Ijue historia ya mgogoro kati ya Iran na Marekani

TRANSPONDER

JF-Expert Member
Aug 3, 2018
399
988
Hodi hodi watu wangu wa kijiweni.

Baada ya kuwa msomaji wa Makala za watu kwa muda mrefu, nimeona mimi pia nisiwe mzigo kwenu bali niwaletee moja kati ya historia za vugu vugu la vita kati ya Marekani na Iran.

Kama inavyosemakana na watu wengi kwamba Iran amejiandaa sana kukabiliana na Marekani katika uwanja wa vita.

Je ni kitu gani hasa kipo kati ya nchi hizo mbili kupelekea mvutano huo? Je ni kwanini mvutano huo unaendelea huku viongozi wakuu wa nchi hizo wakienelea kubadilika?

Basi shuka nayo hii na wewe upate madini haya niliyoyachambua kwa kina sana.

Kwanza ningependa watu wote tuwe na uelewa wa nini maana ya neno “Diplomasia”, ukifungua kamusi ya Cambridge utakuta Diplomasia ni usimamizi wa mahusiano kati ya nchi mbili au ni taaluma ya kushughulika na watu bila kuwakosea au kuwakasirisha.

Diplomasia ndio inachochea usambazaji wa taarifa, mawasiliano na kupeana ujuzi wa aina mbalimbali kati ya nchi na nchi.

Kwa hapa kwetu naweza kutoa mfano wa mtu kama Mzee Kikwete ndiye mwanadiplomasia bora kuwahi kotokea baada ya hayati Baba wa taifa.

Sio kwa kumpendelea bali ni kwa namna alivyoshughulikia matatizo ya ndani nan je ya nchi bila kumwaga damu kiholela. Kupitia diplomasia ndio tunaona vitu kama balozi za nchi nyingine katika nchi fulani.

Turudi kwenye historia yetu, wenzatu hawa wa Iran na Marekani hawajawahi kuwa na uhusiano wa kidiplomasia tangu mwaka 1980. Hii ni kufuatia unyama uliofanywa katika ubalozi wa Marekani miaka hiyo (Nitakuja na hicho kisa mwisho wa historia hii).

Kuvunjwa kwa mahusiano kati ya nchi moja na nyingine huandamana na kufungwa ghafla kwa ofisi za ubalozi katika nchi husika.

Mfano Tanzania tutakapovunja uhusiano na Kenya tutafunga mipaka yote kati yetu na balozi wao tutamtimua, na wao watafanya hivyo hivyo kama si kumteka, basi hilo likitokea kama matokeo ya vita kuna mateka watachukuliwa na baadhi ya mali zitakuwa zimetekwa, lazima kuwe na namna ya nchi hizi mbili kuwa na uwakilishi wa namna nyingine kufuatilia watu na mali zao katika nchi hizo.

Hapo ndipo wataalam wakaja na neno “Protecting power” , Protecting power ni nchi inayowakilisha nchi nyingine katika nchi ambayo haina uhusiano nayo wa kidiplomasia.

Kwa mfano huo wa Tanzania na Kenya basi tungesema Uganda atuwakilishe nchini Kenya basi Uganda angekuwa ni protecting power yetu nchini Kenya.

Vivyo hivyo kwa Marekani na Iran, Pakistan alitumika kama protecting power ya Iran nchini Marekani na Uswisi kama kawaida yake akatumika kama protecting power ya Marekani nchini Iran.

Nimesema Uswisi kama kawaida yake sababu ndiye aliyekuwa protecting power ya Marekani nchini Cuba tangu 1961 hadi 2015 Obama alipofanikiwa kutumia uwezo wake wa kidiplomasia kurudisha uhusiano kamili wan chi hizo mbili uliokufa kipindi Field marshal Fidel Castro anaingia madarakani nchini Cuba.

Kiongozi mkongwe zaidi Mashariki ya kati ambaye ni kiongozi mkuu wa Iran Ali Hossein Khamenei ndiye aliyekataza mawasiliano ya moja kwa moja kati ya Iran na Marekani mwaka 2018 na kuturudisha katika matumizi kamili ya protecting power.

Uhusiano wa nchi hizi mbili ulianza katikati ya karne ya 19 hadi mwishoni mwa karne ya 19, Kipindi ambacho Iran ilikuwa ikiitwa Persia.

Kipindi hicho nchi za uingereza na urusi zilikuwa zikitamani sana kuitawala Iran hivyo Iran ilitawaliwa na hofu iliyoipelekea kuiamini sana Marekani ambayo ilikuwa haina maono ya kutawala nchi nyingine.

