Kinachoendelea TBC1 sasa wako live leo studio kuna waheshimiwa na naibu waziri na waalikwa wengine,wakiwemo wasanii.
Swali langu je hili linatija kwa taifa nani anagharamia haya matukio.
Mkuu Nyanya Mbichi, kwa vile walianza kwa tafrija, wanamaliza kwa tafrija na kupongezana kwa kazi kubwa na nzuri walioifanya kututangazia kombe la dunia!.
Lengo la kuitana ni ku share nazuri na wenzio.
Matukio hayo na mengine yote ya TBC yamegharimiwa na mimi na wewe, yeye na yule, sisi na wao, wale na yule, yeye na yule, na wao, na wale kupitia kodi zetu na hatuna tatizo na hilo.
Kuna sherehe ngapi za kitaifa zinagharimiwa na mabilioni ya shilingi what for, mbona hamsemi?!, badala ya kuishukuru TBC imekuletea kombe la dunia mechi zote bure, ndio kwanza unalaumu!.
Ama kweli watu hawana shukrani, ukimtendea meme, atalalamika, ukimtendea ubaya ndio kabisa!.
Watanzania tumezidi mno kulalamika, kila kitu kulalamika, kwani wewe ulitakaje?, pati iwe ya Brasil tuu tukifanya party huku unaumia roho?!.
Pole!.
Pasco