Ilishakutokea hii?

Ilishakutokea hii?

Yule aliyekuwa mshamba mshamba shule, hata yanayoendelea mjini hayajui, hajui mziki wala fasheni. Alikutongoza ukamjibu kwa dharau kuwa ajiangalie kwanza kabla hajafungua mdomo wake. Form four alipata divisheni one, wakati wewe ulipata four ya D mbili.

Sasa juzi mmekutana mjini anaendesha gari matata sana, yeye anakukumbuka na anakuuliza unaelekea wapi. Unatamani kuwa mke wake kwa sasa lakini hili haliwezekani tena.

Dunia ni duara ni milima tu huwa haikutani.
Na usiwasahau wale wachoyo wa majibu kwenye kudesa wengi maisha ya mtaani wameferi wanakutana na wamba tumepambana vilivyo bwana amejibu maombi sasa wanatunyenyekea.
 
Hii huwa inatokea katika maisha, sio lazima kishuleshule. Kijijini nilipokuwa naishi kulikuwa na jamaa wawili, ambao pale kijijini huwezi kuwaona yaani unaweza kuwapita hata usijue wapo wala kujali. Kwa mawazo ya kijinga ndio unasema washambawashamb.
Tulivyokuja mjini sasa hawa jamaa wako very successful, baada ya kusikia nafanyabiashara fulani inawahusu wamekuwa wateja wangu. Ni aina ya wateja siku akija inakuwa siku bora kibiashara kwenye wiki. Jamaa wako vizuri vibaya mno! Na walivyokuja wao ndio walinikumbusha wewe tumeishi wote kijiji fulani, mimi wala siwakumbuki.
 
think before you act.

msemo mdogo una maana kubwa sana,
 
Hivi naweza kusema "haijawahi kunitokea" kwenye hii mada?
 
😀😀 Si kweli, hizo ni za ma sister do
Tena wale masista do wanaoweza kuimba nyimbo za Celine Dion, Maria Carey nk kwa kizungu mwanzo mwisho, sisi tulikuwa tunawaangalia tu enzi hizo coz tulikuwa washamba kweli.
 
Tena wale masista do wanaoweza kuimba nyimbo za Celine Dion, Maria Carey nk kwa kizungu mwanzo mwisho, sisi tulikuwa tunawaangalia tu enzi hizo coz tulikuwa washamba kweli.
Mkuu wana mambo mengi bado hawajapanga club anakwenda na James au Omary.
 
Kuna faida sana mtoto wa kike ukitongozwa uwe mstaarabu, hata kama hutaki lakini tumia busara kukataa bila kumkashifu mwanaume, after all kutongozwa sio kutukanwa, sasa ngumi za nn? Matokeo yake ndio kama hivyo maisha hayana hatimiliki, leo upo juu kesho unakaliwa juu
 
Yule aliyekuwa mshamba mshamba shule, hata yanayoendelea mjini hayajui, hajui mziki wala fasheni. Alikutongoza ukamjibu kwa dharau kuwa ajiangalie kwanza kabla hajafungua mdomo wake.

Form four alipata divisheni one, wakati wewe ulipata four ya D mbili.

Sasa juzi mmekutana mjini anaendesha gari matata sana, yeye anakukumbuka na anakuuliza unaelekea wapi. Unatamani kuwa mke wake kwa sasa lakini hili haliwezekani tena.

Dunia ni duara ni milima tu huwa haikutani.
Kuna kaka mmoja alikuwa ametoka kwenye familia duni alikuwa anaenda shule bila viatu miguu imeliwa na funza kwa ufupi maisha yaligoma kabisa lakini alisoma kwa bidii sana leo ni chief Accountant wa kampuni moja ukimuona utasema amezaliwa upya ana maisha mazuri sana sana tena sana. Mungu hamtupi mja wake!
 
Kuna kaka mmoja alikuwa ametoka kwenye familia duni alikuwa anaenda shule bila viatu miguu imeliwa na funza kwa ufupi maisha yaligoma kabisa lakini alisoma kwa bidii sana leo ni chief Accountant wa kampuni moja ukimuona utasema amezaliwa upya ana maisha mazuri sana sana tena sana. Mungu hamtupi mja wake!
Na Mungu anajua kuumbua wachekaji wa hali za wenzao
 
Back
Top Bottom