Uaminifu huo ulipelekea Shahs (Jina lililotumika kuwataja wafalme na viongozi wakubwa wa Persia enzi hizo) kuwateua wamarekani Arthur Millspaugh na Morgan Shuster kuwa Majenerali wa kuheshimiwa nchini humo.

Wakati wa vita ya pili ya dunia Iran ilivamiwa na Uingereza pamoja na Muungano wa kisovieti ambao walikuwa na ushirikiano mkubwa na Marekani katika vita.

Japo hilo lilitokea uhusiano wan chi hizi mbili uliendelea bila tatizo lolote baada ya vita mpaka pale serikali ya Mohammad Mosaddegh ilipopinduliwa kijeshi katika mapinduzi yaliyoongozwa na CIA wakisaidiwa na MI6.

Baada ya mapinduzi hayo walimweka kiongozi wao waliomtaka Shah Mohammad Reza Pahlavi na uhusiano wao ukaimarika mara dufu hadi wairan walivyoamka kutoka usingizini na kuja na kile kilichoitwa Mapinduzi ya Iran mwaka 1979 kumuweka mtaalam asiyewachekea Wamarekani The grand Ayatollah Ruhollah Khomeini.

Kwa jina lingine mapinduzi ya Iran yanajulikana kama mapinduzi ya dola la kiislamu. Hapo tunaweza kusema waliamka na kukimbia bila nguo kwa filimbi za Wamarekani ambao bado walikuwa wakiwachezea mchezo wa kuwaweka kwenye sitofahamu iliyosababisha mgogoro wa mafuta mwaka 1979 uliosindikizwa na vita kati ya Iraq na Iran.

Utashangaa kwanini Mmarekani anamchezesha Iran ngoma hiyo, jibu ni jepesi sana kwani utamu wa mafuta ndio ulituulia ndugu zetu zaidi ya mia moja pale Morogoro.

Wamarekani walibaki kwenye mshangao kwani hawakutegemea kama vuguvugu lilikuwa likiendelea Iran lingifikia hatua ya kumtoa madarakani kibaraka wao.

Kwa taarifa ilitumwa na CIA ikulu miezi sita kabla ya mpinduzi ya Iran ilisema kwamba Iran haipo katika harakati za mapinduzi wala vuguvugu litakalopelekea mapinduzi nchini humo.

Kiongozi mpya Khomeini, ambaye wamarekani walipendelea kumuita “Great Satan” alitoa magugu yote yaliyoachwa na shah kwa kuanza na Prime minister na nafasi yake kuwekwa mwanasiasa wa kawaida Mehdi Bazargan ambaye pia alikuwa na mahaba kwa Wamarekani.

Hadi wakati huo Wamarekani walitegemea uhusiano wao na Iran utaendelea kuwa wa kawaida. Wanamapinduzi wa Iran walitaka kumuua kiongozi waliomtoa madarakani.

Kama kawaida yao Wamarekani wakishatafuna kama mua hawatokuhitaji tena Basi serikali ya Jimmy Carter ikakataa kumpa msaada wowote kiongozi aliyepinduliwa ikiwamo kumrudisha madarakani.

Hata pale kiongozi huyo alipougua saratani na kutaka kwenda kutibiwa marekani ubalozi wa marekani mjini Tehran ulikataa kumpa visa ili kukuza uhusiano wao na serikali mpya kuwawezesha kufaidi utamu wa Mafuta.

Lawama ziwaendee wanasiasa wakongwe wa Marekani Kissinger na Rockeffeller waliofanikiwa kumshawishi J Carter kumruhusu Shah akatibiwe Marekani.

Hilo ndilo likawa kosa kubwa kwa Wamarekani kwani wana mapinduzi wa Iran walipata uthibitisho kwamba Kiongozi huyo anapanga njama za dhidi ya mapinduzi yao, hivyo wakamtaja kama kibaraka wa marekani hali iliyopelekea wana mapinduzi hao kupeleka dhoruba ubalozi wa Marekani nchini Iran.

Tarehe 4 Mwezi wa kumi na moja 1979 wanamapinduzi hao waliteka ubalozi wa Marekani jijini Tehran na kuwateka wanadiplomasia wa Mmarekani 52 kwa siku 444.

Waziri mkuu Bazargan alipinga swala hilo la kuchukua mateka ubalozi wa Marekani hali iliyompelekea yeye mwenyewe kujiuzulu baada ya tukio hilo.

