Inawezekana kweli Kikwete ni chaguo la Mungu

hivi maraisi wa nchi wakitoka na huyo raisi wako wa misiba atatoka? ila anaeleweka ni riasi wa wafu na mazishi, ngoja naye zamu yake ifike
Heshimu rais wa nchi na funga domo lako naona unasemewa na unafikiria kutumia masa....ri wewe nyambafu
 
Asingechakachua angeepuka dharau hizi. Ni sawa na kulea mtoto wa kambo, wema wowote akifanyiwa anahisi angekuwa mama yake angemfanyia zaidi. Hata akijitahidi kuwazika wasanii, aanzishe miradi ya aina yoyote bado mioyo ya zaidi ya 64% ya watanzania hawamkubali. Thabo Mbeki alipokataliwa, alikaa kando na kuitunza heshima yake.
 
Kumbe kwenda misibani ni dhambi mbona huyo slaa wenu hatokei kwenye hiyo misiba au kwakua hakuna posho maake watu wa kanda ile kwa kupenda pesa.... Ni noma
 
JK 2005 wakati anagombea alipewa sifa lukuki! Wapo watabiri, maaskofu, wachungaji hata mashehe ambao waridiriki kusema ni chaguo la Mungu! Sielewi walitumia vigezo gani! Mwaka 2013 umeanza na kila kona ni siasa. Hakuna anayefikiria kuleta maendeleo ni uchaguzi tu. Najiuliza nani mwenye huo upako wa Mungu? Ipo haja ya kuepuka kumtaja Mungu kwa mambo ya kijinga ona sasa! Chaguo la mungu linavyotuumiza vichwa! Nani asiye mjua Ben Mkapa enzi zake alionekana kama Idd Amini lakini kwa sasa anaonekana Lulu kwa sababu ya Machaguo mliyoyaita ya Mungu. TUFANYE KAZI! Tuambieni ukweli hata kama unauma!
 
Inategema ni Mungu yupi maana miungu iko mingi lakini hata mungu wa kweli naye kluna wakati anaweza kuruhusu hali tofauti zitokee kwaajili ya yeye kujipatia utukufu lakini pia katika kuwaimarisha watu wake kiimani
Kwani hujasoma neno lake wewe
Je tupate tu mema machoni pa bwana???
 
Sasa huyu JK ana tofauti gani Na Nduli Idd Amin Dada? Idd Amin alianza kuua waandishi wa habari wote walioönekana wanaandika tofauti na anavyotaka

Baadae akahamishia mpango wa mauaji kwa viongozi wa Uganda ng hasa baraza la mawaziri wengi waliuawa na vichwa vyao kuhifadhiwa kwenye chumba maalumu

Wengi waliitwa Ikulu kwa kuhojiwa kama anaenda kinyume na matakwa yake pamoja na kuonyeshwa vichwa wa waliouawa, na waliopona na upanga huo walikuwa wanajikojolea na kukimbilia Ughaibuni

Ndio haya leo tunayashuhudia leo Tanzania watu wananyongwa ovyo, waandishi wa habari wako hatarini hasa wale wanafichua uovu unaofanywa na serikali híi DHAIFU ambayo haijawahi kutokea Tanzania

Wananchi wengi wanalia kwa kunyan'ganywa Ardhi yao ambayo wanaitegemea kwa makazi na kilimo kwa ajili ya kujikimu kwa kilimo kidogo

Uwekezaji usio na tija na taifa hili leo híi umeshika kasi ya ajabu, wananchi kupigwa risasi kila kukicha na wawekezaji wa migodi

Mbuga za wanyama wamemilikishwa kwa miaka 100 hii ni hatari ambayo haijawahi kutokea duniani kote ispokuwa Bongo tu

Uchechezi wa kidini unaoenezwa kwa kasi ya ajabu na watawala wa Tanzania, Nchi ya Tanzania ikiwa inavurugwa kwa nguvu zote na Utawala huu

Hata Idd Amin hakuanza ghafla alianza kwa mmoja kesho watatu keshokutwa watano hatimaye alianza kukusanya mpaka raia na kuwapiga risasi hadharani

Kwa yanayofanyika leo hii Tanzania si ajabu hata Idd Amin atarudi nyuma kwa aliyoyafanya sisi ikawa zaidi maana hali imeanza kutisha

Leo hii serkali ya Chama Cha Mapindizi inahubiri AMANI na wakati hiyo hiyo Serikali inaua raia wake kwa makusudi hii inasikitisha sana

