Inakuwaje mtu kwa vigezo vyote ni mwenye akili za ziada kumbe mjinga?

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,915
30,259
INAKUWAJE MTU KWA VIGEZO VYOTE NI MWENYE AKILI ZA ZIADA KUMBE MJINGA?

Toka udogo wangu nikipenda senema.

Baba alikuwa na "prejector" nyumbani lakini ni ile "silent," haitoi sauti na filamu zake zilikuwa nyembamba.

Lakini katika miaka ya 1960 na utoto kwangu ile ilikuwa mashine niliyoipenda sana kupita kiasi.

Baba siku akifurahi ataitoa uani na kutuonyesha mimi na rafiki zangu filamu za Charlie Chaplin.

Nakumbuka moja ya filamu tuliyokuwa tunaipenda ni Charlie Chaplin kwa udogo wa mwili aliokuwa nao anaingia ulingoni katika masumbwi kupambana na jitu lililoshiba vizuri.

Charlie Chaplin anashinda pambano kwa "knock out."

Niko Nairobi nakaa 680 Hotel katikati ya mji.

Miaka hiyo hapa nyumbani hali ilikuwa ngumu kidogo na ukifika Nairobi unashangazwa na kila kitu.

Ilikuwa umemtoa mtu upande wa Mashariki wa Ukuta wa Berlin ukamshusha upande wa Magharibi.

Naangalia gazeti la Nation upande wa matangazo ya burudani.

Nikaona kuna movie "Heritage Africa," inacheza Nairobi Cinema.

Hii ilikuwa "theatre" ya sifa enzi hizo.

Nikaenda kuangalia movie hii na hadi leo imenikaa kichwani mwangu.

Kisa cha kijana aliyejaaliwa akili zisizo za kawaida na akasoma vizuri Ghana iliyokuwa chini ya ukoloni wa Waingereza akafika hadi Uingereza.

Kijana akashika nafasi ambayo Mwafrika kabla yake hakupata kufikia.

Kichwa kikatuna akawa Mzungu Mwingereza kupita Mwingereza mwenyewe.

Huyu kijana mama yake alipoona mwanae kafika juu kuliko mategemeo ya mtu yeyote akafunga safari kuja Accra mjini kumkabidhi kijana wake mikoba ya wazee wake waliomtangulia ambao walikuwa watu wakubwa wa kuheshimika katika jamii.

Hii mikoba ilikuwa kitu chenye thamani kinachobeba historia ya ukoo toka enzi na enzi kutoka kizazi kimoja hadi kingine.

Mama akamsisitizia mwanae ahakikishe kuwa hakimtoki anakitunza hadi mwisho wa maisha yake.

Akamwambia katika ukoo wao hiyo ni hazina isiyomithilika na ilipatikana kwenye vita kubwa aliyopigana huyo ambae yeye kachukua jina lake.

Ambacho mama hakujua ni kuwa mwanae hakuwa kama babu zake wakuu waliopita.

Yeye alikuwa Mzungu Mweusi aliyekwisha uhama Uafrika.

Aliitazama ile kinga aliyopokea kwa mama yake na kwake alichokiona ni hazina ya thamani kutoka ustaarabu wa kale wa babu zake unaopashwa kuwa katika maonyesho London, British Museum siyo nyumbani kwake ati ndiyo kinga yake.

Huyu kijana kwa kujipendekeza akampelekea ile hazina District Commissioner (DC) ili aifikishe London kwa wataalamu wa mambo ya kale.

Haukupita muda akavamiwa nyumbani kwake na wazalendo wapigania uhuru kwa nia ya kumuua kwa kuwa yeye alikuwa adui wa wananchi sawa na wakoloni.

Bahati nzuri kwake alinusurika kifo.

Mama yake aliposikia mwanae kanusurika kuuawa akaja mjini kumwangalia.

Akamuuliza, "Kile kitu nilichikupa unacho?"

Kijana akajibu, "Sinacho mama nimempa mkubwa wangu Mzungu akipeleke Uingereza."

