Huu wimbo ni wimbo wa Ki-Africa hasa na ndiyo maana wengi wenu mmeupenda.
Cole kafanya ku-Sample huo wimbo na kuuweka kwenye RAP na kwa hilo namsifu.
Hata mie mwenyewe ilibidi niwaagize washikaji majuu waninunulie CD yake na wanitumie.
Wimbo hasa unaitwa Can't Get Enough na video yake haswa hii hapa chini....
Wimbo Original uliandikwa na wanamuziki ambao kwa sasa ni Wazee sana. Hii band ya Balla et Ses Balladins ilikuwa ni band ya serikali na baadhi ya wanamuziki wa band hii walishiriki kupiga miziki ya Miriam Makeba wakati akiishi Guinea, Conacry. Baada ya serikali kushindwa kuidhamini, band ilikufa rasmi kama band ya serikali ila hadi leo wazee hawa huwa wanaonekana mara moja moja wakifanya Concert.
Baadhi ya TV Station, wanaandika watunzi wa wimbo huo ambao ni Kouyate na mwingine simkumbuki kwa jina. Cole kwa kweli kawanyenyua hawa wazee na sasa dunia nzima imeshaanza kuwafatilia na CD zao naanza kuziona ONLINE kwa wingi sasa.
Paullete na Balla Et Ses Balladins, kibao cha mwaka 1980, kutoka Conacry, Guinea.
Wimbo Original uliandikwa na wanamuziki ambao kwa sasa ni Wazee sana. Hii band ya Balla et Ses Balladins ilikuwa ni band ya serikali na baadhi ya wanamuziki wa band hii walishiriki kupiga miziki ya Miriam Makeba wakati akiishi Guinea, Conacry. Baada ya serikali kushindwa kuidhamini, band ilikufa rasmi kama band ya serikali ila hadi leo wazee hawa huwa wanaonekana mara moja moja wakifanya Concert.
Baadhi ya TV Station, wanaandika watunzi wa wimbo huo ambao ni Kouyate na mwingine simkumbuki kwa jina. Cole kwa kweli kawanyenyua hawa wazee na sasa dunia nzima imeshaanza kuwafatilia na CD zao naanza kuziona ONLINE kwa wingi sasa.
Paullete na Balla Et Ses Balladins, kibao cha mwaka 1980, kutoka Conacry, Guinea.
Itakuwa kawapa shavu la nguvu, imetulia kwa kweli.
I wonder if Jigga hana mkono kwene hili since J Cole ni kijana wake.
Kwanza samahani sikuweka LIKE maana Laputopu yangu ina matatizo na nashindwa kuweka LIKE.
Jigga atakuwa na mkono wake na kumbuka hata Mkewe Beyonce, kwenye wimbo wake alitumia chezaji ya vijana wa Msumbiji waitwao Tofo Tofo Boys. Inaonekana wamekuwa na imani au upenzi na Africa kwa nguvu sana na hawaoni shida ya kuchukua vitu na kuvitangaza.
Hawa wazee wameula uzeeni. Mie mwenyewe natamani kuwaona kwenye Concert yao wakishusha vitu vya uhakika maana uzoefu wao kwa kweli utakuwa unatisha.
Beyonce aliposhindwa kucheza / Kujifunza uchezaji wa Tofo Tofo, aliamua kuwafuata Msumbiji na vijana wakapata VIZA na kutua USA ili kutoa shule kwa Beyonce. Vijana nasikia nao Msumbiji wapo juu sana maana News zilikuwa kila sehemu....
Thanks Sikonge... I wanted the Catch! No wonder... sasa nimeipata.
Tamu sana hii...
Thanks Jmushi na Sikonge...!
Pamoja sana mkuu. Nafikiri wanaosema Waafrica hatuwezi kitu, basi inabidi wafikiri mara mbili.
Huu ni mfano halisi wa "Tukiwezeshwa, tunaweza hata sisi......"
Wala hatuitaji kuwezeshwa Mkuu....
Hapo hujamwaga vitu vya gallery ya Femi Kuti Sr....
Kuna mtu alikuwa anaitwa Paul Simon (sijui yupo hai??), yule mzungu msouth afrika mpinga ukaburu alipiga show ya Halale zimbabwe na kumleta Miriam Makeba baada ya kuondoka kwa miaka 27 uhamishoni, natamani nikupe Video hapa ila mautundu yananipiga chenga kuweka video ambazo haipo kwenye site, humo kuna wale "Red Smith and Black Mambazo"....
Najiona kama nipo peponi, jigga tunamkaribisha sana