Ikulu pana mnyama, sura kama mwanangu

Ikulu pana mnyama, sura kama mwanangu

Dotto C. Rangimoto

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2012
Posts
1,985
Reaction score
1,286
IKULU PANA MNYAMA, SURA KAMA MWANANGU.

Nasema nawe kibabu, rafiki yake kileje,
Huwezi wajipa tabu, sijui hata ukoje?
Kwa chai takuadhibu, siulize nawezaje,
Jamii yako ya boflo, chai ni chako kiboko.

Utambe kibabu tamba, utabaki kuwa ngano,
Tamba mjini na shamba, takungoja kwa chano,
Kibabu hauwi mwamba, mbele ya haya meno,
Nguvu yako ya hamira, uko na nini kibabu.

Kote Unguja na Pemba, hata huku kwetu bara,
Kibabu weye watamba, na sandarusi za gwara,
Waununua umwamba, sihasa ni biashara,
Siasa yaweka mtu, sihasa ya mnunua.

Siha ya huyu kibabu, mwenzenu yanipa shaka,
Tembea yake ya tabu, mwendowe apepesuka,
Anahitaji tabibu, kwa joto atetemeka,
Ikulu pana mnyama, suraye kama mwanangu.

Njano5.
0784845394
0762845394 Whatspp
 
Ikulu bado mnya hajafika,Japo sura wanafanana, hakika Afya yake si njema, Japo kwa mabavu anajikongoja.
 
I see...tungo zote hizi kumkandia mtu...Hivi hamuwezi kuninadi kwa namna ya kistaarabu badala ya kutumia mnaodhani ni udhaifu wa mwenzenu?
 
Hiki kibabu kama kichawi, kung'ang'ania asiyoweza,
Maadili hayajuwi, ufisad anauweza,
 
  • Thanks
Reactions: DSN
Ikulu yake kwapani,nyie toeni mimacho
hii ni mali ya kwangu,nani kawambia yenu,familia ile wapi nami nimepazoea
manani kanijalia,lazima wangu akae!!!:bange:
 
Ikulu yake kwapani,nyie toeni mimacho
hii ni mali ya kwangu,nani kawambia yenu,familia ile wapi nami nimepazoea
manani kanijalia,lazima wangu akae!!!:bange:

Mashairi yasiyoeleweka generated from ganja planta yanaendelea kuwatoka, mwaka huu mnakua vichaa aisee!
 
Hata kama kwa ngwala hakika tutawatawala;
Siridhiki na somo kwa ku ukataa mgomo hakika ccm ndio muhamala;
Hakika kelele za chura zitaishia geti la kula.
 
Dotto C. Rangimoto

Wewe hivyo viroba unavyo bwia asubuhi asubuhi matokeo yake ndo hayo unaanza kutunga tunga mashahiri ya ajabu ajabu, nenda kaimbe HIP HOP basi tukuelewe
 
Last edited by a moderator:
Vina finyu.
Haaaa wapi umeambulia patupu vina nini watu ujumbe....kwenye hilo holaaaaaaaaaaa ....pakavu......chuchuchu konda kantukana na weee mtukane ..jikonda hilloooooo!!
 
Back
Top Bottom