Mama alishika kichwa machozi yakimbubujika, "Mwanangu katika ukoo na jamii yetu hapajatokea mtu aliyekuwa na akili zako.

Umeongoza darasani kuanzia darasa la kwanza hadi umekwenda kusoma Ulaya vipi utakuwa mjinga kiasi hiki kukabidhi kinga yetu kwa Mzungu?"

Haukupita muda mrefu kijana aliuliwa na yule yule DC Mzungu aliyempa hazina ya ukoo.

Alikwenda kwake usiku kuidai kinga yake na katika majibizano silaha zilitolewa na ndugu yetu ndiye aliyeuawa kwa kupigwa risasi.

Msomaji wangu hujapata kuona mambo ukajiuliza vipi hili likatendwa na huyu ambae jamii ikimuona ni mtu aliye na akili?

Vipi katenda haya kama jitu ambalo halina elimu yoyote?
Screenshot_20201228-183039.jpg
 
Mzee Mohamed...ulichosahau ni kuwa kusoma kwingi na akili nyingi huweza kumuongezea mtu maarifa lakini sio busara, huyo kijana alikosa busara ndio maana akatenda yalioonekana kama ujinga! waswahili tunasema "Ujanja mwingi mbele kiza"
 
Mohamed Said, Kilembwe,

..vipi ikiwa mhusika amesilimu au amekuwa mkristo je inaswihi kuendeleza mambo ya "kienyeji" ya mababu na mabibi zake?

..wengi mnasahau kwamba kuna baadhi ya Waislamu na Wakristo ambao waliingia ktk imani hizo wakiwa MASHULENI.

..Je, kosa la huyo msomi ni kuikataa mikoba aliyopewa na mama yake, au kosa ni kuikabidhi mikoba hiyo kwa mzungu?

..Je, msomi, Shekhe, Askofu, ... wa jamii yetu Waafrika anapaswa kuwa na hirizi pamoja na "mitambo" mingine ya jadi za mababu na mabibi?

..Jambo lingine ambalo naona hamjalizingatia ni kwamba sinema hiyo imechezwa Afrika Magharibi, na ndugu zetu baadhi yao wanaweza kuwa Waislamu au Wakristo "wazuri" tu, waliohifadhi Quran na Biblia kwelikweli, lakini humohumo wanachanganya na mambo yao ya kienyeji / ndumba.

..Sinema nyingi za ndugu zetu wa Afrika Magharibi lazima zihusishe mambo ya ndumba. Nazichukia kwelikweli.

cc Nguruvi3, Kiranga
 
Mohamed Said, Kilembwe,

..vipi ikiwa mhusika amesilimu au amekuwa mkristo je inaswihi kuendeleza mambo ya "kienyeji" ya mababu na mabibi zake?

..wengi mnasahau kwamba kuna baadhi ya Waislamu na Wakristo ambao waliingia ktk imani hizo wakiwa MASHULENI.

..Je, kosa la huyo msomi ni kuikataa mikoba aliyopewa na mama yake, au kosa ni kuikabidhi mikoba hiyo kwa mzungu?

..Je, msomi, Shekhe, Askofu, ... wa jamii yetu Waafrika anapaswa kuwa na hirizi pamoja na "mitambo" mingine ya jadi za mababu na mabibi?

..Jambo lingine ambalo naona hamjalizingatia ni kwamba sinema hiyo imechezwa Afrika Magharibi, na ndugu zetu baadhi yao wanaweza kuwa Waislamu au Wakristo "wazuri" tu, waliohifadhi Quran na Biblia kwelikweli, lakini humohumo wanachanganya na mambo yao ya kienyeji / dumba.

..Sinema nyingi za ndugu zetu wa Afrika Magharibi lazima zihusishe mambo ya ndumba. Nazichukia kwelikweli.

cc Nguruvi3, Kiranga
JokaKuu,
Sina langu katika hayo niloyoandika.

Nimekileta kisa tuburudike kama hivi kila mtu kutoa mawazo yake.
 
Very interesting insight..

Kila siku katika maisha yetu tunaonana na watu wa aina hii
Wana akili sana yet wapumbavu wa mwisho..
 
