I'm a looser!!

I'm a looser!!

elegy

Member
Joined
Jul 19, 2017
Posts
12
Reaction score
7
habari ndg wa jf..nimatumaini yangu mko salama nami pia niko vzr kiafya japo kimawazo nikizungumkuti...
nihitaji kutoa historia fupi ya maisha yangu inayonifanya nijione tayari mm ni looser..

wazazi wangu waliachana nikiwa na umri wa miaka minne mwaka 1985...tangu kipindi hicho baba hakuwahi kuoa so niliishi nae japo kwa mahangaiko makubwa kwani alikuwa mtu wa urabu..hivyo mara nyingi nilijikuta naishi kwa majirani...masimango ..kudhalauliwa...mashaka vilikuwa sehemu ya maisha yangu...
mwaka 1997 nikahitimu shule ya msingi nikaamua kwenda mjini mwaka 1999 kutafuta...huko nikawa machinga...lakin hamu yangu kubwa ilikuwa nikusoma secondari...basi mungu saidia mwaka 2000 ndg wa baba akakutana na mama yangu huku mjin ikabidi amlete nilipokuwa naishi ukawa mwanzo wa kunfahamu

bahati mbaya mama nae alikuwa ametengana tena na mwanaume aliyekuwa amemuoa baada ya kutengana na baba so akawa anaendesha kesi ya kugawana mali walizochuma ..hakuweza kunipeleka shule japo aliniahidi akipata mgao wake angenipeleka shule....
mwaka 2005 akibidi ajitahidi niende shule japo kesi yake ilikuwa haijaisha ....so akawa barmaid ..iliniuma sana japo sikua na jinsi

mwaka 2015 nikahitimu shada ya elimu uwalimu wa arts ...bahati mbaya sana mama akafaliki nikiwa mwaka watatu semister ya mwisho...

ile kesi alikuwa anashinda lakni nguvu ya pesa ilitawala hivyo yule jamaa alikuwa anakata rufaa kila aliposhindwa..hadi mama anafaliki kesi ilikuwa mahakama kuu....

ilibidi nitafute ushauri wa kisheria hatimae nikasimama mahakamani kudai haki ya mama ..nashukuru mungu na huu utawala wakawa wamenikabidhi hiyo nyumba

ila tatzo nililo nalo ni hofu ya maisha kwani sijapata kazi..pili umri umesonga 36yrs sina mke wala mtoto..sina kaka wala dada...yaniii nahisi tayari i'm looser....

nafikilia niiuze hii nyumba ili nijipange na maisha ya kifamilia...je una ushauri wowote kwa hili? aksanteni kwa kusoma japo ndefu



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanini uuuze nyumba ya urithi????

Acha kujiita your loser na majina mengine. Unajua chochote unachokiwaza moyoni ndio hukutokea.

Wanaumwe 'hawazeeki'....

Swala la ajira ni kilio cha kila mtu Sasa hivi. Cha kufanya tafuta mtaji hata kidogo uanze biashara au kilimo.


Kuna jamaa Ni mlemavu alihitimu chuo mwaka 2016 au 15 kama sijakosea Ila Sasa hivi anamiliki hotel alianza kwa biashara ndogo tuu.
 
nafikilia niiuze hii nyumba ili nijipange na maisha ya kifamilia...je una ushauri wowote kwa hili? aksanteni kwa kusoma japo ndefu



Sent using Jamii Forums mobile app

Mimi nakushauri hivi:

Usiiuze hiyo nyumba. Ukiiuza ndo itakuwa imetoka hiyo na haitokuwa yako tena. Kwa sasa achana kabisa na hilo wazo. Nyumba ni mali ya msingi sana. Ukiiuza unaweza kuja kujuta vibaya sana huko mbeleni.

Pia acha kujiona wewe ni 'looser'. Hukuchagua kuwa na kukulia kwenye hayo mazingira uliyokulia. Hivyo hilo siyo kosa lako.
Kuwa na mke na mtoto/watoto siyo kila kitu maishani. Kuna watu wana wake [siyo mke tu] na watoto na maisha yao ni ya hovyo kupita kipimo.

Umesema una miaka 36. Mbona bado uko kijana sana. Kuna wanaume wanapata watoto wakiwa na miaka 50 na kuendelea. Hilo suala lako lisikukondeshe.

Umesema hujapata kazi. Hujapata kazi gani? Hiyo ya ualimu?

Kwa nini usitafute kibarua cha aina yoyote ile ujishikize nacho huku ukiendelea na juhudi za kutafuta kazi unayoitaka?

