Idd Pazi "Father" Atua CHADEMA

Idd Pazi "Father" Atua CHADEMA

Kipa namba moja wa zamani wa timu ya Simba na Taifa Stars - Idd Pazi "Father"; jana alijiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) akisema ni haki yake kwa mujibu wa Katiba ya nchi, pia kupata fursa ya kupigania rasilimali za taifa kwa maslahi ya wengi.

...

Chacha (Katibu wa Chadema Dar es Salaam) kwa upande wake alisema kitendo cha Father kujiunga na Chadema ni ishara ya wazi kabisa kwamba milango iko wazi kwa kila Mtanzania kujiunga na chama hicho.
 
Huyu jamaa jembe namshauri agombee Temeke 2015
 
Mbona nusu ya wachezaji wanaocheza premieur league hapa bongo ni chadema?kuanzia yanga mpaka african lyon na mwakani ashanti ndani ya nyumba
 
Huyu Iddy father Pazi mbona ana damu ya ccm? Huyu lazima atakuwa KANJANJA kama shibuda
 
Ukiona anaenda huko ujue kajipanga na anaweza kusimama kwa miguu yake. Big up
 
Kipa namba moja wa Simba na Timu ya Taifa Idd Pazi "Father" amejiunga CHADEMA. Alisema CHADEMA ndio Chama pekee kinaweza kuleta mageuzi ya kweli Tanzania.

Source: Tz Daima

Hawa jamaa wanaohamia huku CDM wana nia nzuri kweli ebu wekeni CV ya pazi isije ikawa kama ya MNYIKA, SUGU, NYERERE na wenigine kama hawa. Jamani tuangalie tusije tukazika chama kwa sifa za kijinga.
 
Huyu Iddy father Pazi mbona ana damu ya ccm? Huyu lazima atakuwa KANJANJA kama shibuda

Teh teh teh, CCM watakuwa wamemwangalia CV yake na kugundua size yake ni CDM akaungane na SUGU, MNYIKA, LEMA na wengine ili wasaidie kupiga mayoe
 
Nyanda huyu alikuwa hana mpango wa siasa za vyama...jina lake hata ccm halikuwepo. na namfahamu tangu alipokuwa akichipukia Bandari ya mtwara, nikamfuatilia akiwa majimaji ya songea, hadi wekundu wa msimbazi. Namtakia safari njema km ni kweli...na ajiandae kubwabwaja uwongo kwani ninavyomfahamu alikuwa na kauli thabit isiyoj na ulaghai tofauti na wanasiasa wetu uchwara!
 
Inaonekana siku hizi mtu maisha yakimshinda anakimbilia siasa na CHADEMA ndiyo kichaka wanachoenda kujifichia.

Kwenye uchaguzi mkuu wa 2015 kwa kutumia kura zetu tutawafurumusha wote kutoka huko kichakani ili wakafanye kazi taifa lisonge mbele
Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

Acha utoto wewe mbona maisha yamekushinda usemi kwanza hiyo simu unayotumia ya mother ako.Ndio kusema suleman mathew maisha yememshinda kujiunga ccm.
 
Umaarufu ukipotea ndo mnatafuta njia za kutokea kwenye siasa foolish Pazi jaribu na huku.
 
Mjanja hawezi kushabikia wezi

njoo kamanda tushirikiane kuwadaka mafisadi wakanyee ndo

sishabikii yanga ni ya ma-ccm
 
Back
Top Bottom