Akili ni nini?

Je kukumbatia zama/imani ambazo kwazo kupitia elimu (ambayo ndio humtoa mtu ujinga na kumpa "akili" ) kunamfanya mtu kuitwa mjinga kwa namna ambavyo elimu ilivyompa akili?

Je kuasi au kuacha kufata tamaduni yako kutokana na namna mpya uliyopata ya kufikiri (kupitia shule/kusoma) kunakupa ubatizo wa kuwa wewe ni mjinga?

Je akili ya mtu inawezwa kupimwa nje ya tamaduni yake?...au ujinga wa mtu unawezwa kupimwa kupitia utamaduni au mila ya mtu mwingine?
 
Mzee MS yeye mwenyewe katupilia mbali ubini wa majina ya Kimanyema.
Plato...
Majina yangu yote ninayo ila huwezi mtu ukaandika majina yote.

Mimi ni Mohamed Said Salum Abdallah Mwekapopo Samitungo Muyukwa.

Licha ya majina ya wazee wangu naijua hata historia yao.
 
Mohamed Said, Kilembwe,

..vipi ikiwa mhusika amesilimu au amekuwa mkristo je inaswihi kuendeleza mambo ya "kienyeji" ya mababu na mabibi zake?

..wengi mnasahau kwamba kuna baadhi ya Waislamu na Wakristo ambao waliingia ktk imani hizo wakiwa MASHULENI.

..Je, kosa la huyo msomi ni kuikataa mikoba aliyopewa na mama yake, au kosa ni kuikabidhi mikoba hiyo kwa mzungu?

..Je, msomi, Shekhe, Askofu, ... wa jamii yetu Waafrika anapaswa kuwa na hirizi pamoja na "mitambo" mingine ya jadi za mababu na mabibi?

..Jambo lingine ambalo naona hamjalizingatia ni kwamba sinema hiyo imechezwa Afrika Magharibi, na ndugu zetu baadhi yao wanaweza kuwa Waislamu au Wakristo "wazuri" tu, waliohifadhi Quran na Biblia kwelikweli, lakini humohumo wanachanganya na mambo yao ya kienyeji / ndumba.

..Sinema nyingi za ndugu zetu wa Afrika Magharibi lazima zihusishe mambo ya ndumba. Nazichukia kwelikweli.

cc Nguruvi3, Kiranga
Mi nauliza, Kuna ubaya gani mtu akawa mkristo au muislamu mzuri tu, lakin bado akawa anazingatia mila za mababu zake, Kama matambiko na kinga? Kwanini waafrika tunadharau mila zetu na kuabudu za wazungu? Mbona babu zetu waliheshimu mila, na waliomba mvua ikanyesha kwa wakati, walimfanyia dawa mgumba akazaa nk? Kwanini sasa sisi tunazidharau mila zetu kama zinatusaidia? Angalia Wachagga ni watu wa dini kweli, lakin mtu asikudanganye hakuna watu wanajali mila kama wao, kuanzia mtu anapozaliwa mpaka anapokufa, na hata mwisho wa mwaka wanaenda kufanya matambiko kwa mizimu.. Angalia nchi nzima wao wanaongoza kwa kufanya vizuri na utajiri. Ni muda sasa tuache ujinga na kufata mila za wazee wetu!!
 
Mohamed Said, Kilembwe,

..vipi ikiwa mhusika amesilimu au amekuwa mkristo je inaswihi kuendeleza mambo ya "kienyeji" ya mababu na mabibi zake?

..wengi mnasahau kwamba kuna baadhi ya Waislamu na Wakristo ambao waliingia ktk imani hizo wakiwa MASHULENI.

..Je, kosa la huyo msomi ni kuikataa mikoba aliyopewa na mama yake, au kosa ni kuikabidhi mikoba hiyo kwa mzungu?

..Je, msomi, Shekhe, Askofu, ... wa jamii yetu Waafrika anapaswa kuwa na hirizi pamoja na "mitambo" mingine ya jadi za mababu na mabibi?

