Mamzalendo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2010
- 1,670
- 558
Mkuu Urefu wa mita 20 ni average ya ghorafa 5 hadi 6. Mkuu haya mambo hayahitaji blaa blaa. Tafuta Architect akuchoree kwanza kutokana na mahitaji yako then Structural Engineer atamaliza kazi yako
Structural Engineer atakusaidia kujua utakuwa na slabs za unene upi na saizi ya nondo na idadi yake pamoja na kiasi gani utatumia kwenye slab yako. Atakusaidia kujua utaweka beams za saizi ipi kama ni 230*450mm, 230*500, 230*600 nk pamoja na idadi na saizi ya nondo, atakusaidi kujua pia utatumia nguzo(columns) za saizi ipi na nondo za saizi ipi na idadi yako, njia hizo hizo atatumia kwenye ngazi, vitako(pads) nk.
Hayo yote yanahitaji mahesabu wala hamna longo longo, yote haya yanafanyika baada ya architect kuchora michoro yake yenye mpangilio wa vyumba, elevations zake na sections pia.
Kwa ushauri 0719 021 693
If u want a safe,durable and beautiful building especially storey building be ready to pay this people
1. Architect
2.Structural engineer
3.Electrical engineer
4.Mechanical enginer
5.Quantity surveyor
6.Good Contractor
with this people in ur project u can sleep and dont expect failure.kama kuna nliesahau u can add,
Mkuu unafahamu Architect & Structural Eng yeyote unayemjua utupatie contact zake?
Mimi ni Structural Engineer, Architect yupo, namba yake ni 0713 509 509, 0784 509 509. Huyu ndugu ni Architect mzuri sana. Namba zangu ni 0719 021 693, 0788 869 580
Ushauri mbadala.
Kama nyumba ni ya kuishi na ni ghorofa moja, unaweza ukachanganya nondo na matofali{matofali yatatumika kubeba mzigo(load bearing walls)} na itakusaidia kupunguza idadi ya nondo na size ya nguzo, beams na vitako. Ujenzi wa namna huu unaitwa non framed structure.
Ukitaka usijenge bila kutumia matofali{hapa matofali yatatumika kama partition nk}, lazima utumie nondo nyingi na sizes ya nguzo, beams na vitako itakuwa kubwa. Ujenzi wa namna hiyo unaitwa framed structure. Na ni mzuri sana, very durable
Mkuu Foundation, nishukuru kwa kuwa wazi na msaada kwa jamaa hapo juu. Kama sikosei ni mtu upo siku zote kwenye hii professional.
Nina swali moja kwako: Hivi Tanzania kuna kiwanda cha kutengeneza Pre-Cast Conrete Slab? Hizi zingelisaidia sana watu kama hawa kwani zinakuwa ni rahisi kuzifunga na linakuja gari la Zege na kumaliza kazi. Zipo za aina nyingi na just in case sijaeleweka, ngoja niweke picha hapa chini. Kama kuna mtu anafahamu kuwepo kwa kiwanda kinachotengeneza hizi slab, basi atujulishe.
http://www.structuremag.org/images/0908-en-1.gif
http://www.homebuilding.co.uk/files/ascent-homebuilding/images/0605floors_free.jpg
http://www.ebawe.de/img/bilder-ganze-breite/elementdecken01.jpg