Usikate tamaa. Kama umeweza kukabiliana na madhila yote mpaka umefikia huo umri wa miaka 36 basi naamini utaweza kustahimili yaliyo ya sasa na hata ya baadaye.

Pambana. Usisalimu amri.
 
Pole sana. Hiyo nyumba ndiyo sehemu yako ya kuanzia maisha. Usiuze. Ukiuza hata mama yako huko alipo utamuongezea huzuni zaidi.
Tafuta shughuli yyte ya kufanya. Maisha ya kupanga ni magumu sana. Km sasa hiv hauna hela sasa ukiuza nyumba utaweza kulipia kodi ya chumba? Chumba kwa sasa cha bei ya chini ni 30,000
 
Mimi nakushauri hivi:

Usiiuze hiyo nyumba. Ukiiuza ndo itakuwa imetoka hiyo na haitokuwa yako tena. Kwa sasa achana kabisa na hilo wazo. Nyumba ni mali ya msingi sana. Ukiiuza unaweza kuja kujuta vibaya sana huko mbeleni.

Pia acha kujiona wewe ni 'looser'. Hukuchagua kuwa na kukulia kwenye hayo mazingira uliyokulia. Hivyo hilo siyo kosa lako.
Kuwa na mke na mtoto/watoto siyo kila kitu maishani. Kuna watu wana wake [siyo mke tu] na watoto na maisha yao ni ya hovyo kupita kipimo.

Umesema una miaka 36. Mbona bado uko kijana sana. Kuna wanaume wanapata watoto wakiwa na miaka 50 na kuendelea. Hilo suala lako lisikukondeshe.

Umesema hujapata kazi. Hujapata kazi gani? Hiyo ya ualimu?

Kwa nini usitafute kibarua cha aina yoyote ile ujishikize nacho huku ukiendelea na juhudi za kutafuta kazi unayoitaka?

Usikate tamaa. Kama umeweza kukabiliana na madhila yote mpaka umefikia huo umri wa miaka 36 basi naamini utaweza kustahimili yaliyo ya sasa na hata ya baadaye.

Pambana. Usisalimu amri.
asante mkuu...umenitia moyo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
You are not a looser,you are a winner,ndo maana umeshinda hata hiyo kesi,you are a winner ndo maana leo unasema 'nina nyumba',you are a winner ndio maana pamoja na kuchelewa kusoma leo unasema una bachelor digree.

Hebu kwanza jifunze kufikiri vizuri,forget your age,mwanaume hazeeki.

Hiyo nyumba kwako ni asset,kama vipi pangisha upate mtaji uanze biashara ndogondogo,habari ya ajira kwa sasa ni ngumu sana. Fanya yote ila nyumba usiuze rafiki.
 
ila tatzo nililo nalo ni hofu ya maisha kwani sijapata kazi..pili umri umesonga 36yrs sina mke wala mtoto..sina kaka wala dada...yaniii nahisi tayari i'm looser....

nafikilia niiuze hii nyumba ili nijipange na maisha ya kifamilia...je una ushauri wowote kwa hili? aksanteni kwa kusoma japo ndefu



Sent using Jamii Forums mobile app
You are not a loser, bado una miaka minne. Wanasemaga life begins at 40! Jitahidi mambo yatasonga. Alafu tafuta namna ya kujiajiri. Kutegemea kuajiriwa kwa sasa ni kupoteza muda.
 
Yu'll be a looser ukiuza nyumba
Uuze ili iweje sasa
Unategemea baada ya kuuza utapata hella
Uza ukiwa na a complete plan

IQ standard
 
Nyumba yako ina vyumba vingapi? Unaweza kufanya hivi.

1. Kupangisha chumba kimoja au viwili na wewe uwe unakaa hapo hapo, lakini utapata income kila mwezi.

2. Unaweza kuipangisha nyumba yote kwa mwaka mmoja, miwili au mitatu. Unanunua nyumba nyingine ndogo ya kuishi na pesa zingine zikabaki kwa matumizi na kuanzisha maisha.

Kama nyumba ina kiwanja kikubwa unaweza kuanza kujenga nyumba nyingine hapo hapo pole pole. Halafu baadaye uwe una nyumba mbili, moja ikakupa pesa nyingine ya kuishi.

3. Wewe ni mwalimu unaweza kuanzisha tuition kufundisha wanafunzi.

Usiiuze, itumie hiyo nyumba ikusaidie.
 
