IKULU, DAR: Rais Magufuli afanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Prof. John L. Thornton

Ila huyu jamaa yan anatihasira basi tu ...ss kama mawazir wa nishati na wa sheria walitajwa kwa nn waliowateua wasitajwe!!

Muswada wa sheria kabla yakuwa sheria ni nani anaetia sahihi ya mwisho kuidhinisha!!!?

Tusiiiiii....

Very pissed.
 
Kweli hayo ni maswali ya kijinga kama ulivyo sema wewe mwenyewe.

Tatizo tangu Mwanzo umeshindwa kumuunga mkono Rais, wewe na wenzako hamjulikani mnataka nini hasa.

Look, amekuja Mwenyekiti wa ACACIA ambayo sisi hatuna hata mkataba nae sisi tuna mikataba na makampuni yake.

Amekuja kutaka kujua tatizo na kushirikiana kulitatua. Sasa ulitaka Rais amkamate na kufunga?

Hivi, watangazaji wa ITV wakikosea, Mengi akaenda Ikulu kujadili na kuona namna ya kulimaliza, unamkamata Mengi na kumuweka ndani? Au pale Mtwara kiwanda cha Dangote kikakwepa kodi, Dangote akaja kujua ukweli na nini na kujadili namna ya kulipa, unamkamata Dangote na kumuweka ndani?

Haters mnajiaibisha sana ktk hili. Hakika mmekosa uzalendo na heshma kwa nchi yetu

naona uzalendo ni kutowahusisha marais wastaafu na huu uchafu kana kwamba waziri anaweza kujiamlia jambo kubwa kama kushusha kiwango cha hisa za serikali kutoka 15% hadi 0% bila Mkuu wake kufahamu! Kifupi, kuna tofauti ya uzalendo na mahaba kwa muigizaji! wewe una mahaba hauna uzalendo na wahenga walisema mapenzi hutia upofu!!! sio kosa lako
 
Sijui kama wanadanganya makusudi au ni kwamba hatujui Kiingereza cha huyo Mkanada.

HAKUNA mahala BARICK wanasema wanakubali deni, wanatubu, watalipa.

Jamani, wenzetu hawa wanatumia vichwa vyao kufikiri na kuongea. Hawafiki mwezini kwa vichwa vya panzi. Hawajitamkii tu maneno ovyo ovyo.

CEO wa ACCACIA hawezi kutamka, tena kwa maandishi, kupinga na kukemea ripoti ya Tume halafu mwingine aje nyuma yake aseme wanakiri, wanatubu, watalipa. Haiwezekani!
Hahahahahaaa imewauma Sana sijui wewe Na prof Palamagamba Kabudi nani anayejua Kiingereza.
Kama Acacia walitoa tamko sasa amekuja boss wake Katubu nyie endeleeni kupiga Kelele
 
Per yr almost sisi tunatumia 20 trillions.. Achsna na budget inayopitishwa bungeni sijui 31 trillions tshs. In actual, sense and real numbers roughly inatumika around 20 trillions kwa mwaka..

Sasa wakilipa 100 trillions of tshs.. Sio miaka 5 ya budget? Think it.. Sbb kamati imepata denied halisi ni 108 trillions of tshs tokea 1998 hadi March 2017.. So unafikiri mahesabu yatakuwa tofauti sana kamati? Subiri uone nakuapia utaona
Trillion mia inatoka wapi mkuu????? Mnapata 4% ya mrahaba pekee sasa kma 4% ni 100 trilion in maana ACACIA wanafaida ya trilion 1000?????? Kutoka kwenye makinikia pekee???

Kweli CCM itatawala milele
 
Barrick wameomba mazungumzo so as wanaweza kupewa report zote mbili wakazitumie mahakamani kama ushahidi. Mark my words.
Maana previously waliomba wakanyimwa.
Lumumba are very hopeless, mtu wamashakana kuwa zile ripoti ni uongo, leo eti atalipa. Mzungu katika clip yake hakuna aliposema atalipa! Hawezi kujikomit kijinga namna hivyo za kijinga kama hizo!
 
hizi sio press conference za ufipa, mambo makubwa haya lazima twende kwa procedure

hizo procedure tangu mwanzo hamkuzijua!!? Mfa maji haachi kutapa tapa!! Nitamuunga mkono Rais endapo atapiga stop uchimbaji wowote wa madini hadi sheria mpya nzuri zitungwe zitakazowezesha mikataba mizuri angalau ya 51% zetu kwa 49%za kwao kama alivyotaka Nyerere
 
Anashangaza sana huyu! Kwanini anaukimbia ukweli! Hata kuwajadili mafisadi Mkapa na Kikwete waliotufikisha hapa tulipo hataki! Ni sheria ipi inayotuzuia Watanzania kuwajadili hawa mafisadi wawili!? Kweli dikteta uchwara katika ubora wake!
Mkuu huyu bwana alishasema hatafukua makaburi. Kwa hiyo tusitegemee hata hao mawaziri kama kuna lolote watafanywa. Habari ndio imekwisha hivyo.
 
NI mwehu tu ndie anaweza kuamini kwamba Barrick wamekubali kulipa matrioni yote yale!!! Hao Acacia wenyewe hata wakisema wauze mali zao zote bado hawana ubavu wa kupata angalau Trillion 100!!
hebu kuwa na Adabu wewe hivi unaijua Barrick wewe au unaisikia??? Bajeti yetu kwa mwaka huu tilion30 kwa taarifa yako wale wana uwezo wa kugharamia bajeti ya nchi hii kwa miaka20 ndo wanafilisika
 
Usiwe na haraka.
Win win situation umeipata? Hapo kuna mchezo unataka kuchezeka.Bado hatujavuka mto na tuzizodoane


Vyoyvote vile lkn Muzungu mwenyewe amekuja kutufuta kinyume na huyo takataka wenu alivyokuwa anataka tufanye tumsujudie Muzungu, fvck chadema!
 