Leo hii viongozi wa Chama Cha Mapinduzi wanatoa kauli tata majukwaani zisizo na tija kabisa za uchochezi dhidi ya raia na vyama vya Upinzani huku serikali ikiwa kimya

Sisi Watanzania tuungane tuwe kitu kimoja adui yetu mkubwa ni mmoja tu nae ni CCM
TUFANYE KILA LINALOWEZEKANA KUIONDOA CCM MADARAKANI VINGINEVYO TUNAIPOTEZA TANZANIA MUDA SI MREFU
 
Well said bro! Tulichemka na tukubali kunipanga upya nabkure kebisha makosa yetu

Mzee umekurupuka? kweli hata baada ya kutoka usingizizini bado unaonyesha hasira na choyo kwa mshikaji!. Daka sumu unywe maana mwanaume hagongwi na nyoka mara mbili kwenye shimo moja!
 
Inategema ni Mungu yupi maana miungu iko mingi lakini hata mungu wa kweli naye kluna wakati anaweza kuruhusu hali tofauti zitokee kwaajili ya yeye kujipatia utukufu lakini pia katika kuwaimarisha watu wake kiimani
Kwani hujasoma neno lake wewe
Je tupate tu mema machoni pa bwana???

Hiyo Bibilia ujue umeiandika wewe sio mungu Yehova anaye neno linasema Siwezi kumjaribu mwanadamu niliyemuumba kwa lolote lile isipokuwa majaribu na shida zote zinatoka kwa mwovu
 
Mzee umekurupuka? kweli hata baada ya kutoka usingizizini bado unaonyesha hasira na choyo kwa mshikaji!. Daka sumu unywe maana mwanaume hagongwi na nyoka mara mbili kwenye shimo moja!

I am not sure if you captured my point. I am not a ccm suporter. My concern is a nation and not a political party
 
Nikikumbuka 2005 jinsi watu walivyotekwa akili hua nabaki nasikitika sana, I think uzuri wa mgombea na cheka cheka vili wadanganya watu wakadanganyika hadi kufikia hatua kuona ni chuguo la mungu na sio Mungu
 
