Ilianza Zimbabwe sasa Tanzania inafuatia

EWGM's

JF-Expert Member
Jul 22, 2013
1,521
2,109
Akili za Watanzania waliowengi ni kama bendera huwa wanafata upepo tu, hakuna tofauti ya wasomi wala wauza karanga mitaani. Kwa hurka hii mbaya sioni kama kuna siku tutanasuka kwenye hili tope zito la umbumbu. Nchi ikishakosa utofauti wa uelewa ni ishara tosha kuwa kuna shida.

Sijaelewa bado kama tatizo ni siasa au elimu, ujinga au uvivu, serikali au mazingira. Kwanini idadi ya watu kuwa wapumbavu inaongezeka siku hadi siku?

Ila hala hala kiangazi kinakuja na tope linaanza kukauka hivyo nasema tukiendelea hivi hatapona mtu.Wenye macho na waone na wenye masikio wasikie kama taifa tuko kwenye hali mbaya

==========================================================
UPDATE; 09/10/2017

Mvua zimeshasimama kunyesha na yale madimbwi/mabwawa machache yameanza kukauka. Hii ni ishara tosha kuwa kiangazi kinakuja na mioto michache iliyobaki imeanza kunyauka na mingine kufa kabisa. Ardhi imeanza kuwa ngumu na unyevuunyevu umeanza kupotea, hii ni ishara tosha kuwa ile safari yetu inajikamilisha. Jua likizidi sana ardhi itaanza kuwa ngumu na kuanza kupasuka basi tope limeshakauka.

Weledi haupo tena watu wanafanya mambo kufurahisha mtu/watu au kikundi fulani, kila mjinga au mwerevu mwenye fursa na yeye anaitisha press conference. Ikiwa makanisa yote yanasimama kwenye msingi wa ukistro iweje isahaulike Kristo alisimamia nini na pia upande huu mwingine wanataka kujua idadi yao wako wangapi nchini,hii ni ishara tosha safari imewadia.

Ikishafika mahali Katiba ikawa daftari la mazoezi kwamba sentensi inaweza kupigiwa mstari mwenkundu na sentensi ikaandikwa upya tena na mtu mmoja mpaka hapo tujue tumeshakaribia kufika. Tumenasa kwenye tope zito na linakauka kwa kasi mno ila kila kukicha najiuliza tutachomokaje hapa?

Some problems are so complex that you have to be highly intelligent and well-informed just to be undecided about them.
 
Hahaha, eti tunaamini umaskini wetu unatokana na wazungu. Ilhali tunafanya makosa ya waziwazi wenyewe. Dunia ya leo unasema kuwa Waziri, Mbunge, Mkuu wa Mkoa au Wilaya inahitajika kujua kusoma na kuandika tu. Kisha tukishindwa kutatua changamoto kubwa za kimaendeleo, tunawalaumu wazungu. Haiwezekani. Ukweli unabaki kuwa akili zetu hazijawa tayari kujiletea maendeleo.
 
Tatizo watu walikosea kufanya maamuzi kwenye sanduku la kura, sasa ni mwaka na nusu Tanzania ina hasara kubwa kuliko wakati mwingine wowote.

Hakuna wa kuhoji, uchumi wetu anasimamia Dotto Katibu Mkuu Wizara ya Fedha. This is nonsense! Mshauri wa Fedha eti ni Dotto, hii laana itatumaliza.
 
Hawa waamerika ktk maslahi yao hawana urafiki wala ubinadamu na wana mbinu nyingi za kulipiza kisasi na si ajabu wakaanzisha hata vikundi vya kigaidi ili kuiyumbisha serikali,,,,,,,,Ya Allah tuepushie hiyo zahma kwa kifupi magufuli yuko sawa na anachopigania ni haki ....Conclusively,Allah ndo mpangaji wa yote naamini Tanzania tutawashinda wamarekani ktk hili
 
Binafsi kwa hili la kuchunguza mikataba mibovu na kuirekebisha hata ikibidi kutumia nguvu naiunga mkono serikali.
Huu ni utekelezaji wa vilio vya wananchi miaka nenda miaka rudi kwamba mali zetu zinaibwa mchana kweupe, cha ajabu mnakuja wengine kuiponda serikali aiseee mmmmh!
 
Wawekezaji ni maadui wa maendeleo wa nchi hii, wanatuibia, waondolewe kila kitu tutafanya wenyewe.

Tulipojaribu kuendesha viwanda/mashamba wenyewe baada ya kutaifisha vilikufa kwa wizi wetu wa kufuja mali za mashirika ya umma, kupeana kazi kindugu/kichama na kusimamia sera hovyo za uchumi. Mwisho yamekufa na kubaki historia.

Leo tuna mahakama, tuna wanasheria, bado tunalalamika tunaibiwa. Mika 50+ baada ya uhuru tunataka kurudi kule tulipotoka.

Samahani kusema lakini hii nchi ina watu wajinga sana. Ni viongozi wangapi wanajisomea hata vitabu? Tunapoteza muda na "shiwaladu" na kufanya vitu kwa hisia na kishabiki.

Ujamaa umekula akili zetu tunaona mfanyabiashara anayepata faida ni "mwizi".
 
Tatizo watu walitumia masaburi kufanya maamuzi kwenye sanduku la kura,sasa ni mwaka Na nusu tz INA hasara kubwa kuliko wakati mwingine wowote,hakuna wa kuhoji,uchumi wetu anasimamia dotto katibu mkuu Wizara ya Fedha!!!!!!!this is nonsense,mshauri wa Fedha eti ni dotto,hii laana itatumaliza
PMG and PST!!! Halafu tunalaumu wazungu????
 
Akili za Watanzania waliowengi ni kama bendera huwa wanafata upepo tu, hakuna tofauti ya wasomi wala wauza karanga mitaani. Kwa hurka hii mbaya sioni kama kuna siku tutanasuka kwenye hili tope zito la umbumbu. Nchi ikishakosa utofauti wa uelewa ni ishara tosha kuwa kuna shida. Sijaelewa bado kama tatizo ni siasa au elimu, ujinga au uvivu, serikali au mazingira. Kwanini idadi ya watu kuwa wapumbavu inaongezeka siku hadi siku?

Ila hala hala kiangazi kinakuja na tope linaanza kukauka hivyo nasema tukiendelea hivi hatapona mtu.Wenye macho na waone na wenye masikio wasikie kama taifa tuko kwenye hali mbaya

Some problems are so complex that you have to be highly intelligent and well-informed just to be undecided about them.
si zani kama wewe ni mtanzania na kama mtanzania ulikuta baba ako amekuwekea maisha safi
 
Mmeambiwa Tusubiri Ripoti ya pili mbona watu wameanza Kusema sana kana vile Serikali imeshatoa Tamko.Tusubiri ila tumpongeze Mh.Raisi kubadili ule mtindo wa kupokea Ripoti kisha kufungiwa Kabatini.Mh.Raisi amethubutu na ana utashi wa kubadili yale ya business as usual .Tusubirini Ripoti ya pili ziangaliwe .Ila kwa hii ya kwanza wenzetu ndani ya Wizara na TMAA waubebe msalaba walipewa dhamana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom