Ila wanawake ni "selective" mno!

Nisubiri mpaka ndoa au siyo?
 
Nimejifunza. Ahsante sana Mr. Kiranga!
 
Hata mwanaume usipokuwa selective inamaanisha hujitambui.
Yaani kila Mwanamke unataka upite naye. Mwishowe upate mikosi.

Kwa Hilo Wanawake wapo Right kabisa.
Napenda Wanawake wabaguzi, wanaoringa, ambao hawafikiki kirahisi.
Tycoon nimejifunza kwenye mchango wako. Ahsante Mr. Tycoon
 
Changamoto yako ilianzia katika kumuangalia uso na mwili wake tu.Ulipaswa uende mbele au ndani zaidi.Wao huangalia anamiliki nini ambacho kinamfanya mwanaume aweweseke.Sura siyo ishu.Sura pelekea mama ngedere.🤔
 
Tycoon nimejifunza kwenye mchango wako. Ahsante Mr. Tycoon

Iko hivyo.

Mitazamo ya Watu isiamue katika maamuzi na machaguo yako.

Yaani Kwa vile wewe ni kijana labda unatoka familia Maskini na labda hauna mvuto ati ndio iwe sababu ya kutochagua Wanawake warembo na wenye hadhi. Huko ni kutojitambua.

Halikadhalika na Wanawake.
Muonekano wake na asili yake labda ni umaskini wa kwao. Isiwe kigezo cha Watu kumchagulia wanaume dhaifu au wasio na mvuto autakao(kulingana na vile apendavyo).

Kama Binti anataka kijana mzuri au maarufu, au mwenye Pesa Kwa nini Vijana wasio na hizo Sifa Waumie? Na watake kumdidimiza kisa ya vile anavyoonekana?

Ni kweli hata Mimi demu akinizingua Kwa Sifa ambazo sina ninaweza nami kumzingua ili nipate ahueni, lakini kwake sitaona anamakosa
 
We jamaa fala sana,nimecheka kinoma!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…