Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 16,987
- 20,271
1.Ifahamike kwamba ufisadi wa escrow akaunti msingi wake ni mkataba wa kifisadi wa IPTL uliosainiwa mwaka 1995 kufuatia tatizo la umeme mwaka1994 ambapo ilitakiwa umeme wa dharula ndipo IPTL ikasaini mkataba wa miaka20(1995-2015)..na wamiliki wa kampuni hiyo ya IPTL walikuwa Mechmar ya malaysia mwenye 70% na VIP ya Tz yenye 30% na kwa mujibu wa mkataba tanesco na IPTL walikubaliana kuwa muamuzi wa mwisho kuhusu mgogoro baina yao ni baraza la usuluhishi la migogoro ya kiuwekezaji (international centre for settlement of investment disputes-ICSID)
2. Kosa la kwanza IPTL haikuweza kukamilisha mradi wake 1995 kwenye kipindi cha dharula na badala yake ikakamilisha mwaka 1998. Hii ilikuwa kosa
2. Baada ya kumaliza mwaka1998 IPTL ililalamikiwa na tanesco ICSID kwamba imekuza gharama za uwekezaji na hivyo kukuza gharama za umeme.mwaka 2001 uamuzi wa ICSID ukatoka ikabainika ni kweli IPTL ilikuza gharama kwa kiasi cha dola 27milioni. Hili ni kosa kubwa.
3. Mwaka 2002 IPTL ikanza kuuzia umeme tanesco lakn mwaka 2004 tanesco ikabaini kuwa IPTL ilidanganya kuhusu mtaji. IPTL ilisema 30% ya mtaji ilikuwa nao kama equity sawa na dola 36milion na kwamba 70% ilikopa. Lakn bada ya ukaguzi ikabainika kuwa IPTL haikuweka dola 36milion kama equity bali dola 50 ambapo kwa exchange rate ya wakati huo ya 1:1000, dola50 ilikuwa sawa na tsh elfu50 ambazo hata fundi baiskeli angeweza kuwekeza. Hili ni kosa.
4. Kutokana na kasoro iyo tanesco ikataka gharama ya umeme (tarrif) ishuke kwasababu bei ilizingatia equity ya dola 36milioni kumbe ni sh50000. Mabishano yakaendelea mpaka 2006.
5. Mwaka 2006 serikali na tanesco ikashinikiza ifunguliwe akaunt maalumu (escrow)ili malipo yawekwe huko mpaka mgogoro utapokwisha kuhusu bei sahh ndipo pesa hiyo igawanywe kwa kuzingatia bei sahh baina ya pande mbili ndio mana ilikuwa kosa Pinda kusema pesa yote ya escrow eti ni ya IPTL kabla ya uamuzi kuhusu bei haujafikiwa
6.mwaka 2008 IPTL iliposhindwa kujiendesha ikawekwa chini ya receivership chini ya RITA ambapo ni RITA ikawa inasimamia gharama za uendeshaji
7.mwaka 2013 September ikatoka hukumu ya mahakama kuu chini ya Jaji Utamwa ilojichanganya baada ya VIP mwenye 30% kushtaki na kutaka IPTL iondolewe chini ya receivership na mali zote za IPTL ipewe kampuni ya PAP ya singasinga anaitwa Sethi.hukumu iyo ikaenda mbali na kusema singasinga huyo mwenye rekodi mbaya ya ufisadi tangu Kenya aliposhiriki ufisadi mkubwa mwaka 2002 wa Goldenberg scandal ilokiangusha chama cha KANU chini ya Moi na asiye na rekodi yoyote ya uwekezaji ktk umeme eti mahakama ikasema atazalisha 500MW na kwamba atauzia umeme tanesco kwa bei nafuu ya dola cent6 mpaka8 kwa unit.hukumu iyo inamua ivyo wakati ikijua kuwa mmiliki wa asilimia70 ya IPTL yuko chini ya liquadation Malaysia na zaidi ICSID kuna kesi inayohusu mgogoro wa IPTL na serikali uliofunguliwa na standard chartered bank ambayo ilinunua deni la IPTL mwaka 2005 na ikaruhusiwa kuishtaki serikali ya Tanzania kwenye baraza hilo lenye mamlaka ya mwisho.