Wako wengi wanaopitia hali kama yako. Yaliyopita huwezi kuyabadili ila leo unaweza kuitumia vizuri uijenge kesho.
Pangisha chumba ktk hiyo nyumba upate mtaji. Anza kipato kidogo hata wakucheke.
See you on top
 
Kuzaliwa maskini sio kosa lako ila kufa maskini ni ujinga wako
Nyumba ni aset tosha Ya maisha pangisha baki na chumba 1 then utafute cha kufanya mbona ushabutua maisha ww, usisahau kumuombea mama yk mungu ampe pumziko la amani.

Sent from my TECNO-L8 using JamiiForums mobile app
 
Usikate tamaa kiongozi ,,age's just a number !!
MY TAKE; nyumba usiuze ni asset muhimu sana sababu hata ukiuza ukaoa iyo pesa itakwisha familia wataishije? Cha maana jishughulishe na kibarua chochote mkuu usiangalie elimu yako!!
Mfano; Reginald mengi jamaa mpambanaji sana kaja kuzaa uzeeni tena na mwanamke mrembo sana japo nlikuwa na watoto
NB; usitumie nguvu wala akili nyingi kuwaza kuoa eti 36 ni miaka mingi HAPANA hizo akili na nguvu wekeza kwenye kujiongezea kipato kwa namna mbalimbali iwe biashara au hata kuajiriwa kwa mshahara mdogo
 
Fanya utafiti, angalia chumba kimoja unaweza kupangisha kwa kiasi gani. Angalia unaweza kupangisha vyumba vingapi. Unataka kupangisha wasichana au wanaume, kwa muda gani. Unaweza kuanza na muda mfupi (short contract kama miezi sita hivi) ili kuona kama unapenda kupangisha au upendi. Pia angalia kama hata kama unaweza kuoa na kukaa kwenye vyumba viwili wewe na mke wako. Kuna vitu vyingi unaweza kufanya.

Pia ukipata mtaji unaweza kuanzisha biashara nyingine ndogo ndogo, kama kufuga kuku au kununua chakula mikoani na kuja kuuza Dar es Salaam.

Unasema huna ndugu, umeweza kutafuta familia ya mama yako ndugu zake vijijini kule? Pia jaribu kutafuta marafiki wazuri kwa sababu naona uko lonely kidogo. Umejitahidi sana mpaka ulipofika hapo kwenye maisha yako, tumia hizo hizo jitihada na utafika mbali mbeleni.

Usilinganize maisha yako na mtu mwingine yoyote, apo ndiyo stress kubwa inakuja, kila mtu ana historia yake. Watu wengine wanaota kuwa na nyumba na elimu kama yako.
 
Mimi nakushauri hivi:

Usiiuze hiyo nyumba. Ukiiuza ndo itakuwa imetoka hiyo na haitokuwa yako tena. Kwa sasa achana kabisa na hilo wazo. Nyumba ni mali ya msingi sana. Ukiiuza unaweza kuja kujuta vibaya sana huko mbeleni.

Pia acha kujiona wewe ni 'looser'. Hukuchagua kuwa na kukulia kwenye hayo mazingira uliyokulia. Hivyo hilo siyo kosa lako.
Kuwa na mke na mtoto/watoto siyo kila kitu maishani. Kuna watu wana wake [siyo mke tu] na watoto na maisha yao ni ya hovyo kupita kipimo.

Umesema una miaka 36. Mbona bado uko kijana sana. Kuna wanaume wanapata watoto wakiwa na miaka 50 na kuendelea. Hilo suala lako lisikukondeshe.

Umesema hujapata kazi. Hujapata kazi gani? Hiyo ya ualimu?

Kwa nini usitafute kibarua cha aina yoyote ile ujishikize nacho huku ukiendelea na juhudi za kutafuta kazi unayoitaka?

Usikate tamaa. Kama umeweza kukabiliana na madhila yote mpaka umefikia huo umri wa miaka 36 basi naamini utaweza kustahimili yaliyo ya sasa na hata ya baadaye.

Pambana. Usisalimu amri.
Word...!

Asipokuelewa atakuwa mvivu wa kuelewa
 
Usiuze nyumba ni alama ya jasho la mama yako
ipangishe halafu tafuta pa kupanga kwa nusu ya kodi uliyopangisha
halafu anzia hapo..

Mfano ungekuwa umeishi maisha mazuri utotoni ukasoma
lakini bahati mbaya ukafungwa na ndo unatoka jela leo ungesemaje?
wewe huna bahati mbaya hujakutana tu na wenye bahati mbaya
 
Back
Top Bottom