Kiba
JF-Expert Member
- Mar 23, 2012
- 459
- 62
Habari wana jf. Hakika nina kisa kilichonitokea hadi sasa sijui lakufanya..
Nimeanza mapenzi na msichana tangu mwaka 2008 nikamsubiri hadi kamaliza shule .
Alipomaliza kidato cha nne bahati mbaya hakufaulu. Tukashauriana jinsi ya kufanya ili walau aendele kielimu .
Nikamtafutia chuo akaenda kumaliza chuo mwaka huu tukawa tumepanga kuishi pamoja mkoani Mwanza ninapofanyia kazi. Maskini binti huyu na kazi ya muda hadi matokeo ya chuo yatoke nikamtafutia na kipindi chote cha miaka miwili nilikua namjali sana hadi wazazi wangu wanamfahamu.
Imefika tarehe ambayo kaaga kwao anakuja Mwanza kaaga nyumbani vizuri na kwenda Mjini Arusha kwajili ya safari vizuri .mara gafla akiwa Arusha akawa apatikani kwa siku moja siku ya pili kaka mmoja kanipigia simu majira ya usiku na kuniambia je unamfahamu fulani?
Nikamjibu ndio ? Ni nani kwako ? Nikajibu vizuri ni mchumba wangu .
Kaniuliza una mda gani naye? Nikajibu miaka mitano? Akasema kweli kaka anastahili kuwa mchumba wako hila nami alikua na mahusiano nami kwa kipindi cha mwaka mmoja na hadi naongea nawe nimeachana naye kwa hasira baada ya kuniambia amekuja kuniaga anaenda kwa mchumba wake mjini mwanza ambaye ni wewe? Na nimelala naye siku hii ni ya pili ndio ananiambia.
Akaendelea ulipiga sm akazima leo ukapiga akakuambia yuko mjini na alikua kifuani kwangu.
Akaendelea ili kuakikisha mimi baada ya kukosana naye kutokana na safari nilimnyang'anya simu na ninayo hapa tena ina dakika ngoja nikupigie nayo? Akanipigia nayo kweli.
Wakati huo msichana ananipigia na sm ya dada yake aishie Arusha na kuniambia simu iko chaji?
Kitendo hicho kiliniuma sana hadi sasa nimemwambia aendelee kusubiri Arusha hadi nitakapopata Ushauri.
Naomba ushauri wako nifanyeje?
Nimeanza mapenzi na msichana tangu mwaka 2008 nikamsubiri hadi kamaliza shule .
Alipomaliza kidato cha nne bahati mbaya hakufaulu. Tukashauriana jinsi ya kufanya ili walau aendele kielimu .
Nikamtafutia chuo akaenda kumaliza chuo mwaka huu tukawa tumepanga kuishi pamoja mkoani Mwanza ninapofanyia kazi. Maskini binti huyu na kazi ya muda hadi matokeo ya chuo yatoke nikamtafutia na kipindi chote cha miaka miwili nilikua namjali sana hadi wazazi wangu wanamfahamu.
Imefika tarehe ambayo kaaga kwao anakuja Mwanza kaaga nyumbani vizuri na kwenda Mjini Arusha kwajili ya safari vizuri .mara gafla akiwa Arusha akawa apatikani kwa siku moja siku ya pili kaka mmoja kanipigia simu majira ya usiku na kuniambia je unamfahamu fulani?
Nikamjibu ndio ? Ni nani kwako ? Nikajibu vizuri ni mchumba wangu .
Kaniuliza una mda gani naye? Nikajibu miaka mitano? Akasema kweli kaka anastahili kuwa mchumba wako hila nami alikua na mahusiano nami kwa kipindi cha mwaka mmoja na hadi naongea nawe nimeachana naye kwa hasira baada ya kuniambia amekuja kuniaga anaenda kwa mchumba wake mjini mwanza ambaye ni wewe? Na nimelala naye siku hii ni ya pili ndio ananiambia.
Akaendelea ulipiga sm akazima leo ukapiga akakuambia yuko mjini na alikua kifuani kwangu.
Akaendelea ili kuakikisha mimi baada ya kukosana naye kutokana na safari nilimnyang'anya simu na ninayo hapa tena ina dakika ngoja nikupigie nayo? Akanipigia nayo kweli.
Wakati huo msichana ananipigia na sm ya dada yake aishie Arusha na kuniambia simu iko chaji?
Kitendo hicho kiliniuma sana hadi sasa nimemwambia aendelee kusubiri Arusha hadi nitakapopata Ushauri.
Naomba ushauri wako nifanyeje?