Ijue historia ya jina Makambako

steve_shemej

JF-Expert Member
Nov 26, 2015
1,092
1,433
Makambako ni sehemu maarufu Sana hapa nchini kwakuwa ipo katika njia panda ya kwenda Mbeya, Songea na Iringa

Makambako kwa Sasa inapatikana katika mkoa wa Njombe

HISTORIA YAKE

Kipindi cha ngoni migration wangoni baada ya kuikalia Songea walitamani wajitanue mpaka panapoitwa Iringa kwa Sasa lakini mpango wao ulipata changamoto kila walipofika sehemu inayo itwa Makambako hivi Sasa kipindi hicho palikuwa na jina jingine

Wangoni walipofika eneo hilo walikuwa wanakabiliwa na Vita kubwa kutoka kwa majeshi ya chifu Mkwawa ambapo walipigana Vita mara mbili bila ya kupatikana mshindi mngoni alirudi nyumbani na Mkwawa alirudi kwake mara ya tatu mngoni alipanga Tena shambulio dhidi ya vikosi vya Mkwawa

Vita hii ya tatu Mkwawa alishindwa Vita alipoteza 70% ya Askari wake wote baada ya Mambo kuwa MAGUMU Mkwawa alituma wazee kwenda Songea kwa chifu Songea kuomba Vita isitishwe na wasipigane Tena


Wangoni walikubali na wakaombana wawe watani tangu hapo mhehe na mngoni ni watani


Sasa pale walipokuwa wanapigania wakaamua wapape jina mngoni akaamua paitwe MAKAMBAKU kwa kingoni KAMBAKU ni mtu shupavu mwenye nguvu MAKAMBAKU ni uwingi

Watu walikuwa hawaezi kuita MAKAMBAKU wakawa wanapaita Makambako Kama inavyoitwa Sasa hivi


Hiyo ndyo historia fupi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante kwa historia.. Je ni kweli hizi vita za wangoni na wahehe ziliwahi kupelekea wahehe kutaka kuhamisha mlima fulani waliokuwa wanautumia kwa ibada? Nasikia lengo ilikuwa ni wauchimbe kwa chini waubebe kama mti na mizizi yake.. Wahehe akili zao wanazijua wenyewe 😀😆😀
 
Asante kwa historia.. Je ni kweli hizi vita za wangoni na wahehe ziliwahi kupelekea wahehe kutaka kuhamisha mlima fulani waliokuwa wanautumia kwa ibada? Nasikia lengo ilikuwa ni wauchimbe kwa chini waubebe kama mti na mizizi yake.. Wahehe akili zao wanazijua wenyewe
Vita ya tatu wahehe walifumuliwa saaana wengi wao walikufa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Si kweli, ni uongo kabisa, wahehe hawajawahi kupigwa na wangoni kamwe.....hakuna kabila lililowahi kumpiga mhehe.....hiyo sehemu iliitwa Makambako ikiwa na maana sehemu ambayo mahafari wawili walikutana....yaani ng'ombe dume zilipokutana.....kwa kihehe makambako manaake mafahari
 
Wewe umeanza kuleta ukabila wako unaonekana ni muhehe alafu hujui history haya maelezo yametolewa na mtoa maelezo wa makumbusho ya kalenga hivi unajua hata kwanini wahehe waliitwa wahehe? Acha kubisha usichokijua
Si kweli, ni uongo kabisa, wahehe hawajawahi kupigwa na wangoni kamwe.....hakuna kabila lililowahi kumpiga mhehe.....hiyo sehemu iliitwa Makambako ikiwa na maana sehemu ambayo mahafari wawili walikutana....yaani ng'ombe dume zilipokutana.....kwa kihehe makambako manaake mafahari

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom