Ilikuwaje, baada ya 2005, CDM kufanikiwa kuipiku CUF katika kukubalika huku bara?

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
233



Kuna jambo limekuwa linanitatiza kila siku. Ilikuwaje Chadema iliweza kuipiku CUF katika kukubalika huku Bara? Sote twajua baada ya NCCR kupotea CUF ndiyo ilikuwa moto wa kuotea mbali katika kuihenyesha CCM na hiii ilionekana katika uchaguzi wa 2000 na 2005 hasa katika kura ya urais.

Baada ya 2005 CUF ilianza kupotea pole pole. Bila shaka ni kwa sababu CDM waliweza kuipiku CUF katika hoja ya ufisadi na hii inashangaza -- kwani CUF hawakuiona hoja hiyo na kuifanya yao? Kitu gani kiliwazuia?

Umaarufu wa Chadema ulianzia September 2007 kule Mwembeyanga wakati Dr Slaa aliposimama jukwaani na kuitaja ile orodha ya aibu ya watu 11 ikiongozwa na JK mwenyewe. Hilo lilikuwa ni bonge la bao la kisigino dhidi ya CUF, na tangu hapo chama hicho hakikusimama tena sawasawa – kilianza kuchechemea.

Na uzuri ni kwamba orodha ile ilikuwa ya ukweli mtupu, na ndiyo yakaja mambo ya EPA, Meremeta, Deep Green na mengineyo mengi isipokuwa Richmond ambalo lilianzia katikati 2006.

Ingekuwa ni Profesa Lipumba ndiyo alipanda jukwaani na kutaja orodha kama hiyo, hadi leo hii Chadema ingebakia kama zamani, chama cha Wachagga.


Hii inaonyesha Dr Slaa ana uthubutu na ujasiri wa kuweza kufanya maamuzi magumu na mazito, sifa ambayo Profesa Lipumba hana, ingawa yeye anaweza kuwa anamzidi DR Slaa katika kuyaelewa matatizo ya nchi hii na kuyaelezea kwa ufasaha, lakini si katika ujasiri wa kuchukuwa maamuzi mazito.





 



Kuna jambo limekuwa linanitatiza kila siku. Ilikuwaje Chadema iliweza kuipiku CUF katika kukubalika huku Bara? Sote twajua baada ya NCCR kupotea CUF ndiyo ilikuwa moto wa kuotea mbali katika kuihenyesha CCM na hiii ilionekana katika uchaguzi wa 2000 na 2005 hasa katika kura ya urais.

Baada ya 2005 CUF ilianza kupotea pole pole. Bila shaka ni kwa sababu CDM waliweza kuipiku CUF katika hoja ya ufisadi na hii inashangaza -- kwani CUF hawakuiona hoja hiyo na kuifanya yao? Kitu gani kiliwazuia?

Umaarufu wa Chadema ulianzia September 2007 kule Mwembeyanga wakati Dr Slaa aliposimama jukwaani na kuitaja ile orodha ya aibu ya watu 11 ikiongozwa na JK mwenyewe. Hilo lilikuwa ni bonge la bao la kisigino dhidi ya CUF, na tangu hapo chama hicho hakikusimama tena sawasawa – kilianza kuchechemea.

Na uzuri ni kwamba orodha ile ilikuwa ya ukweli mtupu, na ndiyo yakaja mambo ya EPA, Meremeta, Deep Green na mengineyo mengi isipokuwa Richmond ambalo lilianzia katikati 2006.

Ingekuwa ni Profesa Lipumba ndiyo alipanda jukwaani na kutaja orodha kama hiyo, hadi leo hii Chadema ingebakia kama zamani, chama cha Wachagga.


Hii inaonyesha Dr Slaa ana uthubutu na ujasiri wa kuweza kufanya maamuzi magumu na mazito, sifa ambayo Profesa Lipumba hana, ingawa yeye anaweza kuwa anamzidi DR Slaa katika kuyaelewa matatizo ya nchi hii na kuyaelezea kwa ufasaha, lakini si katika ujasiri wa kuchukuwa maamuzi mazito.