Kikwete kachaguliwa kwa udini au siasa?
ban.maswali.jpg


Ansbert Ngurumo​
amka2.gif
Hali tete inayotikisa taifa sasa katika masuala ya kidini imewafanya baadhi ya wasomaji wa safu hii kuomba mwandishi airudie kwa madhumuni ya kuweka msisitizo. Kwa mara ya kwanza uchambuzi huu ulichapishwa na gazeti hili tarehe 21/11/201. Endelea:
NILIMSIKIA Rais Jakaya Kikwete akitoa hotuba ya ufunguzi wa Bunge la 10. Kuna jambo lilinigusa. Nadhani anataka kutuletea matatizo kwa kujadili – kwa staili aliyochagua – suala la udini.
Alisema katika kampeni za mwaka huu kumeibuka nyufa za udini na kwamba yuko tayari kuchukua hatua za haraka kuziba nyufa hizi. Ni hoja nzito, lakini inazua maswali.
Alipoingia yeye hakukuwa na kelele za udini. Ni kitu gani kinamfanya yeye aone udini katika siasa baada ya miaka yake mitano Ikulu? Kama kweli kuna udini, anawezaje kujivua lawama za serikali yake kujenga mazingira ya kuasisi udini huo?
Mwaka 2005, wakati chati yake kisiasa ikiwa juu, aliyekuwa Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Dk. Methodius Kilaini, alitamka kwamba Kikwete ni chaguo la Mungu.
Wengi tunajua kuwa Askofu Kilaini ni rafiki binafsi wa Rais Kikwete kwa muda mrefu. Tunajua pia kwamba urafiki huo ulijengwa na Kikwete kimkakati, na askofu akajikuta ameingizwa katika mtandao wa Kikwete bila kujua na bila kutaka.
Kwanini, kwa kauli hiyo, iliyotolewa na askofu Mkatoliki, Watanzania hawakumtuhumu Kikwete wala Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kuendekeza udini, wala hawakumtuhumu Askofu Kilaini kwa kuingiza dini katika siasa?
Ikumbukwe kuwa Rais Kikwete alitumia vema kauli hiyo na nyingine, na hata baadhi ya makada na wapiga debe wake walitumia mazingira hayo kujinasibu na ‘misingi na malezi mazuri aliyopewa na Wakatoliki.' Mbona hakuna aliyenyoosha mkono kusema hapa kuna harufu ya udini?
Nasema hivi nikijua kwa dhati kuwa timu ya mtandao wa kampeni ilitumia nguvu nyingi sana kushawishi maaskofu wa madhehebu kadhaa ya dini yamuunge mkono. Namjua hata aliyetumwa kujenga mazingira mazuri kwa baadhi ya maaskofu Wakatoliki ‘wasimpige mawe' Kikwete kabla hata hajajitokeza kugombea.
Walifanya hivyo wakitambua kuwa nguvu ya kanisa ni kubwa na kwamba kama ingetumika dhidi yao wasingepata watakacho. Bahati nzuri, kwa nguvu ya ushawishi waliotumia, kanisa halikumpiga vita. Kwanini hakuna aliyezuka kuzungumzia udini katika siasa za Kikwete?
Ikumbukwe pia, Kikwete ndiye aliyenadi sera za CCM, ikiwamo ya kuwaahidi Waislamu kuwapatia ufumbuzi wa suala la Kadhi Mkuu, ambalo limeleta sokomoko kwa miaka mitano yote. Mbona Watanzania hawakusema Kikwete anaendekeza udini katika siasa?
Ninachokumbuka haraka haraka, mwanzoni kabisa mwa utawala wa Rais Kikwete, yupo Mtanzania mmoja, Nathaniel Limu, aliandika kuhoji uteuzi wa viongozi waandamizi ndani ya serikali ya Kikwete, ambao wengi walikuwa Waislamu.
Kutokana na ukali wa mwandishi Limu, timu ya Rais Kikwete, kupitia kwa swahiba wake, Rostam Azizi, ilimuomba aliyekuwa Mhariri Mtendaji wa Habari Corporation, Salva Rweyemamu kujibu hoja za Limu.
Makala zote mbili, ya Limu na ya Rweyemamu ziliandikwa katika gazeti hili; moja ikikosoa uteuzi wa Rais Kikwete na kuuita wa kidini, na nyingine ikijibu na kutetea uteuzi huo kwamba ulizingatia sifa za walioteuliwa, na hata kuorodhesha majina na nafasi za vigogo Wakristo serikalini. Kwanini Kikwete hakujitokeza kukemea udini?
Yapo magazeti pia ambayo kwa muda mrefu yamekuwa yakiandika habari na makala za udini, na yakihusisha dini za watu na uongozi wa vyama kadhaa vya siasa, hata kwa kuvitaja majina. Serikali iliyosajili magazeti hayo haijawahi kuvichukulia hatua kwa miaka mitano.
Na hata katika kampeni za mwaka huu, magazeti hayo yaliendelea kuandika habari zinazowataja baadhi ya wagombea kuwa ni makafiri, na kwamba wasichaguliwe. Kwanini serikali imekaa kimya hadi baada ya uchaguzi?
Si hilo tu. Hata katika baadhi ya nyumba za ibada, wamesikika viongozi wa kidini wakiwaomba wafuasi wa madhehebu yao wasiwachague makafiri. Na wengine walidiriki kumpigia debe Rais Kikwete katika nyumba hizo hizo za ibada. Kwanini hakujitokeza kukemea kauli hizo wakati ule?
Inafahamika pia kwamba miongoni mwa mbinu chafu za kampeni za chama chake mwaka huu, ni matumizi ya ujumbe mfupi wa simu za mkononi, dhidi ya mgombea urais kupitia CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa, kwa misingi kwamba ni kafiri.
