Uchaguzi 2020 Ilani ya CHADEMA kuhusu Bima ya Afya ina ulaghai

RMC

JF-Expert Member
Nov 16, 2013
1,337
1,752
Katika uzi niliowasilisha awali nilizungumzia kuhusu athari ya ilani ya CHADEMA kwa ndoa na ajira; katika uzi wangu wa pili nilizungumzia kasoro za kiuchumi katika ilani za CHADEMA na ACT-Wazalendo. Katika uzi wangu huu wa tatu, nitazungumzia ulaghai kuhusu utekelezaji wa sera ya bima ya afya kwa wote.

Kwanza unapozungumzia bima yeyote ile maana yake kuna malipo ya mwanzo (premium) ambayo mnufaika aidha analipa yeye mwenyewe au analipiwa sehemu na yeye mwenyewe analipa sehemu ya hiyo premium au analipiwa yote hiyo premium. Kwa suala la bima ya afya ambayo CHADEMA wanajinasibu sana kuwa watawapa watanzania na itakuwa ni nafuu sana kuliko ile inayotozwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, CHADEMA wanapotosha sana.

Siku zote kipato binafsi ch mtu ndicho msingi wa wapi mtu huyo atatibiwa, wapi ataishi, wapi watoto wake watasoma. Hata siku moja hakutakuwa usawa wa kila mtu kutibiwa Aga Khan hospital, Hindu mandal hosptital au hospitali ya wilaya ya serikali.

CHADEMA wanakwepa kutaja kuwa chini ya utawala wao mtanzania atalipa premium shilingi ngapi ili aweze kuwa na bima, na pia bima hiyo itamuwezesha kutibiwa hospitali zipi. Je serikali itachangia shilingi ngapi kwa kila bima ya mtu mmoja ili kumuwezesha kutibiwa hospitali zipi. Ni wazi wanaweza wakampa kila mtu bima lakini bima hiyo isimruhusu mtu huyo kutibiwa hospitali yenye hadhi kama Aga Khan au Hindu Mandal.

CHADEMA kwa kulijua hilo ndio maana katika ilani yao wamesema kuwa watakuwa na bima maalum kwa askari wa majeshi yetu. Hii maana yake ni kuwa bima hiyo ya maaskari itakuwa tofauti na ile ya watanzania wengine wasio maaskari na kwa kwa lugha nyepesi itakuwa na package ambazo hazipo katika bima ya kawaida za watanzania wengine. Kama bima za watanzania wengine zitawawezesha kupata kila aina ya matibabu katika hospitali yeyote kwa nini kuwe na bima maalum ya maaskari? {Angalia ilani ya CHADEMA (d) Ukurasa 93}

Pia hoja nyingine ni suala la uwezo wa kiuchumi la kuwalipia sehemu kubwa ya gharama za bima hiyo watanzania wote. Ieleweke kuwa sekta ya afya ina gharama na ili kuwa na huduma bora za afya kwanza serikali lazima iwe na mapato makubwa sana ili iweze kutenga bajeti kubwa kwa ajili ya sekta ya afya.

Bajeti hiyo ndiyo inayotumika kugharamia mafunzo ya madaktari, wauguzi na wataalam wengine wa afya, kujenga majengo ya kutolea huduma za afya, kununulia mashine za kitabibu, vifaa tiba, vitendanishi, madawa na piakutunza miundombinu ya mataibabu pa,oja na mishahara ya watumishi. Lissu anatolea mfano wa gharama ndogo za bima za Ubelgiji lakini haangalii tofauti kubwa ya pato kati ya nchi ya Ubelgiji na Tanzania.

