Ijapokuwa siombei tena ...

Ijapokuwa siombei tena ...

Egwugu

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2011
Posts
17,558
Reaction score
8,554
Inaeleweka wazi kwamba watanzania tu waoga na wazito sana kureact katika mambo mengi, ijapokuwa hari imekuwa tofauti kidogo katika hili la pesa ya wahanga wa tetemeko. Limewapa mtihani mgumu kweli kweli, na naweza kusema limewajeruhi sana.

Yawezekana ni kipimo cha madhara ya tetemeko lenyewe, sijuhi. Yawezekana ni aina ya maisha wanayoishi waathirika baada ya janga lile, sielewi. Yawezekana ni maumivu baada ya pesa walizozichanga kwa ajiri ya ndugu zao kusikia zimepigwa STOP na Ikulu zisiende tena kusaidia walengwa, bado sifahamu vizuri lakini kila mja ana lake lililomsumbua katika hili, kusema kweli watanzania na hata wasio watanzania wanalaani na kuchukia sana.

Naomba nimalizie kwa swali moja tu.
Hivi ikitokea Kagera ikarudiwa na tetemeko tena hata kesho tu japo siombei, ama likatokea janga kubwa la hivi kokote kwingineko serikali itarudi kwa wananchi kuomba wasadie? na itaanzaje kulisema hili kwa watanzania?
 
Naomba litokee Magogoni..........
 
Mimi nitasaidia waathirika moja kwa moja bila kupitia serikalini kama sintokuwa muathirika
 
kama tulivyokuwa tunasema miongoni mwa sifa za kuwa kiongozi wa ccm ni kutokuwa na haibu mbele za watu
 
Nani kakwambia Wanakagera wanaogopa majanga, nikukumbushe kidogo tu:
  • Kisonono Kali
  • Idd Amin
  • Slimu- siku hizi inaitwa HIV/AIDS
  • Elnino
  • Mnyauko wa migomba, mibuni, viazi
  • Tetemeko la ardhi..
 
Nani kakwambia Wanakagera wanaogopa majanga, nikukumbushe kidogo tu:
  • Kisonono Kali
  • Idd Amin
  • Slimu- siku hizi inaitwa HIV/AIDS
  • Elnino
  • Mnyauko wa migomba, mibuni, viazi
  • Tetemeko la ardhi..
Mv. BUKOBA R.I.P...
 
Back
Top Bottom