Umesahau waraka wa kikristo uliosambazwa kwa waumini wa kikristo hadi katika ngazi ya jumuia kuhimiza kuichagua chadema?
Wasimamizi wa mikutano hiyo walikuwa mapadre
Unajua Gagnija kama kitu kikisemwa na wewe huchukui initiative yeyote kuwa mbali nacho hata kama ni cha uongo watu watadhani ni kweli, tuliokuwepo enzi zile za 90s maandamano na mikutano ya CUF ilikuwa ikitangazwa misikitini, na maandamano mengi yalikuwa yakianza humo hasa baada ya swala ya Ijumaa, mashehe, Bakwata na taasisi zingine za kiislamu zilikuwa hazijifichi kwa hili, lakini on contrary mbali ya Chadema kusemwa cha Kikristo hatuokuona support kutoka kwenye madhehebu hayo, rejea kauli ya Pengo kuwa Kikwete ni chaguo la Mungu.
Kuna jambo limekuwa linanitatiza kila siku. Ilikuwaje Chadema iliweza kuipiku CUF katika kukubalika huku Bara? Sote twajua baada ya NCCR kupotea CUF ndiyo ilikuwa moto wa kuotea mbali katika kuihenyesha CCM na hiii ilionekana katika uchaguzi wa 2000 na 2005 hasa katika kura ya urais.
Baada ya 2005 CUF ilianza kupotea pole pole. Bila shaka ni kwa sababu CDM waliweza kuipiku CUF katika hoja ya ufisadi na hii inashangaza -- kwani CUF hawakuiona hoja hiyo na kuifanya yao? Kitu gani kiliwazuia?
Umaarufu wa Chadema ulianzia September 2007 kule Mwembeyanga wakati Dr Slaa aliposimama jukwaani na kuitaja ile orodha ya aibu ya watu 11 ikiongozwa na JK mwenyewe. Hilo lilikuwa ni bonge la bao la kisigino dhidi ya CUF, na tangu hapo chama hicho hakikusimama tena sawasawa kilianza kuchechemea.
Na uzuri ni kwamba orodha ile ilikuwa ya ukweli mtupu, na ndiyo yakaja mambo ya EPA, Meremeta, Deep Green na mengineyo mengi isipokuwa Richmond ambalo lilianzia katikati 2006.
Ingekuwa ni Profesa Lipumba ndiyo alipanda jukwaani na kutaja orodha kama hiyo, hadi leo hii Chadema ingebakia kama zamani, chama cha Wachagga.
Hii inaonyesha Dr Slaa ana uthubutu na ujasiri wa kuweza kufanya maamuzi magumu na mazito, sifa ambayo Profesa Lipumba hana, ingawa yeye anaweza kuwa anamzidi DR Slaa katika kuyaelewa matatizo ya nchi hii na kuyaelezea kwa ufasaha, lakini si katika ujasiri wa kuchukuwa maamuzi mazito.
______________-
Hayo ni kweli kabisa, inashangaza kwa nini CUF hawakuiona hoja ya ufisadi na kuwawahi CDM. Ni kweli pia hoja ya ufisadi imewaumiza sana CCM, hadi leo iko hoi kabisa kinachowasaidia ni ile nguvu ya dola waliyo nayo.
Lakini nadhani pia suala la mgogoro kule Zanzibar liliwachukuia muda mwingi sana CUF kulishughulikia katika kufikia miafaka mara 2. Hivyo nguvu zao zote zilikuwa kule -- hata viongozi wakuu wa CUF huku Bara walipeleka nguvu zao kule. Vinginevyo sikuona sababu ya Pro Lipumba kutoibaini hoja ya ufisadi kama mtaji mkubwa wa siasa. It's too late.
Lakini ajabau ni kwamba pamoja na sura hii kibwa ya kitaifa, CUF ilizidiwa sana na NCCR huku Bara katika uchaguzi wa kwanza wa 1995. Kwa hiyo mambo yalianza kwenda kombo tangu wakati ule, ingawa kama usemavyo kupotea kwa NCCR kulipandisha chati CUF katika uchaguzi wa 2000 na 2005.
Alijua ni ya wakatoliki wenzake...ndio aliwaogopa CUF zaidi..kwakuwa wanaonglea equality and justice..
Alijua ni ya wakatoliki wenzake...ndio aliwaogopa CUF zaidi..kwakuwa wanaonglea equality and justice..
kwa chaguzi za 1995, 2000 na 2005 cuf haijawahi pata mbunge bara, ila baadaa kupiga kampeni za kisayansi 2010; imepata wabunge 2 ie mtwara na kilwaUmetumia kigezo gani kusema cuf ilikuwa juu ya chadema? cuf haijawahi kukubalika na watu wengi Tz bara. Ukichukua mfano wa wabunge hebu nikumbushe (labda nimesahau) kama ilishapata walau wabunge kumi huku bara
Mahakama ya kadhi ni Tsunami litakapokuja hakuna wakulizuia..japo litawaudhi wakristo wenye roho mbaya..subiri
Unajua Gagnija kama kitu kikisemwa na wewe huchukui initiative yeyote kuwa mbali nacho hata kama ni cha uongo watu watadhani ni kweli, tuliokuwepo enzi zile za 90s maandamano na mikutano ya CUF ilikuwa ikitangazwa misikitini, na maandamano mengi yalikuwa yakianza humo hasa baada ya swala ya Ijumaa, mashehe, Bakwata na taasisi zingine za kiislamu zilikuwa hazijifichi kwa hili, lakini on contrary mbali ya Chadema kusemwa cha Kikristo hatuokuona support kutoka kwenye madhehebu hayo, rejea kauli ya Pengo kuwa Kikwete ni chaguo la Mungu.
Hizi zingine tulizojenga tunaziendeshaje?
Unafurahia kupendelewa na serikali..bado unaweza kujiita mtetezi wa haki?
Serikali imewapendelea wakristo kwa kuwarudishia shule zao na kuwalipia hela za umma through MoU...huo utabaki ni ubaguzi, uwizi, ufisadi uliofanywa na serikali hata kama wakristo mtautetea..
Tutashinda na mtatema tu iko siku..
Sababu:
1.Kuungana kwa CCM na Cuf kumepunguza mvuto na nguvu ya Cuf
2.Magwanda kumteua Slaa kugombea urais kumeongezea mvuto wa chama
3.Magwanda ku-take advantage ya ugumu wa maisha kuishambulia CCM
4.Ukali wa spika Makinda umesaidia kuipa Magwanda public sympathy
5.Migogoro ndani ya CCM nayo imeipa sababu magwanda kupiga kelele
6.Fedha na ufadhili wa CDU umeipa nguvu sana Magwanda kwa kufanya maandamano na makusnyiko
7.Baadhi ya maofisa wa usalama wa taifa kutoa siri za serikali kwa Magwanda
kwa chaguzi za 1995, 2000 na 2005 cuf haijawahi pata mbunge bara, ila baadaa kupiga kampeni za kisayansi 2010; imepata wabunge 2 ie mtwara na kilwa
CUF hawajawahi kuwa na mvuto bara. Walifanya makosa kutokifanya chama chao cha kitaifa. Walijikita zaidi kizanzibari na hawakuweka mipngo mikakati kupenya bara. Watu wa bara ni rahisi kuwapenya lakini sio kwa siasa zile za kizanzibari.