Inawezekana Rais hashauriki au hafikishiwi ushauri; Bombadia moja "imekufa" Mwanza, ATCL inajigamba kuleta Dreamliner

kwani madeni yote serikali inayolipa huwa wanakwambia? nenda hazina au BOT watakwambia lakini ukikaa huku mtaani unabishana huwezi kupata hizo information
Ni kweli ulichokisema kwamba si kila deni la serikali huwa linasemwa, lakini why waanze na kupinga? Why haya yanayoulizwaulizwa yasisemwe? WANAFICHA NINI?
 
Ni kweli ulichokisema kwamba si kila deni la serikali huwa linasemwa, lakini why waanze na kupinga? Why haya yanayoulizwaulizwa yasisemwe? WANAFICHA NINI?
lini na wapi walipinga kuwa hawajalipa deni? naomba unipe hiyo kumbukumbu
 
lini na wapi walipinga kuwa hawajalipa deni? naomba unipe hiyo kumbukumbu
Siyo kupinga kulipa deni, hujanielewa...
Bombadia kukamatwa walianza na kupinga..
Na deni kulipwa hakuna anayelisema, wamelipa kimya kimya, NA HATA KWENYE RIPOTI YA CAG hakuna manunuzi ya ndege

Na kukuonyuesha kuwa kuanza kupinga ndo kawaida yao, HEBU KUMBUKA HAYA...
Loriondi kuuzwa Walianza na kupinga, LAKINI HADI LEO TUNAJUWA LORIO NDO SI YETU, NA WAKALIFUNGIA LILE GAZETI LA MOTOMOTO LILILORIPOTI HABARI HIYO KWA MARA YA KWANZA.....

Zanzibar kujiunga na OIC walipinga pia....

Sasa swli langu, kwa nini inapofika watu kuhoji juu ya jambo fulani, tena lenye maslahi kwa wananchi, WHY WANAANZA NA KUPINGA NA KUTOA MATUHUMA MBALIMBALI KWA MTOA TAARIFA AU MUULIZA MASWALI JUU YA JAMBO HUSIKA?
 
Acha kupotoshwa! Hata hizo jet injini zinatofautiana sana teknoloji kufuatana na watengenezaji na hata toleo! Swala la matengenezo ya injini kitaratibu lina mpangilio wake tofauti. Usidaganywe na watu wenye habari na siyo ujuzi.



Hivi umemsona vizuri au umeamua tu kubisha?!

Alichosema ni ndege "Makabila" 3 tofauti kwa maana kwamba; ingawaje CS300 na Q400 ni ndege za "kabila" moja, lakini mashine zake tofauti... moja ni turboprop engine na nyingine na jet engine!

Kwenye hiyo engines portfolio; ongeza na Dreamliner!

Na concern yake ya kwanza ilikuwa ni uhaba wa mafundi wazalendo!

So, kama unataka kupinga; pinga suala la CS300 & Q400 kuwa na engines tofauti na utuambie engines zao ni zipi hasa!

Aidha, pinga suala la uhaba wa mafundi na tuambie kwamba tuna mafundi walio vizuri kwa mashine za aina zote!

Kinyume na hayo; basi upo hapa kupinga tu ili mradi umepinga tena probably ukipinga mambo usiyo na utaalamu nayo!
 
Nisome taratibu na kwa vituo!!

Hakuna niliposema hadi tuwe na uchumi mzuri bali nimesema favorable business condition... hivi ni vitu viwili tofauti and I know you it so, don't exaggerate mambo!!

Unaweza kuwa na top economy duniani lakini unaweza usiwe na favorable condition hususani for a particular industry and the opposite is true!!

That said, mfano wako wa Ethiopia Airways vs Ethiopians ni irrelevant!

That's one but two, sie tulio na ABC ya uchumi huku tukiwa hatusukumwi na itikadi za kisiasa (though baadhi yenu watu kama cc mnatuita CHADEMA), maelezo yetu yatajikita kwa kuangalia nadharia za kiuchumi!!

Moja; Mchumi (Rational Economist) will always invest kule anakotarajia MAXIMUM return!

Lakini kwavile hii ni government investment; anaweza pia kuangalia socio-economic benefits; especially, impact ya investment husika kwenye ajira na effect yake kwenye sekta zingine za kiuchumi; especially microeconomic sector!

ONLY STUPID Economist ndie angefikia hitimisho kwamba uwekezaji kwenye ndege ndio BEST investment alternative kuliko investment nyingine yoyote ile ambayo ingeweza kufanywa na serikali na kutoa sifa nilizoeleza hapo juu!

Hata kama unafanya uchambuzi/uchanganuzi wa investment tofauti tofauti in favor of the government; uwekezaji kwenye ndege usingeweza kuwapo hata kwenye top 5 best investment alternatives!

Katika mazingira kama hsyo, na kwa kuzingatia limited resources, kwa rational decision makers KATU investment kama hiyo haiwezi kuwa top priority!!

Tena top priority unayoweza kui-finance with cash...

