IGP afunguka kwa wanaochezea amani

IGP afunguka kwa wanaochezea amani

KATI 2

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2012
Posts
214
Reaction score
21
Mkuu wa jeshi la polisi, IGP Said Mwema amesisitiza kuwa jeshi la polisi halitaendelea kuwafumbia macho watu wanaovuruga amani ikiwa ni pamoja na kuchoma nyumba za kuabudia na kuuana kwa kisingizio cha kidini
 
Asubiri muda wake astaafu!hata vijana wake wamemchoka.:rockon:
 
IGP na yeye amekuwa Nape, anaongea ongea tu. Tunataka aanzie na waliomuua Mwangosi. Hana issue kabisaa. Ni boya
 
Mkuu wa jeshi la polisi, IGP Said Mwema amesisitiza kuwa jeshi la polisi halitaendelea kuwafumbia macho watu wanaovuruga amani ikiwa ni pamoja na kuchoma nyumba za kuabudia na kuuana kwa kisingizio cha kidini

.....

Eboo...hivi kumbe jeshi la polisi lilikuwa linawafumbia macho!
 
Mkuu wa jeshi la polisi, IGP Said Mwema amesisitiza kuwa jeshi la polisi halitaendelea kuwafumbia macho watu wanaovuruga amani ikiwa ni pamoja na kuchoma nyumba za kuabudia na kuuana kwa kisingizio cha kidini

......

Sasa kwanini walikuwa wanafumba macho muda wote huu? walidhani wakifumba macho ndio havitokei?
 
Mkuu wa jeshi la polisi, IGP Said Mwema amesisitiza kuwa jeshi la polisi halitaendelea kuwafumbia macho watu wanaovuruga amani ikiwa ni pamoja na kuchoma nyumba za kuabudia na kuuana kwa kisingizio cha kidini

......

Halitaendelea kuwafumbia macho? Kwa hiyo lilikuwa linawafumbia macho mwanzoni kwa kuwa walikuwa wanatekeleza mambo yao? Angoje FBI wamfundishe kazi.
 
[h=2]Mtwara, polisi waua raia kwa risasi akidai malipo ya korosho, OCD apata kipigo[/h]
Leo saa sita mchana, wananchi wa kijijina kata ya mtimbwilimbwi, tarafa ya nnyamba, mtwara vijijini, walifunga barabara kutoka mtwara kwenda tandahimba na newala, wakiwa wanaishinikiza serikali iharakishe na kusimamia utaratibu wa upatikanaji wa malipo ya pili ya zao la korosho.

Mkuu wa wilaya alifika kuongea na wananchi, akawa hajatoa majibu yeyote ya kuwaridhisha wananchi wananchi wakamzomea, baada ya hapo mkuu wa wilaya aliita polisi kuja kuwatawanya wananchi hao kwa mabomu, lakini katika mambomu hayo mwananchi mmoja anayejulikana kwa jina la said,mfanyabiashara amepigwa na risasi ya moto na kufariki hapo hapo.

Baada ya kufariki wananchi walitafuta gari wakapakia maiti, walipokuwa kwenye gari, ocd akiwa na nguo za kiraia alianza kupongeza jeshi la polisi, na kuwabeza wananchi kuwa wanapenda fujo, wananchi kwa kuwa hawamfahamu walimpatia kipigo cha kutosha hadi akaokolewa na wanaomfahamu. Kamanda wa polisi mkoa wa mtwara, amethibitisha kuwepo kwa fujo katika eneo hilo ila hajui kama kuna mtu amepigwa na askari na kufariki kwa kuwa aliowatuma bado hawajapeleka taarifa ofisini kwake.

- chanzo- ghula.​
 
Hapo anajisumbua tu mbona maana ni vigumu kuua mto katikati ya mkondo..kitakachofanyika ni kusababisha maji yatafute mkondo mwengine.

Angetafuta chanzo cha maji aone kama ataweza kupambana nayo kukikausha kisiendelee kuto a maji kuelekea kwenye mkondo.

