A
Anonymous
Guest
Mimi ni mwandishi katika moja ya magazeti hapa Nchini Tanzania na memba wa miaka mingi wa Jamii Forums, katika majukumu yangu nimefanikiwa kupata nafasi ya kuandika makala na habari mbalimbali za kijamii, kuna hii moja kuhusu Jeshi la Magereza, nilivyomgusia Mhariri wangu akakataa kuitumia.
Nikaona kuliko kuwa kimya bora na kwa kuwa nimeshaifanya bora nitumie platform ya JF kufikisha ujumbe huu hata kama sitajulikana lakini naamini nitakuwa nimewasaidia Watanzania wenzangu wengi kama mamlaka zitaamua kuchukua hatua:
Makala yenyewe inahusu hivi:
Baadhi ya Askari wa Magereza wa Gereza la Ukonga Jijini Dar es Salaam inadaiwa wanajigharamikia kuwasafirisha watuhumiwa kwenda mikoani bila kurejeshewa pesa zao kwa wakati huku wakidai kuna ubaguzi katika kulipa pesa hiyo.
Mmoja kati ya maofisa wa Gereza hilo ambaye hakutaka jina lake litajwe amedai changamoto hiyo ni kubwa ambapo amedai wanaodai pesa yao ni wengi lakini hawana sehemu ya kueleza kero hiyo kwa kuwa mazingira yaliyopo ni kwamba Askari akikosoa suala hilo au kuhoji anatishiwa kuhamishwa kupelekwa maeneo ya pembezoni, hali hiyo imeendelea kuwafanya wawe na hofu ya kueleza changamoto zao.
"Malalamiko makubwa ambayo yapo kwetu ni kwamba tunadai kuanzia malipo yetu ya kuanzia Mwaka 2015 mpaka mwaka huu (2023) lakini inaonekana kwamba madeni ya 2015 yameshalipwa na yamefutwa lakini walilipwa watu wachache sana wengine hatukulipwa" ameeleza Ofisa huyo.
Anaendelea kueleza "Na sasa hivi wanasema watalipa madeni kwamba waliomba Shilingi Bilioni 6 lakini wamepewa Shilingi Bilioni 3, cha kushangaza mfano mimi kuna watu unaweza kwenda nao safari wao wanalipwa baada ya kutumia gharama zao lakini wewe ulipwi miaka na miaka.
“Wanaopewa kipaumbele cha kulipwa kama mkisafiri nao mara nyingi ni wale Maafisa wakubwa lakini wenzangu na mimi huku chini Mungu saidia.
“Hakuna sababu za wazi kwa nini hawatulipi, tunahisi kuna upigaji maana wanajua hakuna wa kusema popote huo ndio utamaduni uliojengwa.
"Yaani kinachoonekana zile hela zimeshatolewa lakini watu wamezipiga na kila tunapojaribu kuhoji chinichini tunatishiwa kuhamishwa kupelekwa porini ambako huwezi kuonana na mtu yeyote anayeweza kukusaidia.
"Tunaomba mtusaidie sisi kupaza sauti hatuna pa kusemea tunapokuwa tunasema wanatukandamiza tunaonekana kabisa tunaonewa na ukitaka kusema utaambiwa askari unatakiwa kuwa mvumilivu.
"Mfano inapotokea unampeleka mtuhumiwa Tabora, Mwanza, Mbeya, Kagera au Rukwa yule mtuhumiwa analipiwa nauli na kila kitu na Serikali lakini mimi nauli najigharamikia, hela ya gesti mimi, nauli na chakula kila kitu mimi unakuta tayari nimeshadhulumu familia yangu kisha malipo yenyewe yanakaa kwa muda mrefu.
“Unaweza kukuta yamekaa miaka saba ndio mnakuja kulipwa na kulipwa kwenyewe hamlipwi madeni yote," anasema Ofisa huyo.
Anadai kuwa changamoto hiyo pia ipo kwenye baadhi ya magereza mengine yaliyopo Nchini.
Katika kufahamu sababu ambazo upelekea watuhumiwa kutumia usafiri wa umma Ofisa huyo anasema "Kulingana na kwamba magari ni shida tunatumia mabasi na tunalipa nauli kutoka mifukoni mwetu."
Aidha, Ofisa mwingine (jina kapuni) kutoka Gereza la Ukonga amedai changamoto hiyo ipo lakini kumekuwepo na hofu kubwa ya wadai kuchukua hatua kutokana na mazingira yanayowazunguka.
"Hili jambo tungekuwa kwenye sekta nyingine lingeshasikika sana lakini huku sisi hatuna sauti, tunaumia sana, wanakwambia uende na risiti, lakini inapita miaka bila kulipwa, tunavunjika moyo tunaomba mtusemee sisi huku hatuwezi kusema utaamka asubuhi umeamishwa."