SIAMINI kwamba eti kuna wataalam walimshauri vizuri katika hili! I believe kilichom-influence JPM ndo hicho ulichosema "zamani ni sisi wenyewe ndio tulikuwa tunalalamika kwanini tusiwe na ndege zetu wenyewe!"

UPO SAHIHI! Leo hii tunaopinga kununua ndege, miongoni mwetu ndio hao hao tulikuwa tunalalamika kutokuwa na ndege zetu wenyewe!

Unfortunately, mimi sio mmoja wao! Nilipinga wakati wa JK na ninapinga sasa!!

Kilichom-influence JPM ni soka la kucheza na mashabiki uwanjani!

CONCLUSION: Ndege, HAPANA lakini SGR... Yes though sina uhakika kama route iliyopewa kipaumbele ndio route bora kuliko zote kiuchumi!
Kila mtu na mtazamo wake, kwangu ndege ni muhimu na SGR ni muhimu pia. Zipo markets nyingi tu huko nje kilichokuwa kinatukwamisha ni political will, ile hali ya sisi kujiona hatuwezi.

Awamu ya tano inayo political will ndio maana kuna uthubutu wa kufanya mambo tena wa hali ya juu sana.
 
Acha kupotoshwa! Hata hizo jet injini zinatofautiana sana teknoloji kufuatana na watengenezaji na hata toleo! Swala la matengenezo ya injini kitaratibu lina mpangilio wake tofauti. Usidaganywe na watu wenye habari na siyo ujuzi.
We unaongea mambo gani wewe!!

Soma, elewa context kabla hujakurupuka kujibu! On top of that; elewa maana ya nukuu!!
 
Kila mtu na mtazamo wake, kwangu ndege ni muhimu na SGR ni muhimu pia. Zipo markets nyingi tu huko nje kilichokuwa kinatukwamisha ni political will, ile hali ya sisi kujiona hatuwezi.

Awamu ya tano inayo political will ndio maana kuna uthubutu wa kufanya mambo tena wa hali ya juu sana.
Of course, wanayo political will huku pia wakisukumwa na maamuzi ya kisiasa!

Mtu hahitaji kuwa mjuvi sana wa mambo kufahamu hii come back imelenga sana national pride and not commercial viability!!

Uzuri ni kwamba, watu kama sie mlitubishia hata kwenye suala la makinikia tukizungumzia commercial inviability ya ku-invest kwenye copper concentrate smelters... mkatubishia kutwa kuchwa but today yanayoendelea yana-reflect tulichosema wakati ule!
 
kwa hiyo kwa sababu hatuna mafundi wazalendo basi tusiwekeze kwenye ndege, dah watz hizi akili za namna hii tunatoa wapi?
Nikuulize wewe... hizi akili za kudanganya mbele ya kadamnasi unazitoa wapi?! Ni wapi amepinga ununuzi wa ndege wakati amesema dhahiri shahiri kwamba:
Sisi wengine tuliiopongeza "idea" ya kununua ndege aina ya bombadia tukiwa na matumaini ya kuanza kwanza na "local routes", tukisimama tuhamie kwenye "regional routes" na tuki-settle mambo yetu na IATA tuhamie kwenye "international routes".
Mtu anayepinga anaweza kuongea hayo?!

Tunaopinga tupo lakini hapo umeingia cha kike!

Na kama hukusoma thread mzima lakini ukakimbilia kupinga kama nilivyokueleza hapo awali; hiki ndicho ameongea kuhusu kuwa na ndege makabila 3 tofauti ilihali hatuna raslimali watu:
Wakati tukiwa hatuna hata wataalamu wa kutosha wa kuhudumia ndege za bombardier kwa maana ya wahandisi wazalendo,tayari serikali imeagiza ndege za makabila mawili tofauti,yaani CS300 na Dreamliner.Ni ukweli kuwa hata wahandisi waliobobea tunaowategemea katika shirika letu kwa sasa ili kuhudumia bombadia zetu ni kutoka Ethiopia,Misri na Malawi.Hawa wanalipwa na serikali yetu,hawa vijana wazalendo ndio tunaendelea kuwasomesha na kuwaongezea ujuzi ili wapate leseni hata za kuzisimamia bombardia zetu
Inawezekana hujauona umuhimu wa hiyo hoja kwa sababu umekuja kufanya counterattack!!

Unfortunately, umekuja kufanya counterattack bila kuisoma thread mzima na kuielewa na matokeo yake; unabisha ambavyo havipo! Na kwa nyongeza tu:
Kuhudumia ndege za makabila matatu tofauti katika shirika moja ni kukaribisha kabuli na kifo cha kiuchumi.
Hizo ndo concerns za mleta mada in relation to ndege za makabila matatu tofauti!