Chanzo kikubwa ni wanasiasa wanaohubiri chama fulani ni cha dini fulani chaongozwa na padre au Shehe mbaka wananchi wanapata hisa za udini plus ukabila..azue kama ataweza basi fujo nazo zitaisha.
 
IGP si walewale tu! Hana jipya zaidi ya kadi ya CCM na kufumbia macho maovu ya jeshi lake! Kumbe kweli anajua kilichokua kinafanyika ila alikua anafumba macho?

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
si kwamba wanawafumbia macho, Polisi mara kwa mara wamekuwa wakitoa elimu kwa wananchi kuhusiana na utii wa sheria bila shuruti na polisi jamii, ulinzi shirikishi ili wananchi wakielewa vizuri umuhimu wake basi wataweza kusaidiana na polisi katika wakuwabaini na kuwafichuwa wahalifu.
 
si kwamba wanawafumbia macho, Polisi mara kwa mara wamekuwa wakitoa elimu kwa wananchi kuhusiana na utii wa sheria bila shuruti na polisi jamii, ulinzi shirikishi ili wananchi wakielewa vizuri umuhimu wake basi wataweza kusaidiana na polisi katika wakuwabaini na kuwafichuwa wahalifu.

......

kwa hiyo hata raia wanaowaua nao huwa hawana utiii,mtuhumiwa kufia mikonon mwao ni UTII BILA SHURUTI?
 
Wanawafumbia macho hata polisi wao wanaoua raia hovyo,shemeji yake ''dhaifu" anachekesha!
 
Mkuu wa jeshi la polisi, IGP Said Mwema amesisitiza kuwa jeshi la polisi halitaendelea kuwafumbia macho watu wanaovuruga amani ikiwa ni pamoja na kuchoma nyumba za kuabudia na kuuana kwa kisingizio cha kidini

Huyu jamaa kweli kilaza, hadi aelezwe wajibu wake na shemeji yake Kikwete ndio anaibuka na kupiga mkwara. Our expectations ni kuwa siku ile ile Ustaadh Ilunga anatoa DVD ya kushawizi mauaji kesho yake alitakiwa kudakwa, sio kupima upepo kwanza dini nyingine zitareact vipi...
 
Mkuu wa jeshi la polisi, IGP Said Mwema amesisitiza kuwa jeshi la polisi halitaendelea kuwafumbia macho watu wanaovuruga amani ikiwa ni pamoja na kuchoma nyumba za kuabudia na kuuana kwa kisingizio cha kidini
IGP Anatekeleza haya

"Ndugu zangu;
Watanzania hatujawahi kuwa hivi, kumetokea nini? Miaka yote Watanzania ni watu tunao tambua na kuheshimu tofauti za dini zetu mbalimbali tunazo abudu.Watanzania ni waelewa na kwa ajili hiyo tume kuwa tuna vumiliana kwa tofauti zetu na ndiyo maana tume kuwa tunaishi pamoja kidugu, kwa umoja na kushirikiana kwa mambo yote yanayo tuhusu maishani isipokuwa wakati kila mmoja anapoingia kwenye nyumba ya ibada kumuomba Mola kwa misingi na taratibu ya dini yake.
Watanzania wa dini zote na makabila tofauti wanaishi nyumba moja,wanasoma pamoja, wanafanya kazi pamoja kwa udugu, upendo, umoja na ushirikiano.Kuna koo na familia zenye watu wa dini tofauti, wengine Waislamu na wengineWakristo. Wapo Waislamu na Wakristo wameoana, wamezaa na wamejukuu na kila mmoja amebakia kuwa mfuasi wa dini yake. Wapo pia ambao hawakuoa lakini wamezaa watoto na wanashirikiana kulea watoto wao. Hayo ndiyo maisha ya Watanzania nahiyo ndiyo Tanzania yenye amani na utulivu tuliyozaliwa, kukua na kuishi.Nawasihi sana Watanzania wenzangu, tuienzi na kuidumisha tunu hiiwaliyotujengea mababu zetu.

