Kwanza siamini kama ni kweli CHADEMA wanaweza kuchukua maamuzi ya hovyo kama hayo lakini ikiwa ni kweli basi ni kama nashuhudia anguko la CHADEMA siku za usoni! Na hata Lowassa akismama kama mgombea urais na akashinda, serikali yake haitakuwa na legitimacy ya kupambana na ufisadi kama wapenzi wa CHADEMA wanavyoaminishana! Mtu aliyezungukwa na Chenge, Rostam na Karamagi atapata wapi ujasiri na moral authority ya kupambana na ufisadi! Watu wazima bila aibu eti wanatamka hadharani kwamba Lowassa ni msafi kwa kuwa hajafikishwa mahakamani! Ni hoja gani za hovyo kama sio za kipumbavu kama hii?!! Ina maana Rostam Aziz nae ni msafi? Chenge nae ni msafi? Karamagi nae ni msafi? Kikwete nae ni msafi? Anna Tibaijuka nae ni msafi? Mkapa nae pamoja na kuanzisha kampuni Ikulu na kujiuzia Kiwira nae ni msafi? Huyu na yule nao ni wasafi? Ni nani miongoni mwao amewahi kufikishwa mahakamani ikiwa hoja ni kwamba hajafikishwa mahakamani?
It's very unfortunately ikiwa haya yasemwayo yatatimia basi moja kwa moja CHADEMA itakosa uhalali wa kupambana na ufisadi na kimsingi, itakuwa imewasaliti wale wote ambao waliungana na CHADEMA kwa kuamini wana nia ya dhati! Rais ni nafasi kubwa sana kwenye taifa ambalo katiba yake imetoa madaraka makubwa mno kwa rais! Hivi Lowassa ndo ameshakaa pale Magogoni, ni nani mwenye ubavu wa kumdhibiti? Mbowe?
I am afraid habari hizi zikiwa za ukweli, si tu kwamba CHADEMA itakosa moral authority ya kuusemea ufisadi bali watakuwa wamekiweka rehani chama mikononi mwa wapambe wa Lowassa waliopo CCM na wale wanaomfadhili! Na ikitokea amesimama na bado CHADEMA ikashindwa, basi huo utakuwa ndio mwanzo wa anguko la CHADEMA kwa maana kitakachobaki ni kulaumiana kwa kuamini, kama si kumkaribisha Lowassa, si ajabu wangeshinda! Lawama zitakazokuja kutokana na ukweli kwamba wapo wana-CHADEMA mahiri ambao hawatakubaliana na upuuzi huu na hivyo kuamua kuachana na chama! Na ikiwa watashinda, CHADEMA itakuwa imetekwa na wana-Lowassa... hapatakuwa na mwenye ubavu wa kumtimua rais wa nchi, rais mwenyewe mwenye kariba ya Lowassa! Tusije kushangaa tukakuta akina Mbowe wanabadilika kuwa wapangaji kama ilivyokuwa kwa akina Mabere Nyaucho Marando mbele ya Mrema!!! Na hakuna kosa kubwa kama kumlinganisha Lowassa na Dr. Slaa kwamba hata Slaa alitoka CCM na baadae akaja kuisumbua!
Dr. Slaa ingawaje alitokea CCM lakini alidumu sana madhabahuni kuliko ndani ya CCM! Huyu hakuwa na watu CCM tofauti na Lowassa ambae ameanza kuusaka uraisi kupitia CCM kwa takribani miaka 25 sasa! Watu wa Lowassa alionao CCM ni watu wenye nguvu kwenye siasa za Tanzania! Mbowe na wenzake kamwe hawatakuwa na ubavu wa kuwadhibiti watu kama hawa! Miongoni mwa wagombea wote ambao walijitokeza CCM, sidhani kama kuna mgombea ambae ungemlinganisha na Lowassa kuwa kwake ndani ya chama! Wakati kuna kila dalili Dr. Slaa alitoka CCM kv alitaka kuwahudumia wananchi wake kwa namna yoyote ile, lengo la Lowassa ni kuupata urais kwa namna yoyote ile.... hizi ni two different goals!
But lastly, CCM sio wapumbavu... wanajua wanachofanya! Si kwamba hawakufahamu madhara ya kumkata Lowassa... lazima walikuwa na Plan B! Watu wasipoangalia itakuwa ni kama samaki aliyerushiwa chambo bila kufahamu chambo ile imeficha ndoana!!
Jipigeni kisu wenyewe na kama Lowassa atasimama kwa tiketi ya urais basi waombee wasishinde urais ila tu asababishe kupata wabunge wa kutosha manake akishachukua urais, balaa lake litakuwa si dogo! Na kama watafanya uendawazimu wa NCCR wa kumpatia na uenyekiti kabisa, then nitatangulia kusema R.I.P CHADEMA!
Kwa vyovyote vile hali ya kisiasa nchini haitakuwa kama ilivyo, inabadilika. Lowassa akitoka ndani ya CCM na kwenda upinzani na kama ataendelea ku 'command' heshima na mashabiki aliokuwa nao itabadilisha kabisa mfumo iwe ameshinda urais au hakushinda. Nafikiri na natumaini kuwa kuanzia uchaguzi huu na hasa baada ya uchaguzi tutaanza rasmi mfumo wa vyama vingi - yaani mfumo wa chama dola utaondoka.
Unayoyasema yote yana ukweli na tumeyaona nchi nyingi na hasa jirani zilizopitia huko tunakokwenda; wapinzania wanaungana kwa sababu wana 'common enemy' lakini baada ya hapo akishatoka wanarudiana wao. Kinachotokea tu ambacho ni kizuri ni kwamba mabadiliko hayo hayarudi nyuma yanasonga mbele. Kwenye suala la ufisadi katika siasa zetu, wewe mwenyewe umethibitisha katika andiko lako wote uliowataja kama mafisadi wanendelea kututawala na hata huyo aliyeko sasa kwa matarajio naye unasema ni fisadi! Kwa hiyo haina tofauti iwe fisadi anatawala kupitia chama tawala cha sasa au cha upinzani wote ni mafisadi tu.