Kwa hiyo unakubali dhahabu wanaiba kama kawa? kwanini huheshimu watu wenye data? unaweza kutoa ushahidi wa wizi wa dhahabu? Kama wewe ambaye hujafika mgodini unaamini wanaiba je wale walioenda kufanya utafiti? Dogo unajichanganya sana, badilika usiwe kama Tundu.
Wanaiba sana tena ACACIA ni majizi mno hilo nakubali napongeza pia juhudi za kudai madini yetu 100% ingawa ningependa zaisi tubane dhahabu na mrahaba kuliko makinikia pekee

However shida yangu kwenye huu uzi mnatupotosha sisi wengine kuwa eti wamekubali kulipa trilion 103 ??? Ssa nikuulize wwe kama makinikia pekee ni trilion 103 je dhahabu original itakuwa shingapi??? Na kma kweli ni hicho kiasi je mmesahau kuwa ssi tutapata tu mrahaba wa 4% ambao ni chini ya trilion 5??

Naunga mkono hoja ila kwa hili mnapotosha
 
Hakuna kiasi kilichotajwa, hapo ni mawasiliano yatafanyika kwanza. Sasa wewe kwa akili yako, unataka nini? Ndoto yako ya usiku ni IPI?
Barua imeshasema Mwenyekiti na Rais wamekutana kwa mazungumzo na kwamba Acacia wapo tayari kulipa fedha ambazo Tanzania imezipoteza kutokana na kampuni kampuni hiyo kuendesha shughuli zake hapa nchini!!!

Rais nae amesisitiza kwa kusema pamoja na Mwenyekiti kukubali kuilipa Tanzania lakini....

Wewe unadai hakuna kiasi kilichotajwa! Kivipi unasema hakuna kiasi kilichotajwa wakati ripoti ilionesha wazi kiasi cha kodi tuliyopaswa kulipwa lakini imepotea?! Kiwango cha chini kabisa kilichotajwa ni shilingi trilion 68.5 na kiwango cha juu shilingi trilioni 108 kutokana na mapato ghafi ya zaidi ya shilingi trilioni 380.

Kwamba mini nataka nini? Jibu ni very simple... mosi, LAZIMA tulipwe stahiki yetu! Lakini pamoja na yote hayo, wasitubandikie ma-figure yasiyo-reflect hali halisi!!!

Kama kwa miaka 19 makinikia peke yake yalizalisha trilioni 380, ina maana kwa wastani, kwa mwaka makinikia peke yake yanazalisha trilioni 20.

Sasa kama makinikia peke yake yanazalisha trilioni 20, vp kuhusu dhahabu isiyotokana na makinikia?!

Sidhani kama kuna kampuni yoyote ya madini duniani inayoweza kuzalisha pesa nyingi kiasi hicho kwa mwaka!!!!

Mimi ugomvi wangu tangu ripoti ya kwanza ni uhalisia wa takwimu!!!!

Ilipotoka ile ripoti ya kwanza haraka nili-deal na takwimu! Wala sikujisumbua ku-standardize viwango vya GGM lakini hata kwa kuacha data zingine constant na kisha ukaingiza tu zile za ripoti ya kwanza, nikakuta annually tungekuwa tunazalisha 260 tons za dhahabu na among top 3 world gold producer!!!

Hizi figures zimekaa kisiasa mno bila kujua ni wenyewe ndio zitakuja kuwatafuna hizi takwimu!! Kwa mfano, kama ripoti imeshasema kiwango cha juu cha kodi tulichopoteza ni trilioni 108; nitashangaa sana tena sana nikisikia serikali na Acacia wamekubaliana Acacia walipe trilion 10 kwa muda wa miaka 15; potelea mbali hata kama ndani ya miaka 5!!!
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation ambayo ni mmiliki mkubwa wa kampuni ya Acacia Mining Limited Prof. John L. Thornton na kukubaliana kuwa kampuni hiyo ipo tayari kufanya mazungumzo na Serikali ya Tanzania ili kulipa fedha ambazo Tanzania imezipoteza kutokana na kampuni hiyo kuendesha shughuli zake hapa nchini.

Baada ya Mazungumzo hayo Prof. John L. Thornton amesema kampuni yake ipo tayari kufanya mazungumzo na Tanzania yatakayozingatia maslahi ya pande zote mbili na pia ipo tayari kulipa fedha zote ambazo inapaswa kulipa kwa Tanzania.

Kwa upande wake Mhe. Rais Magufuli amesema Serikali inakaribisha mazungumzo hayo na itaunda jopo la wataalamu watakaofanya majadiliano na kampuni ya Barrick Gold Corporation ili kufikia makubaliano ya kulipwa fedha zinazodaiwa na namna kampuni hiyo itakavyoendesha shughuli zake nchini maslahi ya pande zote mbili.
wapumzike” amesema Mhe. Rais Magufuli.


Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
14 Juni, 2017


Kuna tofauti kubwa kati ya taarifa ya Ikulu (G. Msigwa) na walichokisema Mh Rais na Prof Thornton hapo kwenye clip.

Ni aibu na fedheha kutolewa kwa taarifa ambayo ina mapungufu makubwa namna ile kutoka taasisi yetu nyeti.
 
Back
Top Bottom