Insha Maridadi 4: Mtaani Kwetu Wazazi Walifanya "Birthdays" za Watoto Marehemu... na siyo ya aliye hai...

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,478
39,997
1081407

Na. M. M. Mwanakijiji
Huwezi kuamini kuwa haya niliwahi kuyaona pale mtaani kwetu. Wazazi wawili ambao walikutana ujanani baada ya kila mmoja kupoteza mtoto wa kuzaa. Walipofunga ndoa Mungu akawajalia kupata mtoto mwingine, ambaye wote walimpenda na waliona fahari na baraka kuwa naye. Kwa muda mrefu wazazi wale walikuwa wakifanya kumbukumbu ya watoto wao waliopoteza lakini walifanya sherehe kubwa ya kuzaliwa kwa mtoto wao yule mmoja mpendwa. Walifanya hivyo kwa muda mrefu lakini baadaye wazazi wale waliacha kumfanyia sherehe ya kuzaliwa yule mtoto wao aliye hai; walianza kufanya sherehe za kuzaliwa kwa watoto wao marehemu.

Jambo hili lilikuwa linatushangaza sana pale mtaani. Hatukuelewa kwanini walikuwa wanafanya vile. Siku moja hata hivyo wazee pale mtaani waliamua kuwaendea wale wazazi na kuzungumza nao. Wazazi wale walisema tu kuwa ilikuwa ni gharama sana kufanya sherehe ya mtoto aliye hai; lakini kwa vile kila mmoja aliwahi kuwa na mtoto wake aliyempenda sana kabla ya kukutana basi kila mmoja aliona kila inapofika kumbukumbu ya kuzaliwa kwa watoto marehemu basi washirikiane kuadhimisha siku hiyo. Wazee waliwaambia kuwa ule ulikuwa ni mwiko; walikuwa wanamchulia mtoto wao aliye hai.

Wale wazazi walisikiliza kwa makini na kuyapa uzito maneno ya wazee wa mtaa wetu (mimi nikiwa mmoja wapo). Wakaamua kuanzia mwaka unaofuatia kutokufanya tena sherehe za kumbukumbu za watoto marehemu na kuanza mara moja kufanya sherehe kubwa ya kuzaliwa kwa mtoto wao yule aliye hai. Wale marehemu walibakia kwenyey picha na kwenye mioyo yao; na kama wakitaka kuadhamisha basi waliadhimisha bila kufanya sherehe yoyote kubwa. Ila siku ya kuzaliwa kwa mtoto wao waliamua kuifanya sherehe kubwa, ya furaha na mtaani pote tulikuwa tukialikwa na tuliungana nao katika furaha yao.

Nilipotafakari tukio hili pale mtaani; likanikumbusha tukio jingine nimewahi kulisikia la watu waliokuwa wanafanya kitu kama hiki… Nitawasimulia siku nyingine.

Niandikie: mwanakijiji@jamiiforums.com
 
Mkuu Mwanakiji, nimebaini kuwa kila mmoja kati ya wale wazazi anampenda zaidi mtoto wake marehemu aliyemzaa nje ya ndoa na mwanamke/mwanaume mwingine alipokuwa kijana. Japokuwa si rahisi kwa mtu kumsahau mtoto wake aliyefariki, ni ajabu kidogo kufanya hizo kumbukumbu on the expense of the living one. Labda hii ndoa yao ipo kwa malengo maalum, siyo kama tunavyojua sisi.
 
Hakuna pesa ya kuchezea ,watumishi hawana mishahara mipya kwa mwaka wa tatu sasa. Hivi hata kama ungekuwa ni wewe ungefanyaje?

Hizi sherehe za muungano ziende tu. Kwanza muungano wenyewe umejaa malalamiko kibao.
 
Halafu kuna dalili kwamba mzazi mmoja kati ya hawa hampendi mtoto huyu kiukweli! Anatamani nae Afe,kuna na watoto wa jirani nao nimewaona wakimnon'goneza mama yake vijineno! Si vya kheri!!
 
Kwani huyu mtoto hakui tu!!! Maana amezaliwa muda mrefu sasa.

Inafaa tukiishia kumwish happy birthday tanzania basi inatosha, keki na soda tunakula sana.

Unajua mtoto anapokua watu hufanya sherehe za kuzaliwa kila mwaka hadi akifika kama miaka ishirini au ishirini na moja. Baada ya hapo watu wanaanza kusherehekea ile miaka mikubwa (30, 45, 50, 55, 60, halafu jubilii 75 na kwenda juu.. ni sherehe kubwaaa
 
Halafu kuna dalili kwamba mzazi mmoja kati ya hawa hampendi mtoto huyu kiukweli! Anatamani nae Afe,kuna na watoto wa jirani nao nimewaona wakimnon'goneza mama yake vijineno! Si vya kheri!!
Au wanaweza kuwa wote wanaombea afe ili kila mtu achukue hamsini zake..
 
Back
Top Bottom