Ndugu Wananchi;
Kuna wenzetu kwa sababu wanazozijua wao na kwa manufaa wanayoyajua waowanataka kutuvurugia nchi yetu hii nzuri. Tusiwape nafasi wachochezi hawa kwanihawatutakii mema na wala hawazitakii mema dini zetu na nchi yetu. Sisi katikaSerikali hatuta sita kuwachukulia hatua wale wote wanaochochea chuki za kidini,wanaodharau vitabu vitakatifu vya dini nyingine na wanao kejeli dini nyingine.
Nimewakumbusha Polisi na mamlaka husika kote nchini wasifanye ajizikwenye matukio ya namna hiyo. Wawachukulie hatua stahiki wale wote wanaohusika.Nimewataka wazingatie msemo wa Kiswahili usemao "ajizi nyumba ya njaa".Wachochezi wa mifarakano na chuki za kidini wasipodhibitiwa ipasavyo wataletamaafa kwa Watanzania wasiokuwa na hatia. Nimewakumbusha Wakuu wa Wilaya naMikoa kama walinzi wa amani wa maeneo yao ya uongozi, watimize ipasavyo wajibuwao. Pia nimewataka Polisi wakamilishe mapema upelelezi wa makosa ya vurugu zakidini na wahusika wafikishwe haraka kwenye vyombo vya sheria ili iwe fundisho kwa wengine.

Ndugu Wananchi;
Naendelea kuwasiliana na viongozi wa dini kuzungumza nao juu ya wajibu wao maalum wa kuhakikisha kuwa wafuasi wao hawawi chanzo au sehemu ya tatizo na mifarakano miongoni mwa waumini wa dini mbalimbali nchini. Hali kadhalika naitumia nafasi hiyo kuwakumbusha umuhimu wa kuzungumza na wenzao wa upande mwingine kutatua tofauti au matatizo yanayo athiri uhusiano mwema baina yao.

Ndugu Wananchi;
Kuna msemo maarufu usemao "mjenga nchi ni mwananchi na mbomoa nchi nimwananchi". Naomba tuwe wajenga nchi na kamwe tusikubali kuwa wabomoa nchi.Hivi tukiibomoa nchi yetu tutakwenda wapi? Tutaishi wapi? Tusikubali kugeuka wakimbizi ndani ya nchi au nje ya nchi yetu.
Kwa mara nyingine tena, napenda kutumia nafasi hii kuwapa mkono wa pole makanisa, familia, ndugu na jamaa wote wa Mchungaji Kachila na Padri Mushi.Sote tunafahamu machungu waliyonayo kwa kuondokewa na wapendwa wao. Serikali na wapenda amani wote nchini wapo pamoja nanyi katika kipindi hiki kugumu. Vilevile natoa rambirambi zangu nyingi kwa waumini wote wa Kanisa la PentekosteAssemblies of God na Kanisa Katoliki Tanzania kwa kuondolewa ghafla na viongoziwao. Tuzidi kumwomba Mwenyezi Mungu azipumzishe kwa amani roho za viongoziwetu. Amin."
Alisema Rais Jakaya Kikwete kwenye hotuba yake ya mwisho wa mwezi wa February 2013.
 
Kama ni kweli amemaanisha tunataka tuone akimkamata Mwigulu Mchemba aonyeshe cd ya Chadema aliyosema anayo.
Akishindwa tuamini ameamua kubwabwaja kama wanasiasa wa Ccm
 
igp na yeye amekuwa nape, anaongea ongea tu. Tunataka aanzie na waliomuua mwangosi. Hana issue kabisaa. Ni boya
kwani muuaji si alijisalimisha mwenyewe na alipelekwa mahakamani na ku plea manslaughter?
 
Eboo...hivi kumbe jeshi la polisi lilikuwa linawafumbia macho!

Yeye kama IGP ana matatizo, lakini mwajiri wake ana matatizo makubwa zaidi maana msimamo wake haukueleweka kwa subordinates wake.
Huoni baada ya Mkulu kubweka dhidi ya wahuni wa kidini, IGP naye kaibuka?
 
Back
Top Bottom