Katika uzi wangu wenye kichwa cha habari “Kasoro za kiuchumi katika ilani za CHADEMA na ACT Wazalendo” nimehoji kuwa waeleze matarajio (projection) ya ukuaji wa uchumi kila mwaka kwa miaka yote mitano, GDP ya kila mwaka kwa figures ili iweze kujulikana kwa uhakika chini ya sera zao pato la nchi litakuwaje. Pato la nchi ndio msingi wa mapato ambayo serikali itakuwa inakusanya kwa njia ya kodi na yasiyo ya kodi. Pia waeleze makusanyo yao ya kodi yatakuwa asilimia ngapi ya GDP kila mwaka na pia mapato ya ndani ya serikali kwa ujumla yatakuwa asilimia ngapi ya GDP kila mwaka. Wataje pia kwa figures (projections) watakuwa wanakusanya shilingi ngapi kila mwaka

Pia niliwataka CHADEMA na ACT Wazalendo watueleze (projections) watatumia shilingi ngapi kati ya makusanyo hayo ya kila mwaka kulipa mishahara hiyo mikubwa wanayoahidi na pia kulipa madeni ambayo watapaswa kuendelea kulipa. Baada ya hapo tutaweza kujua kiasi cha mapato kinachobakia kwa ajili ya kutekeleza hayo mambo makubwa wanayoahidi na watukukotolee matumizi yote kuanzia afya, elimu bure, mikopo ya elimu ya juu, maji, nyumba, viwanda, masoko nk ambavyo hasa CHADEMA wamekuwa wakidai watafanya.

Kwa kulinganisha Ubelgiji yenye watu milioni 11 GDP yake ni Dola za Marekani Bilioni 529.61 mwaka 2019 wakati Tanzania yenye watu milioni 56, GDP yake ilikuwa shilingi trilioni 139.9 takribani Dola za Marekani Bilioni 60 kwa kipindi hicho. Matumizi ya serikali ya Ubelgiji katika sekta ya afya yalikuwa asilimia 10 ya GDP yake (Dola za Marekani Bilioni 53). Tanzania hata wakitumia asilimia kumi kama Ubelgiji bado matumizi yatakuwa kidogo kwa sababu ya GDP ndogo na idadi kubwa ya watu.

Hivyo CHADEMA wanavyoaminisha watu kwamba watatoa huduma bora za afya wanapaswa watueleze kwanza bajeti yao ya sekta ya afya itakuwa shilingi ngapi na watapata wapi pesa hiyo. Uwepo wa bima sio muarobaini wa kuwa na huduma bora za afya kwa sababu katika nchi yeyote kuna gharama ambazo zinabebwa na serikali moja kwa moja ndio maana huko Ubelgiji gharama za bima anayolipia mtu mmoja ni ndogo lakini hiyo haina maana kuwa ndio gharama halisi ya matibabu pimdi huyo mtu akiugua au kwa kuwa wengine hawataugua basi ndio kusema kuwa hiyp hela yote ya bima iliyokusanywa itatosha kugharamia wote watakaougua, la hasha.

Lissu na CHADEMA wanapswa wajielimishe kuhusu masuala ya uchumi badala ya kuchukulia kuwa kila kitu kinawezekana kufanyika na kama hakikufanywa na serikali iliyopo madarakani basi ni kwa sababu haikutaka. Uchumi hauendi hivyo.
 
Lissu na CHADEMA wanapswa wajielimishe kuhusu masuala ya uchumi badala ya kuchukulia kuwa kila kitu kinawezekana kufanyika na kama hakikufanywa na serikali iliyopo madarakani basi ni kwa sababu haikutaka. Uchumi hauendi hivyo.
Mkuu wewe ndio mweupe sana kwenye uchumi eti una compare GDP ya Belgium na Tz ili useme haiwezekani? Sasa nikupe challenge.

Model ya bima ya afya wametohoa Rwanda ina hiyo special package ya Jeshi alafu kuna wafanyakazi wa umma, then kuna wale wenye kipato cha chini kabisa wasio kwenye sekta rasmi n.k

2. Justification yake ni kwamba michango inategemea income bracket uliyopo. Rwanda wameigawa mara 4 kwahiyo utachangia kulingana na uwezo wako wa kiuchumi lakini wale waliopo chini kabisa yaani wanaoishi kwenye umaskini wa kutupwa basi serikali inawachangia totally wakishirikiana na mfumo wa crowdfunding wa kijamii tunaweza uita "Ujirani mwema"

3. Mchango wa serikali ya Rwanda ni almosy 14% pekee kwahiyo haiathiri mapato ya Serikali kabisa kwenye kuendesha mfuko.

4. Usichofahamu ni kwamba mfuko ukiwa na pesa zinazungushwa kwenye biashara mbalimbali na masoko ya hisa hivyo pesa inazaa ili mfuko uwe unakua zaidi na kupunguza risk ya float.