Rais Kikwete alishindwa kuwazuia wanachama wake kufanya kampeni hizo. Na walipogundua kwamba kampeni ya kidini dhidi ya Dk. Slaa ingeweza kuwafanya waamini wa upande mwingine nao wajihami, wakaanza propaganda za kumshutumu kwamba anatumia makanisa kufanya kampeni!
Kilichomzuia kuwazuia wafuasi wake kufanya kampeni za kidini kwa kutumia sms ni kitu gani? Mbona hakujitokeza kukemea baadhi ya misikiti na makanisa wakati wa kampeni? Anapata wapi leo nguvu ya kukemea matawi wakati amepalilia mizizi ya tatizo hilo hilo?
Lakini pia anaposema kwamba uchaguzi huu umefanyika kwa misingi ya udini, anataka kusema kwamba hizo kura milioni tano alizotangazwa kupata ni za watu wa imani moja (Waislamu) pekee? Anataka kusema kwamba kama Wakristo wangepiga kura za udini Dk. Slaa angepata kura milioni mbili zilizotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)?
Au anataka kusema kwamba anajua zaidi, kwamba Wakristo walimchagua Mkristo, na Waislamu walimchagua Mwislamu, lakini kura zilizopigwa sizo zilizotangazwa?
Ipo pia hoja iliyotolewa na Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship. Mwaka 2000 alimpigia debe mgombea urais kupitia TLP, akimpinga rais aliyekuwa madarakani, Benjamin Mkapa.
Mbona hakuna aliyehoji udini katika siasa? Ni kitu gani kinawafanya watawala wafikirie kwamba kwa kuwa mwaka huu Askofu Kakobe ameendelea kuwapinga, alipinga dini zao si udhaifu wao wa uongozi?
Kama ambavyo baadhi ya watu wamejadili, watawala wamekuwa na tabia ya kuchomeka hoja za ajabu ajabu kama nia ya kuwaondoa Watanzania katika mijadala mizito ya kitaifa.
Na sote tumeshuhudia mbinu yao hii katika kampeni za uchaguzi mwaka huu. Hata baadhi ya vyombo vya habari vilivyomuunga mkono Rais Kikwete na CCM, jambo ambalo si kosa kisera vilishindwa kumjenga mtu wao, vikaishia kutafuta namna ya kubomoa washindani wake, hasa Dk. Slaa.
Lakini havikujua kwamba udhahifu wa kiuongozi wa Rais Kikwete wa miaka mitano iliyopita, usingeweza kuboreshwa au kutetewa kwa mashabulizi dhidi ya washindani wake.
Na tayari baadhi yetu tunajua mikakati yao ya kipropaganda ya kutumia mashambulizi dhidi ya kina Dk. Slaa na wenzao kuelekea 2015. Tunasubiri kuona ufundi utakaozitengeneza!
Lakini mwandishi mmoja, Richard Mgamba, amehoji: "Tanzania kuna udini upi? Nani mdini? Ukiomba Mahakama ya Kadhi kosa, ukiomba OIC dhambi; askofu akikosoa serikali tayari kuna udini. Hivi kweli nchi hii kuna udini au ni uoga wa viongozi wetu? Huko mtaani mbona tunaishi salama Wapagani, Waislamu na Wakristo? Huo udini wanauona watu wa usalama tu na bwana mkubwa? Jamani tusiingie kwenye mitego ya kipuuzi.
Udini kama ungekuwepo hapa, leo hii huko mitaani kwetu kungekuwa hakukaliki. Kama kuna Mkristo fulani mwendawazimu haina maana Wakristo wote wanafikiria hivyo, na pia kama kuna Mwislamu mmoja kichaa, haina maana Waislamu wote wako hivyo.
"CCM inadai ina wanachama milioni 5 nchi nzima. Imepata kura milioni 5.8 mwaka huu. Ina maana imepigiwa kura na wasio na vyama laki nane. Mwaka 2005 ilipata kura milioni 8.9, sasa ina maana hizo kura zilizopotea milioni 3.1 ni za Wakristo?
"Hivi mbona hatujiulizi uhalali wa watu milioni 19.5 kujiandikisha kupiga kura, kisha wanaojitokeza ni milioni 8.5 tu, hao milioni kumi na moja wako wapi? Hawa wote walikufa, au walisafiri au waliamua kutokupiga kura ghafla?"
Sasa Rais Kikwete atuambie. Amechaguliwa na Waislamu milioni tano? Au amechaguliwa na wana CCM milioni tano? Au amechaguliwa na Watanzania milioni tano?
Na huu ndio uongo wa takwimu za watawala. Kama wana CCM ni milioni tano, na rais anachaguliwa na watu milioni tano, basi amekosa uhalali wa kutawala Watanzania takriban milioni 45.
Na kama amechaguliwa na Waislamu milioni tano, basi maana yake CCM ni chama cha watu wa imani moja tu, jambo ambalo si kweli. Na kama miongoni mwa waliompigia kura Kikwete wamo Wakristo, basi hoja yake ni potofu.
Maana natambua kuwa idadi ya Wakristo nchini inazidi milioni tano. Vile vile idadi ya Waislamu ni kubwa kuliko milioni tano. Kwa mujibu wa ensaiklopidia ya Wikipedia, hadi mwaka 2007, idadi ya Waislamu na Wakristo nchini inazidiana kidogo, na wote wako kati ya asilimia 30 na 40 ya Watanzania wote.
Kama Waislamu wote wangehamasishwa rasmi kumchagua Mwislamu mwenzao, na kama wangekubali wote, Kikwete na Profesa Lipumba wangegawana kura.
Na kama Wakristo wangekuwa wamehamasishwa rasmi kumchagua Mkristo mwenzao na wakakubali, kura za Dk. Slaa zingekuwa nyingi kuliko milioni tano alizopata Kikwete.
Lakini suala la msingi analopaswa kujiuliza Kikwete ni hili. Hoja hii ya udini aliirithi kutoka kwa Rais Mkapa au imeota mizizi katika miaka mitano ya utawala wake?

