Prof. Kikaya Bin Karubi amewahi kuwa balozi wa DR Congo nchini Zimbabwe, n.k waziri wa zamani, mhadhiri vyuo vikuu Johannesburg na Kinshasa na mshauri wa rais wakati wa utawala wa rais Joseph Kabange Kabila pia CEO wa African Desk

Balozi Prof. Kikaya Bin Karubi

TOKA MAKTABA :
16 Dec 2023
Reception in honor of Ambassador Kikaya Bin Karubi at African Desk HQ in Dar-es-salaam, Tanzania.


View: https://m.youtube.com/watch?v=eO9l1L-9X0s

img

Chief Executive Officer

PROF BARNABE KIKAYA BIN KARUBI​

Prof Barnabe Kikaya is Distinguished Research Associate in the Centre for African Diplomacy and Leadership (CADL) at the University of Johannesburg. And Professor of Strategic Communication at the University of Kinshasa. He holds a Ph. D from Boston University in the US.

Diversity of Experiences​


A former DRC Ambassador to Zimbabwe and the UK, he was Presidential Diplomatic.
Advisor between 2015-2018, and the President’s Special Assistant from 2004-2006.
He was one of the lead negotiators during the Sun City negotiations in 2001. Prof Kikaya is a former Editor-in-Chief of the French Service of Channel Africa for the SABC.
Prof Kikaya is an accomplished advisor, strategist and consultant, and prolific publisher
 
Jean-Pierre Bemba Gombo atoa tuhuma nzito katika mahojiano


View: https://m.youtube.com/watch?v=7VLj3y_luu8

Jean-Pierre Bemba Gombo atoa tuhuma nzito dhidi ya rais wa zamani Joseph Kabila na Katumbi Moise Seriano gavana wa Katanga kuwa ...

Wanamipango ya kufanya nchi isitawalike pia wanahusika na njama za kupindua serikali ya Kinshasa ya rais Felix Tshisekedi ..

Jean-Pierre Bemba Gombo anadai kuwa rais wa zamani Joseph Kabila siyo mtoto wa kibaolojia wa Mzee Laurent Desire Kabila .... Jean-Pierre Bemba Gmbo abanwa athibitishe madai hayo na mwandishi makini anayotoa ktk mahojiano exclusive ...

Pia Jean-Pierre Bemba Gombo anadai kuwa Mzee Laurent Desire Kabila alijitangaza kibabe yaani kuchujya madaraka ya urais akiwa Lubumbashi kinyume na .... watawala wa Kigali ambao walikuwa na mawazo kuwa ....

Jean-Pierre Bemba Gombo anadai Rwanda ilikuwa ina mipango ya kuigawa (balkanization) Congo kikanda, lakini mzee Laurent Kabila alikuwa anataka Congo ibaki nzima moja ..

Jean-Pierre Bemba Gombo anazidi kudai kuwa AFC / M23 wanafadhiliwa na Joseph Kabila ..

Jean-Pierre Bemba Gombo anadai Congo ni moja na kamwe haiwezi kuwa watumwa wa Joseph Kabila kikaragosi wa Rwanda ..

Jean-Pierre Bemba Gombo kuwa kuna idiolojia ya kusambaza uwongo ..

Jean-Pierre Bemba Gombo wakongomani lazima waambiwe ukweli juu ya Joseph Kabila, Moise Katumbi .... walitaka kuingilia website ya Tume ya Uchaguzi kupindua matokeo ya uchaguzi uliopita nchini (Congo) ...lakini mkuu wa nchi alipofahamishwa alichukua hatua za haraka kuzuia website ya Tume kudukuliwa ...

Jean-Pierre Bemba Gombo anaongeza udukuzi hio uliopozuiwa Moise Katumbi akakimbia nchi kupitia ziwa Tanganyika akaingia nchini Zambia ...

Jean-Pierre Bemba Gombo anadai kanisa Catholic nalo halikufurahi pale rais Felix Tshikesedi alivyoamua elimu bure kwa wote, maana kanisa lilikuwa linapata pesa nyingi kutoza wanafunzi ... kanisa na cardinal hawakufurahi

Jean-Pierre Bemba Gombo anasema rais Felix Tshisekedi ndiyo shujaa wa taifa , kwa kusimama kupinga ubeberu wa Rwanda ..

Jean-Pierre Bemba Gombo kuhusu mapendekezo ya maridhiano na AFC / M23 ni ngumu maana waasi wanapitia kwanza Kigali kupata ushauri hivyo siyo wazalendo...

Jean-Pierre Bemba Gombo kuhusu bajeti ya kijeshi kupungua huku majimbo ya Kivu ya Kaskazani na Kivu Kusini ni maamuzi ya rais pengine kutoa mwanya wa njia ya kidiplomasia itumike ... badala ya vita dhidi ya AFC / M23
 
Back
Top Bottom