5. Unasema GDP ya Belgum blah blah, sasa naomba ufaham Tz imeizidi GDP ya Rwanda karibu mara 6.7 kwa data za 2018. Sasa kama Rwanda kufikia 2011 walikua na coverage ya 90% bima ya afya sisi tunashindwa nini??

Tusiishi kwa kukariri tujifunze Rwanda tupunguze ujuaji.
 
Mkuu wewe ndio mweupe sana kwenye uchumi eti una compare GDP ya Belgium na Tz ili useme haiwezekani? Sasa nikupe challenge.

Model ya bima ya afya wametohoa Rwanda ina hiyo special package ya Jeshi alafu kuna wafanyakazi wa umma, then kuna wale wenye kipato cha chini kabisa wasio kwenye sekta rasmi n.k

2.Justification yake ni kwamba michango inategemea income bracket uliyopo. Rwanda wameigawa mara 4 kwahiyo utachangia kulingana na uwezo wako wa kiuchumi lakini wale waliopo chini kabisa yaani wanaoishi kwenye umaskini wa kutupwa basi serikali inawachangia totally wakishirikiana na mfumo wa crowdfunding wa kijamii tunaweza uita "Ujirani mwema"

3. Mchango wa serikali ya Rwanda ni almosy 14% pekee kwahiyo haiathiri mapato ya Serikali kabisa kwenye kuendesha mfuko.
4. Usichofahamu ni kwamba mfuko ukiwa na pesa zinazungushwa kwenye biashara mbalimbali na masoko ya hisa hivyo pesa inazaa ili mfuko uwe unakua zaidi na kupunguza risk ya float.

5. Unasema GDP ya Belgum blah blah, sasa naomba ufaham Tz imeizidi GDP ya Rwanda karibu mara 6.7 kwa data za 2018. Sasa kama Rwanda kufikia 2011 walikua na coverage ya 90% bima ya afya sisi tunashindwa nini??

Tusiishi kwa kukariri tujifunze Rwanda tupunguze ujuaji.
 
Mkuu wewe ndio mweupe sana kwenye uchumi eti una compare GDP ya Belgium na Tz ili useme haiwezekani? Sasa nikupe challenge.

Model ya bima ya afya wametohoa Rwanda ina hiyo special package ya Jeshi alafu kuna wafanyakazi wa umma, then kuna wale wenye kipato cha chini kabisa wasio kwenye sekta rasmi n.k

2.Justification yake ni kwamba michango inategemea income bracket uliyopo. Rwanda wameigawa mara 4 kwahiyo utachangia kulingana na uwezo wako wa kiuchumi lakini wale waliopo chini kabisa yaani wanaoishi kwenye umaskini wa kutupwa basi serikali inawachangia totally wakishirikiana na mfumo wa crowdfunding wa kijamii tunaweza uita "Ujirani mwema"

3. Mchango wa serikali ya Rwanda ni almosy 14% pekee kwahiyo haiathiri mapato ya Serikali kabisa kwenye kuendesha mfuko.
4. Usichofahamu ni kwamba mfuko ukiwa na pesa zinazungushwa kwenye biashara mbalimbali na masoko ya hisa hivyo pesa inazaa ili mfuko uwe unakua zaidi na kupunguza risk ya float.

5. Unasema GDP ya Belgum blah blah, sasa naomba ufaham Tz imeizidi GDP ya Rwanda karibu mara 6.7 kwa data za 2018. Sasa kama Rwanda kufikia 2011 walikua na coverage ya 90% bima ya afya sisi tunashindwa nini??