Majambia ya Omar Mahita ndio yalikimaliza cuf huku bara pili tabia Prof Lipumba kuwekeza zaidi mikoa yenye mwelekeo wa dini yake
 
ILIKUWAJE BAADA YA 2005 CHADEMA KUFANIKIWA KUVIPIKU VYAMA VYOTE VYA SIASAwKATIKA KUKUBALIKA HUKU BARA?? rekebisha kichwa cha habari tafadhali
 
Majambia ya Omar Mahita ndio yalikimaliza cuf huku bara pili tabia Prof Lipumba kuwekeza zaidi mikoa yenye mwelekeo wa dini yake
Pamoja na juhudi kubwa iliyofanywa na wabunge wa CDM wakiongozwa na Dr . Slaa na Zitto iliweza kwa kiasi kikubwa kuinyanyua CDM. Lakini hata hivyo siku hizi uelewa wa wananchi umekuwa mkubwa sana tofauti na miaka ile, pia uovu na makosa ya wazi yanayofanywa na serikali ya CCM indirect umewapa umaarufu sana CDM kuliko CUF.
 
Umaarufu wa Chadema haukuanzia Mwembe Yanga 2007 nakumbuka mwaka 1995 Nyerere mwenyewe alikiri chama kilicho makini ni Chadema, alikuwa anajua kutokana na source zake kuwa waanzilishi wa vyama vingine kama NCCR Mageuzi na CUF ni wachumia tumbo.

Hata hivyo kilichoimaliza CUF na baadae Chadema kuipiku ni dhana iliyoanzishwa na CCM kukipaka kuwa ni chama cha kidini.
 
Ukiondoa ccm ambayo huwezi kufananisha na.chama.chochote kwa.bara la.Africa ukiondoa.ANC
 


Kuna jambo limekuwa linanitatiza kila siku. Ilikuwaje Chadema iliweza kuipiku CUF katika kukubalika huku Bara? Sote twajua baada ya NCCR kupotea CUF ndiyo ilikuwa moto wa kuotea mbali katika kuihenyesha CCM na hiii ilionekana katika uchaguzi wa 2000 na 2005 hasa katika kura ya urais.

Baada ya 2005 CUF ilianza kupotea pole pole. Bila shaka ni kwa sababu CDM waliweza kuipiku CUF katika hoja ya ufisadi na hii inashangaza -- kwani CUF hawakuiona hoja hiyo na kuifanya yao? Kitu gani kiliwazuia?

Umaarufu wa Chadema ulianzia September 2007 kule Mwembeyanga wakati Dr Slaa aliposimama jukwaani na kuitaja ile orodha ya aibu ya watu 11 ikiongozwa na JK mwenyewe. Hilo lilikuwa ni bonge la bao la kisigino dhidi ya CUF, na tangu hapo chama hicho hakikusimama tena sawasawa – kilianza kuchechemea.

Na uzuri ni kwamba orodha ile ilikuwa ya ukweli mtupu, na ndiyo yakaja mambo ya EPA, Meremeta, Deep Green na mengineyo mengi isipokuwa Richmond ambalo lilianzia katikati 2006.

Ingekuwa ni Profesa Lipumba ndiyo alipanda jukwaani na kutaja orodha kama hiyo, hadi leo hii Chadema ingebakia kama zamani, chama cha Wachagga.


Hii inaonyesha Dr Slaa ana uthubutu na ujasiri wa kuweza kufanya maamuzi magumu na mazito, sifa ambayo Profesa Lipumba hana, ingawa yeye anaweza kuwa anamzidi DR Slaa katika kuyaelewa matatizo ya nchi hii na kuyaelezea kwa ufasaha, lakini si katika ujasiri wa kuchukuwa maamuzi mazito.

Umaarufu wa chadema unatokana na waraka na utaishi ...vivyo hivyo tukishamuweka rais kutoka ccm mkristo..period.
 
Sababu:
1.Kuungana kwa CCM na Cuf kumepunguza mvuto na nguvu ya Cuf
2.Magwanda kumteua Slaa kugombea urais kumeongezea mvuto wa chama
3.Magwanda ku-take advantage ya ugumu wa maisha kuishambulia CCM
4.Ukali wa spika Makinda umesaidia kuipa Magwanda public sympathy
5.Migogoro ndani ya CCM nayo imeipa sababu magwanda kupiga kelele
6.Fedha na ufadhili wa CDU umeipa nguvu sana Magwanda kwa kufanya maandamano na makusnyiko
7.Baadhi ya maofisa wa usalama wa taifa kutoa siri za serikali kwa Magwanda
 
Hujui kuwa CUF na CCM ni wanandoa? kumbuka ndoa yoyote huanza kwa wanandoa kutongozana, kutoa posa na mwisho ndoa, sasa wakati yote haya yanafanyika ndipo chama kikaanza kupoteza mvuto kwa wananchi, na siku zote kama unamwamini mtu halafu huyo mtu unayemwamini ikatokea akajenga urafiki na mtu usiyemwamini ni lazima utapoteza matumaini naye
A friend of my enemy is my enemy too:fencing:
 
Umaarufu wa Chadema haukuanzia Mwembe Yanga 2007 nakumbuka mwaka 1995 Nyerere mwenyewe alikiri chama kilicho makini ni Chadema, alikuwa anajua kutokana na source zake kuwa waanzilishi wa vyama vingine kama NCCR Mageuzi na CUF ni wachumia tumbo.

