Johnsecond
JF-Expert Member
- May 4, 2010
- 1,076
- 211
Wakati kijana niliogopa sana kuwa na wapenzi wengi ila ilikuja ikatokea nikawa na wengi japo walipungua mpaka akabaki mmoja. kilichosababisha ni hiki hapa; nilikuwa nikimtongoza msichana akikataa naachana naye natongoza mwingine akikataa naenda kwa mwingine lakini kwa vipindi tofauti. Kumbe hawa watu ukimtongoza anakuweka kwenye waiting list, du zilikuja zamu zangu zikafika sehemu zote nikajiona kama super star vile (loveable) kumbe mpumbafu. Wengine wakitaka lunch tu, wengine simu, wengine viwanja, wengine biashara, wengine chips na wengine walitaka mapenzi tu na wengine kuolewa. Ni kipindi a,mbacho huwa sikisahau. Nawashauri watongozaji (Vijana) msibananishe sana vipindi vya kutongoza mtashindwa kuchagua wakikubari wote pamoja . . .