Ingekuwa enzi za mzee wa msoga, hizi fursa zisingeachwa zipite.

fdizzle

JF-Expert Member
Jul 29, 2015
1,891
2,367
Haujapita muda mrefu tangu Tanzania itembelewe (kimya kimya) na mwanasoka maarufu duniani David Beckham.
Wakati huyo mchezaji alipotembelea Tanzania ingawa wengine wanasema ni Kenya yalitolewa maoni mbali mbali na wadau kuwa serikali ingefanya japo kujipendekeza ili angalau huyo jamaa aandike kuwa yupo Tanzania kwani itasaidia kuongeza watalii kwa kuwa huyo mchezaji ana mashabiki wengi duniani na pia anafahamika na wengi (hata wale wasio fuatilia mpira ukitaja hilo jina asilimia kubwa wanajua unamzungumzia mchezaji).
Baadhi waliponda kama kawaida yao maana hatufanani kimtazamo kuwa hakukuwa na haja ya kujipendekeza kwake.
Sasa kuna habari kuwa mchezaji mwingine maarufu duniani Wayne Rooney anatarajia kuitembelea Tanzania hivi karibuni.
Hizi ni fursa za kuongeza watalii kwa kuwatumia hawa wachezaji na hivyo kuongeza pato la taifa lakini kwa masikitiko makubwa wa husika hawalioni hili.
Nawaza tu, ingekuwa enzi za mzee wa msoga, hizi fursa zisingeachwa zipite hivi hivi.

Sent from my TECNO-Y6 using JamiiForums mobile app
 
Thinking locally, acting locally (tena chattlism) vs thinking globally, acting locally!
 
Ndio maana nilukuwa nawaza pale maliasili na utalii angekaa kijana mmoja anayekwenda na wakati anayejua biashara...Muwekeni hata Ruge muone kazi
Khaa, kwann unaidharau sana hii nchi mkuu?!

Sent from my HUAWEI G510-0200 using JamiiForums mobile app
 
~~~>>>>Nakumbuka baba yangu alinifunza kuwa "Uongozi ni staili"....... Kila kiongozi na staili yake.
 
Ndio maana nilukuwa nawaza pale maliasili na utalii angekaa kijana mmoja anayekwenda na wakati anayejua biashara...Muwekeni hata Ruge muone kazi
Ruge anajua biashara gani ?

- Anachojua ni kudhulumu vijana wenye unique ideas wasio na mitaji idea zao huku akijificha kwenye kichaka cha kuwasaidia
 
Haujapita muda mrefu tangu Tanzania itembelewe (kimya kimya) na mwanasoka maarufu duniani David Beckham.
Wakati huyo mchezaji alipotembelea Tanzania ingawa wengine wanasema ni Kenya yalitolewa maoni mbali mbali na wadau kuwa serikali ingefanya japo kujipendekeza ili angalau huyo jamaa aandike kuwa yupo Tanzania kwani itasaidia kuongeza watalii kwa kuwa huyo mchezaji ana mashabiki wengi duniani na pia anafahamika na wengi (hata wale wasio fuatilia mpira ukitaja hilo jina asilimia kubwa wanajua unamzungumzia mchezaji).
Baadhi waliponda kama kawaida yao maana hatufanani kimtazamo kuwa hakukuwa na haja ya kujipendekeza kwake.
Sasa kuna habari kuwa mchezaji mwingine maarufu duniani Wayne Rooney anatarajia kuitembelea Tanzania hivi karibuni.
Hizi ni fursa za kuongeza watalii kwa kuwatumia hawa wachezaji na hivyo kuongeza pato la taifa lakini kwa masikitiko makubwa wa husika hawalioni hili.
Nawaza tu, ingekuwa enzi za mzee wa msoga, hizi fursa zisingeachwa zipite hivi hivi.

Sent from my TECNO-Y6 using JamiiForums mobile app
Du wa Bodi ya Utalii hampo huku JF? Wakumbusheni matangazo ya EPL. Waelezeni kwamba mbona mchezaji Leon anayecheza na Wayne Rooney mpo naye Ngorongoro na Manyara tangu juzi. Waabieni mnafanya nini na Sports Pesa wanaomleta Rooney. Unajua Tanzania ili uonekane unafanya mambo makubwa lazima uwe na domo la kubwabwaja.
 
Back
Top Bottom