..Jambo lingine ambalo naona hamjalizingatia ni kwamba sinema hiyo imechezwa Afrika Magharibi, na ndugu zetu baadhi yao wanaweza kuwa Waislamu au Wakristo "wazuri" tu, waliohifadhi Quran na Biblia kwelikweli, lakini humohumo wanachanganya na mambo yao ya kienyeji / ndumba.

..Sinema nyingi za ndugu zetu wa Afrika Magharibi lazima zihusishe mambo ya ndumba. Nazichukia kwelikweli.

cc Nguruvi3, Kiranga
Asili yetu ni hayo unayoita ndumba, tusisahau mila na desturi zetu na kukazania dini zilizoletwa na wakoloni... Kwa nini kila taratibu walizozikuta Africa zionekane hazifai? Ila tamaduni za wakoloni ndizo zionekane zinafaa? Ukristo /uislamu ni dini za wazungu/waarabu na ni tamaduni za wakoloni.

Tunatakiwa tukumbuke katika miiko, taratibu, mila na desturi zetu watu weusi.

Mbona hatushangai kuna Mataifa yanayofuata Buddhism, Hinduism na huko kote wanafuata tamaduni zao na si za wazungu? Hawa wapo sahihi ndio maana hata kuendelea imewezekana.

Angalia sisi hata kujiongoza tu ni shida kwa kuwa tumerukia mambo ambayo hayatufai. Njia zetu za asili za kuongoza zilikuwa Safi sana na tuliishi vizuri na taratibu zilifuata.

Sasa angalia kufuata ya mkoloni imetuletea viongozi ambao ni wakoloni weusi pia wanyonyaji.

Tufuate vya kwetu.

Sent from my STK-L21 using JamiiForums mobile app
 
Mi nauliza, Kuna ubaya gani mtu akawa mkristo au muislamu mzuri tu, lakin bado akawa anazingatia mila za mababu zake, Kama matambiko na kinga? Kwanini waafrika tunadharau mila zetu na kuabudu za wazungu. Mbona babu zetu waliheshimu mila, na waliomba mvua ikanyesha nk? Kwanini sasa sisi tunadharau kama inatusaidia?
Na sasa mvua isiponyesha ukiomba mvua haiji unaambiwa Mungu hujibu kwa wakati wake....
Kama sina chakula leo... Nikiomba Mungu atanipa hata baada ya miaka 10 ndicho tunachoambiwa ni sahihi.!

Tumejisahau sana sisi Waafrika.

Sent from my STK-L21 using JamiiForums mobile app
 
Mohamed Said, Kilembwe,

..vipi ikiwa mhusika amesilimu au amekuwa mkristo je inaswihi kuendeleza mambo ya "kienyeji" ya mababu na mabibi zake?

..wengi mnasahau kwamba kuna baadhi ya Waislamu na Wakristo ambao waliingia ktk imani hizo wakiwa MASHULENI.

..Je, kosa la huyo msomi ni kuikataa mikoba aliyopewa na mama yake, au kosa ni kuikabidhi mikoba hiyo kwa mzungu?

..Je, msomi, Shekhe, Askofu, ... wa jamii yetu Waafrika anapaswa kuwa na hirizi pamoja na "mitambo" mingine ya jadi za mababu na mabibi?

..Jambo lingine ambalo naona hamjalizingatia ni kwamba sinema hiyo imechezwa Afrika Magharibi, na ndugu zetu baadhi yao wanaweza kuwa Waislamu au Wakristo "wazuri" tu, waliohifadhi Quran na Biblia kwelikweli, lakini humohumo wanachanganya na mambo yao ya kienyeji / ndumba.

..Sinema nyingi za ndugu zetu wa Afrika Magharibi lazima zihusishe mambo ya ndumba. Nazichukia kwelikweli.

cc Nguruvi3, Kiranga
Huyo msomi alipaswa kuikataa hiyo mikoba kama aliona kuwa hakuihitaji. Kuikubali na kisha kuigawa kwa Mzungu hakutenda haki.
 
Back
Top Bottom