Tusiishi kwa kukariri tujifunze Rwanda tupunguze ujuaji.

Soma vizuri uelewe hoja yangu kisha ujibu accordingly. Kama kila mtanzania atapata bima inayomuwezesha kupata huduma bora kwa nini kuwe na bima maalum kwa ajili ya askari? Huoni hapo tayari kuna tofauti ya huduma. Je huyo mtanzania mwenye hiyo bima atatibiwa Hindu mandal au Aga khan au ataishia hospitali ya wilaya?

Msingi wa hoja yangu ni kuwa kipato binafsi cha mtu ndicho huamua akate bima ya aina gani, atibiwe wapi, mtoto wake asome wapi siyo blah blah.

Mpaka sasa nimepost uzi aina tatu soma zote ujibu hoja kwa hoja.
 
Labda ungeelezea hizi bima wanazolipiwa watu katika ngazi za mitaa/vijiji a,bazo viongozi wanajinasibu nazo japo ni wananchi wachache wanazimudu ni kwa ajili ya kwenda Muhimbili au Agakhan? Suala hapa ni kupata huduma za afya ktk hospotali/ zahanati na vituo vya afya vinavyowazunguka. Lakini kwa vile status yako unaishi mjini umewaza Muhimbiki na Agakhan. Umewafikiria wanachi huko vijijini ambao hata uwezo wa kupata huduma ktk zahanati na vituo vya afya hawana? Hebu jenga hoja zako kuanzia kwenye zahanati na vituo vya aafya.
 
Soma vizuri uelewe hoja yangu kisha ujibu accordingly. Kama kila mtanzania atapata bima inayomuwezesha kupata huduma bora kwa nini kuwe na bima maalum kwa ajili ya askari? Huoni hapo tayari kuna tofauti ya huduma. Je huyo mtanzania mwenye hiyo bima atatibiwa Hindu mandal au Aga khan au ataishia hospitali ya wilaya?
Msingi wa hoja yangu ni kuwa kipato binafsi cha mtu ndicho huamua akate bima ya aina gani, atibiwe wapi, mtoto wake asome wapi siyo blah blah.
Mpaka sasa nimepost uzi aina tatu soma zote ujibu hoja kwa hoja.
Nshasema kutoa huduma kwa wote inategemeana na michango yao ambayo inatokana na vipato vyao.
Sasa hyo ya jeshi, watumishi wa umma n.k ni classifications tu hivyo zinaweza ongezwa au punguzwa ila haziathiri utoaji huduma wowote ule.

Hata basic marketing tu kuna issue ya segmentation unagawa soko kutokana na atrributes zinazofanana so hakuna kosa lolote hapo na hiyo model ndio inatumika maeneo mengi duniani hamuwezi soko zima mkawa na kipato sawa na bidhaa sawa (package) lakini walau itakua bora kuliko ukose vyote.

Ilani haiwezi chambua kila component hiyo itakua kazi ya sera ya taifa ya afya/ bima n.k. shida umesoma ilani tu bila kusoma model za bima ya afya duniani kote ili ukikosoa uwe na comparison sio kusema haiwezekani wakati Rwanda hao wamefika 90%.

Unashangaza
 
Labda ungeelezea hizi bima wanazolipiwa watu katika ngazi za mitaa/vijiji a,bazo viongozi wanajinasibu nazo japo ni wananchi wachache wanazimudu ni kwa ajili ya kwenda Muhimbili au Agakhan? Suala hapa ni kupata huduma za afya ktk hospotali/ zahanati na vituo vya afya vinavyowazunguka. Lakini kwa vile status yako unaishi mjini umewaza Muhimbiki na Agakhan. Umewafikiria wanachi huko vijijini ambao hata uwezo wa kupata huduma ktk zahanati na vituo vya afya hawana? Hebu jenga hoja zako kuanzia kwenye zahanati na vituo vya aafya.
Huko wilayani kwa sasa kuna bima CHF . Nyinyi mmekuwa mkibeza huduma za bima zinazotolewa sasa mkisema ni ghali na mbovu. Lakuni hiyo bima ya CHF wananchi wanachangia kidogo nafikiri sh 30,000 tu na wanatibiwa hadi hospitali ya wilaya. Kuna bima ya NHIF nayo mnaibeza kuwa ni ghali eti mnadai sh laki sita ni nyingi wakati mwenye nayo anatibiwa hospitali ya hadhu kama Hindu mandal. Ndio maana nikawataka mseme hiyo yenu rahisi mtu atatibiwa Hindu mandal?
Acheni ubabaishaji muwe wakweli katika haja zenu.