8.Hukumu ya Jaji utamwa haikujua kuwa hoja ya biashara kwa maana ya bei na kiasi cha umeme ambao tanesco itanunua kwa IPTL sio kazi ya mahakama bali ni makubaliano ya tanesco kwa kutegemea mahitaji..na zaidi mwanahisa mkubwa alikuwa under liquidation malaysia na zaidi kulikuwa na kesi ICSID
9.pamoja ya Jaji Utamwa kudai mali zote za IPTL ipewe kampuni ya singasinga ya PAP bado ieleweke kuwa pesa za escrow hazikuwa mali ya IPTL kwakua uamuzi kuhusu mgogoro wa bei haukuwa umefanywa kokote na zaidi ulikuwa unasubilia hukumu ya ICSID
10. Mwaka 2014 Feb, ICSID ilifanya uamuzi wa awali kwamba ni kweli IPTL ina overcharge tanesco na kuelekeza pande mbili zikafanye hesabu upya ndani ya siku90 zilizoisha may2014.
11. Msingi wa hukumu ile ungesaidia kujua ni kwa kiasi gani iptl imeibia tanesco tangu 2002 mpaka 2013 katika bei.. (overcharge)
12. Tanesco na serikali hawakutoa ushirikiano ndani ya siku90 kutekeleza uamuzi huo ambao una faida kwa nchi kwasababu tayari tangu sept2013 pesa ya escrow imeshaliwa. Huu ndio uzalendo?
12. Kwanini serikali imekosea kufanya malipo haya kwa haraka?;
a. Kipindi malipo haya yanasukumwa kwa nguvu BOT itoe waziri wa fedha alikuwa anaumwa na wakati malipo yanafanyika nov2013 tayari waziri mgimwa alikuwa amekata kauli hospital afrika kusini
b. Kampuni ya singasinga ya PAP ilokomba fedha hiyo sio mmiliki halali wa IPTL ndio mana mpaka sasa hakutoa share certificate ya yeye kuuziwa 70% za Iptl ambazo ziko chini ya Mechmar. Kwann serikali imemuamini bila uthibitisho huo?
C.kama kweli alinunua asilimia 70 ya share za mechamar zilizo iptl angelipa capital gain tax lakn hakuna ushahidi huo kama alivo na ushahidi wa kununua hisa 30 za VIP
d.ushahidi mwingine ni kwamba wakati PAP inasema ilinunua IPTL tangu 2010 ukweli ni kwamba tangu 2008 mpaka 2013 IPTL ilikuwa under receivership chini ya RITA na hivyo isingewezekana kisheria share zake iuze
E. Ushahidi mwingine kampuni yenyewe ya mechmar imeandika barua gazeti la citizen na kwa wakili wake Tanzania asyla attorney kupinga kuwa haijauza hisa zake za IPTL kwakuwa ilikuwa under kiquidation na ikielekeza kuwa huyo PAP anaedai kuwa alinunua hisa hizo awaoneshe share certificate.
F. Hakuna ushahidi wa malipo ambayo PAP ameonesha alifanya kununua share za VIP kabla ya kupata pesa za escrow. .ndio mana mmiliki wa PAP aliandika barua BOT kulalamika kuwa kampuni ya PAP ni ya kitapeli isilipwe kwakua ilikuwa haijamlipa wakati huo ilikuwa novemba mwanzoni kabla pesa haijatoka escrow..hii maana yake PAP alilipa VIP bada ya kuchota pesa za escrow. Kwamba alinunua hisa bada ya kufaidi hisa. Hii haikubaliki kisheria
Kwa ujumla suala hili ni aibu nyingine kwa taifa ambalo Tanesco inadaiwa zaidi ya 400bn leo inatapanya 200bn kizembe namna hii. Lakn zaidi liquidator wa mechmar ataidai serikali na kulipwa...standard chartered ambae alikuwa anaidai serikali na kesi haijafika mwisho nae tutamlipa..huyu singasinga atabaki na mitambo ya iptl na ametudhulumu hizo 200bn za escrow pamoja na gharama ambazo iptl ilikuwa ina overcharge ambazo ilipaswa turejeshewe zaidi ya 150m dola za tangu 2002 mpaka 2013.
Ni aibu watu wanaosema ni wazalendo leo wanashabikia nchi kuporwa 200bn na singasinga mwenye rekodi mbaya. Ushahidi wote nitauweka wazi bungeni na nitahakikisha ninauweka wazi kwenye mitandao yote y kijamii ili kila mtanzania aelewe huu mzima wa IPTL ulioshindikana tangu awamu ya pili mpaka leo.
