mlaizer
JF-Expert Member
- Jan 31, 2011
- 233
- 41
ukiwa na pesa nyingi ni dhambi?Wakili maarufu jijini Arusha, anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kukutwa na kiasi kikubwa cha fedha kwenye akiba yake binafsi, zinazodaiwa kuingia kwa njia isiyo halali. Wakili huyo aliyejijengea umaarufu nchini kutokana na uendeshaji kesi zake, anadaiwa kukamatwa Agosti 2, mwaka huu wakati akiendesha gari lake la kifahari aina ya Escalade, Polisi wa Kimataifa Interpol walimshikilia kabla ya kumfikisha Kituo Kikuu cha Polisi.
Inadaiwa chanzo cha Interpol kufuatilia nyendo zake, inatokana na akiba ya wakili huyo kukutwa na kiasi cha zaidi ya Sh30 bilioni zinazodaiwa kuingizwa njia zisizo halali.
Source: Mwananchi
kama ni jasho lake kuna shida gani?sheria inasemaje juu ya hili? ikiwa kama hajawahi kuwa mtumishi wa umma kuna shida?