Sima pia thread zangu mbili kisha mjibu hoja.
 
Nshasema kutoa huduma kwa wote inategemeana na michango yao ambayo inatokana na vipato vyao.
Sasa hyo ya jeshi, watumishi wa umma n.k ni classifications tu hivyo zinaweza ongezwa au punguzwa ila haziathiri utoaji huduma wowote ule.

Hata basic marketing tu kuna issue ya segmentation unagawa soko kutokana na atrributes zinazofanana so hakuna kosa lolote hapo na hiyo model ndio inatumika maeneo mengi duniani hamuwezi soko zima mkawa na kipato sawa na bidhaa sawa (package) lakini walau itakua bora kuliko ukose vyote.

Ilani haiwezi chambua kila component hiyo itakua kazi ya sera ya taifa ya afya/ bima n.k. shida umesoma ilani tu bila kusoma model za bima ya afya duniani kote ili ukikosoa uwe na comparison sio kusema haiwezekani wakati Rwanda hao wamefika 90%.

Unashangaza
Mimi mwenyewe natibiwa kwa bima zaidi ya miaka 25 tena hisoutali kubwa hivyo naelewa concept ya bima sio tu za afya hata aina zingine.
In short huduma hazitafanana kwa watu wote, kuna watakaotibiwa hospitali za chini na kuna watakaotibiwa hadi Aga Khan. Hivyo huduma zitatofautiana kama zinavyotofautiana sasa kwa mwenye bima ya CHF, NHIF na Strategies.
 
Mkuu wewe ndio mweupe sana kwenye uchumi eti una compare GDP ya Belgium na Tz ili useme haiwezekani? Sasa nikupe challenge.

Model ya bima ya afya wametohoa Rwanda ina hiyo special package ya Jeshi alafu kuna wafanyakazi wa umma, then kuna wale wenye kipato cha chini kabisa wasio kwenye sekta rasmi n.k

2. Justification yake ni kwamba michango inategemea income bracket uliyopo. Rwanda wameigawa mara 4 kwahiyo utachangia kulingana na uwezo wako wa kiuchumi lakini wale waliopo chini kabisa yaani wanaoishi kwenye umaskini wa kutupwa basi serikali inawachangia totally wakishirikiana na mfumo wa crowdfunding wa kijamii tunaweza uita "Ujirani mwema"

3. Mchango wa serikali ya Rwanda ni almosy 14% pekee kwahiyo haiathiri mapato ya Serikali kabisa kwenye kuendesha mfuko.

4. Usichofahamu ni kwamba mfuko ukiwa na pesa zinazungushwa kwenye biashara mbalimbali na masoko ya hisa hivyo pesa inazaa ili mfuko uwe unakua zaidi na kupunguza risk ya float.

5. Unasema GDP ya Belgum blah blah, sasa naomba ufaham Tz imeizidi GDP ya Rwanda karibu mara 6.7 kwa data za 2018. Sasa kama Rwanda kufikia 2011 walikua na coverage ya 90% bima ya afya sisi tunashindwa nini??

Tusiishi kwa kukariri tujifunze Rwanda tupunguze ujuaji.