Na nitaandika kitabu kuhusu sakata hili ambalo kabla ya mwalimu Nyerere hajatuacha duniani alitaja kama mfano wa ufisadi mbaya africa.
(imetolewa na David Kafulila)
2. Kosa la kwanza IPTL haikuweza kukamilisha mradi wake 1995 kwenye kipindi cha dharula na badala yake ikakamilisha mwaka 1998. Hii ilikuwa kosa
2. Baada ya kumaliza mwaka1998 IPTL ililalamikiwa na tanesco ICSID kwamba imekuza gharama za uwekezaji na hivyo kukuza gharama za umeme.mwaka 2001 uamuzi wa ICSID ukatoka ikabainika ni kweli IPTL ilikuza gharama kwa kiasi cha dola 27milioni. Hili ni kosa kubwa.
3. Mwaka 2002 IPTL ikanza kuuzia umeme tanesco lakn mwaka 2004 tanesco ikabaini kuwa IPTL ilidanganya kuhusu mtaji. IPTL ilisema 30% ya mtaji ilikuwa nao kama equity sawa na dola 36milion na kwamba 70% ilikopa. Lakn bada ya ukaguzi ikabainika kuwa IPTL haikuweka dola 36milion kama equity bali dola 50 ambapo kwa exchange rate ya wakati huo ya 1:1000, dola50 ilikuwa sawa na tsh elfu50 ambazo hata fundi baiskeli angeweza kuwekeza. Hili ni kosa.
4. Kutokana na kasoro iyo tanesco ikataka gharama ya umeme (tarrif) ishuke kwasababu bei ilizingatia equity ya dola 36milioni kumbe ni sh50000. Mabishano yakaendelea mpaka 2006.
5. Mwaka 2006 serikali na tanesco ikashinikiza ifunguliwe akaunt maalumu (escrow)ili malipo yawekwe huko mpaka mgogoro utapokwisha kuhusu bei sahh ndipo pesa hiyo igawanywe kwa kuzingatia bei sahh baina ya pande mbili ndio mana ilikuwa kosa Pinda kusema pesa yote ya escrow eti ni ya IPTL kabla ya uamuzi kuhusu bei haujafikiwa
6.mwaka 2008 IPTL iliposhindwa kujiendesha ikawekwa chini ya receivership chini ya RITA ambapo ni RITA ikawa inasimamia gharama za uendeshaji
7.mwaka 2013 September ikatoka hukumu ya mahakama kuu chini ya Jaji Utamwa ilojichanganya baada ya VIP mwenye 30% kushtaki na kutaka IPTL iondolewe chini ya receivership na mali zote za IPTL ipewe kampuni ya PAP ya singasinga anaitwa Sethi.hukumu iyo ikaenda mbali na kusema singasinga huyo mwenye rekodi mbaya ya ufisadi tangu Kenya aliposhiriki ufisadi mkubwa mwaka 2002 wa Goldenberg scandal ilokiangusha chama cha KANU chini ya Moi na asiye na rekodi yoyote ya uwekezaji ktk umeme eti mahakama ikasema atazalisha 500MW na kwamba atauzia umeme tanesco kwa bei nafuu ya dola cent6 mpaka8 kwa unit.hukumu iyo inamua ivyo wakati ikijua kuwa mmiliki wa asilimia70 ya IPTL yuko chini ya liquadation Malaysia na zaidi ICSID kuna kesi inayohusu mgogoro wa IPTL na serikali uliofunguliwa na standard chartered bank ambayo ilinunua deni la IPTL mwaka 2005 na ikaruhusiwa kuishtaki serikali ya Tanzania kwenye baraza hilo lenye mamlaka ya mwisho.
