Ikulu kuwafutia posho Wabunge!

Ikulu kuwafutia posho Wabunge!

Wabunge wanaonewa bureee! Vikao kama tender boards kwenye taasisi za umma wajumbe hulipwa posho ya laki 2 per sitting ndani masaa yasiyozidi 4. Vikao vya board za wakurugenzi za mashirika wajumbe hulipwa kuanzia laki 4 na kuendelea. Vikao vingine vyote katika taasisi za umma wajumbe hulipwa kati ya elfu 50000 hadi laki 2 kutegemeana na uwezo wa taasisi. Semina, workshops, trainings etc zote wahusika hujilipa kati ya 50000 hadi laki 2. Sijui kwa nini tunakomalia posho za wabunge tu

Hao wajumbe ni wangapi na wanakutana kwa siku ngapi kwa mwaka?

Je, unadhani kwamba hawastahili?

Ubunge ni uwakilishi, hata mishahara yao haipaswi kuwa mikubwa na "posho za kukaa kitako" ndo kabisa hawastahili. Unalipwaje posho kwa uwakilishi? Imekuwa ajira hiyo?
 
Rais tumempa mamlaka atekeleze mambo, nasikitika nae analalamika sasa nani atatenda?. Soma hapa kwenye FB yake




Hatuwezi kuvumilia kuona taasisi za umma zikitumia mamilioni ya fedha kwa ajili tu ya posho kwa watumishi wake. Taasisi hizi kwa mfano Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) ambazo ni mali ya umma zinapaswa kutumia fedha hizi kwa ajili ya kukuza na kujiboresha zenyewe na sekta husika zaidi na zaidi na si vingineyo.
 
Kwenye ukurasa wake wa fb rais Kikwete amekemea matumizi ya posho kwenye taasis za umma,ametolea mfano TANAPA

Hoja imepotoshwa. JK alitoa changamoto kwa TANAPA kutangaza vivutio vya Utalii wa Tanzania hadi Far East na kutobaki maofisini (nchini) wakigawana Posho. Kwa maoni yangu hakutoa kauli ya maana ya kupinga posho hizo na wala hakugusa kiivo Taasisi za Umma, ameisaidia TANAPA kubaini maeneo mengine ya posho (kwa ruksa ya Rais mwenyewe). Kwani ziara za kutangaza vivutio nje ya nchi hufanyika bila watu kulipwa posho?
 
So unawatetea wabunge au board memberz?
Wabunge wanaonewa bureee! Vikao kama tender boards kwenye taasisi za umma wajumbe hulipwa posho ya laki 2 per sitting ndani masaa yasiyozidi 4. Vikao vya board za wakurugenzi za mashirika wajumbe hulipwa kuanzia laki 4 na kuendelea. Vikao vingine vyote katika taasisi za umma wajumbe hulipwa kati ya elfu 50000 hadi laki 2 kutegemeana na uwezo wa taasisi. Semina, workshops, trainings etc zote wahusika hujilipa kati ya 50000 hadi laki 2. Sijui kwa nini tunakomalia posho za wabunge tu
 
Imepotoshwaje?pitia wol yake kombo
Hoja imepotoshwa. JK alitoa changamoto kwa TANAPA kutangaza vivutio vya Utalii wa Tanzania hadi Far East na kutobaki maofisini (nchini) wakigawana Posho. Kwa maoni yangu hakutoa kauli ya maana ya kupinga posho hizo na wala hakugusa kiivo Taasisi za Umma, ameisaidia TANAPA kubaini maeneo mengine ya posho (kwa ruksa ya Rais mwenyewe). Kwani ziara za kutangaza vivutio nje ya nchi hufanyika bila watu kulipwa posho?
 
Mbona asijitambulishe huku JF na kutoa hayo maona yake huku?
 
Mdau kombo soma hapa!
Rais tumempa mamlaka atekeleze mambo, nasikitika nae analalamika sasa nani atatenda?. Soma hapa kwenye FB yake




Hatuwezi kuvumilia kuona taasisi za umma zikitumia mamilioni ya fedha kwa ajili tu ya posho kwa watumishi wake. Taasisi hizi kwa mfano Mamlaka ya Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) ambazo ni mali ya umma zinapaswa kutumia fedha hizi kwa ajili ya kukuza na kujiboresha zenyewe na sekta husika zaidi na zaidi na si vingineyo.
 
kwani wazee wa DSM nao wapo Facebook hizo? kauli si huwa anaztoa mbele yao
 
KIUCHUMI CLASSICAL, (si
kimaadili): Kitendo cha
wabunge kuongezewa POSHO
ni cha KUPONGEZWA
KABISA!!!!! kwa kuwa: 1. Posho
ni INCENTIVE TO WORK. Hivyo
ufanisi wa mbunge utaimarika
ktk kutumikia wananchi, 2.
Kitendo hiki kitashawishi
ELITES WA NCHI HII kuhamia
bungeni 2015!! hivyo bunge
litaingiliwa na wataalam (who
search for green pasture)
watakaokuwa chachu ya
maendeleo kupitia mipango
na maamuzi..., 3. Posho
ITAPUNGUZA (sio kumaliza)
tabia ya wabunge kujihusisha
na ubadhirifu, na biashara
nyingine.
 
sioni haja ya kuwafutia posho wabunge rather tuwaongezee watumishi wengine posho.
 
Msanii kiongozi ameamua kuchonganisha kati
ya wabunge na spika so wamn'goe Tu
 
Back
Top Bottom