Tangu jana nilipojibu hoja zako za kukosoa uzi wangu na kukutaka ujibu hoja kwa hoja umeshindwa kujibu.
Sasa naongeza:

Unalaumu mimi kulinganisha Tanzania na Ubelgiji, lakini unasahau kuwa Lissu ndiye alianza kulinganisha huduma za afya za Tanzania na Ubelgiji na kujinasibu kuwa ataboresha ili tufanane nao. Nami nilimkosoa kuwa hawezi kwa kutumia data za Ubelgiji na Tanzania.

Kama kweli umesomea uchumi unafahamu kuwa katika uchumi comparison ni lazima aidha kwa subjects tofauti au kati ya vipindi tofauti au vyote viwili. Hata wewe mwenyewe umelinganisha Tanzania na Rwanda.

Unanilaumu mimi kuonyesha GDP ya Ubelgiji imeizidi ya Tanzania karibia mara tisa lakini wewe mwenyewe unasema GDP ya Tanzania ni kubwa mara sita kuliko Rwanda! in9aonyesha hujui unasimamia nini.

Unasema mfuko wa bima unawekeza kwenye masoko ya hisa etc, kwani nani aliyebisha hilo? Ndio maana Bima wanachukua premium mwanzoni ili wawekeze wawe na uwezo zaidi kutoa huduma husika lakini hiyo haimaanishi kuwa ndio wawe na uwezo kupindukia.

There is limitation. Primium anayolipa mnufaika ndio determinant ya ubora wa huduma atakayopata kwa sababu licha ya uwekezaji bado8 kuna kiwango cha chini kinachohitajika ili kutoa aina fulani ya huduma ya bima na hilo huwa linafanyika kitaalam.

Kuna watu hapa nchini wana bima zinazowaruhusu kutibiwa hadi nje ya nchi kama India.

Nasisitiza kipato cha mtu ndicho kitaamua achangie bima ipi na extent ya ubora wa huduma sio blah blah zenu. Nina uhakika hamuwezi kujibu kwa sababu mnajua kuwa mnafanya ubabaishaji.

Katika majibu yako kwa uzi wangu mwingine kuhusu uchumi unalaumu mimi kufanya comparison ya uwiano wa makusanyo kwa GDP. Pia unanishangaa eti kutumia wastani wa Africa kama basis ya kusema hamuwezi kufikia uwiano wa makusanyo ya kodi ya asilimia 25.

Wewe kweli ni mchumi? Hujui kuwa kutumia data zilizopita kwa ajili ya kufanya forecast ya baadae ni kitu kinachokubalika katika uchumi! Ulisoma econometrics?

Kweli hujui umuhimu wa mean (wastani)! Mimi nimeangalia wastani wa Africa, Kenya ambayo ni majirani zetu na kisha trend ya Tanzania ndipo nikaja na conclusion yangu based on data. Sasa na wewe unatakiwa unipinge kwa data. Uchumi unahusisha sana kucheza na data sio blah blah.

Nina hakika mashabiki karibia wote wa Lissu hawajaisoma ilani ya CHADEMA .

Pia umedai watu hawachangii thread zangu! Kwanza kuna kusoma na pia kuna kuchangia, kama mtu hata kusoma hataki atawezaje kuchangia? Umeiishaona mada za matusi, kukashifu zinavyosomwa humu jf na kule twitter? Inategemea taste/ interest ya msomaji.

Wanaopenda kusoma critical issues siku zote ni wachache hata waandishi wetu wa habari wamo.
 
Mimi mwenyewe natibiwa kwa bima zaidi ya miaka 25 tena hisoutali kubwa hivyo naelewa concept ya bima sio tu za afya hata aina zingine.
In short huduma hazitafanana kwa watu wote, kuna watakaotibiwa hospitali za chini na kuna watakaotibiwa hadi Aga Khan. Hivyo huduma zitatofautiana kama zinavyotofautiana sasa kwa mwenye bima ya CHF, NHIF na Strategies.
Huko wilayani kwa sasa kuna bima CHF . Nyinyi mmekuwa mkibeza huduma za bima zinazotolewa sasa mkisema ni ghali na mbovu. Lakuni hiyo bima ya CHF wananchi wanachangia kidogo nafikiri sh 30,000 tu na wanatibiwa hadi hospitali ya wilaya. Kuna bima ya NHIF nayo mnaibeza kuwa ni ghali eti mnadai sh laki sita ni nyingi wakati mwenye nayo anatibiwa hospitali ya hadhu kama Hindu mandal. Ndio maana nikawataka mseme hiyo yenu rahisi mtu atatibiwa Hindu mandal?
Acheni ubabaishaji muwe wakweli katika haja zenu.