Kitendo cha waandamanaji wa Iran kuwateka wanadiplomasia wa marekani kilikuwa kinapingana na sharia ya kimataifa inayokataza kukamata wanadiplomasia wa nchi nyingine na inazuia askari wa nchi mwenyeji kuingia katika eneo la ubalozi wa nchi ngeni.

Swali la kujiuliza ni “Je Marekani alikubali tu watu wake washikiliwe nchini Iran kwa siku 444 bila kuwaokoa?” Jibu ni hapana.

Hapa ndipo Marekani alipata aibu ya karne pale alipojaribu kuwakomboa wanadiplomasia wake.

Hii wenyewe waliita Operation Eagle Claw.
Ngoja kidogo niwadorishie operesheni hiyo kwa uchache, tiririka nayo!

SEHEMU YA PILI inaendelea post inayofuata
 
SEHEMU YA PILI

Operation Eagle Claw kwa jina lingine iliitwa operation Tabas nchini Iran, Ni operesheni iliyoamriwa na rais wa marekani Jimmy Carter kwa lengo kuu la kuwaokoa wanadiplomasia wake 52 walioshikiliwa nchini Iran. Operesheni hii ilifeli vibaya sana na kupelekea rais Jimmy Carter kutopata nafasi nyingine ya kurudi ikulu katika duru ya pili ya uchaguzi. Kwani katika operesheni hii kikundi cha wanajeshi wa Delta force walikutana na vikwazo vingi vilivyopekea kufeli kwa jaribio hilo la uokozi. Helikopta nane za jeshi la marekani zilitumwa lakini tano tu ndio zilifanikiwa kufika zikiwa na uwezo wa kufanya kazi. Moja ya helikopta hizo ilikwama katika dhoruba ya mchanga , nyingine upanga wake ulikutwa ukiwa na alama za kutaka kumeguka na ya tatu iliyosalia ilikuwa na shida katika mfumo wake wa oil.

Hapa kuna jambo moja lazima tujifunze kutoka kwa wenzetu, katika kupanga mission zao huwa wanakuwa na kitu kinachoitwa “possibity sets” yani tunafanya nini kama ikitokea hivi na nini kama ikitokea vile , hata kwenye operesheni hii ya eagle Claw walifanya hivyo na walikubaliana kwamba endapo helikopta chini ya sita kati ya zile nane zitafika Iran zikiwa katika hali nzuri (ikimaanisha kama zitaharibika helikopta Zaidi ya mbili njiani) basi mission hio itafutwa na kukubali kuwa imeshindikina, ingawa katika mahesabu ya kawaida helikopta nne tu zingetosha kukamilisha ile mission lakini wamarekani sio kama sisi, wanajipenda mno na hawawezi kuweka rehani maisha ya wanajeshi wao kwa uzembe. Hivyo kamanda aliyekuwa akiongoza operesheni hiyo akamshawishi rais wa marekani afute hiyo mission naye Jimmy Carter akafuta. Wakati wanajiandaa kugeuza helikopta moja wapo ikapata ajali na mbaya zaidi ilikuwa imebeba wanajeshi na mafuta ya ndege ikalipuka na kuua wanajeshi nane waliokuwa kwenye helikopta hiyo. Wamarekani walichukizwa sana na matokeo hayo na kuamua kumnyima Carter ungwe ya pili ya urais.

Tofauti na nchi fulani hapa jirani, ajali ya kizembe ilitokea miaka ya 96 wakaendelea kucheka na rais wao na kumpa nafasi ya pili ya urais hali iliyozidi kuwadidimiza kiuchumi na kuwaongezea deni la taifa. Wamarekani hawana mahaba na rais , wao wanamahaba na maendeleo pamoja na usalama wao.

Basi baaa ya operation Eagle claw kufeli kiongozi mpya wa Iran Ayatollah Ruhollah Khomein akaanzisha propaganda kwamba operesheni hiyo ya wamarekani ilifeli sababu ilikuwa ni mpango wa Mungu katika kuilinda Iranna serikali yake mpya. Baada ya propaganda hiyo wairan wakaamua kumuumiza kichwa Zaidi mmarekani kwa kuwatawanya wale mateka 52 katika sehemu mbali mbali za Iran ili kuzuia kabisa jaribio lingine la kuja kuwakomboa.

Rais Jimmy Carter na timu yake hawakupata usingizi kwani waliendelea kuplan majaribio mbali mbali ya kuokoa lakini walishindwa mahesabu na kuyafuta kabla ya utekelezaji , Yaani hii ni kama vile Mange Kimambi alivyokuwa anawaza yeye na kichwa chake kuhusu maandamano na kuishia maneno matupu, Carter alifanya hivyo ili asimalize urais wake kwa aibu ya kushindwa kuwakomboa watu wake.

