Samson Ernest
JF-Expert Member
- Aug 28, 2014
- 1,119
- 1,569
Yer 10:10 SUV
[10] Bali BWANA ndiye Mungu wa kweli; Ndiye Mungu aliye hai, Mfalme wa milele; Mbele za ghadhabu yake nchi yatetemeka, Wala mataifa hawawezi kustahimili hasira yake.
Imani zipo nyingi, kila mmoja anaweza akawa na mtazamo wake na uelewa wake kuhusu Mungu au miungu, wapo wanachanganya miungu mingine na Mungu, kwa kuamini wote tunabudu Mungu mmoja.
Wengine tunatamka vinywani Mungu mmoja, ila tukija kwenye ukweli tunagundua hatuna Mungu mmoja, wapo wana miungu mingine ila wanajidanganya ni Mungu mmoja.
Katika andiko hili, tunaona tamko hili la kipekee la kibiblia ambalo ni la kimonotheism, monotheism ni imani ya Mungu mmoja wa kweli.
Watu wanaoamini Mungu wa kweli katika Yesu Kristo, hao wanaweza kusema Mungu wao ni mmoja na wa kweli, nje na hapo sio Mungu wa kweli, na hamuwezi kuwa kitu kimoja katika imani na mtu asiyemwamini BWANA Yesu.
Moja ya mapingamizi na makatazo ya msingi aliyoyaweka Mungu wetu ni ibada ya sanamu, hapa ameonyesha vile miungu ya mataifa mengine ni ya uongo, sio hivyo tu haina uhai.
Mungu anajiweka bayana kuwa Yeye ni wa kweli na ana uhai, na sio sanamu sizizo na roho wala uhai wowote ndani yake, na haziwezi kusema chochote.
Unaweza kujiuliza Mungu wa kweli ni yupi? Mungu wa kweli ni yule aliyeumba mbingu na nchi ambapo tupo sasa, anayejifunua wazi kwa watu wake, ambaye ndani yake hakuna udanganyifu au uongo wowote.
Mwanzo 1:1
Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.
Tumewahi kuona au tunaona sanamu hazina uhai, hazina uwezo wa kuzungumza, hazitembei, na haziwezi kutenda jambo la maana.
Tofauti na Mungu wa Israeli, Yeye ni hai, anaongea, anatenda wazi wazi, anahukumu kwa haki, muumbaji wa vinavyoonekana na visivyoonekana, na anaweza kuingilia historia ya mtu na kuibadilisha kabisa.
Jambo ambalo miungu haina sifa hiyo, hata kama kuna watu wanaamini miungu yenye uhai, bado haina uwezo wa kuwa na sifa kama ya Mungu wa kweli, maana mwenye kutoa uhai ni Mungu wa kweli tu. Sifa yake kuu yupo kila mahali kwa wakati mmoja, ni wa milele, na anahukumu kwa haki, sifa ambayo hata Shetani hana.
Mungu huyu wa kweli sio wa Israeli tu, huyu ni Mungu wa mataifa yote au ulimwengu mzima, mataifa yote yana haki sawa ya kuwajibika kwa Mungu wao, hakuna upendeleo wala ubaguzi katika hili.
Kila mwamini au kila mmoja wetu anapaswa kumtazama Mungu kwa jicho lingine, hofu ya kiungu inapaswa kuwa ndani ya kila mwamini, toba ya kweli inapaswa kuwa sehemu ya maisha ya mwamini, na ibada ya kweli na safi inapaswa kuwa ndani ya mwamini.
Soma neno ukue kiroho
Liwe jua iwe mvua soma biblia na kutafakari
Mungu akubariki sana
Samson Ernest
[10] Bali BWANA ndiye Mungu wa kweli; Ndiye Mungu aliye hai, Mfalme wa milele; Mbele za ghadhabu yake nchi yatetemeka, Wala mataifa hawawezi kustahimili hasira yake.
Imani zipo nyingi, kila mmoja anaweza akawa na mtazamo wake na uelewa wake kuhusu Mungu au miungu, wapo wanachanganya miungu mingine na Mungu, kwa kuamini wote tunabudu Mungu mmoja.
Wengine tunatamka vinywani Mungu mmoja, ila tukija kwenye ukweli tunagundua hatuna Mungu mmoja, wapo wana miungu mingine ila wanajidanganya ni Mungu mmoja.
Katika andiko hili, tunaona tamko hili la kipekee la kibiblia ambalo ni la kimonotheism, monotheism ni imani ya Mungu mmoja wa kweli.
Watu wanaoamini Mungu wa kweli katika Yesu Kristo, hao wanaweza kusema Mungu wao ni mmoja na wa kweli, nje na hapo sio Mungu wa kweli, na hamuwezi kuwa kitu kimoja katika imani na mtu asiyemwamini BWANA Yesu.
Moja ya mapingamizi na makatazo ya msingi aliyoyaweka Mungu wetu ni ibada ya sanamu, hapa ameonyesha vile miungu ya mataifa mengine ni ya uongo, sio hivyo tu haina uhai.
Mungu anajiweka bayana kuwa Yeye ni wa kweli na ana uhai, na sio sanamu sizizo na roho wala uhai wowote ndani yake, na haziwezi kusema chochote.
Unaweza kujiuliza Mungu wa kweli ni yupi? Mungu wa kweli ni yule aliyeumba mbingu na nchi ambapo tupo sasa, anayejifunua wazi kwa watu wake, ambaye ndani yake hakuna udanganyifu au uongo wowote.
Mwanzo 1:1
Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.
Tumewahi kuona au tunaona sanamu hazina uhai, hazina uwezo wa kuzungumza, hazitembei, na haziwezi kutenda jambo la maana.
Tofauti na Mungu wa Israeli, Yeye ni hai, anaongea, anatenda wazi wazi, anahukumu kwa haki, muumbaji wa vinavyoonekana na visivyoonekana, na anaweza kuingilia historia ya mtu na kuibadilisha kabisa.
Jambo ambalo miungu haina sifa hiyo, hata kama kuna watu wanaamini miungu yenye uhai, bado haina uwezo wa kuwa na sifa kama ya Mungu wa kweli, maana mwenye kutoa uhai ni Mungu wa kweli tu. Sifa yake kuu yupo kila mahali kwa wakati mmoja, ni wa milele, na anahukumu kwa haki, sifa ambayo hata Shetani hana.
Mungu huyu wa kweli sio wa Israeli tu, huyu ni Mungu wa mataifa yote au ulimwengu mzima, mataifa yote yana haki sawa ya kuwajibika kwa Mungu wao, hakuna upendeleo wala ubaguzi katika hili.
Kila mwamini au kila mmoja wetu anapaswa kumtazama Mungu kwa jicho lingine, hofu ya kiungu inapaswa kuwa ndani ya kila mwamini, toba ya kweli inapaswa kuwa sehemu ya maisha ya mwamini, na ibada ya kweli na safi inapaswa kuwa ndani ya mwamini.
Soma neno ukue kiroho
Liwe jua iwe mvua soma biblia na kutafakari
Mungu akubariki sana
Samson Ernest