Sima pia thread zangu mbili kisha mjibu hoja.

Sijaelewa hoja yako? Unataka watibiwe Hindu Mandal level au issue ni coverage ya bima?

Nishasema marketing inahusu segmentation hivyo lazima vifurushi na michango vitofautiane.

Hata ukiwa unatibiwa hospitali ya kawaida ila maadam una bima ni bora kuliko utumie pesa ya mfukoni.

Na ambacho hufahamu mfuko ukiweza hamasisha watu let's say zaidi ya million 20 kujiunga obvious gharama za mchango zinashuka sababu mnakuwa wengi so mnaingiza mzigo mkubwa kwenye mifuko.

Hapa hoja ni kila mtu kuwa na bima hayo ya kutibiwa uswazi au AAR ni suala dogo tu afterall mkiingia wengi kwenye bima serikali itabidi ipanue wigo wa huduma za vituo vya afya ili ziwe na dawa za kutosha, personnel wa kutosha mwisho wa siku huna haja ya kwenda Hindu Mandal wakati unaweza pata huduma zote kwa ubora ma nafuu.
 
Tangu jana nilipojibu hoja zako za kukosoa uzi wangu na kukutaka ujibu hoja kwa hoja umeshindwa kujibu.


Unalaumu mimi kulinganisha Tanzania na Ubelgiji, lakini unasahau kuwa Lissu ndiye alianza kulinganisha huduma za afya za Tanzania na Ubelgiji na kujinasibu kuwa ataboresha ili tufanane nao. Nami nilimkosoa kuwa hawezi kwa kutumia data za Ubelgiji na Tanzania.

Mkuu ambacho hatuelewani ni kipi?

Mie nachopinga ni kurely kwa Sub sahara average na GDP ya Belgium ili kusema Tz hatuwezi kufanya suala X. Hoja niliyojenga ni kwamba kma GDP ndio inaamua kivipi Rwanda imefanikiwa kuwapa bima 90% ya Rais wake?

Umewahi sikia Economic Tigers wa Asia nchi kma Singapore,S.Korea,Hong kong n.k. kipindi ambacho Asia ilikua imechoka kiuchumi baada ya vita kuu za dunia na chaos nyingi hapo katikati hao jamaa walitokea tu out of nowhere booom wakapaa kiuchumi.

Walikua level moja na Tz kufikia miaka ya 60 ila kufikia miaka ya 90 walituacha zaidi ya mara 30!! Ikimaanisha usiangalie mazingira yanayokuzunguka ili kukadiria maendeleo yako.

Cha msingi hapa sisi tunaangalia kwamba tunakua by 8% hizi data ndio zituhusu. Hatuwezi sema uchumi wetu utaporomoka kisa tu average ya sub sahara labda ni chini ya 5%. Forecast Unafanya kwa data zinazokuhusu hizo sub sahara ni comparison tu ya kujua status yako ulipo.

Mbona umeme mnadai mmefikisha kwa 90% ya Watanzania ilihali average ya sub sahara ni chini ya hapo? Au mnasema kwamba average ya sub sahara ingezuia kazi za REA?
 
