Hajar nakubaliana ma
AmorEy kwa asilimia mia. Siku hizi hakuna taarabu bali uchafu na uchafuzi tu wenyewe wanaita Taradance!
Wasikilize Culture na Nad Ikhwan Swafaa au Malindi ukipenda, kisha rudi nyuma enzi za kina Almarhum Shakila Said, Mwanahela
Asma Hani, Sharmila, Ursulla kwenye mashairi ya kumtoa nyoka pangoni(sio nyoka yule lakini) na sauti za vinanda haswaa
Nenda nchi jirani ya Kenya utafute nyimbo za kina Matano Juma, Juma Bhalo(Mungu Amrehemu), Maulid Juma, Zuhura Swaleh na wengineo uone utajiri wa muziki wa taarabu asilia
Siku hizi hakuna kitu na ndio wanatukanisha Taarabu hao