Ikiwa kweli: Lowassa atasambaratisha

Ikiwa kweli: Lowassa atasambaratisha

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Uvumi unakolea kuvuma. Uzushi unakolezwa na kuchagizwa kwa picha tengenezwa na halisi. Ukaribisho usio na vitisho unakaribia mwisho. Ni kumhusu Waziri Mkuu Mjiuzulu,Edward Ngoyai Lowassa. Lowassa anatajwatajwa kama aliye njiani kujiunga na CHADEMA na baadaye kupeperusha bendera ya UKAWA kwenye ngazi ya Urais hapo Oktoba. Yaani,Lowassa ataingia kilingeni kupambana na CCM yake!

Lowassa,ni jana tu, amekaribishwa UKAWA na kuanza kusafishwa. Ikasemwa kuwa Lowassa ni msafi na aliyeponzwa na mfumo. Kauli mbilimbili toka kwa watu wawili: wale na hawa. Lowassa amesemwa,ametajwa na hata kutengenezewa picha za kikaoni na CHADEMA. Yeye amekuwa kimya. Hakuzungumza wala angalau kujitokeza hadharani. Amekuwa kimya hadi anatisha.

Ukimya wa Lowassa una mitazamo miwili. Wa kwanza, Lowassa anajipanga ili apangike na ndipo afunguke. Afanye kweli. Hapo uzushi utakuwa ukweli. Yale ya 'lisemwalo lipo...kama halipo laja' yatatimia. Huo ni Upande A. Mtazamo wa pili,upande B, ni kuwa yote yanayosemwa na kuandikwa ni uongo mtupu. Ndiyo maana Lowassa anajinyamazia tu akiwacheka wasiochoka kuhangaika!

Ikiwa kweli, yaani ukijidhihiri upande A, Lowassa atakuwa ni jiwe sambaratishi. La kuogofya. Atasambaratisha UKAWA/CHADEMA na CCM-anapokwenda na anapotoka. Wapo wanachama wa pnde hizo watakaohama. Wapo watakaobaki kimwili lakini kiakili wakiwa wametoka au kuwemo na Lowassa. Lowassa atachochea uhamaji au usaliti CCM. Wanaomkubali wanatamani kufika naye mbali. Hawajakata tamaa. Watahama naye CCM au kubaki kupika chakula humo na kumpelekea Lowassa. Na kura zitapigwa kwa Lowassa.

Atakapohamia hakutabaki salama. Wapo watakaomkimbia au kubaki naye kinafiki. Hawa ni wale wanaoamini kuwa Lowassa si msafi na hafai. Wa aina hii watasusa au kusuasua directly au indirectly. Kura zao zitapepea. Atakapohamia napo patatikisika na kusambaratika. Maji yatachafuka katika bwawa atakalotoka na hata kwenye bwawa atakaloingia. Mambo hayatabaki hivi hivi.

Hakika, Lowassa akihamia UKAWA atakuwa jiwe sambaratishi. Lakini, ijulikane ya kuwa CCM iko imara na tayari kwa mpambano wa Oktoba!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Aione: Kiherehere, Tetty
 
zito,abwao na shibuda arfi, wakihama ni sawa ila lowasa kuhama kwake inakuwa tabu.toeni kwanza boriti katika jicho lako ndo uone kwa wenzako
 
Kikubwa adui afe iwe umetumia mshale au RPG, ie, mkoloni mweusi aondolewe the rest tutajua mbele ya safari. Tunang'oa the old system na kuweka the new one. In maendeleo Kwenda mbele! Bob Marley aliimba katika wimbo 'Who that cap fit' nanukuu......

"Your worse enemy could be your best friend, and your best friend your worse enemy"
 
VUTA-NKUVUTE

Mkuu hela ya Lowassainahamia kusambaratisha UKAWA kama vile ilivyotaka kusambaratisha CCM,ni vizuri wazee wa kitengo pale CCM waliliona hilo,kwa wanachosema viongozi wa UKAWA ni sawa na kula matapishi yao,yote hiyo ni tamaa,sasa nimeamini kuwa viongozi wa kisiasa wote ni wa aina moja,sijui wakati walipokuwa wanamsema Lowassa hapo mwanzo,kuna tofauti gani na hivi sasa,eti hajapelekwa mahakamani je wakati wakimsema na kumnanga alikuwa amepelekwa mahakamani?Ni ajabu akina Lipumba ,Mbowe,Makaidi,Slaa wakiwa watumwa wa pesa na utukufu wa magogoni,na hawataupata tumewashutukia.
 
Last edited by a moderator:
VUTA-NKUVUTE

Mzee wangu uliyoyasema ni ya kweli,Watanzania hatuko salama tena ndani ya UPINZANI wala ndani ya CCM kote kumechafuka.