 
Sasa huyu JK ana tofauti gani Na Nduli Idd Amin Dada? Idd Amin alianza kuua waandishi wa habari wote walioönekana wanaandika tofauti na anavyotaka

Baadae akahamishia mpango wa mauaji kwa viongozi wa Uganda ng hasa baraza la mawaziri wengi waliuawa na vichwa vyao kuhifadhiwa kwenye chumba maalumu

Wengi waliitwa Ikulu kwa kuhojiwa kama anaenda kinyume na matakwa yake pamoja na kuonyeshwa vichwa wa waliouawa, na waliopona na upanga huo walikuwa wanajikojolea na kukimbilia Ughaibuni

Ndio haya leo tunayashuhudia leo Tanzania watu wananyongwa ovyo, waandishi wa habari wako hatarini hasa wale wanafichua uovu unaofanywa na serikali híi DHAIFU ambayo haijawahi kutokea Tanzania

Wananchi wengi wanalia kwa kunyan'ganywa Ardhi yao ambayo wanaitegemea kwa makazi na kilimo kwa ajili ya kujikimu kwa kilimo kidogo

Uwekezaji usio na tija na taifa hili leo híi umeshika kasi ya ajabu, wananchi kupigwa risasi kila kukicha na wawekezaji wa migodi

Mbuga za wanyama wamemilikishwa kwa miaka 100 hii ni hatari ambayo haijawahi kutokea duniani kote ispokuwa Bongo tu

Uchechezi wa kidini unaoenezwa kwa kasi ya ajabu na watawala wa Tanzania, Nchi ya Tanzania ikiwa inavurugwa kwa nguvu zote na Utawala huu

Hata Idd Amin hakuanza ghafla alianza kwa mmoja kesho watatu keshokutwa watano hatimaye alianza kukusanya mpaka raia na kuwapiga risasi hadharani

Kwa yanayofanyika leo hii Tanzania si ajabu hata Idd Amin atarudi nyuma kwa aliyoyafanya sisi ikawa zaidi maana hali imeanza kutisha

Leo hii serkali ya Chama Cha Mapindizi inahubiri AMANI na wakati hiyo hiyo Serikali inaua raia wake kwa makusudi hii inasikitisha sana

Leo hii viongozi wa Chama Cha Mapinduzi wanatoa kauli tata majukwaani zisizo na tija kabisa za uchochezi dhidi ya raia na vyama vya Upinzani huku serikali ikiwa kimya

Sisi Watanzania tuungane tuwe kitu kimoja adui yetu mkubwa ni mmoja tu nae ni CCM
TUFANYE KILA LINALOWEZEKANA KUIONDOA CCM MADARAKANI VINGINEVYO TUNAIPOTEZA TANZANIA MUDA SI MREFU

nafikiria wewe huko timamu na uchadema umekukaa kichwani wakati wa mkapa sio nyinyi mliokuwa mnamponda kusema tz kuna ukapa na sera ya kubinafsisha yeye ndie alieasisi vipi waliokufa pemba, ati leo ndio umamsifia mkapa na kumfananisha jk na iddi amini ni ujuha wa mwisho.
 
nafikiria wewe huko timamu na uchadema umekukaa kichwani wakati wa mkapa sio nyinyi mliokuwa mnamponda kusema tz kuna ukapa na sera ya kubinafsisha yeye ndie alieasisi vipi waliokufa pemba, ati leo ndio umamsifia mkapa na kumfananisha jk na iddi amini ni ujuha wa mwisho.

Acha upumbavu wewe usio na maana yeyote ni wapi CHADEMA imetajwa hapa kwenye threed? Hapa inalaumiwa Serikali yetu ya sasa inayööngozwa na Dr huyu wa kupewa chini ya Chama Cha Mapinduzi
Sasa kama akili yako imekutuma kwa CHADEMA lakini ni sawa kwa sasa kila ukiisema serkali kwa uchafu wanaooufanya wewe NI CHADEMA TU, híi CHADEMA imewakalia vibaya sana nini! Mbona ni Kawaida tu hii CHADEMA inawaogopesha nini mbona simple sana!
 
Back
Top Bottom