Inakuchukua muda gani kuanza kutafuta mpenzi baada ya kuachana?

farfat

Senior Member
Jun 10, 2021
158
265
Tupo katika kipindi cha toba kwa dini zote, Islamic na Christian tupo katika Ramadan na Kwa Resma, ni matumaini yangu mnashirki vyema na Mungu awabariki.

Kwa hakika mahusiano hayajawahi kuwa rahisi iwe katika uchumba ama ndoa. Kuna ups n down nyingi za kukatisha tamaa, ila wakudumu wanadumu na wakuachana wanaachana.

Lengo hasa la kuleta uzi huu kwenu wanajukwaa wenzangu ni kutaka kujua, huwa mnatumia njia gani kujipooza na maumivu ya kuachana na mwenzi kwa sababu yoyote ile na huchukua muda upi kuanza kutafuta mpenzi mpya wa kuanza nae mahusiano mapya?

Najua fika changamoto ni nyingi na haziishi, hata mpenzi mpya nae huja na changamoto zake (no body is perfect ). Je, kuna haja ya kutafuta mpenzi mpya kwa haraka ili aje ku kuziba nafasi ya mwenzi alietoka?

Vipi kwa ME na KE, uharaka na utayari wa kuanza upya umekaaje?

ANGALIZO: Mpenzi unaemtaka wewe hutengenezwa na wewe mwenyewe na sio jambo rahisi kumtengeneza huyo mtu na ndio maana maumivu huwa makali mtu huyo mkiachana.

Muwe na mfungo mwema.

Alamsik.
 
Kwanza mwanaume unaanzaje tu kuwa na mwanamke mmoja pekee? Wanawake wapo wengi Sana tena wa kumwaga, unajichagulia idadi unayotaka mwenyewe.

Kwa hiyo ukiachana na mmoja wait unaendelea na yule mwingine/ wengine. Kwenye mahusiano lazima uwe na back up mazee.
 
Tupo katika kipindi cha toba kwa dini zote, Islamic na Christian tupo katika Ramadan na Kwa Resma, ni matumaini yangu mnashirki vyema na Mungu awabariki.



Alamsik.
Sikaagi muda mrefu mimi napenda Mapenzi.. Hapa nilipo natafuta bado yaani nikimuacha nilienae nakua active sana na wanaonitongoza kutafuta mwingine.
 
Pale nyege zinapochukua hatam kiti cha mbele kabisa na huwezijizuia , hasa kipindi cha mvua, kama hichi
 
Sikaagi muda mrefu mimi napenda Mapenzi.. Hapa nilipo natafuta bado yaani nikimuacha nilienae nakua active sana na wanaonitongoza kutafuta mwingine.
Kwa kiasi kikubwa nilichokiona ni kwamba ktk kuachana mwanamke huwa haumii sana tofauti na mwanaume but inategemea na hali ya kuachana.. majuto kwa mwanamke huja baadae sana
 
Siku hiyo hiyo tu tafuta mtu mwingine. Hakunaga mambo ya kupendana na kuwekana mioyoni zama hizi
 
ni bora ujipe muda kidogo kwasababu unaweza kuanzisha mahusiano ili kuondoa maumivu ila siku maumivu yakiisha ndo utagundua kua uliyenae humpendi, shida nyingine ndo zitaanzia hapo
 
Hakuna muda maalum.

Ila ni vyema kuishi mwenyewe kwanza, kujitathmini na kuponyesha maumivu ya hisia.

Itasaidia kujua wewe binafsi ulikosea wapi na ufanyaje ili makosa Yako yaliyochangia kuachana yasijitokeze tena.

Inasaidia kuwa mpya, kujipenda, kusamehe , hivyo itakuwa rahisi wewe kupenda upya tena mtu mwenye vigezo unavyotaka.

Inasaidia kujua maisha yanawezekana bila mwingine, hivyo kujifunza kutafuta furaha Yako bila kutegemea uipate Kwa mwingine.

Mwisho kabisa utaingia kwenye mahusiano mapya ukiwa na Ari ya upendo lakini pia hutaumia sana ikiwa mwisho utakuwa mbaya
 
Back
Top Bottom