Nimeshafanya maamuzi magumu kwangu mimi Bintiyo RAIS mpaka dakika hii sina lakini Mbunge wangu atabaki kuwa yule yule JJMnyika,maana naujua utendaji wake na ninaelewa kwa sasa kiakili kifikra yuko katika njia panda kama tulivyo wengine.Lakini ninajua atavumilia ili tuweze kushinda pande yetu.

Rais sina sababu:

1.Hata Magufuli siyo MSAFI,huyu ndiye yule aliyeuza nyumba za serikali na isitoshe akaamua bila hata haya kuikabidhisha moja kwa mamsapu yake ya kando....

2.Magufuli aliyeshindwa kupiga vita RUSHWA na UFISADI kwenye wizara yake sidhani kama ataweza kupiga vita RUSHWA akiwa RAIS na akiwa amezungukwa na wapiga deal,wenye pesa zao,wawekezaji ambao wengi wao ni marafiki wa huyu anayetoka....

3.Magufuli ameapa kuwa atayaendeleza yale yote yaliyofanywa na mtangulizi wake,duh sasa hapa naona ukuaji mkubwa wa RUSHWA,UFISADI,MADAWA ya KULEVYA,UGAWAJI wa MALI ASILI zetu...Kusafiri nje kila siku bila kuwa bila kujali hali halisi ya UCHUMI wetu.

Mzee hapa sina rais kwa pande hii.

Kwa UKAWA huku wakiweka huyu MASAI watanisamehe hata yeye siwezi kumpa KURA yangu,hivyo Mzee wangu KURA yangu ya URAIS nimebaki nayo mwenyewe...........
 
Last edited by a moderator:
Kwanza siamini kama ni kweli CHADEMA wanaweza kuchukua maamuzi ya hovyo kama hayo lakini ikiwa ni kweli basi ni kama nashuhudia anguko la CHADEMA siku za usoni! Na hata Lowassa akismama kama mgombea urais na akashinda, serikali yake haitakuwa na legitimacy ya kupambana na ufisadi kama wapenzi wa CHADEMA wanavyoaminishana! Mtu aliyezungukwa na Chenge, Rostam na Karamagi atapata wapi ujasiri na moral authority ya kupambana na ufisadi! Watu wazima bila aibu eti wanatamka hadharani kwamba Lowassa ni msafi kwa kuwa hajafikishwa mahakamani! Ni hoja gani za hovyo kama sio za kipumbavu kama hii?!! Ina maana Rostam Aziz nae ni msafi? Chenge nae ni msafi? Karamagi nae ni msafi? Kikwete nae ni msafi? Anna Tibaijuka nae ni msafi? Mkapa nae pamoja na kuanzisha kampuni Ikulu na kujiuzia Kiwira nae ni msafi? Huyu na yule nao ni wasafi? Ni nani miongoni mwao amewahi kufikishwa mahakamani ikiwa hoja ni kwamba hajafikishwa mahakamani?

It's very unfortunately ikiwa haya yasemwayo yatatimia basi moja kwa moja CHADEMA itakosa uhalali wa kupambana na ufisadi na kimsingi, itakuwa imewasaliti wale wote ambao waliungana na CHADEMA kwa kuamini wana nia ya dhati! Rais ni nafasi kubwa sana kwenye taifa ambalo katiba yake imetoa madaraka makubwa mno kwa rais! Hivi Lowassa ndo ameshakaa pale Magogoni, ni nani mwenye ubavu wa kumdhibiti? Mbowe?

I am afraid habari hizi zikiwa za ukweli, si tu kwamba CHADEMA itakosa moral authority ya kuusemea ufisadi bali watakuwa wamekiweka rehani chama mikononi mwa wapambe wa Lowassa waliopo CCM na wale wanaomfadhili! Na ikitokea amesimama na bado CHADEMA ikashindwa, basi huo utakuwa ndio mwanzo wa anguko la CHADEMA kwa maana kitakachobaki ni kulaumiana kwa kuamini, kama si kumkaribisha Lowassa, si ajabu wangeshinda! Lawama zitakazokuja kutokana na ukweli kwamba wapo wana-CHADEMA mahiri ambao hawatakubaliana na upuuzi huu na hivyo kuamua kuachana na chama! Na ikiwa watashinda, CHADEMA itakuwa imetekwa na wana-Lowassa... hapatakuwa na mwenye ubavu wa kumtimua rais wa nchi, rais mwenyewe mwenye kariba ya Lowassa! Tusije kushangaa tukakuta akina Mbowe wanabadilika kuwa wapangaji kama ilivyokuwa kwa akina Mabere Nyaucho Marando mbele ya Mrema!!! Na hakuna kosa kubwa kama kumlinganisha Lowassa na Dr. Slaa kwamba hata Slaa alitoka CCM na baadae akaja kuisumbua!

