In case You missed it: Watch Darwin's Nightmare!

Kuhusu suala la silaha sijui liko vipi, ila mengine yaliyosemwa kwenye hiyo filamu ni ukweli mtupu! Mimi nimeshuhudia wananchi wa Bukoba wakiuziwa hayo mapanki!
sio siri inabidi tuombe kwa ajili ya nchi yetu! Yaani hawa viongozi wetu wanasafirisha samaki wetu wazuri halafu wanatuletea samaki wenye mionzi!
 
mpendwa,

kwa nini usidownload, mbona ipo tele kwenye torrents?

jaribu na nina uhakika utafanikiwa

ubarikiwe sana

Glory to God!!
 
Yap yap ipo kwenye torrent kama una modem jiunge na kifurushi cha 1GB zen ishushe au kama unatumia mashine za job/chuo search kwa google torrent yake ipo mie mwenyewe nilidownload
 
Kaka ule ulooneshwa ktk muvi ile ni uhalisia wa maisha ya watu wa kanda ya ziwa kula mapanki n c uzushi,but tulibminishwa ni kutuchafua ili kuukwepa UKWELI usiofichika.
 
Leo nimeicheki tena, kweli japo yanayosemwa ni ya ukweli, lakini ililenga kutudhalilisha WATANZANIA.

Umedhalilishwa??
Movie imekudhalilisha? Kivipi?. Sasa umedhalilishwa na maisha ya watanzania wenzako?
Mwenyewe umesema yote uliyoona mle ni ukweli sasa umedhalilishwa kivipi?
Kilichokudhalilisha ni movie inayoonesha watoto wa mitaani, au biashara ya ngono au vikao vinavyofanyika ktk miji mikubwa na watawala wetu kwa kutumia pesa za walipa kodi.

Au mimi ndio sijakuelewa mkuu. Hebu fafanua umedhalilishwa vipi na nani.
 
Umedhalilishwa??
Movie imekudhalilisha? Kivipi?. Sasa umedhalilishwa na maisha ya watanzania wenzako?
Mwenyewe umesema yote uliyoona mle ni ukweli sasa umedhalilishwa kivipi?
Kilichokudhalilisha ni movie inayoonesha watoto wa mitaani, au biashara ya ngono au vikao vinavyofanyika ktk miji mikubwa na watawala wetu kwa kutumia pesa za walipa kodi.

Au mimi ndio sijakuelewa mkuu. Hebu fafanua umedhalilishwa vipi na nani.
mkuu asilimia kubwa ya wabongo tunapenda kusifiwa tu hatupendi kuelezwa ukweli,mfano lowasa alipotenda maovu kamati ya bunge ikayaweka wazi kwa kuponda utendaji wake alijiuzuru huku akisema amezalilishwa.pia hata JK nae malalamiko yake hususani hotuba yake ya majuzi analalamika hivyohivo.
Ukweli ni kwamba kilichopo kwenye move hiyo ni kweli mtupu apende asipende hiyo ndio hali halisi kama anaasira ya kudhalilishwa akajitoe muhanga ikulu kwani ndio imeongoza kumdhalilisha
 
Nimekaa mwanza kwa miaka minne,ni ukweli usiopingika kua mapanki ndio chakula kikuu na kinachopatikana kwa bei rahisi pale mwanza.hakuna aliedhalilishwa pale,illa kama wewe ni magamba lazima uhisi hivyo kwani ndio mlio zoea kuishi kwa kudanganya.
 
Niliyemuazima hakunirudishia miaka mine iliyopita. Sasa sijui kudhalilika kunakujaje. Kifupi,samaki anatolewa minofu inayopakiwa kwenye ndege kwenda kuuzwa nje kwa pesa nyingi! Wanaonyesha,mabaki ya kichwa na mfupa wa kiwiliwili,ndivyo vinavyoliwa pwani ya ziwa Victoria. Na maisha ya pwani hayo, uchangudoa,pombe haramu na za kienyeji, vibanda hasara,watoto wa mitaani wanavuta na kujifunza kunusa petroli,n.k. kisha ndege iliyopeleka nchi za nje minofu, inarudi na silaha[zilikuwa zinapelekwa nchi za jirani kwa waasi]. Darwin anaonyesha bila kuficha sura halisi ya tatizo. Watanzania tuna tatizo la unafiki na kutokuwa wazi. Kufunika chini ya kapeti matatizo.Wakati unapoweka wazi ndiyo mwanzo wa utatuzi wa kudumu.Mfano ajali za meli. Darwin alifanya kazi ambayo ingefanywa na tume ya watu kadhaa,na kulipwa mamilioni,na wakati mwingine wasifichue kila kitu,kwa vigezo dhaifu hivyo hapo juu.. Watanzania tubadilike!
 
mkuu ata mimi naitaji sijawahi kuiona,ntaipataje? msaada please!
 
Kipindi kile mama mmoja wa Kiingereza alihojiwa kuhusu hiyo movie akiwa Uk, alisema "kuanzia sasa sitanunuwa tena minofu ya sangara inayoletwa ulaya ili kudhibiti hali inayoendelea ukanda wa ziwa Victoria". Je sisi Watanzania tulichukuwa hatuwa gani? Kuipiga marufuku movie? Kuwa-harass waliompokea director wa ile movie? Still najiuliza. Yaani Muingereza kawa Mzalendo kwa Tanzania kuliko Watanzania wenyewe.
 
Back
Top Bottom