Inaonekana RC Makalla anaiongoza Dar, aidha asiyoijua kabisa au kwa kutaka sifa tu

The Phylosopher

JF-Expert Member
Mar 11, 2015
1,503
2,046
Ndugu wanabodi kama mtakumbuka vizuri, tukiwa mwanzoni kabisa mwa kukabiliana na changamoto ya COVID-19 mwaka uliopita, ni Serikali hii hii iliamuru level seat kwa daladala zote zinazofanya kazi hapa mkoani Dar.

Mara tu baada ya amri hiyo, hali ya usafiri wa umma ilikuwa tete, kwani abiria walikuwa wengi sana, jambo lililopelekea Serikali kuruhusu pikipiki bajaji na gari ambazo ni maalumu kwa kubebea wanafunzi vikaidhinishwa kubebea abiria, ili kujaribu kunusuru hali.

Pamoja na jitihada zote hizo, hali ya usafiri ilibaki kuwa tete. Bado kulikuwa na adha kubwa ya usafiri.

Ilikuwa kawaida sana kusubiri gari kituoni kwa zaidi ya saa nne hadi tano.

Kwa hali ya kawaida miundombinu ya usafiri Dar imezidiwa sana na idadi ya watu, ambapo hata kukiwa kawaida kabisa hali ya usafiri ni tete.

Hapa ndipo najiuliza, ina maana huyu mkuu wetu wa mkoa haijui Dar kweli? Ni kweli covid ni tatizo lkn kwa nini kiongozi anatoa tangazo ambalo halina uhalisia wowote?
 
Tatizo sio wingi wa watu tatizo ni miundo mbinu tu ndugu root ya nusu saa Gari imeenda na kurudia abiria Tena inatumia masaa 5 kwenda tu Sasa hapo ndio tusingizie wingi wa watu
 
Makalla anatoa matamko mengi yasiyo tekelezeka, suala la kusimamisha abiria kwenye daladala kwa Dsm linaonekana kuwa gumu kutokana na wingi wa abiria kulinganisha na mikoani.

Anatakiwa atulie ajue ni kwa jinsi gani atapambana na Corona angalau kwa kuhakikisha kila mtu anaetoka nyumbani asubuhi ana barakoa na sanitizer.

Hivi vitu sio bei kubwa, umekosekana muamko kwa jamii yetu naona bado wengi hawana habari, labda ndio wanasubiri kuugua Corona kwanza ili waanze kujilinda, wakishatoka kufufuliwa kwa kanisani kwa Gwajima.
 
Ndugu wanabodi kama mtakumbuka vizuri, tukiwa mwanzoni kabisa mwa kukabiliana na changamoto ya COVID-19 mwaka uliopita, ni Serikali hii hii iliamuru level seat kwa daladala zote zinazofanya kazi hapa mkoani Dar.

Mara tu baada ya amri hiyo, hali ya usafiri wa umma ilikuwa tete, kwani abiria walikuwa wengi sana, jambo lililopelekea Serikali kuruhusu pikipiki bajaji na gari ambazo ni maalumu kwa kubebea wanafunzi vikaidhinishwa kubebea abiria, ili kujaribu kunusuru hali.

Pamoja na jitihada zote hizo, hali ya usafiri ilibaki kuwa tete. Bado kulikuwa na adha kubwa ya usafiri.

Ilikuwa kawaida sana kusubiri gari kituoni kwa zaidi ya saa nne hadi tano.

Kwa hali ya kawaida miundombinu ya usafiri Dar imezidiwa sana na idadi ya watu, ambapo hata kukiwa kawaida kabisa hali ya usafiri ni tete.

Hapa ndipo najiuliza, ina maana huyu mkuu wetu wa mkoa haijui Dar kweli? Ni kweli covid ni tatizo lkn kwa nini kiongozi anatoa tangazo ambalo halina uhalisia wowote?
Mwachieni Makalla afanye kazi.
So far yuko vizuri.
 
Kwa mazingira ya JIJI LA DAR yalivyo....

Unataka mkuu wa mkoa aseme nini kipindi hiki cha KUPAMBANA na UVIKO?!!

Pamoja na kuonekana lockdowns zinasaidia...ila serikali yetu sikivu haikutaka KULISIMAMIA HILO....yote kwa kuijua ulivyo utafutaji wa riziki wa wananchi.....

#KaziIendelee
#NchiKwanza
 
Back
Top Bottom