Hata hivyo kilichoimaliza CUF na baadae Chadema kuipiku ni dhana iliyoanzishwa na CCM kukipaka kuwa ni chama cha kidini.

Alijua ni ya wakatoliki wenzake...ndio aliwaogopa CUF zaidi..kwakuwa wanaonglea equality and justice..
 
Hata hivyo kilichoimaliza CUF na baadae Chadema kuipiku ni dhana iliyoanzishwa na CCM kukipaka kuwa ni chama cha kidini.

Mkuu,

Kuna dhana ya uchaga na ukatoliki iliyosambazwa sana dhidi ya CDM ingawa madhara yake hayajatishia uhai wa chama. Pengine tujiullize, kwanini CUF walipata madhara makubwa sana tokana na dhana ya udini huku bara, dhana hii yaweza kuwa na ukweli fulani? Nakumbuka kipindi cha nyuma kidogo swala zikiendeshwa kabla ya mkutano wa hadhara. This was suicidal!
 


Kuna jambo limekuwa linanitatiza kila siku. Ilikuwaje Chadema iliweza kuipiku CUF katika kukubalika huku Bara? Sote twajua baada ya NCCR kupotea CUF ndiyo ilikuwa moto wa kuotea mbali katika kuihenyesha CCM na hiii ilionekana katika uchaguzi wa 2000 na 2005 hasa katika kura ya urais.

Baada ya 2005 CUF ilianza kupotea pole pole. Bila shaka ni kwa sababu CDM waliweza kuipiku CUF katika hoja ya ufisadi na hii inashangaza -- kwani CUF hawakuiona hoja hiyo na kuifanya yao? Kitu gani kiliwazuia?

Umaarufu wa Chadema ulianzia September 2007 kule Mwembeyanga wakati Dr Slaa aliposimama jukwaani na kuitaja ile orodha ya aibu ya watu 11 ikiongozwa na JK mwenyewe. Hilo lilikuwa ni bonge la bao la kisigino dhidi ya CUF, na tangu hapo chama hicho hakikusimama tena sawasawa – kilianza kuchechemea.

Na uzuri ni kwamba orodha ile ilikuwa ya ukweli mtupu, na ndiyo yakaja mambo ya EPA, Meremeta, Deep Green na mengineyo mengi isipokuwa Richmond ambalo lilianzia katikati 2006.

Ingekuwa ni Profesa Lipumba ndiyo alipanda jukwaani na kutaja orodha kama hiyo, hadi leo hii Chadema ingebakia kama zamani, chama cha Wachagga.


Hii inaonyesha Dr Slaa ana uthubutu na ujasiri wa kuweza kufanya maamuzi magumu na mazito, sifa ambayo Profesa Lipumba hana, ingawa yeye anaweza kuwa anamzidi DR Slaa katika kuyaelewa matatizo ya nchi hii na kuyaelezea kwa ufasaha, lakini si katika ujasiri wa kuchukuwa maamuzi mazito.

Umetumia kigezo gani kusema cuf ilikuwa juu ya chadema? cuf haijawahi kukubalika na watu wengi Tz bara. Ukichukua mfano wa wabunge hebu nikumbushe (labda nimesahau) kama ilishapata walau wabunge kumi huku bara
 
Mkuu,

Kuna dhana ya uchaga na ukatoliki iliyosambazwa sana dhidi ya CDM ingawa madhara yake hayajatishia uhai wa chama. Pengine tujiullize, kwanini CUF walipata madhara makubwa sana tokana na dhana ya udini huku bara, dhana hii yaweza kuwa na ukweli fulani? Nakumbuka kipindi cha nyuma kidogo swala zikiendeshwa kabla ya mkutano wa hadhara. This was suicidal!
Unajua Gagnija kama kitu kikisemwa na wewe huchukui initiative yeyote kuwa mbali nacho hata kama ni cha uongo watu watadhani ni kweli, tuliokuwepo enzi zile za 90s maandamano na mikutano ya CUF ilikuwa ikitangazwa misikitini, na maandamano mengi yalikuwa yakianza humo hasa baada ya swala ya Ijumaa, mashehe, Bakwata na taasisi zingine za kiislamu zilikuwa hazijifichi kwa hili, lakini on contrary mbali ya Chadema kusemwa cha Kikristo hatuokuona support kutoka kwenye madhehebu hayo, rejea kauli ya Pengo kuwa Kikwete ni chaguo la Mungu.
 