Naongeza kuwa kutokana kuwepo kwa utamaduni wa hofu imepelekea pia baadhi ya Askari Magereza kukosa pesa za likizo pamoja na pesa nyingine ambazo hutakiwa kutolewa kwa nyakati tofauti kulingana na taratibu.
Nikaona kuliko kuwa kimya bora na kwa kuwa nimeshaifanya bora nitumie platform ya JF kufikisha ujumbe huu hata kama sitajulikana lakini naamini nitakuwa nimewasaidia Watanzania wenzangu wengi kama mamlaka zitaamua kuchukua hatua:
Makala yenyewe inahusu hivi:
Baadhi ya Askari wa Magereza wa Gereza la Ukonga Jijini Dar es Salaam inadaiwa wanajigharamikia kuwasafirisha watuhumiwa kwenda mikoani bila kurejeshewa pesa zao kwa wakati huku wakidai kuna ubaguzi katika kulipa pesa hiyo.
Mmoja kati ya maofisa wa Gereza hilo ambaye hakutaka jina lake litajwe amedai changamoto hiyo ni kubwa ambapo amedai wanaodai pesa yao ni wengi lakini hawana sehemu ya kueleza kero hiyo kwa kuwa mazingira yaliyopo ni kwamba Askari akikosoa suala hilo au kuhoji anatishiwa kuhamishwa kupelekwa maeneo ya pembezoni, hali hiyo imeendelea kuwafanya wawe na hofu ya kueleza changamoto zao.
"Malalamiko makubwa ambayo yapo kwetu ni kwamba tunadai kuanzia malipo yetu ya kuanzia Mwaka 2015 mpaka mwaka huu (2023) lakini inaonekana kwamba madeni ya 2015 yameshalipwa na yamefutwa lakini walilipwa watu wachache sana wengine hatukulipwa" ameeleza Ofisa huyo.
Anaendelea kueleza "Na sasa hivi wanasema watalipa madeni kwamba waliomba Shilingi Bilioni 6 lakini wamepewa Shilingi Bilioni 3, cha kushangaza mfano mimi kuna watu unaweza kwenda nao safari wao wanalipwa baada ya kutumia gharama zao lakini wewe ulipwi miaka na miaka.
“Wanaopewa kipaumbele cha kulipwa kama mkisafiri nao mara nyingi ni wale Maafisa wakubwa lakini wenzangu na mimi huku chini Mungu saidia.
“Hakuna sababu za wazi kwa nini hawatulipi, tunahisi kuna upigaji maana wanajua hakuna wa kusema popote huo ndio utamaduni uliojengwa.
"Yaani kinachoonekana zile hela zimeshatolewa lakini watu wamezipiga na kila tunapojaribu kuhoji chinichini tunatishiwa kuhamishwa kupelekwa porini ambako huwezi kuonana na mtu yeyote anayeweza kukusaidia.
"Tunaomba mtusaidie sisi kupaza sauti hatuna pa kusemea tunapokuwa tunasema wanatukandamiza tunaonekana kabisa tunaonewa na ukitaka kusema utaambiwa askari unatakiwa kuwa mvumilivu.
"Mfano inapotokea unampeleka mtuhumiwa Tabora, Mwanza, Mbeya, Kagera au Rukwa yule mtuhumiwa analipiwa nauli na kila kitu na Serikali lakini mimi nauli najigharamikia, hela ya gesti mimi, nauli na chakula kila kitu mimi unakuta tayari nimeshadhulumu familia yangu kisha malipo yenyewe yanakaa kwa muda mrefu.
“Unaweza kukuta yamekaa miaka saba ndio mnakuja kulipwa na kulipwa kwenyewe hamlipwi madeni yote," anasema Ofisa huyo.
Anadai kuwa changamoto hiyo pia ipo kwenye baadhi ya magereza mengine yaliyopo Nchini.
Katika kufahamu sababu ambazo upelekea watuhumiwa kutumia usafiri wa umma Ofisa huyo anasema "Kulingana na kwamba magari ni shida tunatumia mabasi na tunalipa nauli kutoka mifukoni mwetu."
Aidha, Ofisa mwingine (jina kapuni) kutoka Gereza la Ukonga amedai changamoto hiyo ipo lakini kumekuwepo na hofu kubwa ya wadai kuchukua hatua kutokana na mazingira yanayowazunguka.
"Hili jambo tungekuwa kwenye sekta nyingine lingeshasikika sana lakini huku sisi hatuna sauti, tunaumia sana, wanakwambia uende na risiti, lakini inapita miaka bila kulipwa, tunavunjika moyo tunaomba mtusemee sisi huku hatuwezi kusema utaamka asubuhi umeamishwa."
Naongeza kuwa kutokana kuwepo kwa utamaduni wa hofu imepelekea pia baadhi ya Askari Magereza kukosa pesa za likizo pamoja na pesa nyingine ambazo hutakiwa kutolewa kwa nyakati tofauti kulingana na taratibu.