Taarifa iliyotolewa hivi Punde na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu jijini Dar es salaam, imeeleza kuwa kumeitishwa Mkutano na waandishi wa habari Jumatatu asubuhi Ikulu jijini Dar es Salaam.
Mkutano utafanyika saa tatu kamili asubuhi na kila chombo kimetakiwa kutuma Mwandishi pamoja na mpiga picha ambao wametakiwa kuwa tayari wameketi vitini ifikapo saa Mbili Unusu bila kuchelewa wala kukosa.
Agenda ya mkutano huo ni "SHUGHULI MAAUM" na hakuna ufafanuzi zaidi uliotolewa.
Ikumbukwe pia kwamba mchana Jumatatu Rais ataongea na wazee wa Dar es salaam.
Huenda (NARUDIA "HUENDA") Mkutano wa wazee ukatumika kufafanua yatakayotoka katika mkutano na wanahabari Asubuhi.
Kesho kuna kila dalili zinaonyesha kuwa wazeealioalikwa wamepewa maswali ya kuuliza. Maaana nasikia wameambiwa waende walioalikwa tu. Wengine wafuatilie kwa radio na TV.