Iran walimwacha aaibike kwani dakika chache baada ya kuachia ikulu January 20 1981 mateka wote wa marekani nchini Iran wakaachiwa huru na kumaliza sitofahamu hiyo ya siku 444 kufungia wamarekani nchini Iran.

Wale viongozi shupavu hawakosekani kwa Secretary of state Cyrus R Vance ilijua kabisa operation eagle claw itafeli hivyo alijiuzulu kabla ya operation lakini CIA walizuia taarifa hiyo isiende public hadi pale walipokuwa tayari kutangazia umma.

Moja ya kauli iliyotumika na Ayatollah kumkebehi Carter ni hii alipokuwa akihutubia watu wake “nani ameharibu helikopta za Carter? Ni sisi? Hapana ni mchanga umefanya, ni wakala wa Mwenyezi Mungu, Upepo ni wa Mungu na ule mchanga ni wakala wa Mwenyezi Mungu. Kama wanaweza wajaribu tena.”

Kufuatia swala hilo marekani na Iran walifunguliana kesi katika mahakama ya The Hague huko uholanzi , Mgogoro huo ndio uliozaa mpasuko kati ya nchi hizo mbila hadi hii leo, hebu tuendelee na mgogoro huo Kuanzia 1981 baada ya utawala wa Carter hadi leo hii Trump akiwa madarakani.

…..usikae mbali na simu yako leo natoa uvivu wa kuwa msomaji siku zote.

SEHEMU YA TATU inaendelea post inayofuata
 
SEHEMU YA TATU
Baada ya usingizi wa masaa matano ndipo niliposikia kokolikoooo sauti laini ya jogoo la mjini iliyoniamsha kabla ya muda niliopanga , ikabidi nipitie comments za wadau hapa kijiweni , nikavutiwa na comment ya mchangiaji mmoja aiyetaka kufananisha Operation Eagle Claw na movie ya delta Force, nashukuru sana kwa comment zenu maana zinanipa moyo wa kuandika , wenyewe tunasema raha ya kuandika upate msomaji , na inakupa moyo Zaidi pale msomaji anapotoa mawazo yake au anauliza swali, hapo ndipo unapata mwanya wa kufunguka Zaidi yale madini yaliyojificha Zaidi ndani ya ubongo wa mwandishi.

Basi kuongeza ladha ya uzi najibia maneno mawili juu ya movie ya delta force ambayo Chuck Norris alikuwa starling wa hiyo movie. Nikweli kwenye delta force tunaona mmarekani akipigina na mwarabu kama ilivyo katika movie nyingi za kivita, movie hii ilizinduliwa tarehe February 14, 1986 na kisa kilichomfanya muongoza filamu mahiri wa enzi hizo Menahem Golan kuja na movie hiyo ni tukio la utekaji ndege ya Trans World Airlines Flight 847 (TWA Flight 847) tarehe 14 June 1985 lilifanywa na wanaislamu waliotaka waislamu (Shi’ite muslims) 700 walioshikiliwa huko Israel kuachiwa huru, Shi’ite inaweza kuwa jina geni kwako lakini ni kiinereza tu la neno Shia , tawi mojawapo katika Dini ya kiislamu ukiacha lile la Sunni.

Watekaji hao hawakuwahi kujulikana ni akina nani mpaka hapo baadae magharibi wakawatupia lawama kikundi cha Hezbollah ambao nao walikataa kuhusika , tuhuma hizo zilielekezwa kwa kikundi cha Hezbollah baada ya kukamatwa kwa Muhamed Ali Hamad ambaye alikuwa mmoja wa watekaji na mfuasi mkubwa wa kikundi cha Hizbollah. Watu wanaakili Jamani , wakati sisi tunamlamba miguu marekani hawa akina Muhammed walifanikiwa kuteka ndege na kuua mwanajeshi wa majini wa marekani na baadhi ya matakwa yao kutimizwa ndipo kuwaachia huru mateka mwaka 1985, Mmarekani anaangalia tu. Watu watukutu wapo , msimcheke congo na Somalia kwa kuendelea kukaliwa na magaidi , ni vile tu hawajapata sababu ya kuja kutuadabisha, japo naamini Nchi yetu ina usalama bora Zaidi barani afrika tunaweza kuwamaliza hata kabla hawajapata wazo hilo.

