IGP Mangu na Kamanda Sirro wajiuzulu sasa!

Mzalendo2015

JF-Expert Member
Aug 14, 2012
6,697
9,048
Wana JF,
Kwa hali ya kisiasa,kiulinzi na kiusalama inayoendelea kwa sasa, viongozi waandamizi wa Jeshi la Polisi kwa maana ya IGP Ernest Mangu na Wasaidizi wake Kamishina Simon Ciro na wengine wanapaswa kujiuzulu!
Nasema hivi kwasababu kiukweli kabisa wameshindwa kusimamia majukumu yao.

Kitendo cha Mkuu wa wa Mkoa wa Dar Bwana Paulo Makonda kuanza kuingilia kazi za Kipolisi kiasi cha yeye Makonda kuonekana ndiye anayepanga mbinu na mikakati ya kupambana na uhalifu ikiwemo madawa ya kulevya kumelidhslilisha Jeshi hilo!

RC Makonda alianza kama utani kuwa anawajua wavutaji wa Shisha, Ugoro na Bangi na akaenda mbali zaidi kwa kuwatuhumu Jedhi la Polisi akiwemo Kamanda Ciro kuwa anawatetea watu hao kupokea dau la milioni 5 tano kutoka kila gwiji wa Shisha!

Lakini mbaya zaidi na kali kuliko ni hii ya juzi kuhsu madawa ya kulevya baada ya Makonda kuwatuhumu tena Polisi kuwa wahusika WAKUU WAKIWEMO POLISI 12!! Baada ya tamko hilo tulikna jinsi Mangu, Ciro na Polisi alivyohaha kujisafisha kwa kuwaksmata wenzao 12 harakaharaka!

Kwa kiongozi makini idara yako kutuhumiwa kuhusika na makosa makubwa ya jinai kama hili la Madawa ni aibu kubwa sana! Je, IGP na Kamanda wake wa Kanda Maalumu walikuwa wapi wakti vijana wao(askari)walipokuwa wakifanya haya madudu?
Kama Polisi wenyewe wanajihusisha na biashara hii au kuvuta tutegemee nini hapo?Jibu ni HAKUTAKUWA NA UFANISI WOWOTE!!!!!
Tunaomba JPM atengue uteuzi wa IGP Mangu na Kamanda Ciro maana tayari wamepoteza sifa za kuongoja Jesji la Polisi! Lakini pia JPM atengue uteuzi wa RC Makonda ampangie kazi nyingine kwa kutaka kuvuruga amani ya nchi kwa kuingilia mihimili isiyo muhusu. Nashauri Makonda APELEKWE CCP MOSHI AKAJIFUNZE UPOLISI KAZI INAYO ONEKANA KUMFAA NA SIYO UKUU WA MKOA!! Makonda kwa sasa ameanza kujifanya mungu mtu kwa kukashfu Jeshi la Polisi na Bunge la JMT lakini pia kuidhalilisha Ofisi ya Rais kwa kumhusisha Rais na ukiukwaji mkubwa wa Sheria na Katiba ya nchi! Rais ajue kuwa tayari Wabunge wote CCM na UKAWA wameungana Bungeni kutaka Makonda aitwe kujieleza mbele ya Kamati ya Sheria,Haki na Kinga!
Hii tayari ni kutangaza VITA KATI YA BJNGE NA SERIKALI na hii si hali nzuri kiutawala! Kama Rais atadndelea kumkingia kifua Makonda basi ajue anajiangamiza mwenyewe, CCM na Serikali yake!

Wasalaam.
 
Sirro alikuwa blackmaiked na Makonda, kwa kuwa makonda alikuwa ana mwambia mara hawezi kazi, mara Sirro hawez kamata watu kwa kuwa yeye mwenyewe anahusika na madawa. Ki ukweli mchizi alikuwa hana jinsi na yeye anataka wanae wale, so hawezi jiuzulu ila as long as Madere yupo ata endelea kumtumia kwa kumtisha hivo hivo.
Police wana fanya vitu so unprofessional, yet wanajua ili wamridhishe makonda na baba ake wanapaswa wafanye hivo
 
Mkuu wajiuzuru na familia zao zitakula nini? Ngoja wakubaliane tu na hali halisi ilivyo
 
Huyu Kamanda Sirro sijajua lakini kuna siri kubwa sana kati yake Makonda kuhusu hili sakata la madawa ya kulevya.
 
Njaa ni mbaya sana lakini woga ni mbaya zaidi. Hawa wateule sasa hivi wanafanya kazi kwa woga. Tena nafikiri wanadhani kuwa Makonda yuko karibu sana na mzee na labda wanafikiri ni mshauri wa karibu wa mzee, tena yawezekana wanafikiri kuwa naweza kuwachongea kwa mzee. Kwa hiyo usishangae kuona hata IGP anamwogopa makonda kwa madhanio tu. Woga ni zaidi ya njaa. Woga ni dhambi kubwa dhidi ya nafsi na Mungu.

Hawa hawawezi kujiuzulu sababu ya njaa na woga!
 
Wewe ukitaka kupima ubora wa igp linganisha matukio ya chaguzi kuu tangu kuanza mfumo wa vyama vingi.

Na washawasha!
 
Hivi kwa nini Magu asimchague makonda kuwa igp....mana anafiti nafasi yake...
 
kituko ni siku moja nipo kwenye mkutano wa RC Makonda kikazi....Alimpigia Simu Rais katikati ya Mkutano na wananch na kumweka Rais Loudspeaker ....kitendo hicho kilishangaza wengi binafsi nilikiona nikama amemkosea adapu Rais. Maana Rais hakujuwa kama amewekwa Loudspeaker ...je Rais angeongea mambo mengine nyeti ya kiserekali ingekuwaje?..
 
Tanzania hata uwe kichaa huwezi kukubali ujiuzuru labda uwe na roho wa MUNGU ndani yako
 
kituko ni siku moja nipo kwenye mkutano wa RC Makonda kikazi....Alimpigia Simu Rais katikati ya Mkutano na wananch na kumweka Rais Loudspeaker ....kitendo hicho kilishangaza wengi binafsi nilikiona nikama amemkosea adapu Rais. Maana Rais hakujuwa kama amewekwa Loudspeaker ...je Rais angeongea mambo mengine nyeti ya kiserekali ingekuwaje?..

Kama ulisikiliza speech ya Gwajima kamaliza yote kuhusu Makonda. Huyu anasumbulia na ushamba wa Kisukuma maana alikuwa hajawahi kushika madaraka makubwa!
Makonda bado hajakomaa kuongoza watu na ana wivu wa kike uliopitiliza!!!!
 
Hapo ulipoandika milioni tano sahihisha,ilikuwa wauzaji wa shisha watano walimfuata na kumshawishi mkuu wa mkoa wawe wanampa milioni kumi kila mmoja kwa kila mwezi kwahiyo jumla ilikuwa iwe milioni 50 kila mwezi.
 
Back
Top Bottom