8.Hukumu ya Jaji utamwa haikujua kuwa hoja ya biashara kwa maana ya bei na kiasi cha umeme ambao tanesco itanunua kwa IPTL sio kazi ya mahakama bali ni makubaliano ya tanesco kwa kutegemea mahitaji..na zaidi mwanahisa mkubwa alikuwa under liquidation malaysia na zaidi kulikuwa na kesi ICSID
9.pamoja ya Jaji Utamwa kudai mali zote za IPTL ipewe kampuni ya singasinga ya PAP bado ieleweke kuwa pesa za escrow hazikuwa mali ya IPTL kwakua uamuzi kuhusu mgogoro wa bei haukuwa umefanywa kokote na zaidi ulikuwa unasubilia hukumu ya ICSID
10. Mwaka 2014 Feb, ICSID ilifanya uamuzi wa awali kwamba ni kweli IPTL ina overcharge tanesco na kuelekeza pande mbili zikafanye hesabu upya ndani ya siku90 zilizoisha may2014.
11. Msingi wa hukumu ile ungesaidia kujua ni kwa kiasi gani iptl imeibia tanesco tangu 2002 mpaka 2013 katika bei.. (overcharge)
12. Tanesco na serikali hawakutoa ushirikiano ndani ya siku90 kutekeleza uamuzi huo ambao una faida kwa nchi kwasababu tayari tangu sept2013 pesa ya escrow imeshaliwa. Huu ndio uzalendo?
12. Kwanini serikali imekosea kufanya malipo haya kwa haraka?;
a. Kipindi malipo haya yanasukumwa kwa nguvu BOT itoe waziri wa fedha alikuwa anaumwa na wakati malipo yanafanyika nov2013 tayari waziri mgimwa alikuwa amekata kauli hospital afrika kusini
b. Kampuni ya singasinga ya PAP ilokomba fedha hiyo sio mmiliki halali wa IPTL ndio mana mpaka sasa hakutoa share certificate ya yeye kuuziwa 70% za Iptl ambazo ziko chini ya Mechmar. Kwann serikali imemuamini bila uthibitisho huo?
C.kama kweli alinunua asilimia 70 ya share za mechamar zilizo iptl angelipa capital gain tax lakn hakuna ushahidi huo kama alivo na ushahidi wa kununua hisa 30 za VIP
d.ushahidi mwingine ni kwamba wakati PAP inasema ilinunua IPTL tangu 2010 ukweli ni kwamba tangu 2008 mpaka 2013 IPTL ilikuwa under receivership chini ya RITA na hivyo isingewezekana kisheria share zake iuze
E. Ushahidi mwingine kampuni yenyewe ya mechmar imeandika barua gazeti la citizen na kwa wakili wake Tanzania asyla attorney kupinga kuwa haijauza hisa zake za IPTL kwakuwa ilikuwa under kiquidation na ikielekeza kuwa huyo PAP anaedai kuwa alinunua hisa hizo awaoneshe share certificate.
F. Hakuna ushahidi wa malipo ambayo PAP ameonesha alifanya kununua share za VIP kabla ya kupata pesa za escrow. .ndio mana mmiliki wa PAP aliandika barua BOT kulalamika kuwa kampuni ya PAP ni ya kitapeli isilipwe kwakua ilikuwa haijamlipa wakati huo ilikuwa novemba mwanzoni kabla pesa haijatoka escrow..hii maana yake PAP alilipa VIP bada ya kuchota pesa za escrow. Kwamba alinunua hisa bada ya kufaidi hisa. Hii haikubaliki kisheria
Kwa ujumla suala hili ni aibu nyingine kwa taifa ambalo Tanesco inadaiwa zaidi ya 400bn leo inatapanya 200bn kizembe namna hii. Lakn zaidi liquidator wa mechmar ataidai serikali na kulipwa...standard chartered ambae alikuwa anaidai serikali na kesi haijafika mwisho nae tutamlipa..huyu singasinga atabaki na mitambo ya iptl na ametudhulumu hizo 200bn za escrow pamoja na gharama ambazo iptl ilikuwa ina overcharge ambazo ilipaswa turejeshewe zaidi ya 150m dola za tangu 2002 mpaka 2013.
Ni aibu watu wanaosema ni wazalendo leo wanashabikia nchi kuporwa 200bn na singasinga mwenye rekodi mbaya. Ushahidi wote nitauweka wazi bungeni na nitahakikisha ninauweka wazi kwenye mitandao yote y kijamii ili kila mtanzania aelewe huu mzima wa IPTL ulioshindikana tangu awamu ya pili mpaka leo.
Na nitaandika kitabu kuhusu sakata hili ambalo kabla ya mwalimu Nyerere hajatuacha duniani alitaja kama mfano wa ufisadi mbaya africa.
(imetolewa na David Kafulila)