Mkuu ambacho hatuelewani ni kipi?
Mie nachopinga ni kurely kwa Sub sahara average na GDP ya Belgium ili kusema Tz hatuwezi kufanya suala X. Hoja niliyojenga ni kwamba kma GDP ndio inaamua kivipi Rwanda imefanikiwa kuwapa bima 90% ya Rais wake?
Umewahi sikia Economic Tigers wa Asia nchi kma Singapore,S.Korea,Hong kong n.k. kipindi ambacho Asia ilikua imechoka kiuchumi baada ya vita kuu za dunia na chaos nyingi hapo katikati hao jamaa walitokea tu out of nowhere booom wakapaa kiuchumi. Walikua level moja na Tz kufikia miaka ya 60 ila kufikia miaka ya 90 walituacha zaidi ya mara 30!! Ikimaanisha usiangalie mazingira yanayokuzunguka ili kukadiria maendeleo yako.
Cha msingi hapa sisi tunaangalia kwamba tunakua by 8% hizi data ndio zituhusu. Hatuwezi sema uchumi wetu utaporomoka kisa tu average ya sub sahara labda ni chini ya 5%. Forecast Unafanya kwa data zinazokuhusu hizo sub sahara ni comparison tu ya kujua status yako ulipo.

Mbona umeme mnadai mmefikisha kwa 90% ya Watanzania ilihali average ya sub sahara ni chini ya hapo? Au mnasema kwamba average ya sub sahara ingezuia kazi za REA?
Acha kuzunguka, kwani Lissu aliposema CHADEMA watatpoa huduma bora za afya kwa kufananisha na Ubelgiji alitegemea nini? Mimi nimeonyesha kwa data kuwa ili utoe huduma za kiwango hucho utahitani kuwa na kipato zaidi ya ubelgiji ukixingatia sisi tuko mara tano zaidi kuliko wabelgijibna uchumii wetu uko chini mara tisa kuliko wao. Huo muujiza hauwezekani.

Hata sasa bila bima kwa baadhi bado watu wakienda hospitali wanatibiwa mfano wazee wote wanatibiwa bure.

Wilaya mbalimbali zina mfumo wa bima ila bado haujamfikia kila mtu lakini hilo linaendelea kufanyika.

Ninachokataa ni hicho mnachodanganya watu kuwa chini yenu huduma zitakuwa bora.

Jinsi uwezo wa kiuchumi unavyoongezeka ndivyo huduma za afya zitakavyoendelea kuboreshwa.

Comparison, forecast au projection katika uchumi ni vitubvya kawaida.
 
Sijaelewa hoja yako? Unataka watibiwe Hindu Mandal level au issue ni coverage ya bima?
Nishasema marketing inahusu segmentation hivyo lazima vifurushi na michango vitofautiane.
Hata ukiwa unatibiwa hospitali ya kawaida ila maadam una bima ni bora kuliko utumie pesa ya mfukoni.
Na ambacho hufahamu mfuko ukiweza hamasisha watu let's say zaidi ya million 20 kujiunga obvious gharama za mchango zinashuka sababu mnakuwa wengi so mnaingiza mzigo mkubwa kwenye mifuko.

Hapa hoja ni kila mtu kuwa na bima hayo ya kutibiwa uswazi au AAR ni suala dogo tu afterall mkiingia wengi kwenye bima serikali itabidi ipanue wigo wa huduma za vituo vya afya ili ziwe na dawa za kutosha, personnel wa kutosha mwisho wa siku huna haja ya kwenda Hindu Mandal wakati unaweza pata huduma zote kwa ubora ma nafuu.
Niliposrma hindumandal au Aga Khan hospitals nilikuwa namaanisha hadhi kwa sababu hata ukiwa huna hela bado utaugua magonjwa ambayo pengine yatahitaji matibabu ambayo hayapatikani hospitali za wilayani au vituo vya afya au zahanati mfano kusafisha figo, CT Scan, vipimo vya moyo nk. Sasa kama una hiyo bima lskini huwezwi kutibiwa magonjwa makubwa bado unaita hiyo bima ni bora?

Badala ya kufanya ujanja ujanja muwe wakweli hiyo bima yenu itamgharimu mtu shilingi ngapi kuliinganisha na bima zinazotolewa sasa na ataweza kupata huduma zipi ili sasa watu walingamishe .
 
Back
Top Bottom