Hoja kwamba anapinga ununuzi ni hoja yako wewe kwa sababu, kama nilivyosema hapo awali; umekuja hapa kufanya counterattack lakini kwa kukosa umakini; you jumped in without dotting all the i's and crossing the t's!
Ndege duniani zipo za jamii mbili jet engine na hizo panga boi, hao Ethiopia wana bombardier panga boi, Airbus na boeing, kwa hiyo wana ndege jamii tatu kama sisi sasa huo mfano wake ulikuwa na maana gani?
Ndo maana nikasema ulikimbilia kufanya counterattack bila kusoma vinginevyo usingeleta hii hoja!

Mosi; maelezo ya hapo juu tayari yanajibu hoja yako! Hapo juu umeshaambiwa kwamba hata mafundi wa Bombardier, miongoni mwao wanatoka Ethiopia! That having said, Ethiopia isn't our match... kwavile Ethiopia Airline ni shirika kongwe na the most successful airline in Africa; hawa wenzetu tayari wana raslimali watu (Engineers) wa kutosha kuweza ku-handle mashine za aina tofauti!

Na si hivyo tu; pia hapa:

Mashirika mengi duniani na hasa yanayotaka kuinuka kurudi ktk ushindani wa soko la usafiri wa anga,huwa wana kitu wanaita "Fleet Commonality"; yaani shirika la ndege linaamua kununua au kukodisha ndege za jamii moja, zinazotoka kwa manufacturer mmoja lkn zikawa na model pamoja na generation tofauti.
Sisi ni Ethiopia tofauti kwa sababu, wakati Ethiopia tayari ni well established airline; sisi ndo kwanza tuna-struggle kurudi kwenye biashara!

Hoja ya mleta mada ambayo hukuielewa ni kwamba; wenzetu wanapoamua kurudi kwenye airline business, wanachofanya ni kuwa na ndege za aina moja ili ku-capitalize available human resources!
kwanza ni mfano aliopotosha na bado akaendelea kutudanganya KQ wameuza dreamliner wakati inaendelea kufanyakazi.
Usibadilishe magoli; hoja nilizokupa tangu awali ni kuhusu rationale ya ATCL kuwa na ndege zenye makabila 3 tofauti! Vipi tena unachomokea hoja za KQ kuuza Dreamliner?! Au unatafuta dirisha la kuchomokea?
kama umeamua kuwa zwazwa sio wote tutakubali lazima tufuatilie kama yanayosemwa ni kweli
TAMBO & MAJIGAMBO havilipiwi kwahiyo we endelea tu kujitapa kwamba ni mfuatiliaji lakini hapo juu ume-prove otherwise kwa kushindwa kwenda sambamba na kilichoandikwa kwenye only single thread!!
 
Mkuu mleta mada mafanikio HUWA HAYAJI KIRAHISI RAHISI kama sisi tunavyotaka...

Siku zote up and down zipo tu ILA SIKU MOJA TUTAFIKA na mkubali mkatae MAGUFULI kwenye hili la NDEGE Kafanya maajabu mno NA ANASTAHILI KUPONGEZWA sema ndio hivyo tena WATU WANACHUKI TU mpaka kufikia kutoona mazuri.

Mlio wengi humu JF kuharibika kwa INJINI ya hiyo ndege(KAMA NI KWELI IMEHARIBIKA) NI FURAHA KWENU...maana mpo kusubiri kuona mabaya tu(Na inawezekana mnakesha mkiomba kabsa) ili mpate pakusemea LAKINI MAZURI hamuyaoni kabsa
Ukiona watu wanafurahi kwa maanguko yako basi jitafakari.

Maajabu si lazima yamaanishe jambo zuri tu, hata kutandika mkwaju golini kwako ni maajabu pia, lkn yanarudisha timu nyuma.
 
We unaongea mambo gani wewe!!

Soma, elewa context kabla hujakurupuka kujibu! On top of that; elewa maana ya nukuu!!
Nilichosema ndio hivyo una haki ya kubaki na hilo unaloamini. Context!!!
 
Of course, wanayo political will huku pia wakisukumwa na maamuzi ya kisiasa!

Mtu hahitaji kuwa mjuvi sana wa mambo kufahamu hii come back imelenga sana national pride and not commercial viability!!

Uzuri ni kwamba, watu kama sie mlitubishia hata kwenye suala la makinikia tukizungumzia commercial inviability ya ku-invest kwenye copper concentrate smelters... mkatubishia kutwa kuchwa but today yanayoendelea yana-reflect tulichosema wakati ule!
Mkuu chige tutoe muda muafaka kwa wataalam wa kufanya mambo ya kitaalam.

Huyu aliyepewa ATCL aiendeshe ni mtanzania mtaalam ambaye alikuwa kule Senegal akifanya mambo makubwa tu. Tuwape muda wataalam wafanye yao ya kitaalam.

Hao Waethiopia unaowaongelea waliwapa muda wataalam wao na matunda ndio haya yanayoonekana kwa kila mtu.
 
Aviation industry run by the government in Tanzania is a "White Elephant Project" driven more by political gerrymandering than economic sense and that's why it often collapses and even now it's heading to the "Limbo".
 
Back
Top Bottom