Dr. Slaa ingawaje alitokea CCM lakini alidumu sana madhabahuni kuliko ndani ya CCM! Huyu hakuwa na watu CCM tofauti na Lowassa ambae ameanza kuusaka uraisi kupitia CCM kwa takribani miaka 25 sasa! Watu wa Lowassa alionao CCM ni watu wenye nguvu kwenye siasa za Tanzania! Mbowe na wenzake kamwe hawatakuwa na ubavu wa kuwadhibiti watu kama hawa! Miongoni mwa wagombea wote ambao walijitokeza CCM, sidhani kama kuna mgombea ambae ungemlinganisha na Lowassa kuwa kwake ndani ya chama! Wakati kuna kila dalili Dr. Slaa alitoka CCM kv alitaka kuwahudumia wananchi wake kwa namna yoyote ile, lengo la Lowassa ni kuupata urais kwa namna yoyote ile.... hizi ni two different goals!

But lastly, CCM sio wapumbavu... wanajua wanachofanya! Si kwamba hawakufahamu madhara ya kumkata Lowassa... lazima walikuwa na Plan B! Watu wasipoangalia itakuwa ni kama samaki aliyerushiwa chambo bila kufahamu chambo ile imeficha ndoana!!

Jipigeni kisu wenyewe na kama Lowassa atasimama kwa tiketi ya urais basi waombee wasishinde urais ila tu asababishe kupata wabunge wa kutosha manake akishachukua urais, balaa lake litakuwa si dogo! Na kama watafanya uendawazimu wa NCCR wa kumpatia na uenyekiti kabisa, then nitatangulia kusema R.I.P CHADEMA!
 
El apewa Othman Masoud kuwa mgombea mwenza.
Masoud ni mwanasheria mkuu wa Zanzibar aliefukuzwa kwa kukataa katiba ya chenge.
Ni kijana msomi na makini
Timu imetimia na mechi imenogaa
 
ccm in a new suit!

Kama ukawa watamsimamisha Lowassa kuwania u-rais, akishinda itakuwa ni ccm wameshinda kwa goli la mkono. Akishindwa pia ni ccm imeshinda goli halali. Hitimisho: Upinzani utakuwa umejichimbia kaburi na kujizika.

Natamani sana kama katiba ingeruhusu mgombea binafsi. Hii ingesaidia sana vyama vya siasa kufanya maamuzi ya kidemokrasia ndani ya vyama na kuepuka ubabe na kuburuzana.
 
Tulia, umekula vya mwanaume, vumilia, upate dawa..Lumumba wapata kichaaaaa
 
ccm in a new suit!

Kama ukawa watamsimamisha Lowassa kuwania u-rais, akishinda itakuwa ni ccm wameshinda kwa goli la mkono. Akishindwa pia ni ccm imeshinda goli halali. Hitimisho: Upinzani utakuwa umejichimbia kaburi na kujizika.

Natamani sana kama katiba ingeruhusu mgombea binafsi. Hii ingesaidia sana vyama vya siasa kufanya maamuzi ya kidemokrasia ndani ya vyama na kuepuka ubabe na kuburuzana.

Lengo ni kuondoa jina "CCM" MAANA LINALETA Ukakasi kulitaja.
 
nasemaje bora lowassa fisadi nnaemjua kuliko mgeni nisiemjua..!
ZIMWI LIKUJUALO HALIKULI LIKAKWISHA
 
msitishe watu, iwe ccm au ukawa atakeishinda mambo yataenda, nani anataka fujo? badala ya kuhimizana kwamba siasa ziwepo za amani mtu anatisha watu, njoo lowasa, njoo magufuli uwanjani.....
 
Kuna watu waoga isee!!! Hivi nyie mnaojiita wapinzani huku mkiogopa Lowasa kuingia upinzani mmezaliwa wakati wa vyama vingi nini, yaani kwa akili zenu mnafikiri mnaweza kuumba mtu mpya mkamweka kuwa rais? Kwani hawa wa upinzani kina Slaa,Mbowe, Saif Hamad, Lipumba,Mtei etc wamesoma na kulelewa na upinzani? UPINZANI MAANA YAKE NI KUTOKUBALIANA NA KILE KINACHOFANYWA NA WASHIRIKA WAKO.UNAANZA KUPINGA UKIWA NDANI UNATOKA NJE UNAENDELEA KUWAPINGA WALE. NA HII INATOKANA NA MFUMO TENDAJI. Kama wewe ni mpinzani kweli wa mfumo wa ccm,piga kura yako kwa hata JIWE litakalowekwa na Ukawa ili upate mfumo tofauti na ule wa mwanzo.
 
Picha za kutengenezwa hizi hapa eeeeh?
Nyie mtanyooka tu mwaka huu.
Hivi hata huyo mlinzi wake nae alitengenezwa?
 

Attachments

  • 1438076738418.jpg
    1438076738418.jpg
    57.1 KB · Views: 286
  • 1438076754865.jpg
    1438076754865.jpg
    59.2 KB · Views: 266
Back
Top Bottom