Tusihamishe akili sana , turudi kwenye historia yetu wa marekani , najua hadi sasa kuna ambao walifikiri Iran waliamua tu kuwaachia mateka hao wa marekani bila makubaliano yoyote, lahasha hawa nao walikuwa wanajitambua , walitupa heshima na sisi kwani mgogoro wao ulitatuliwa barani afrika katika nchi ya Algeria January 19 1981, hizo zote ni jitahada za kutotua mzigo huo kwa serikali mpya inayoingia madarakani. Jina la mkutano huo lilikuwa “Algeria Declaration” na lengo kuu lilikuwa kusuluhisha kile kilichoitwa “Iran hostage crisis” huku dalali wa dili hilo akiwa ni serikali ya Algeria .

Mateka wote 52 wa marekani waliachiwa huru na kuruhusiwa kurejea nchini marekani kutokana na makubaliano yafuatayo.
Marekani hatajihusisha tena kisiasa au kijeshi katika maswala yoyote ya ndani nchini Iran
Marekani itazifungulia assets zote za iran na kuwaondolea Iran vikwazo vyote vya kibiashara.
Mataifa yote yatafuta madai yao waliyofungua katika mahakama ya The Hague Uholanzi
Madeni yote ya Iran kwa taasisi za marekani yatalipwa.

Maamuzi katika mahakama ya marekani Juu ya kusafirisha mali za kiongozi aliyepinduliwa hayatahusishwa na “soverign Immunity principle” na yatatekelezwa. (nitaielezea hii principle na vituko vyake)
Baada ya kisanga hicho tunaweza kusema Jimmy Carter ndiye msababishi wa fungwa kwa mahusiano ya kidiplomasia kati ya Iran na marekani kuanzia tarehe 21 mwezi wan ne mwaka 1980 hadi leo hii.

January 20, 1980 kama ilivyo tamaduni ya wamarekani ndio tarehe yao kuapisha marais kila baada ya miaka minne, Hii ndio siku Jimmy Carter ameachia rasmi ofisi na kumkabidhi kijiti Rais Ronald Regan kwa aibu ya kuchezewa mchezo wa kijinga na Iran kwa siku 444, Ronald alikuwa na deni kubwa kwa wamerakani kwani ile chuki dhidi ya Iran bado ilikuwepo , hivyo lazima aionyeshe dunia kwanini wamarekani wamemwani yeye na kumfanya Jimmy Carter kuwa rais wa awamu moja nchini humo.

Bendera ya marekani haitumiki kizembe kwenye vita, maana wana vita nyingi za kupigana ,miezi nane tu baada ya kongamano la Algeria , Carter kuachia urais na Reagan kupokea kijiti , ikaanznishwa balaa nyingine nchini Iran, mara hii marekani akiwa anaichezea kwa “remote control”

Huo ndio ubabe wa kiintelijensia , kutumia remote kama unacheza game ya FIFA kwenye PC yako , unamchagua Man U kama timu yako na upande wa computer unampa Arsenal kumaliza hasira za Juzi hapa arsenal kumfunga Man U, yaani kama uliangalia game kibanda umiza ukasikia matusi na kuchekwa na watoto wa sekondari unaweza jikuta umeweka beginner mode na ukawapiga arsenal kama 20 hivi. Ndivyo Ronald Regan alivyopanga kufanya, baada ya marekani kupigiwa kibanda umiza kule Iran na Algeria akaamua kucheza game akamchagua Iraq upande wake na kwenda kwenda kukipiga na Iran, hii ndio raha ya game kuche FIFA, embu tujionee ilikuwaje kuwaje mmarekani aliwachezesha ngoma hiyo kwa miaka nane Iran , Je hapo ndio tutapata sababu ya baba yake Christian Ronaldo kumpenda Reagan hadi kumpa mwanae jina na Ronaldo ?

Ngoja tunawe uso , tufanye mazoezi na tukalijenge taifa, nikirudi naumaliza utawala wa Reagan katika uhusiano wake na Iran , Usikae mbali na usiache kudondosha comment………..
SEHEMU YA NNE
POST #52



Se
Screenshot_20200105-053721_WhatsApp~2.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sisi tunatambua Ayatollah na Kikundi chake ndo chanzo cha machafuko hapo mashariki ya kati, Shia Theocracy imeishiwa nguvu......Ayatollah asione aibu ni muda sahihi wa kukabidhi nchi kwa wananchi kwasasa... SHIA THEOCRACY HAS FAILED
 
Back
Top Bottom