tpaul
JF-Expert Member
- Feb 3, 2008
- 21,484
- 17,678
Habari wana MMU? Naingia kwenye mada moja kwa moja bila kuwachosha. Naomba kuwashirikisha kisa kimoja na mpenzi wangu Salma. Tumekuwa kwenye mahusiano kwa takribani miaka 2 ijapokuwa kimtindo. Siku za nyuma nilimfungulia kibiashara akawa anajishughulisha nacho lakini baadaye alikula mtaji biashara ikafa. Pamoja na kula mtaji bado nilikuwa nimepanga kumfufulia biashara au kumfungulia biashara nyingine.
Mwezi uliopita nilisafiri kwenda Mwanza lakini kabla ya kusafiri nilimuita aje nikate kiu na kumuachia pesa ya matumizi. Nilimpigia na kumtumia sms nyingi lakini hakuja. Huwa ana kawaida hii lakini mm niliamua kuendelea naye kwa kuwa hunipa kitu roho inapenda. Na pia sio mwaminifu kiviiile lakini naenda naye hivyo hivyo.
Nilipoona hataki kuja kwangu nimuachie pesa na kukata kiu, nikaondoka zangu. Nilipofika Mwanza nikakaa siku 3 nikaona sms yake akiniomba nimtumie pesa ya matumizi. Sikumtumia aisee. Huwa sifanyi ujinga huo. Nilimuambia asubiri hadi nirudi maana kabla ya kuondoka nilimuomba apitie pesa ya matumizi hakutaka kuja.
Basi nimekaa huko Mwanza yapata mwezi mmoja kisha nikarudi huku mkoani. Baada ya kurudi nilimpigia simu aje kuchukua pesa ya matumizi akawa haji. Baadaye nikaanza kumbebeleza ndipo akaja sasa. Alipokuja si akaanza kuniwekea masharti kwamba bila kumfungulia biashara hataki nikate kiu. Nikamuangalia nikasema huyu dawa yake nyepesi. Nikamuacha aondoke aniache na kiu yangu lakini nikaapa kutomtafuta tena.
Hivi sasa nipo kwenye mchakato wa kutafuta mpenzi mpya. Unajua mpenzi wako wa KIKE akishajua kwamba unamshobokea sana huanza kuleta nyodo. Nimeamua kumuacha mazima huyu mshenzi, hawezi kuniwekea masharti kwenye issue za mapenzi. Atakuwa kanichoka anatafuta sababu ya kuachana. Kwani kuachana shilingi ngapi? Akafie huko mbele nitapata mpenzi mwingine bora kulikp yeye. Mpuuzi mkubwa!
Kuna baadhi ya watu nimewasimulia kisa hiki wamenilaumu kuwa nimefanya uamuzi wa kukurupuka. Hebu niambie tatizo langu ni lipi katika huu muachano.
Mwezi uliopita nilisafiri kwenda Mwanza lakini kabla ya kusafiri nilimuita aje nikate kiu na kumuachia pesa ya matumizi. Nilimpigia na kumtumia sms nyingi lakini hakuja. Huwa ana kawaida hii lakini mm niliamua kuendelea naye kwa kuwa hunipa kitu roho inapenda. Na pia sio mwaminifu kiviiile lakini naenda naye hivyo hivyo.
Nilipoona hataki kuja kwangu nimuachie pesa na kukata kiu, nikaondoka zangu. Nilipofika Mwanza nikakaa siku 3 nikaona sms yake akiniomba nimtumie pesa ya matumizi. Sikumtumia aisee. Huwa sifanyi ujinga huo. Nilimuambia asubiri hadi nirudi maana kabla ya kuondoka nilimuomba apitie pesa ya matumizi hakutaka kuja.
Basi nimekaa huko Mwanza yapata mwezi mmoja kisha nikarudi huku mkoani. Baada ya kurudi nilimpigia simu aje kuchukua pesa ya matumizi akawa haji. Baadaye nikaanza kumbebeleza ndipo akaja sasa. Alipokuja si akaanza kuniwekea masharti kwamba bila kumfungulia biashara hataki nikate kiu. Nikamuangalia nikasema huyu dawa yake nyepesi. Nikamuacha aondoke aniache na kiu yangu lakini nikaapa kutomtafuta tena.
Hivi sasa nipo kwenye mchakato wa kutafuta mpenzi mpya. Unajua mpenzi wako wa KIKE akishajua kwamba unamshobokea sana huanza kuleta nyodo. Nimeamua kumuacha mazima huyu mshenzi, hawezi kuniwekea masharti kwenye issue za mapenzi. Atakuwa kanichoka anatafuta sababu ya kuachana. Kwani kuachana shilingi ngapi? Akafie huko mbele nitapata mpenzi mwingine bora kulikp yeye. Mpuuzi mkubwa!
Kuna baadhi ya watu nimewasimulia kisa hiki wamenilaumu kuwa nimefanya uamuzi wa kukurupuka. Hebu niambie tatizo langu ni lipi katika huu muachano.