Unajua Gagnija kama kitu kikisemwa na wewe huchukui initiative yeyote kuwa mbali nacho hata kama ni cha uongo watu watadhani ni kweli, tuliokuwepo enzi zile za 90s maandamano na mikutano ya CUF ilikuwa ikitangazwa misikitini, na maandamano mengi yalikuwa yakianza humo hasa baada ya swala ya Ijumaa, mashehe, Bakwata na taasisi zingine za kiislamu zilikuwa hazijifichi kwa hili, lakini on contrary mbali ya Chadema kusemwa cha Kikristo hatuokuona support kutoka kwenye madhehebu hayo, rejea kauli ya Pengo kuwa Kikwete ni chaguo la Mungu.

Umesahau waraka wa kikristo uliosambazwa kwa waumini wa kikristo hadi katika ngazi ya jumuia kuhimiza kuichagua chadema?

Wasimamizi wa mikutano hiyo walikuwa mapadre
 
Kwa hoja rojorojo kama hizi, mahakama ya kadhi sahauni kabisa. Hamtaweza hata kumconvince m.kwere, jamaa yenu kwa urojorojo wa hoja zenu.
Alijua ni ya wakatoliki wenzake...ndio aliwaogopa CUF zaidi..kwakuwa wanaonglea equality and justice..
 
Umetumia kigezo gani kusema cuf ilikuwa juu ya chadema? cuf haijawahi kukubalika na watu wengi Tz bara. Ukichukua mfano wa wabunge hebu nikumbushe (labda nimesahau) kama ilishapata walau wabunge kumi huku bara
nathani umempasha ukweli CUF haijwahi kukubalika bara kipindi Prof. Lipumba anapata kura nyingi ni kutokana na NCCR-Mageuzi kudorora na CHADEMA kutoa support kwa mgombea wa CUF kwa kutoweka mgombea! Hii iliwafanya wana CUF kubweteka na mbaya zaidi pale ule mkataba wa ushirikiano ulipokufa baada ya Chacha Wangwe kufariki hali ikaanza kuwa tete na umashuhuri wa CUF ukapotelea mbali! Wahenga wanasema usiunyee mkono unaolia nao...
 
Kwa hoja rojorojo kama hizi, mahakama ya kadhi sahauni kabisa. Hamtaweza hata kumconvince m.kwere, jamaa yenu kwa urojorojo wa hoja zenu.

Mahakama ya kadhi ni Tsunami litakapokuja hakuna wakulizuia..japo litawaudhi wakristo wenye roho mbaya..subiri
 
Kwa hoja rojorojo kama hizi, mahakama ya kadhi sahauni kabisa. Hamtaweza hata kumconvince m.kwere, jamaa yenu kwa urojorojo wa hoja zenu.
Kweli mkuu inawezekana huwa wana madai ya msingi lakini wakati wa kujenga hoja wanawaachia watu kama hawa kuandika, na sababu wanazotoa mfano......"kwa vile umewarudishia wakristu shule zao na sisi tunaomba zetu" bila kuja na draft plan wataziendelezaje baada ya miaka 10 ndio maana mkwe.re anawatolea nje.
 
Kweli mkuu inawezekana huwa wana madai ya msingi lakini wakati wa kujenga hoja wanawaachia watu kama hawa kuandika, na sababu wanazotoa mfano......"kwa vile umewarudishia wakristu shule zao na sisi tunaomba zetu" bila kuja na draft plan wataziendelezaje baada ya miaka 10 ndio maana mkwe.re anawatolea nje.

Hizi zingine tulizojenga tunaziendeshaje?

Unafurahia kupendelewa na serikali..bado unaweza kujiita mtetezi wa haki?

Serikali imewapendelea wakristo kwa kuwarudishia shule zao na kuwalipia hela za umma through MoU...huo utabaki ni ubaguzi, uwizi, ufisadi uliofanywa na serikali hata kama wakristo mtautetea..

Tutashinda na mtatema tu iko siku..
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom